Nani anastahili tuzo ya Nobel katika marais 6 tuliowahi kuwa nao Tanzania?

Douglas, heading yako inawaaminisha watu tuzo ya Nobel ni kwa marais tu kitu ambacho sio hata ya watani wetu wa Jadi Kenya hapo ilikwenda kwa Mama Wangarĩ Muta Maathai ambaye alikua mwanaharakati wa kijamii, mazingira na siasa then kama mbunge na naibu waziri to add up alikua mwanamke wa kwanza ukanda wa eastern africa kuwa na PhD na Nobel price yake ilikua category ya maendeleo thabiti, demokrasia na amani na mwanamke wa kwanza mwafrika kupata tuzo hiyo.

Hata hivyo ni kweli urais ama nyanja ya siasa hutolewa pia kama ilivyo tokea kwa Obama, Mandela, PM wa Ethiopia ambayo huhusisha mambo ya amani. Nyanja ya siasa/amani haikua lengo kuu la Nobel ingawa iliongezwa na kuwa maarufu kutokana na urafiki wake na Bertha Von Stunner ambaye alikua mwanaharakati wa amani.

Nguli wa kimapinduzi ya Vietnam aliyewahi kuchaguliwa kupewa tuzo na akaikataa ni Lê Đức Thọ. Na mwenzake Henry Kissinger baadae aliigawa charity home na mpunga akaurudisha.

Back to Tanzania, kwa marais wenye chances ni Samia Suluhu, J Kikwete na Mwinyi Mzee as nimewatoa JPM, Mkapa na JKN coz ni marehemu as tangu 1974 Nobel prize hawatoi kwa posthumously yaani wafu unless awe amechaguliwa kabla ya tarehe y kufa na mchakato umekamilika. Wote wangekua hai basi ningefikir JK Nyerere.Why? Kuchangia amani kwa ukanda wa Afrika na dunia enzi za uhuru wa Africa.
Mambo haya yaliishia 1961 kwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani.

Ni kama ilivyoniumaga kwa nini Mahatma Gandhi hakupewa despite kuwa nomiated zaidi ya mara nne. Nahisi hadi leo Nobel Prize Committee wanalijutia.

Siasa ndio ina run dunia no matter hatuwasikii akina Maria Curie na the likes walotufikisha hapa tulipo na gudunzi zao mbali mbali na wakapewa The Nobel Prize.

Nimepanua mjadala kidogo, mleta maada nina imani sijaweka matusi wala uchangiaji wa povu kama ukivoomba ingawa nimetype huku navuta mneri.

Rest In Peace Sir Abel Nobel.



Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
Umetufaa kwa viwango vilivyotukuka. Umepanua uelewa wetu, umeonyesha njia na namna ya kutanua mjadala. Ni kweli tuzo haijasitirika kwa wanasiasa pekee ila hao ndiyo wako kwenye global spotlight kwamba hadi sasa labda hatuna mwanasayansi aliyefanya ugunduzi wa kunyanyua nyusi za dunia.
 
always nyerere ni best, akifuatia na fulan simtaji ili kuondoa kelele za wale majamaa wa upande ule, na kuna vikundi vyakipuuzi hupenda kumbeza nyerer kuwa alifanya mambo ya hovyo ktk sakata la.......,

Hawa watu wanasahau kuwa nyerer alipambana sana kuhakikisha hii nchi inafika ilpofika leo, wakat huo mababa na mababu wa hawa walalamikaji, walikuwa bize maporini wakikimbizana nusu uchi na wanyamapori, sasa matoto yao leo hii yanajiona yamestaharabika wala hayana shukrani kwa wapigania uhuru, yanatusi na kushusha samani ya uhuru na amani hii.
 
Mtemi Hangaya!
Kwa kufuta riba kwenye mikopo ya elimu ya juu, amerejesha Amani kwenye mioyo ya mamimilioni ya watanzania wa kizazi hiki na vizazi vijavyo.
Familia nyingi ziliteseka kutokana na uwezo mdogo wa wazazi kuendesha familia kwa kuwa pesa nyingi zilikuwa zinaenda kwenye marejesho ya mkopo na riba!
Long live chief Hangaya!
Kuna mtazamo (perspective) wa warasimu kwamba riba na marejesho vilitumika kupanua wigo wa kudahili idadi kubwa ya wanafunzi wapya ili wasiendelee kubaki nyumbani. Nini maoni yako zaidi Bemendazole.
 
