Nani anastahili tuzo ya Nobel katika marais 6 tuliowahi kuwa nao Tanzania?

Ila pia, sina hakika kama Tuzo hii ni ya nchi za Magharibi au ya jumuiya za kimataifa, Alfred B. Nobel ni Mswedish ambayo ni nchi iliyokuwa rafiki wa Tz wakati huo wa mawazo hayo ya Mwl Nyerere yaliyopingwa na Magharibi yalipokuwa yakitoka.

“Having come into contact with a civilization which has over-emphasized the freedom of the inpidual, we are in fact faced with one of the big problems of Africa in the modern world. Our problem is just this: how to get the benefits of European society – benefits that have been brought about by an organization based upon the inpidual — and yet retain African’s own structure of society in which the inpidual is a member of a kind of fellowship.”

Julius Kambarage Nyerere as quoted in the New York Times Magazine on 27 March 1960. -
Yawezekana kilichomkwamisha Mwl kutopewa tuzo ya Nobel ni uamuzi wake binafsi wa kuipiga Uganda, kung'oa na kupandikiza uongozi 1979, uamuzi ambao aliuchukuwa baada ya Jumuiya za Kimataifa kumkalia kimya hata alipoziandikia barua kwamba nchi yake imevamiwa hivyo wachukuwe hatua kumuagiza adui aondoke kwa amani. Kimya cha Jumuiya za Kimataifa huenda kilichukuliwa na Mwl kama muhuri na saini ya Jumuiya hizo kwamba jitetee/jihami, ilhali baada ya uamuzi huo wa Mwl, Jumuiya hizo zikaja kupiga kelele baada ya kuona uwezo wa kivita wa Tz kwamba Mwl ameenda hadi chumbani kwa adui kinyume na mila na desturi za Jumuiya za Kimataifa ambazo Tz iliziridhia kwa kuwa mwanachama. Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilidharau Tz kwamba haina silaha za kumdhibiti adui hivyo Mwl angesurrender na hivyo kusingekuwa na vita au vita vingehamia kwenye meza-mduara za Jumuiya hizo kutafuta suluhu (ambayo huenda Mwl alistukia janja hiyo kwamba labda Jumuiya hizo zilitaka kumpa adui mkoa wa Ziwa Magharibi sasa Kagera), kumbe wasijuwe kwamba yawezekana kweli Mwl hakuwa na silaha lakini kumbe alikuwa na ujuzi, akili na utaalam wa silaha za adui na zile ambazo adui hana na kwamba falsafa ya vita ya Mwl ilikuwa ni stratejia ya kumpiga adui kwa kutumia silaha zake mwenyewe kwa asilimia kubwa. "Vamia, teka, chukuwa, shambulia, songambele" Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilitumia sababu hii kumuona Mwl kwamba hastahili tuzo ya Nobel, kwamba ni mvamizi kama adui alivyokuwa mvamizi pia (Balance of Perspective).

Hiyo ya Mwl ni tofauti na JK ambaye alivamia Anjuan, akang'oa na akakabidhi kwa Comoros KWA KIBALI CHA JUMUIYA ZA KIMATAIFA akiwemo mkoloni Mfaransa.
 
Wewe kweli Kichuguu👍👍👍, ila, siyo kweli kwamba wanafalsafa wanaendelea kuishi hata kama wamekufa? Mawazo yao yanaendelea kusaidia vizazi na vizazi?
... wewe mwenyewe umeonya kejeli halafu mwenyewe unaleta kejeli kwa member! Funny!
 
Ila pia, sina hakika kama Tuzo hii ni ya nchi za Magharibi au ya jumuiya za kimataifa, Alfred B. Nobel ni Mswedish ambayo ni nchi iliyokuwa rafiki wa Tz wakati huo wa mawazo hayo ya Mwl Nyerere yaliyopingwa na Magharibi yalipokuwa yakitoka.

“Having come into contact with a civilization which has over-emphasized the freedom of the inpidual, we are in fact faced with one of the big problems of Africa in the modern world. Our problem is just this: how to get the benefits of European society – benefits that have been brought about by an organization based upon the inpidual — and yet retain African’s own structure of society in which the inpidual is a member of a kind of fellowship.”

