Ukichukulia huo msemo literary kua hakuna kama mama na hivyo baba ana umuhimu utakua unakosea njia... Ni kwanini inasemekana hakuna kama mama?
Mama ni kiumbe ambae katika viumbe woote tunamchukulia sana for granted. Huyu mama ndo kakubeba wewe tumboni kwako (hebu naomba u pause kidogo na tafakari hili suala - kua the whole of you, mwili wako huo wote ulitoka ndani ya tumbo lake). Mama ni Mwalimu, rafiki, dakitari, mtabiri, mpenzi wa kweli, dereva na vitu vingine viingi ambavyo naamini hata wewe pia unaelewa. Asprin niseme nini hapa... Nani kama mama ??? Mama anaamini wewe ndo wewe no matter your weakness (sometimes anapalilia hata hizo weakness), Mama anakuambia mwanangu Aprin mimi nakupenda na as long as am still there you will always be safe, sitakubali dunia ikusumbue... Niambie mwanangu; unasema unahitaji niwaongeze wewe na mkeo mtaji - usijali nitaongea na baba....
Baba on the other hand ni nguza yako ya kuegemea, ni jeshi lako la kukimbilia iwapo kuna wasi wasi wowote wa mashambulizi, ni mtu akuoneshae kua hii dunia you can overcome anything ukitumia nguvu, determination, focus na akili. Ni mtu ambae anakusimamie but ikifika wakati wa wewe kusimama anakujulisha kua nawe sasa ni ngazi, anakwambia kabisa kama wewe huna hivi huna nafasi katika hii dunia hivyo jiandae kua defeated - na anakujulisha kua kama utashindwa kua mwanajeshi katika mambo yote yakuzungukayo na kukusumbua basi mi sio commander wako...
Ni wachache saana wamepata bahati ya kupata committed Fathers hata kama wamelelewa nao, but kwa wale woote walojaliwa kulelewa na mama zao ilikua ni rahisi kupata a committed mom though ndio kuna exceptions..