Kuna mtazamo (perspective) wa warasimu kwamba riba na marejesho vilitumika kupanua wigo wa kudahili idadi kubwa ya wanafunzi wapya ili wasiendelee kubaki nyumbani. Nini maoni yako zaidi Bemendazole.
Sio sawa kukunyang'anya ela yako ili kusomesha mtoto wa mwingine. Kwa nini nguvu yako ilee mtoto wa mwingine? Je wa kwako akikosa mkopo atasomeshwa na nani?
 
Ali Hassan Mwinyi Baba wa demokrasia. Aliondoa mifumo ya kijamaa na kuweka hii ya kisasa..
Na watu hawafahamu, huyu Mzee Mwinyi ni muasisi wa sera NYINGI za hayati Ben, ikiwemo na hiyo TRA. Huyu Mzee alkua mvumilivu lkn mwenye confidence, ssie na papara mwenye kupenda democracy. Huyu NDO aliruhusu vyama vingi, alipokea nchi ikiwa uchumi wake haujatengamaa kutokana na vita. Mambo mengi SANA tunayotumia Hadi Sasa ni kwasababu yake. Mwinyi ni Mwinyi, mwanaume na nusu.
 
Na watu hawafahamu, huyu Mzee Mwinyi ni muasisi wa sera NYINGI za hayati Ben, ikiwemo na hiyo TRA. Huyu Mzee alkua mvumilivu lkn mwenye confidence, ssie na papara mwenye kupenda democracy. Huyu NDO aliruhusu vyama vingi, alipokea nchi ikiwa uchumi wake haujatengamaa kutokana na vita. Mambo mengi SANA tunayotumia Hadi Sasa ni kwasababu yake. Mwinyi ni Mwinyi, mwanaume na nusu.
Kamaradi Ngaiwoye,

Ni Mzee Ruksa huyu ndiyo amemsifia JPM mara kadhaa bila kificho kwamba kafanya mengi mazuri kwa muda mfupi kiasi ambacho akamtamania urefu wa muda wa kukaa ofisini baada ya 2025! Unadhani Mzee Ruksa alikuwa sahihi? Tusaidie Kamaradi wetu.
 
Tuzo ya kimataifa ya Nobel iliyoanzishwa na Bw Alfred Bernhard Nobel, Mswidi mbobezi wa kemia, uhandisi, mvumbuzi, mjasiriamali na mdiakonia (matendo ya huruma (philanthropist)) imetoa tuzo hiyo kwa Wanafizikia watatu kwa mpigo.

Swali:
Katika safu ya marais 6 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unadhani nani kati yao angeweza kustahili tuzo hiyo maarufu?

Kwa sababu zipi?

Kwanini imeshindikana?

Afrika Kusini wana Laureate 3, Liberia 2, DR Congo 1, Ethiopia 1, Kenya 1, Tanzania tumekwama wapi na juhudi zote nzuri za #AMANI YA NCHI, #ULINZI WA AMANI YA DUNIA, #UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA, #MIUNDOMBINU BORA, #MUUNGANO WA PEKEE DUNIANI, #OAU, #KUANZISHWA KWA NON ALIGNED MOVEMENT, #SOUTH SOUTH COMMISSION, #SADC, #EAC, na mengine mengi mazuri kimataifa. Ni Mwl. Nyerere ndiye aliingiza China kwenye kundi la mataifa yenye kura ya turufu katika Umoja wa Mataifa. Aidha alikuwa mmoja wa washauri wa Malkia wa Uingereza lakini hata tuzo ya heshima ya juu Uingereza ya "Sir" hakuwahi kuipewa. Naomba nikope maneno ya Paulo Mtume aliyeuliza hivi "Enyi Wagalatia mmerogwa na nani? Wagalatia.3:1"

Yote hayo na mengine mengi mazuri ya Tz bado Kamati ya Nobel haizioni tu?