Julius Kambarage Nyerere as quoted in the New York Times Magazine on 27 March 1960. -
Yawezekana kilichomkwamisha Mwl kutopewa tuzo ya Nobel ni uamuzi wake binafsi wa kuipiga Uganda, kung'oa na kupandikiza uongozi 1979, uamuzi ambao aliuchukuwa baada ya Jumuiya za Kimataifa kumkalia kimya hata alipoziandikia barua kwamba nchi yake imevamiwa hivyo wachukuwe hatua kumuagiza adui aondoke kwa amani. Kimya cha Jumuiya za Kimataifa huenda kilichukuliwa na Mwl kama muhuri na saini ya Jumuiya hizo kwamba jitetee/jihami, ilhali baada ya uamuzi huo wa Mwl, Jumuiya hizo zikaja kupiga kelele baada ya kuona uwezo wa kivita wa Tz kwamba Mwl ameenda hadi chumbani kwa adui kinyume na mila na desturi za Jumuiya za Kimataifa ambazo Tz iliziridhia kwa kuwa mwanachama. Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilidharau Tz kwamba haina silaha za kumdhibiti adui hivyo Mwl angesurrender na hivyo kusingekuwa na vita au vita vingehamia kwenye meza-mduara za Jumuiya hizo kutafuta suluhu (ambayo huenda Mwl alistukia janja hiyo kwamba labda Jumuiya hizo zilitaka kumpa adui mkoa wa Ziwa Magharibi sasa Kagera), kumbe wasijuwe kwamba yawezekana kweli Mwl hakuwa na silaha lakini kumbe alikuwa na ujuzi, akili na utaalam wa silaha za adui na zile ambazo adui hana na kwamba falsafa ya Mwl ya vita ilikuwa ni stratejia ya kumpiga adui kwa kutumia silaha zake mwenyewe kwa asilimia kubwa. "Vamia, teka, chukuwa, shambulia, songambele" Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilitumia sababu hii kumuona Mwl kwamba hastahili tuzo ya Nobel, kwamba ni mvamizi kama adui alivyokuwa mvamizi pia (Balance of Perspective).

Hiyo ya Mwl ni tofauti na JK ambaye alivamia Anjuan, akang'oa na akakabidhi kwa Comoros KWA KIBALI CHA JUMUIYA ZA KIMATAIFA ikiwemo mkoloni Mfaransa.
 
... wewe mwenyewe umeonya kejeli halafu mwenyewe unaleta kejeli kwa member! Funny!
Kumradhi dudus,

Nimetumia jina lake kama alivyoliandika. Sina hakika kama jina lako laweza kuwa kejeli kwako uliyelichagua. Aidha, kwa sanaa ya lugha, jina hilo la Kichuguu linaelezea aliye juu badala ya aliye chini katika umahiri wa jambo na ndiyo maana nikaweka msisitizo kwamba siyo kejeli kwa kuongezea emoji 3 za "Thumb-up" ambazo maana yake siyo kejeli pia. Otherwise kama na yeye ameelewa hivyo kwamba hilo jina lake nimelirejea kwa kejeli basi kwa fursa hii namtaka radhi. Binafsi naamini tuko vizuri na tuendelee kupata maarifa mengi ya kutujenga.
 
Katika waliokua wana stahili ni mwalimu nyerere, lakini kwangu mwenye na kustahili zaidi ni Benjamin Wiliam mkapa!
Sababu ziko nyingi sana, lakini yule mzee ndie amejenga structure ya nchi yetu, na tutaenda na vision yake kwa kipindi kirefu sana.

Hata atokee nani ajaribu kubadilisha muundo aliyounda mkapa atashindwa tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ali Hassan Mwinyi Baba wa demokrasia. Aliondoa mifumo ya kijamaa na kuweka hii ya kisasa..
 
Nyerere hata kumfikiria wasingemfikiria kwa politics zake za kijamaa ingawaje naamini alikuwa kiongozi mzuri,kwa hawa wazungu ujamaa sio mbaya tuu,ujamaa is considered evil na hawana compromise na hilo, nakumbuka i was in states when Mwalimu passed away, nikaona in one newspaper wameandika Julius Nyerere a long time dictator .......nilishangaa sana na sikuamini nilichoona siku hiyo
 
Katika waliokua wana stahili ni mwalimu nyerere, lakini kwangu mwenye na kustahili zaidi ni Benjamin Wiliam mkapa!
Sababu ziko nyingi sana, lakini yule mzee ndie amejenga structure ya nchi yetu, na tutaenda na vision yake kwa kipindi kirefu sana.

Hata atokee nani ajaribu kubadilisha muundo aliyounda mkapa atashindwa tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa, ni kweli kabisa kwa sababu baada ya Azimio la Arusha kuondoka hatukuwa na dira yoyote (so far nchi imekuwa na dira 3: Uhuru, Azimio la Arusha na hii ya Big Ben ya 2025), lakini Pendael24: baada ya 2025 taifa litahitaji dira nyingine isukwe, achilia zile za Jumuiya za Kimataifa. What if akija kiongozi ambaye atatupa dira kali zaidi ya hii ya Big Ben?
 
Yawezekana kilichomkwamisha Mwl kutopewa tuzo ya Nobel ni uamuzi wake binafsi wa kuipiga Uganda, kung'oa na kupandikiza uongozi 1979, uamuzi ambao aliuchukuwa baada ya Jumuiya za Kimataifa kumkalia kimya hata alipoziandikia barua kwamba nchi yake imevamiwa hivyo wachukuwe hatua kumuagiza adui aondoke kwa amani. Kimya cha Jumuiya za Kimataifa huenda kilichukuliwa na Mwl kama muhuri na saini ya Jumuiya hizo kwamba jitetee/jihami, ilhali baada ya uamuzi huo wa Mwl, Jumuiya hizo zikaja kupiga kelele baada ya kuona uwezo wa kivita wa Tz kwamba Mwl ameenda hadi chumbani kwa adui kinyume na mila na desturi za Jumuiya za Kimataifa ambazo Tz iliziridhia kwa kuwa mwanachama. Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilidharau Tz kwamba haina silaha za kumdhibiti adui hivyo Mwl angesurrender na hivyo kusingekuwa na vita au vita vingehamia kwenye meza-mduara za Jumuiya hizo kutafuta suluhu (ambayo huenda Mwl alistukia janja hiyo kwamba labda Jumuiya hizo zilitaka kumpa adui mkoa wa Ziwa Magharibi sasa Kagera), kumbe wasijuwe kwamba yawezekana kweli Mwl hakuwa na silaha lakini kumbe alikuwa na ujuzi, akili na utaalam wa silaha za adui na zile ambazo adui hana na kwamba falsafa ya vita ya Mwl ilikuwa ni stratejia ya kumpiga adui kwa kutumia silaha zake mwenyewe kwa asilimia kubwa. "Vamia, teka, chukuwa, shambulia, songambele" Yawezekana Jumuiya za Kimataifa zilitumia sababu hii kumuona Mwl kwamba hastahili tuzo ya Nobel, kwamba ni mvamizi kama adui alivyokuwa mvamizi pia (Balance of Perspective).

Hiyo ya Mwl ni tofauti na JK ambaye alivamia Anjuan, akang'oa na akakabidhi kwa Comoros KWA KIBALI CHA JUMUIYA ZA KIMATAIFA akiwemo mkoloni Mfaransa.
labda nobel ya uharo
 
Mbetewa,
Kuna haki za binadamu kisiasa, haki za binadamu kijamii, haki za binadamu kiuchumi, ni kundi lipi unaongelea ili tupate maarifa mkuu.
Magufuli alikuwa mbaya sa kwenye haki za binadamu kisiasa kwa kuanzisha biashara ya kununua Wapinzani.
Mbaya Kwenye haki za kijamii Kwa kuendesha siasa za kibaguzi kikanda na kiukabila.
Mbaya kwenye haki za binadamu kiuchumi kwa kuua bei na masoko ya mazao yetu kama korosho.
So hafai tuzo yoyote zaidi ya kulaaniwa tu ardhini na mbinguni.
 
mwl nyerere ndio rais pakee aliesaini hati za kunyonga watu Sasa hili naona Ni doa
Vipi kama alisaini kwa matakwa ya sheria lakini hakutekeleza unyongaji, hili linaweza kumnyima fursa? Ila kwa ufahamu wangu ni kuwa ukisaini tu lazima utekelezwe, usipotekelezwa ina maana hujasaini. Kwa kumbukumbu zilizopo ni kuwa hakuna hata mmoja aliyesaini hati ya aina hiyo Tz, ndiyo maana wadau wa haki za binadamu wamekuwa wakichagiza kwamba sheria hii ifutwe maana haitekelezwi. Mwenye maarifa zaidi ya haya atusaidie.
 
Magufuli alikuwa mbaya sa kwenye haki za binadamu kisiasa kwa kuanzisha biashara ya kununua Wapinzani.
Mbaya Kwenye haki za kijamii Kwa kuendesha siasa za kibaguzi kikanda na kiukabila.
Mbaya kwenye haki za binadamu kiuchumi kwa kuua bei na masoko ya mazao yetu kama korosho.
So hafai tuzo yoyote zaidi ya kulaaniwa tu ardhini na mbinguni.
Ahsante kwa maarifa yako. Ila siyo kwamba maisha yana sura mbili (chanya na hasi), kwamba kuna upande wa pili wa shilingi wa waliodhulumiwa mali zao kama ardhi, mifugo, waliotolewa jela kwa msamaha kila tulipoadhimisha siku ya uhuru kama walivyofanya pia watangulizi wake kwa mujibu wa sheria, taasisi za kidini zilizopoteza maliwakfu zao na zikarudishiwa. Vipi tukiangalia upande mmoja tu wa shilingi je, kuna mtu duniani atastahili tuzo hiyo na zingine zilizopo duniani? Tuongeze tena maarifa mkuu.
 
Tuzo ya kimataifa ya Nobel iliyoanzishwa na Bw Alfred Bernhard Nobel, Mswidi mbobezi wa kemia, uhandisi, mvumbuzi, mjasiriamali na mdiakonia (matendo ya huruma (philanthropist)) imetoa tuzo hiyo kwa Wanafizikia watatu kwa mpigo.

Swali:
Katika safu ya marais 6 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unadhani nani kati yao angeweza kustahili tuzo hiyo maarufu?

Kwa sababu zipi?

Kwanini imeshindikana?

Afrika Kusini wana Laureate 3, Liberia 2, DR Congo 1, Ethiopia 1, Kenya 1, Tanzania tumekwama wapi na juhudi zote nzuri za #AMANI YA NCHI, #ULINZI WA AMANI YA DUNIA, #UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA, #MIUNDOMBINU BORA, #MUUNGANO WA PEKEE DUNIANI, #OAU, #KUANZISHWA KWA NON ALIGNED MOVEMENT, #SOUTH SOUTH COMMISSION, #SADC, #EAC, na mengine mengi mazuri kimataifa. Ni Mwl. Nyerere ndiye aliingiza China kwenye kundi la mataifa yenye kura ya turufu katika Umoja wa Mataifa. Aidha alikuwa mmoja wa washauri wa Malkia wa Uingereza lakini hata tuzo ya heshima ya juu Uingereza ya "Sir" hakuwahi kuipewa. Naomba nikope maneno ya Paulo Mtume aliyeuliza hivi "Enyi Wagalatia mmerogwa na nani? Wagalatia.3:1"

Yote hayo na mengine mengi mazuri ya Tz bado Kamati ya Nobel haizioni tu?

Angalizo:
Changia mawazo yako kwa kutuonyesha hekima na busara zako ili tufaidike na maarifa yako, usichangie jazba za kuonyesha kejeli, dharau na matusi, utakuwa umetunyima maarifa yako.
Douglas, heading yako inawaaminisha watu tuzo ya Nobel ni kwa marais tu kitu ambacho sio hata ya watani wetu wa Jadi Kenya hapo ilikwenda kwa Mama Wangarĩ Muta Maathai ambaye alikua mwanaharakati wa kijamii, mazingira na siasa then kama mbunge na naibu waziri to add up alikua mwanamke wa kwanza ukanda wa eastern africa kuwa na PhD na Nobel price yake ilikua category ya maendeleo thabiti, demokrasia na amani na mwanamke wa kwanza mwafrika kupata tuzo hiyo.

Hata hivyo ni kweli urais ama nyanja ya siasa hutolewa pia kama ilivyo tokea kwa Obama, Mandela, PM wa Ethiopia ambayo huhusisha mambo ya amani. Nyanja ya siasa/amani haikua lengo kuu la Nobel ingawa iliongezwa na kuwa maarufu kutokana na urafiki wake na Bertha Von Stunner ambaye alikua mwanaharakati wa amani.

Nguli wa kimapinduzi ya Vietnam aliyewahi kuchaguliwa kupewa tuzo na akaikataa ni Lê Đức Thọ. Na mwenzake Henry Kissinger baadae aliigawa charity home na mpunga akaurudisha.

Back to Tanzania, kwa marais wenye chances ni Samia Suluhu, J Kikwete na Mwinyi Mzee as nimewatoa JPM, Mkapa na JKN coz ni marehemu as tangu 1974 Nobel prize hawatoi kwa posthumously yaani wafu unless awe amechaguliwa kabla ya tarehe y kufa na mchakato umekamilika. Wote wangekua hai basi ningefikir JK Nyerere.Why? Kuchangia amani kwa ukanda wa Afrika na dunia enzi za uhuru wa Africa.
Mambo haya yaliishia 1961 kwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani.

Ni kama ilivyoniumaga kwa nini Mahatma Gandhi hakupewa despite kuwa nomiated zaidi ya mara nne. Nahisi hadi leo Nobel Prize Committee wanalijutia.

Siasa ndio ina run dunia no matter hatuwasikii akina Maria Curie na the likes walotufikisha hapa tulipo na gudunzi zao mbali mbali na wakapewa The Nobel Prize.

Nimepanua mjadala kidogo, mleta maada nina imani sijaweka matusi wala uchangiaji wa povu kama ukivoomba ingawa nimetype huku navuta mneri.

Rest In Peace Sir Abel Nobel.



Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Mie ningeigawa katikati kwa Mkapa na Kikwete! Namkubali Nyerere lakini utawala wake sikuushuhudia sana! Mkapa na Kikwete kila mmoja ana mengi mazuri ya kukumbukwa kwa wananchi, Sera nzuri za kiuchumi za Mzee wa Lupaso zilifanya tufutiwe madeni yaliyokuwa mzigo mkubwa na kikwazo cha maendeleo yetu, Mkapa pia alifungua milango mingi ya ajira na kuleta nafuu ya maisha! Kikwete aliboresha sana maisha ya wananchi, Alisaidia sana kuondoa vikwazo vingi vilivyokuwepo kwa wananchi kupata elimu ya juu, ambapo mambo ya urasimu kupitia multriculation yaliondolewa vyuoni, vyuo vya elimu ya juu vingi vilianzishwa! Alitoa mikopo mpaka kwa wanafunzi hewa! Aliajiri kila mwaka na kuna makundi waliingia ajirani moja kwa moja toka vyuoni, adha za kusota vijiweni bila ajira walizipata wachache mno! Alipandisha madaraja na mishahara kila mwaka na zaidi alilipa hadi watumishi hewa, na bado mtaani fedha ilicheza vizuri! Kwa hakika hawa wawili natoa 50/50 ! Mh. Samia Suluhu sio rais mstaafu hivyo hatuwezi kumjaji kwa pamoja na hawa wastaafu, yeye tutamjaji baada ya kumaliza muda wake!
 
Mtemi Hangaya!
Kwa kufuta riba kwenye mikopo ya elimu ya juu, amerejesha Amani kwenye mioyo ya mamimilioni ya watanzania wa kizazi hiki na vizazi vijavyo.
Familia nyingi ziliteseka kutokana na uwezo mdogo wa wazazi kuendesha familia kwa kuwa pesa nyingi zilikuwa zinaenda kwenye marejesho ya mkopo na riba!
Long live chief Hangaya!
 
Back
Top Bottom