Nani Kasema Tibaijuka Kafukuzwa Uwaziri ?

Nani Kasema Tibaijuka Kafukuzwa Uwaziri ?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,240
Reaction score
44,481
WAkati mwingine Watanzania tunasoma zaidi ya kile kilichosemwa au kuandikwa na kutoka huko tunafikia mahitimisho yetu sisi wenyewe. Wote waliopata nafasi ya kusikia hotuba ya Rais Kikwete wanajua kwa uhakika kuwa hakusema amemfukuza kazi au amemuondoa Uwaziri Anna Tibaijuka. Anasema "walimwomba" lakini hakutuambia kama alikubali au bado anafikiria. Inaonekana kana kwamba wamempa nafasi Tibaijuka kutangaza kujiuzulu nafasi yake badala ya kumfukuza.

Kitu ambacho hadi hivi sasa hatujui kwa uhakika ni kama baada ya kuombwa Tibaijuka amekubali au la. Kwa sababu kama angekuwa amekubali Rais angekuwa amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri na hata kututangazia huyo "mwingine" ni nani. Kwa vile Tibaijuka hajakubali ombi la Rais na kwa vile Rais hajatangaza mbadala (replacement) ya Tibaijuka inashawishi akili kuwa Anna Tibaijuka bado ni waziri akiendelea kutafakari ombi hilo la Rais.

Nani anabisha?
 
WAkati mwingine Watanzania tunasoma zaidi ya kile kilichosemwa au kuandikwa na kutoka huko tunafikia mahitimisho yetu sisi wenyewe. Wote waliopata nafasi ya kusikia hotuba ya Rais Kikwete wanajua kwa uhakika kuwa hakusema amemfukuza kazi au amemuondoa Uwaziri Anna Tibaijuka. Anasema "walimwomba" lakini hakutuambia kama alikubali au bado anafikiria. Inaonekana kana kwamba wamempa nafasi Tibaijuka kutangaza kujiuzulu nafasi yake badala ya kumfukuza.

Kitu ambacho hadi hivi sasa hatujui kwa uhakika ni kama baada ya kuombwa Tibaijuka amekubali au la. Kwa sababu kama angekuwa amekubali Rais angekuwa amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri na hata kututangazia huyo "mwingine" ni nani. Kwa vile Tibaijuka hajakubali ombi la Rais na kwa vile Rais hajatangaza mbadala (replacement) ya Tibaijuka inashawishi akili kuwa Anna Tibaijuka bado ni waziri akiendelea kutafakari ombi hilo la Rais.

Nani anabisha?

Fumbo umfumbia mwelevu na mjinga ulinga'amua
 
WAkati mwingine Watanzania tunasoma zaidi ya kile kilichosemwa au kuandikwa na kutoka huko tunafikia mahitimisho yetu sisi wenyewe. Wote waliopata nafasi ya kusikia hotuba ya Rais Kikwete wanajua kwa uhakika kuwa hakusema amemfukuza kazi au amemuondoa Uwaziri Anna Tibaijuka. Anasema "walimwomba" lakini hakutuambia kama alikubali au bado anafikiria. Inaonekana kana kwamba wamempa nafasi Tibaijuka kutangaza kujiuzulu nafasi yake badala ya kumfukuza.

Kitu ambacho hadi hivi sasa hatujui kwa uhakika ni kama baada ya kuombwa Tibaijuka amekubali au la. Kwa sababu kama angekuwa amekubali Rais angekuwa amefanya mabadiliko ya baraza la mawaziri na hata kututangazia huyo "mwingine" ni nani. Kwa vile Tibaijuka hajakubali ombi la Rais na kwa vile Rais hajatangaza mbadala (replacement) ya Tibaijuka inashawishi akili kuwa Anna Tibaijuka bado ni waziri akiendelea kutafakari ombi hilo la Rais.

Nani anabisha?

kujiuzuru kwa Tibaijuka au kufukuzwa kazi kwake hatufaidiki lolote.Kinachohitajika ni hao majambazi yatoke ktk utumishi wa umma.
 
Ile kauli ya tunaomba utupishe ili tufanye uteuzi mwingine ina maana gani?
 
nimeongea nae kw cim anasema bado ni waziri wa Ardhi Nyumba na Makaazi ameniambia kama atajiuzulu Rais JK ataendelea kumshangaa sana
 
Ndugu MM, tukifikiri namna hiyo tutakua tumekosea. Alichoonyesha JK jana ni lugha ya kulazimika kumwondoa Tibaijuka baada ya yeye mwenyewe(Tiba) kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha kwake.

it was an Ironic language. Natagemea siku za usoni atatangazwa waziri mwingine na au kufanyika mabadiliko katika baraza.
 
kwa hiyo kama maeambiwa atupishe inamaana atang`ang`ania???

Isitoshe jk katumia tafsida tuu badala ya kusema nimemfukuza akapunguza ukali wa maneno na kusema tupishe

hahahah kama vile tunaposema mfamasia mzawa badala ya kusema muuza gongo
 
kujiuzuru kwa Tibaijuka au kufukuzwa kazi kwake hatufaidiki lolote.Kinachohitajika ni hao majambazi yatoke ktk utumishi wa umma.
Hilo ndilo hitaji pekee la watanzania?! Hatuhitaji majambazi hao warudishe mali zetu walizopora?
 