Angalizo:
Changia mawazo yako kwa kutuonyesha hekima na busara zako ili tufaidike na maarifa yako, usichangie jazba za kuonyesha kejeli, dharau na matusi, utakuwa umetunyima maarifa yako.

Hata kupendekezwa hawaja pendekezwa bahati mbaya hakuna anaye stahili
 
Yawezekana kilichomkwamisha Mwl kutopewa tuzo ya Nobel ni uamuzi wake binafsi wa kuipiga Uganda, kung'oa na kupandikiza uongozi 1979, uamuzi ambao aliuchukuwa baada ya Jumuiya za Kimataifa kumkalia kimya hata alipoziandikia barua kwamba nchi yake imevamiwa hivyo wachukuwe hatua kumuagiza adui aondoke kwa amani. Kimya cha Jumuiya za Kimataifa huenda kilichukuliwa na Mwl kama muhuri na saini ya Jumuiya hizo kwamba jitetee/jihami, ilhali baada ya uamuzi huo wa Mwl, Jumuiya hizo zikaja kupiga kelele baada ya kuona uwezo wa kivita wa Tz kwamba Mwl ameenda hadi chumbani kwa adui kinyume na mila na desturi za Jumuiya za Kimataifa ambazo Tz iliziridhia kwa kuwa mwanachama. Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilidharau Tz kwamba haina silaha za kumdhibiti adui hivyo Mwl angesurrender na hivyo kusingekuwa na vita au vita vingehamia kwenye meza-mduara za Jumuiya hizo kutafuta suluhu (ambayo huenda Mwl alistukia janja hiyo kwamba labda Jumuiya hizo zilitaka kumpa adui mkoa wa Ziwa Magharibi sasa Kagera), kumbe wasijuwe kwamba yawezekana kweli Mwl hakuwa na silaha lakini kumbe alikuwa na ujuzi, akili na utaalam wa silaha za adui na zile ambazo adui hana na kwamba falsafa ya vita ya Mwl ilikuwa ni stratejia ya kumpiga adui kwa kutumia silaha zake mwenyewe kwa asilimia kubwa. "Vamia, teka, chukuwa, shambulia, songambele" Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilitumia sababu hii kumuona Mwl kwamba hastahili tuzo ya Nobel, kwamba ni mvamizi kama adui alivyokuwa mvamizi pia (Balance of Perspective).

Hiyo ya Mwl ni tofauti na JK ambaye alivamia Anjuan, akang'oa na akakabidhi kwa Comoros KWA KIBALI CHA JUMUIYA ZA KIMATAIFA akiwemo mkoloni Mfaransa.
Mkuu samahani,naomba kuuliza..Hivi wewe unahisi tukipigana na Uganda leo hii 2021 kuna uwezekano kiasi gani wa kuwachapa tena?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama ingehusisha na Mawaziri Wakuu, basi Salim Ahmed Salim angekuwa kashaichukua
Katika mawaziri wakuu waliongoza Tanzania kipindi kifui basi Dr Salim ndiye namba moja kwahiyo uwezekano ni mdogo mno tukija kwa cheo alichokuwa nacho AU pale basi wamarekani wasingekubali maana kwa zile figisu alizofanyiwa na wamarekani baada ya kutaka kugombea ukatibu mkuu wa UN hakika hazikuwa ndogo na pengine angelikua mwafrika wa kwanza kushika wadhifa wa ukatibu mkuu wa UN.
 
Mkuu samahani,naomba kuuliza..Hivi wewe unahisi tukipigana na Uganda leo hii 2021 kuna uwezekano kiasi gani wa kuwachapa tena?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahahaaa swali la mtego hilo mkuu.

Kwa mujibu wa wavuti wa Global Firepower, UG ni 89th,out of 140, ours is ranked 112th. Jiangalizie mwenyewe kwenye link nyingine hapo chini.

Top 20 Most Powerful Militaries In Africa 2016

NB. Nadhani hao wengine wamescore nafasi nzuri kwasababu nchi zao ziko vitani kwa muda mrefu na hivyo wana mafunzo mengi na vifaa bora vingi.
Ila nadhani mara nyingi taarifa hizi zina usiri mkubwa kiasi kwamba wanaokusanya takwimu kwa ajili ya kulinganisha hawapewi taarifa za kutosha.
 
