Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 31,010
- 60,472
Dah babu unapenda sifa kweli!!Hebu rudia tena kwa sauti tafazali.
Dah babu unapenda sifa kweli!!Hebu rudia tena kwa sauti tafazali.
Mungu BABA wa Mbinguni, Hakuna kama wewe!...Hakuna kama Mungu ambaye ni BABA.Kwa jina la mama, na la mwana na roho mtakatifu amen!!
Wataukubali taratibu tu kiongozi,unajua hii hakuna kama mama ilijengeka sana kwenye jamii yetu ndiyo maana baba akaonekana kumbe yeye ni less important na substitute yake inaweza kuwepo!twende nao taratibu mpwa watatuelewa
Oryt oryt
sasa unanichanganya
Halafu mbona black woman hapo chini hasemi neno?!:bange:
we dont share the same background lizzy,Hiyo mentality ililetwa na nini kama sio reality??Tukubali tu kwamba kwenye familia ya kawaida yenye mama na baba mama ndo anaongoza kwa mengi!Mama akichelewa kuamka kuna nafasi kubwa ya watoto kuchelewa shule tofauti na baba maana wengi wao hata hawajui watoto wanaendaga shule saa ngapi!!Baba anafanya kazi na kuleta mshahara nyumbani ila muda anaotumia na watoto wake unahesabika...mama nae anaenda kazini akirudi anafanya za nyumbani na bado kiasi kikubwa cha malezi kinamhusu yeye!In most families haya ndo maisha japo kuna zile chache ambazo wazazi wote wanashughulika na watoto equally!!Nimekua kwenye aina zote mbili kwahiyo naujua umuhimu wa baba ila MAMA COMES FIRST!
Kina nani hao ambao wako kama baba? Wajomba? Mababu? Mashemeji? Kina nani hasa?
Nikukimbie wewe!!!!!!!!!
Haiwezi kutokea mpenzi....
Hujanikosea wala sidhani kama unafikiria kufanya hivyo
Nimeamua kuwa kimya nikufatilie kwa umakini,,,lol
Kuonyesha nakupenda nimeandika ki-afro afro:evil:
Dingi ndio mpango mzima, pasipo yeye bia ningeinywea ukubwani, bt kwa kuwa alikua mlevi enzi hzo alijenga mazoea ya kunipeleka bar, huko ndiko nikachukua maujuzi!
Hapo penye rangi, ndo umenena mkuu!
Kutokana na ule upendo mkubwa wa mama kwa watoto wake (kuanzia tumboni hata malezi), ndo maana jamii imesema hakuna kama mama! Na kwa uzoefu wangu mdogo, wababa wengi huwa hawana muda na watoto kabisa, kwahiyo unakuta watoto hawako karibu kabisa na baba yao. Baba anakuwa yeye ni wa kuhakikisha mahitaji muhimu yanapatikana nyumbani., basi. Lakini muda wa kucheza na watoto na kutengeneza mahusiano ya karibu hakuna! Baba anakuwa anaogopwa kweli...mhhhh!!!!!
Lakini najua kabisa wapo wababa wachache ambao watoto wao, watasema...hakuna kama baba, kwasababu wametengeza mahusiano ya karibu na watoto wao. Mtoto anapoumwa, sio kazi ya mama peke yake kukesha au kumwangalia mtoto!
Hayo ni mawazo yangu mimi!
Hakuna aliyepo kama baba yangu. Baba yangu ndo shujaa wangu. Ingawa nampenda mama yangu lakini mapenzi yangu kwa baba yanayazidi yale ya mama. Msiniulize kwa nini. Ni jambo zito sana.
Kwa hiyo hapo utaona kuwa inategemea na uhusiano mtu alionao na mzazi/ wazazi wake. Mimi binti yangu ananipenda kuliko maelezo. Ukimwuliza 'who is your hero?'.....anakujibu bila kusita 'my daddy is my hero'. Kwake ni 'nani kama baba'. Humwambii na humwelezi kitu kuhusu baba yake. She's a daddy's a girl and I savor every bit of it.