Ninavyoelewa mimi, na kama nilivyoelewa wakati fisadi mkuu akijikosha kwa wanoitwa wazee wa Dar, bani kwamba, anaombwa (hapa akiona ni vema akubali na kama akiona si vema akatae, kwa kuwa si kila ombi ni lazima likubalike), awapishe. Na akikubali ombi la kuwapisha, watateua mwingine lakini kabla hajakukubali basi ni dhahiri hakuna uteuzi mpya.

Kikubwa hata kinachotawala ni utashi wa Tiba, kukubali ama kukataa. Hakuna amri, nguvu, shuruti wala ulazima katika suala hili. Kama kungekuwa na nguvu yoyote yenye ulazima, basi angebebwa na kuwekwa pahala pengine, ili wengine wapite.

Hii ndiyo strength ya raisi wa 4 wa jamhuri wa muungano wa ccm.

Anawaomba waharifu, waamue kujihukumu kama wakitaka.

Ile kauli ya tunaomba utupishe ili tufanye uteuzi mwingine ina maana gani?
 
WALIMU WAONGEZWE MISHAHARA kwani kaz waliyonayo ni kubwa mno!
yaani hata hiyo kauli ya jk bado haieleweki tu!
 
kujiuzuru kwa Tibaijuka au kufukuzwa kazi kwake hatufaidiki lolote.Kinachohitajika ni hao majambazi yatoke ktk utumishi wa umma.
upo njee ya uzi

tibaijuka bado hajakubali ombi la rais kwa kuwa anaonewa

kosa la tiba ni kupokea hela kimyakimya yafaa aonywe kama wengine na si kufukuzwa
kosa la akina muhongo ni kubwa maramia ya lile la tibaijuka ila hata onyo hapewi

mramba yupo mahakamani kwa kuitia serikali hasara ya bil 11. je muhongo maswi na mkuya wametia hasara ya sh ngapi mpaka wasamehewe

kesi ya mramba na yona ifutwe wapewe onyo kama kawaida
 
Nimesema hili tangu jana.....Prof Tibaijuka hadi sasa ni waziri wa ardhi na sidhani kama hata ikulu imeshatoa statement rasmi ya kutengua.....Rais jana hakutengua uteuzi wake .....waandishi wa habari sijui wametoa wapi nukuu ya Tibaijuka kufutwa kazi ......
 
Mkuu

Kuna wakati Watanzania wanadanganywa kirahisi sana.
Kwanza, Anna Tibaijuka hajawa tatizo la Escrow hata kidogo.
Kilichotokea kwake ni poor judgement katika kukubali pesa zinazokwenda katika taasisi kuingizwa katika account yake binafsi.

Rais hajasema amemfukuza, alichosema ni kumuomba awapishe wamteu mwingine
Ukiangalia vema maneno hayo, ni ule ujanja ujanja wa mjini wa kucheza na akili za watu
Rais anapoweka watu njia panda inatisha sana maana haeleweki

Hata hivyo tutambue kuwa wiki nzima magazeti ya serikali yamekuwa yakimpigia debe na kumtetea waziri Mhongo
Hoja kubwa ni kuwa anasambaza umeme na kutekeleza ilani ya CCM.
Hata kama ni mhalifu hilo si baya ukilinganisha na kazi yake.

Hapa Watanzania wanasahau kuwa EL naye aliambiwa kujenga shule za kata.
Hatujui kwanini hakupewa benefit of doubt kama anayopewa Mhongo.

Ili kuhakikisha wananchi na Wadanganyika wanaondoka katika mada ya uhalifu na wahalifu halisi, na ili kuwasahaulisha tatizo zima, upo mpango mahususi wa kumfanya Anna Tibaijuka kama Escrow.

Ukisoma katika mitandao na magazeti, hakika Anna Tibaijuka amekuwa mhalifu mkubwa wa Escrow Kuliko Ruge au Singa singa.

Amekuwa tatizo kuliko Mbena, katibu wa Rais aliyeandika barua kushinikiza malipo ya wafanyabiashara kama alivyosema Rais.

Tibaijuka amekuwa tatizo kubwa kuliko waziri mkuu aliyejua uozo wote.

Anna amekuwa tatizo kuliko bodi ya Tanesco iliyohusika katika uhalifu

Anna ni tatizo kuliko Bank kuu iliyotoa mapesa kwa shinikizo la mwanasheria.

Ni makusudi kabisa watu wanalazimishwa kushangilia kuondoka kwa Anna ambako hakujasemwa kama Kafukuzwa ili kuwasahaulisha tatizo halisi.

Na kweli Watanzania wamenunua ujinga huo.
Kwamba Escrow ni Anna Tibaijuka.Siyo akina Chenge, Ngeleja, na wengine ambao hatujui majina yao yanahusiana vipi na wakubwa.

Anna Tibaijuka amekuwa tatizo kuliko Stanbic na Mkombozi.

Anna Tibaijuka amekuwa tatizo kuliko katibu mkuu Maswi au katibu mkuu kiongozi aliyetaka suala la Escrow lisitishwe kutokana na barua ya mahakama.

System inafanya kazi, inajua ikimfanya Anna kama Escrow, Watanzania watasahAu taarifa za CAG na PCCB, watajiunga mitaani kushangilia mbuzi wa kafara 'Anna'' Na kweli wanashangilia na wamesahau uozo mzima.
 
Back
Top Bottom