Alitofautiana na Mwl kimantiki. Mwl aliamini maskini kusaidiwa, Big Ben aliamini maskini kutosubiri mana adondoshewe (toka kwenye hazina za serikali au mtu binafsi) bali anayeweka bidii ya kujikwamua akipewa mana katika sura ya sera na sheria, aliamini maskini wa kweli ni aliyenyimwa uwezo wakati wa uumbaji e.g. mwenye mtindio wa ubongo na ulemavu mwingine unaompunguzia thamani ya ubinadamu wake kwa asilimia kubwa sana. Huyo ndiye Big Ben wa Brisbane, Big Ben wa Gleneagles, Big Ben wa Malta, Big Ben wa Doha, Big Ben wa New york (Baraza kuu la Umoja wa mataifa). Mwanzoni kwenye uongozi wake, akihutubia mikutano na makongamano ya kimataifa, wazungu wa Magharibi walidhani hana jipya na walipoteza hamu ya kumsikiliza wakifikiri ni sura B ya Mwl Mjamaa. Baadaye wakaja kukubali kwamba "Don't judge a book by its cover title"

Jitihada za Big Ben na wenzake wengine kama Mh. Thabo Mbeki, Mh. Meles Zenawi, Mh. Olusegun Obasanjo, Mh. Abdelaziz Bouteflika na wengineo wenye nguvu kama za hawa zilisaidia kuundwa kwa tume ya Afrika ya Mh. Tonny Blair Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, tume ambayo pamoja na mambo mengine ilishughulikia suala la mzigo wa madeni ya Afrika na uwezekano wa misaada zaidi kupatikana, tume ambayo ilikuwa ni muhimu sana kwa wakati huo baada ya ule mpango wa muda mrefu wa HIPC kusuasua katika kutimiza malengo yake.

Big Ben aliona suala ambalo wengi hawakuliona au walidhani lisingeweza kuzaa matunda; lile la ni kwa vipi dunia ya tatu ingesimama na kutekeleza malengo ya MDG ya Umoja wa Mataifa bila ya kuziwezesha nchi hizi za dunia ya tatu? Alipambana na kupata kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa baada ya kazi kubwa ya ushawishi akishirikiana na viongozi wenzake hao ambao uwezo na nafasi zao za ushawishi ni mkubwa pia, lengo likiwa ni kuhakikisha nguvu ya pamoja inatumika katika kufikia matarajio.

Big Ben siku zote alipopata dondoo (wazo), hakuibahilia na kuifanya mali-akili yake binafsi (personal intellectual property), isipokuwa aliamini kusema kwa nguvu moja na sauti moja kama wana wa Afrika hivyo alilazimika kushirikiana na viongozi wenzake wa Afrika dondoo hiyo ambayo wangeijenga na baadaye kuipeleka katika ulingo wa kimataifa wakiwa wamoja. Ninamwona kama kiongozi aliyeabudu umoja badala ya ubinafsi. Kwake mafanikio yaliyotokana na yeye aliyafanya kuwa ya umma mzima.
Punguza font mkuu, nimeshindwa kusoma
 
Hahahahaaa swali la mtego hilo mkuu.

Kwa mujibu wa wavuti wa Global Firepower, UG ni 89th,out of 140, ours is ranked 112th. Jiangalizie mwenyewe kwenye link nyingine hapo chini.

Top 20 Most Powerful Militaries In Africa 2016

NB. Nadhani hao wengine wamescore nafasi nzuri kwasababu nchi zao ziko vitani kwa muda mrefu na hivyo wana mafunzo mengi na vifaa bora vingi.
Ila nadhani mara nyingi taarifa hizi zina usiri mkubwa kiasi kwamba wanaokusanya takwimu kwa ajili ya kulinganisha hawapewi taarifa za kutosha.
Wakati wa Nyerere inaonekana tulikuwa pia na intelijensia nzuri sana sisi Tanzania..

Do you think tunao watu sahihi kwenye idara zetu za ujasusu kwa kuangalia mambo yanavyoenda humu nchini na tunavyoshirikiana na nchi za jirani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom