Nani huyu Angellah Jasmine Kairuki

Nani huyu Angellah Jasmine Kairuki

Status
Not open for further replies.
WOS SIO kama watu wanaongea umbeya, nadhani pamoja na mapungufu ya hiyo Lugha lakini kikubwa, watu wanachokiongelea kuwa huyo mtu anaingia kwenye Bunge na Pia Uwaziri (Wizara ya Mama Six) kwa kupitia migongo ya watu, kuanzia kwa mama yake Ester Mkwizu na Rostam Aziz pamoja na Ngereja, tunasema ni kupendelewa mbona wakina Nape wanaangaika wenyewe kwa nguvu zao?
HApa hakuna majungu bali tuaangalia jinsi kikundi cha watu kinavyokuwa na uwezo wa kustructure uongozi wa nchi hii

Kaka Kituko, UMBEA ni taarifa inayotolewa isiyo na uthibitisho na ushaidi.... Mpaka sasa zaidi ya circumstantial connection kwamba mtu huyu anafanya kazi Vodacom, ambapo ametokea Ngeleja na kazaliwa na Esther Mkwizu, hakuna ushahidi wowote wa maana wa kum discredit,

Nashangaa unafanya comparison kati ya Angellah na Nape, ukiangalia kwa msingi wa mtu kupanda kwenye ngazi za siasa kwa jina, basi Nape ana jina kubwa kwenye duru za siasa za TZ kuliko Angellah....NAPE ni mtoto wa Muasisi wa CCM....Nape ni Mjumbe wa NEC, hivyo.....mfano wako haiko relevant kabisa hapa kwamba anaangaika kwa nguvu zake.... Huyu Angellah anaongelewa as if, ni mtoto wa RASHID KAWAWA au KIONGOZI Wa juu MStaafu au aliyepo madarakani..... Mbona hamuongelei majina mengine yaliyomo kwenye orodha ile....Kama sikosei Orodha ina majina 100....laiti....huyu mmoja kakosea nini?

Tufanye uchambuzi...lakiini uwe ni uchambuzi wa substance na sio majungu, lest we categorize ourselves kwenye kundi la SIMPLE MINDS...zinazodiscuss PEOPLE... JAMII FORUM inaundwa na GREAT THINKERS...wanaodiscuss IDEAS kwa kutumia hoja na facts zilizo na uhakika.
 
Ajifunze kuandika basi, sio anajiaibisha kwa maswala madogo yanayoonyesha uvivu na uzembe, wengine watamuona a semi literate nincompoop without a econd glance.

Web image ni kitu muhimu sana, she should know that.

Kama ma lawyer wasomi wenyewe ndio hawa, we really need that Cultural Adjustment Programme.

Kiingereza kina kazi gani bungeni? kama unajua kukisoma na kuelewa cha kuandika kitamsaidia vipi mtanzania?

Nyani Ngabu.
Tangu mwanzo kuandika kiingereza ndilo pungufu kubwa uliloliona. huyu ni mbunge alieenda shule kati ya wengi walioishia darasa la saba. Profesor Maji marefu atakuwa mbunge wetu ifikapo October 30. Tafuta elimu yake uone. CCM wameshindwa kabisa kufanya chochote, kwa taarifa tu, Maji marefu amemshinda mtu makini katika tasnia ya Uhasibu.

Naamini kabisa ukikubali kuwa katikati hutaangaika sana na uwezo wa huyu dada kushindwa kuandika kiingereza, utaangalia zaidi uwezo wake na kumpa nafasi ya kuthibitisha elimu yake kwa vitendo.
 
Mzimu wa Ufisadi ulilipotezea taifa muda wa miaka mitatu bila kujadili mambo ya maendeleo, nashangaa kwamba leo bado mjadala ni RA. We are wasting our precious time kumjadili mtu ambaye kama si mungu kuamua, hakuna litakalobadilika.

Moods, Ni vizuri mada ziwe zinafungwa ili kuendelea na maisha. Topic yoyote yenye neno ufisadi au RA nashauri isipite kwani inatupotezea muda. Kama kungekuwa na manufaa basi wananchi wa Igunga wangemkataa lakini ni kinyume chake.

Respect
 
Naamini kabisa ukikubali kuwa katikati hutaangaika sana na uwezo wa huyu dada kushindwa kuandika kiingereza, utaangalia zaidi uwezo wake na kumpa nafasi ya kuthibitisha elimu yake kwa vitendo.

Kama hayo maandishi ni yake kweli basi kwangu mimi keshashindwa kuthibitisha hiyo elimu yake inayodaiwa kuwa anayo.

Na ni bora aende huko bungeni kwa vilaza wenzake kuliko ku practise law....lawyer gani hajui hata kuandika? Syntax mbovu, punctuation hovyo, diction isiyoeleweka.....lawyer gani huyu?
 
Kama hayo maandishi ni yake kweli basi kwangu mimi keshashindwa kuthibitisha hiyo elimu yake inayodaiwa kuwa anayo.

Na ni bora aende huko bungeni kwa vilaza wenzake kuliko ku practise law....lawyer gani hajui hata kuandika? Syntax mbovu, punctuation hovyo, diction isiyoeleweka.....lawyer gani huyu?

Kaka Hebu nenda Wizara ya sheria tafuta miswaada ya sheria aliyoandika huyo dada ili utoe hukumu yako juu ya writting skills zake...au ukitaka nenda kwenye firm yao pale umpatie kazi ashindwe ndio ujithibitishie kama hana uwezo...la sivyo kwa sasa utaishia ku speculate tu...
 
Ni vigumu sana kuingia kwenye mambo ya siasa Tanzania bila support ya namna fulani.Iwe ni kupitia wazazi, ndugu, jamaa au marafiki, ndivyo hali ilivyo.Huyu dada apewe nafasi kuonyesha atakachowezesha kufanya badala ya kumchambua kama karanga hapa. ( Najua kuna watu wako stand-by kunijibu kwa mashambulizi yasiyo na lazima). Tujiulize swali moja tu: Hivi tukimchambua kuwa ati mama yake anahusiana na wanasiasa wa Tz, Mumewe ni mwanaye marehemu Dr Kairuki, mara ohh ni mwanasheria na mfanyabishara, yote haya yatamzuia kuingia mjengoni? Jibu is so obvious- a resounding NO! Why waste energy and time gossiping about her ( yes it is gossip coz its small talk which is unproductive!).

Tumeshamjua "mbunge mtarajiwa" viti maalum vya wanawake CCM kuwa professionaly ni mwanasheria, pia ni mjasiriamali, ni mke wa mtu, she is young- inatosha.


WoS:

Support ya namna fulani ndiyo ipi? Huyu binti namfahamu vizuri - Hana mchango wowote anaoweza kuupeleka bungeni kusaidia kutetea haki za Wafanyakazi wa Tanzania - Hajui Wafanyakazi wa Tanzania wana matatizo gani - Nimeshekaa naye meza moja tukala tukanywa na kuongea - Upeo wake ni mdogo sana - Yes I mean it! Nafasi wapewe wenye kuonyesha japo uwezo wa kuchambua masuala to a certain degree!

She has reached so far kwa "kubebwa" - she can not stand on her own feet!

Ni makosa kusema inatosha, wakati huyu ni mbunge mteuliwa kupitia viti maalumu - hatuna sehemu ya kumuhoji atatufanyia nini - huyu hatafanya kampeini - anasubiri kuapishwa TU - Sehemu pekee ya yeye kuelewa nini tunahitaji kutoka kwake ni maeneo kama haya - Tukinyamaza na yeye atanyamaza!
 
Mzimu wa Ufisadi ulilipotezea taifa muda wa miaka mitatu bila kujadili mambo ya maendeleo, nashangaa kwamba leo bado mjadala ni RA. We are wasting our precious time kumjadili mtu ambaye kama si mungu kuamua, hakuna litakalobadilika.

Moods, Ni vizuri mada ziwe zinafungwa ili kuendelea na maisha. Topic yoyote yenye neno ufisadi au RA nashauri isipite kwani inatupotezea muda. Kama kungekuwa na manufaa basi wananchi wa Igunga wangemkataa lakini ni kinyume chake.

Respect

You must be kidding!

Hekima = Wisdom (right?)

You have selected the wrong ID!
 
Kaka Hebu nenda Wizara ya sheria tafuta miswaada ya sheria aliyoandika huyo dada ili utoe hukumu yako juu ya writting skills zake...au ukitaka nenda kwenye firm yao pale umpatie kazi ashindwe ndio ujithibitishie kama hana uwezo...la sivyo kwa sasa utaishia ku speculate tu...

I am a million times better than she is on anything you can imagine therefore I won't waste my time....
 
WoS:

Support ya namna fulani ndiyo ipi? Huyu binti namfahamu vizuri - Hana mchango wowote anaoweza kuupeleka bungeni kusaidia kutetea haki za Wafanyakazi wa Tanzania - Hajui Wafanyakazi wa Tanzania wana matatizo gani - Nimeshekaa naye meza moja tukala tukanywa na kuongea - Upeo wake ni mdogo sana - Yes I mean it! Nafasi wapewe wenye kuonyesha japo uwezo wa kuchambua masuala to a certain degree!

She has reached so far kwa "kubebwa" - she can not stand on her own feet!

Ni makosa kusema inatosha, wakati huyu ni mbunge mteuliwa kupitia viti maalumu - hatuna sehemu ya kumuhoji atatufanyia nini - huyu hatafanya kampeini - anasubiri kuapishwa TU - Sehemu pekee ya yeye kuelewa nini tunahitaji kutoka kwake ni maeneo kama haya - Tukinyamaza na yeye atanyamaza!

Ahaa kumbe tunaangaika hapa kumfahamu mgombea huyu wakati Baba ENOCK unamfahamu.....hebu tueleze Mbunge mtarajiwa huyu amefanya kazi miaka mingapi? Ni hoja zipi zimekufanya udhani hawezi kutetea maslahi ya wafanyakazi? Ulipokutana naye kuongea mlikuwa mkiongelea habari za uwakilishi wa wafanyakazi au mlikuwa kwenye kikao cha harusi?

We are very much concerned na mgombea mmoja ambaye ni msomi....tunapoteza muda wa kuwachambua wagombea wengine wa viti maalum kutoka ccm, CHADEMA na CUF ambao si ajabu asilimia kubwa ni wa kidato cha nne.....

Ninahisi mjadala wa mgombea huyu uko personalized......I wouldnt waste my time to fall in this trap ya wanao settle scores zao
 
Mtu akishapewa msaada na RA tu, you must question his/her integrity.

Asikundanganye mtu, RA na EL ndo vinara wa kupachika watu wanaowataka katika serikali ya mbayuwayu. Na siyo kwamba wanawapachika kwa bahati mbaya no.... they will be useful when time comes.

Hii inatosha kumtoa kasoro Angellah!!!

Bye.
 
I am a million times better than she is on anything you can imagine therefore I won't waste my time....

If you think you a million times better than she is....then wewe ungetufaa BUNGENI...ninashauri Ukagombee ili ulisaidie taifa. Angalizo, ukienda huko, usiendeshe mambo kiubabaishaji kama hivi unavyofanya uchambuzi pasipo kuwa na data kamili na kutegemea circumstantial evidence .... tabia za aina hii...ndio zinalipeleka taifa letu pabaya....supposedly, wewe na watu wa aina yako ndio wasomi wetu wenye kujiamini uwezo wao.
 
If you think you a million times better than she is....then wewe ungetufaa BUNGENI...ninashauri Ukagombee ili ulisaidie taifa. Angalizo, ukienda huko, usiendeshe mambo kiubabaishaji kama hivi unavyofanya uchambuzi pasipo kuwa na data kamili na kutegemea circumstantial evidence .... tabia za aina hii...ndio zinalipeleka taifa letu pabaya....supposedly, wewe na watu wa aina yako ndio wasomi wetu wenye kujiamini uwezo wao.

Sipendi siasa na siwafai bungeni.

Na mbabaishaji ni wewe. Mimi nimesema "kama" hayo maandishi ni yake. Sasa 'kama' na wewe hujui maana na matumizi ya neno 'kama', kati yangu na wewe nani mbabaishaji?
 
nyie hamjafahamu tu haya ni malipizo ya Mgaya na TUCTA! katika hao wawili hamna hata mmoja ambaye yuko TUCTA au vyama vya wafanyakazi! CCM imefanya makusudi kuondoa kipengele kilichokuwa kinasema wawakilishi wa wafanyakazi lazma wawe wawakilishi wa vyama vya wafanyakazi yaani kama TUCTA! CCM hawataki nguvu ya TUCTA bungeni!
 
WOS SIO kama watu wanaongea umbeya, nadhani pamoja na mapungufu ya hiyo Lugha lakini kikubwa, watu wanachokiongelea kuwa huyo mtu anaingia kwenye Bunge na Pia Uwaziri (Wizara ya Mama Six) kwa kupitia migongo ya watu, kuanzia kwa mama yake Ester Mkwizu na Rostam Aziz pamoja na Ngereja, tunasema ni kupendelewa mbona wakina Nape wanaangaika wenyewe kwa nguvu zao?
HApa hakuna majungu bali tuaangalia jinsi kikundi cha watu kinavyokuwa na uwezo wa kustructure uongozi wa nchi hii

Mkuu hakika nakubalina nawe 100%. Kuna watanzania wamepoteza kabisa mwelekeo wa kutojitambua kutokna na kushambuliwa na chembechembe za "itikadi, dini, rangi, kabila, tabaka, na hata jinsia!".

Ndio hawa wanaofikia kushindwa kuona hatima yao na watoto wao kwa misingi tu ya kutetea/kupinga jambo ambalo dosari yake inaonekna kwa macho na akili ya kawaida ya mtu.
Haya mambo kujuana na kubebana ndio yameipeleka nchi yetu hapa ilipo na unashangaa hao hao watanzania washindwa kuona matabaka yanayojaribu kutengenezwa katika mfumo wa uongozi wa nchi hii.

Labda tufike wakati tukae kimya tukiamini kuwa "wenye nacho wataongezewa na wale wasio nacho, hata kile kidogo watanyang'anywa".

Hivi kama mfumo tunaoenda nao ni huu wa watoto wa "wakubwa na wenye nazo" kupasiwa kamba na wazazi wao ili waendelee kutawala wale walio masikini, mnadhani mnajenga jamii ya jinsi gani hapo?....Mpime kwa mizani sawa, hivi hawa wabunge walioteuliwa wakitajwa kuwa wanawakilisha makundi fulani (ikiwemo) kundi la wafanyakazi, ni kweli wamepitishwa kwa kuzingatia vigezo sahihi na wanasifa zinazohitajika kuwakisha kundi husika au wamepitishwa kwa kuwa tu wana nguvu ya kiuchumi ndani ya jamii yetu???

Tusizungumzie ushabiki wa itikadi zetu na jinsia katika masuala yaliyo wazi !!

Vuteni taswira ya miaka ishirini ijayo hii nchi itakuwaje, Je, watu kama akina Mizengo Peter Pinda wanaojiita sasa "Watoto wa Wakulima" watathubutu kusimama katika safu ya uongozi wa nchi hii???.

Je, ikiwa mafisadi papa ndio waliowasimika viongozi wenu madarakani, mnatarajia watoto wenu watathbutu kusimama kupingana na maovu yeyote?.

YAPO MENGI MAGUMU YANAKUJA MSIYOWEZA KUYATABIRI SASA!!!
 
Mkuu hakika nakubalina nawe 100%. Kuna watanzania wamepoteza kabisa mwelekeo wa kutojitambua kutokna na kushambuliwa na chembechembe za "itikadi, dini, rangi, kabila, tabaka, na hata jinsia!".

Ndio hawa wanaofikia kushindwa kuona hatima yao na watoto wao kwa misingi tu ya kutetea/kupinga jambo ambalo dosari yake inaonekna kwa macho na akili ya kawaida ya mtu.
Haya mambo kujuana na kubebana ndio yameipeleka nchi yetu hapa ilipo na unashangaa hao hao watanzania washindwa kuona matabaka yanayojaribu kutengenezwa katika mfumo wa uongozi wa nchi hii.

Labda tufike wakati tukae kimya tukiamini kuwa "wenye nacho wataongezewa na wale wasio nacho, hata kile kidogo watanyang'anywa".

Hivi kama mfumo tunaoenda nao ni huu wa watoto wa "wakubwa na wenye nazo" kupasiwa kamba na wazazi wao ili waendelee kutawala wale walio masikini, mnadhani mnajenga jamii ya jinsi gani hapo?....Mpime kwa mizani sawa, hivi hawa wabunge walioteuliwa wakitajwa kuwa wanawakilisha makundi fulani (ikiwemo) kundi la wafanyakazi, ni kweli wamepitishwa kwa kuzingatia vigezo sahihi na wanasifa zinazohitajika kuwakisha kundi husika au wamepitishwa kwa kuwa tu wana nguvu ya kiuchumi ndani ya jamii yetu???

Tusizungumzie ushabiki wa itikadi zetu na jinsia katika masuala yaliyo wazi !!

Vuteni taswira ya miaka ishirini ijayo hii nchi itakuwaje, Je, watu kama akina Mizengo Peter Pinda wanaojiita sasa "Watoto wa Wakulima" watathubutu kusimama???.

Je, ikiwa mafisadi papa ndio waliowasimika viongozi wenu madarakani, mnatarajia watoto wenu watathbutu kusimama kupingana na maovu yeyote?.

YAPO MENGI MAGUMU YANAKUJA MSIYOWEZA KUYATABIRI SASA!!!

Hili tatizo la usultani tumelilea hadi likawa cancer inayotafuna ndani kwa ndani hadi sasa tumetambua when it is too late!
Chunguza toka nchi ipate uhuru ni nani wanatawala?
1. Wengi wana asili ya uchifu huko walikotoka
2. Wengi walipata uongozi kwa kujuana ( cronism and nepotism)
3. Utamaduni umejengeka kwa miaka yote karibia hamsini ya uhuru.

My point is, tusimwangalie Angella tu, tatizo ni systemic na ndio maana wale ambao hawana wa kuwashika mikono kuwavuta wanajifanyia mambo yao wenyewe na kujijengea empire zao kwingineee.
Having said that, simaanishi kuendelea kukumbatia mfumo huu bali tupambane nao strategically na sio kusemasema hapa tu ilhali JF haina uwezo kuwaondoa kwenye hayo mapendekezo ya kuwasimika ubunge.How it should be done, I have no clue, tuwaache wenyewe wenye kujiita mabingwa wa analysis na strategists watupe the HOWS!
 
Wakati tunaiangalia Tanzania yetu katika scope ya miaka mitano au kumi, mafisadi wameshapiga darubini na kuangalia vipi watasalimika miaka 20-30 ijayo. Ndiyo maana sishabikii akina January Makamba kugombea ubunge Bumbuli, au huyu binti tunayemjadilia hapa kupewa nafasi ya ubunge. Mafisadi wameshajipanga. Wanaandaa watu wao kuchukua nafasi za ubunge kulinda madhambi yao katika miongo ijayo na sasa hivi wana harakati za kuhakikisha CCM inasalimika katika uchaguzi mwaka huu na 2015. Kuna kijana mmoja mtangazaji aliajiriwa na VOA mwaka jana. Ameondoka bila kuaga kwa sababu amegombea ubunge huko kwao, na kapitishwa na CCM lakini kafadhiliwa na Manji. I happen to know the young man, hana ideology, hana vision, lakini anafikiria tu shillingi millioni 12 na zaidi atakazolipwa kama mbunge, na kwa bahati aukwae unaibu waziri. Hii ni anatomy ya kuendelezwa kwa utawala wa kifisadi Tanzania. They are already looking and planning ahead.
 
Wakati tunaiangalia Tanzania yetu katika scope ya miaka mitano au kumi, mafisadi wameshapiga darubini na kuangalia vipi watasalimika miaka 20-30 ijayo. Ndiyo maana sishabikii akina January Makamba kugombea ubunge Bumbuli, au huyu binti tunayemjadilia hapa kupewa nafasi ya ubunge. Mafisadi wameshajipanga. Wanaandaa watu wao kuchukua nafasi za ubunge kulinda madhambi yao katika miongo ijayo na sasa hivi wana harakati za kuhakikisha CCM inasalimika katika uchaguzi mwaka huu na 2015. Kuna kijana mmoja mtangazaji aliajiriwa na VOA mwaka jana. Ameondoka bila kuaga kwa sababu amegombea ubunge huko kwao, na kapitishwa na CCM lakini kafadhiliwa na Manji. I happen to know the young man, hana ideology, hana vision, lakini anafikiria tu shillingi millioni 12 na zaidi atakazolipwa kama mbunge, na kwa bahati aukwae unaibu waziri. Hii ni anatomy ya kuendelezwa kwa utawala wa kifisadi Tanzania. They are already looking and planning ahead.

Hapo hapoooooooooo kwenye nyekundu
 
Ndugu zangu habari za siku tele. Nimerejea na kuona hii post hapa nikavutiwa kuchangia. Kwanza kabisa nianze kwa kusema kuwa huyu dada kwa shule tu alizosoma ana uwezo wa kuwa Mbunge mzuri na wa kutetea wanyone watanzania kama tulivyo sisi. Kama kawa Katibu wa Mary Nagu akiwa waziri wa sheria, ni mwanasheria pale chambers basi ni mhitmu mzuri sana wa kwenda kwenye jengo letu la watunga sheria za nchi anatufaa sana. Pili, niseme tu kama kuna mtu kagombea naye akashindwa akaona ni vyema alete topic hii hapa kama njia moja ya kumshambulia..basi mtu ameambulia patupu. Huyu dada anafahamika kwa utendaji uliotukuka serikalini na hata pale Vodacom kwa muda mfupi tu aliokaa. Hana uhusiano wowote na fisadi Rostam, huyu ni mwanadada saaaafi kabisa. sipo hapa kumtetea la hasha ila sifa zake tuu zinatosha muktetea binafsi.

Tatu, nashauri tuwe watu serious wa kuchangia tuache ushabiki husiokuwa wa maana hata kidogo na wala hauna tija. Nia ni kuelimishana. Sasa tutaelimishana vipi kama tupo humu kwa kushambuliana tuu...??? Aidha sioni ni kwa nini watu kama akina Membe waingizwe kwenye mjadala huu, hata mumewe sioni haja hata kidogo. Tuachanae na ushabiki husio kuwa wa manufaa jamani.


Salaam, Ramadhan Kareem
 
Kama ni suala la ufadhili sio kwa Angela Kairuki. Hana haja ya ufadhili wa fedha za mafisadi. Kama wapo ambao wamefadhiliwa na mafisadi na ushahidi tunao, hao ndio wa ku-deal nao hasa. Unafahamu kuna wagombea wengine wameshindwa na nahisi hapa kuna dada mmoja mwandishi wa habari, aliyeshindwa anhusika na majungu haya ya ndugu yetu Angela.... nakuomba kama unahusika achana na majungu na kubali kushindwa
 
Watu kama akina Jnauary Makamba ndio wa kuwaangalia wamefadhiliwa na mafisadi na hilo linafahamika sana. Nani hasiyefahamu kuwa kuna kipindi alionekana Dubai akiwa na Rostam Aziz...??
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom