Nani anakumbuka David Wakati?

David Wakati alikuwa mzungumzaji wangu sana tukikutana. Nikipenda sana vipindi vyake hasa, "Nipe Habari."

Signature tune ya kiindi hiki ilikuwa nyimbo maarufu, ''South of the Border.''

Katika kipindi hiki cha kila Jumamosi usiku David Wakati alifanya kipindi kilichonigusa sana alipofariki Raymond Chihota Harare na pia alipofariki Mamboleo Rashid Makoko London.

Raymond Chihota alipata kuwa mtangazaji wa TBC katika miaka ya mwanzoni 1960s kabla ya kwenda Urusi kwa masomo ya juu.

Ray kama alivyojulikana alikuwa mmoja wa vijana wa Chipukizi Club pamoja na marehemu Henin Seif, Hussein Shebe, Salum Hiriz kwa kuwataja wachache wakiendesha kipindi kilichopendwa sana na vijana wakati ule wakiwa na bendi wakipiga muziki wa Kizungu wa akina Elvis Presley, Cliff Richard na Beatles.

Kipindi hiki kikirushwa Jumamosi mchana kwa jina la "Chipukizi Club."

David Wakati aliwatia moyo hawa vijana kufanya kipindi kile hadi kilipopigwa marufuku na Regional Commissioner wa Dar es Salaam Mustafa Songambele.

David Wakati alikuwa na kipaji cha hali ya juu cha kueleza mambo na alimweleza vyema Ray Chihota.

Halikadhalika alimweleza Mamboleo Rashid Makoko kwa ukarimu wake kwa Watanzania waliokuwa wanafika London.

Akiwaalika nyumbani kwake na kuwapa kila aina ya msaada.

Mamboleo Rashid Makoko aliondoka Tanganyika mwaka 1958 na hakutaka kurudi. Alirudishwa kwao Tanga kuzikwa.

Namkumbuka David Wakati mwaka wa 1991 wakati akiwa Mkurugenzi wa Radio Tanzania. Serikali ilijikuta ikipambana na Waislam katika suala la elimu.

Waislam waliigeuza Shule ya Muslim kuwa seminari Nyerere akatoa agizo shule irejeshwe katika hali yake ya zamani.

Ugomvi huu ulikuwa umetoka mbali.

Vijana wa Kiislam wakifahamika kama Warsha walikuwa wamejipenyeza ndani ya BAKWATA ili kuibadili. Jukumu lao la kwanza walilojipa ilikuwa kuboresha shule za Kiislam.

Hapa ndipo walipopambana na serikali.

Ili kupinga amri ile ya serikali Warsha ikaitisha mkutano Shule ya Kinondoni agenda kuu ikiwa hali ya elimu ya Waislam Tanganyika toka uhuru.

Mkurugenzi wa RTD David wakati ndiye aliyeingia studio kusoma tangazo la kuwaonya Waislam kutoitika mwito wa mkutano ulioitishwa na Warsha.

David Wakati kwa ile sauti yake nzito ya wastani alisema mkutano huo ni haramu na Waislam watakaohudhuria watakamatwa.

David Wakati akiupenda Ukristo wake na ukitaka kumfaidi ni pale RTD inaporusha matangazo ya moja kwa moja kutoka St. Joseph's Cathedral wakati wa Pasaka au Mkesha wa Christmas yeye akiwa mtangazaji.

Palitokea malalamiko kuwa David Wakati katika moja ya vipindi vyake kaweka ''signature tune,'' nyimbo ya kanisani, yaani ''hymn.''

Alilieleza hili katika kipindi akakana kuwa nyimbo ile ni ya kanisani na akaendelea kuitumia.

Picha: Chipukizi Club waliokaa kulia ni Henin Seif na kushoto ni Hussein Shebe. Kulia aliyesimama ni Raymond Chihota.

Mamboleo Rashid Makoko



Umeuliza nani anamkumbuka David Wakati. Mimi ni mmojawapo. Ni kweli kabisa kwamba hata kipindi David Wakati akiwa Mkurugenzi Mkuu wa Radio Tanzania, bado alikuwa akishiriki kufanya kazi za kawaida za utangazaji. Kipindi cha 'Nipe Habari' hakikuwa na mtangazaji mwingine, mbali na David Wakati; labda awe na udhuru. Asilimia 90 ya vipindi hivyo alikuwa anavitangaza yeye mwenyewe. Ilikuwa kama mtangazaji mwingine akishika zamu inakuwa kama kipindi hakikuwepo siku hiyo. Kinapooza sana. Sawasawa na kipindi cha Majira kutangazwa na mwingine zaidi ya Ben Kiko. Msikilizaji huridhiki. David Wakati pia alikuwa akisoma taarifa za habari za Kiingereza ikijulikana kama Idhaa ya Nje. Nahisi walikuwepo watangazaji wachache tu Radio Tanzania waliokuwa wakikimudu Kiingereza ya kutosha, kama Rochus Matipa. Kwa hiyo ilibidi wapeane zamu hao wachache waliokuwa wanaimanya hiyo lugha. Matangazo kwenye ibaada za Kikristu wakati wa Noeli au Pasaka nayo alikuwa akiyamudu vizuri sana. Yeye alikuwa Anglikana. Lakini alikuwa akienda po pote pale ibaada inapofanyika na anafanya vizuri kabisa; iwe Kanisa Katoliki au la Kiluteri. Mola amlaze pema.
 
Idu...
Usiogope ukweli.

Nikatalie pale una ushahidi kuwa mimi ni muongo.

Niliwahi kufanya mahojiano na Al Jazeera walikuja kunihoji nyumbani kwangu na walivuruga ukumbi wangu wote kwa kupanga sitting room yangu wapate picha na sauti vizuri.

Tanganyika's Independence Struggle topic yetu.

Swali la mwisho walinambia kesho wanakwenda Ikulu kumhoji Rais Kikwete wanaomba kufanya rejea ya maswali yao kutokana na niliyowaeleza na kutaja jina langu.

Niliwaruhusu.
Naamini katika ukweli na haki.

View attachment 1802577

Mahojiano na Al Jazeera 2007

Idu,
Al Jazeera wakaja tena mwaka wa 2008 safari hii mahojiano yetu tulifanya Tanga.

Kwa nini walirudi mara ya pili?

Ukiniuliza nitakujibu In Shaa Allah.

View attachment 1802585
Mzee Mohamed Kwa nini walirudi mara ya pili?
 
Mzee Mohamed Kwa nini walirudi mara ya pili?
Idu...

Tuliishia pale mwisho wa kipindi nilipoulizwa kama mtangazaji anaweza kutafuta ithibati kwa Rais kwa yale niloyosema.

Kwanza kuhusu mchango Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Pili kama kuna ubaguzi dhidi ya Waislamu katika elimu na fursa zilizoko katika serikali na kwengineko.

Na mengineyo mfano wa hayo.

Baadae nikapata taarifa kuwa Al Jazeera walipokuwa Zanzibar vipindi vyoye walivyokuwa wamefanya vilipotea hotelini walipofikia.

Baada ya mwaka karibu wakaja Tanga tukafanya kipindi kingine.
Kipindi hiki hakikurushwa hadi leo na hawakuniambia kwa nini.
 
Idu...

Tuliishia pale mwisho wa kipindi nilipoulizwa kama mtangazaji anaweza kutafuta ithibati kwa Rais kwa yale niloyosema.

Kwanza kuhusu mchango Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Pili kama kuna ubaguzi dhidi ya Waislamu katika elimu na fursa zilizoko katika serikali na kwengineko.

Na mengineyo mfano wa hayo.

Baadae nikapata taarifa kuwa Al Jazeera walipokuwa Zanzibar vipindi vyoye walivyokuwa wamefanya vilipotea hotelini.

Baada ya mwaka kariba wakaja Tanga tukafanya kipindi kingine.

Kipindi hiki hakikurushwa hadi leo na hawakuniambia kwa nini.
Mzee Mohamed unastori nzuri sana ila linapokuja suala la uonevu juu ya waislamu na ubaguzi dhidi ya waislamu hapa Tanzania ndio ukakasi unataokea.
 
Uzalendo...
Mimi ni lazima niheshimu fikra zako.
Huo ndiyo ustaarabu wa mazungumzo.

Hilo la Waislam na ubaguzi wa elimu umelileta wewe na kwa kuwa umelileta naweza ukipenda kukuletea watu wakubwa waliopata kulieleza tena wengine ndani ya vyombo vya serikali: Aboud Jumbe, Prof. Malima, Kitwana Kondo.

Pia waandishi wasomi: P van Bergen, Hamza Njozi, John Sivalon.

Ndugu yangu kuna mengi usiyoyajua.

Vyombo vya habari hivi viwili RTD na The Nationalist na Uhuru chini ya Martin Kiama (RTD), Magazeti ya TANU chini ya Benjamin Mkapa nimekutananayo katika tafiti zangu.

Nayajua vyema.

Nina hakika nikikuwekea niyajuayo utastaajabu.

Nasubiri kauli yako niweke links.
Naona sasa ukiwa kwenye vijiwe vya kahawa mapipa unakenua mpaka jino la mwisho,Samia anateua viongozi wa nchi utasema anateua viongozi wa misikiti na madrasa!

Rais wa hovyo kutokea tangu uhuru,nchi imemshinda inapoelekea Mabeyo achukue nchi!
 
Mzee Mohamed unastori nzuri sana ila linapokuja suala la uonevu juu ya waislamu na ubaguzi dhidi ya waislamu hapa Tanzania ndio ukakasi unataokea.
Idu...
Labda nikuulize swali.

Unadhani haya nisemayo hayana umuhimu au ni uongo?

Nimeweka hapa hotuba ya Kitwana Kondo kuhusu ubaguzi katika elimu.

Nimeweka pia aliyoandika Aboud Jumbe kuhusu udini katika serikali.

Bahati mbaya hili limekuwa jambo nyeti serikali inasikia lakini inaona bora kubaki kimya.

Wewe si wa kuwajibu Waislam kuhusu hili.

Hili ni jukumu la serikali yenyewe kutoa majibu.

Ikiwa hupendi kusikia Waislam wakieleza dhulma iliyodumu dhidi yao toka uhuru hii ni bahati mbaya kwako.

Mimi hili sitaacha kulisema.

Sinong'oni nimasema na nyote mnasoma tena nikitumia jina langu.

Sijajificha kama vile Kitwana Kondo hakujificha na Aboud Jumbe hakujificha.

Allah anawaasa Waislam katika Qur'an anatuambia tusidhulumu na tusikubali kudhulumiwa.
 
Idu...
Labda nikuulize swali.
Unadhani haya nisemayo hayana umuhimu au ni uongo?

Nimeweka hapa hotuba ya Kitwana Kondo kuhusu ubaguzi katika elimu.
Nimeweka pia aliyoandika Aboud Jumbe kuhusu udini katika serikali.

Bahati mbaya hili limekuwa jambo nyeti serikali inasikia lakini inaona bora kubaki kimya.
Wewe si wa kuwajibu Waislam kuhusu hili.

Hili ni jukumu la serikali yenyewe kutoa majibu.

Ikiwa hupendi kusikia Waislam wakieleza dhulma iliyodumu dhidi yao toka uhuru hii ni bahati mbaya kwako.

Mimi hili sitaacha kulisema.
Sinong'oni nimasema na nyote mnasoma tena nikitumia jina langu.

Sijajificha kama vile Kitwana Kondo hakujificha na Aboud Jumbe hakujificha.

Allah anawaasa Waislam katika Qur'an anatuambia tusidhulumu na tusikubali kudhulumiwa.

Idu...
Labda nikuulize swali.
Unadhani haya nisemayo hayana umuhimu au ni uongo?

Nimeweka hapa hotuba ya Kitwana Kondo kuhusu ubaguzi katika elimu.
Nimeweka pia aliyoandika Aboud Jumbe kuhusu udini katika serikali.

Bahati mbaya hili limekuwa jambo nyeti serikali inasikia lakini inaona bora kubaki kimya.
Wewe si wa kuwajibu Waislam kuhusu hili.

Hili ni jukumu la serikali yenyewe kutoa majibu.

Ikiwa hupendi kusikia Waislam wakieleza dhulma iliyodumu dhidi yao toka uhuru hii ni bahati mbaya kwako.

Mimi hili sitaacha kulisema.
Sinong'oni nimasema na nyote mnasoma tena nikitumia jina langu.

Sijajificha kama vile Kitwana Kondo hakujificha na Aboud Jumbe hakujificha.

Allah anawaasa Waislam katika Qur'an anatuambia tusidhulumu na tusikubali kudhulumiwa.
No comment.
 
Idu...
Nafurahi kufanya mjadala nawe.
Mzee Mohamed, kuhusu akina Sykes kama unavyoeleza ni kweli walitoa mchango mkubwa kwenye kupigania uhuru wa taifa letu na kisha TANU ikaanzishwa. Ni kweli pia walikuwa waislamu lakini walijitoa kwa taifa lao sio kwa sababu ni waislamu. Walijitoa kama watanzania kwa nia njema kusaidia taifa lao.

Kama kuna makosa yalitokea wakabaguliwa basi iwekwe wazi walibaguliwa kama akina Sykes na sio sababu ni waislamu.

Hayo mengine weka kando kwanza.
 
Mzee Mohamed, kuhusu akina Sykes kama unavyoeleza ni kweli walitoa mchango mkubwa kwenye kupigania uhuru wa taifa letu na kisha TANU ikaanzishwa. Ni kweli pia walikuwa waislamu lakini walijitoa kwa taifa lao sio kwa sababu ni waislamu. Walijitoa kama watanzania kwa nia njema kusaidia taifa lao.

Kama kuna makosa yalitokea wakabaguliwa basi iwekwe wazi walibaguliwa kama akina Sykes na sio sababu ni waislamu.

Hayo mengine weka kando kwanza.
Idu...
Historia nzima ya Waislam katika kupigania uhuru imefutwa na ilikuwa mtafiti akiwa anakuja Tanzania na akaleza kuwa nia ya utafiti wake inahusu Uislam alikuwa hapati kibali cha utafiti.

Unawajua ni masheikh wangapi walikuwa mstari wa mbele katika TANU?

Hata mmoja hayuko katika historia ilyochapwa mwaka wa 1981 na Chuo Cha CCM Kivukoni.

Unajua historia ya Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika?

Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU, Sheikh Yusuf Badi wa Lindi, Sheikh Abdallah Rashid Sembe wa Tanga kwa kukutajia wachache.

Hii ndiyo sababu ya mimi kutafiti na kuandika kitabu cha Abdul Sykes.
 
Idu...
Historia nzima ya Waislam katika kupigania uhuru imefutwa na ilikuwa mtafiti akiwa anakuja Tanzania na akaleza kuwa nia ya utafiti wake unahusu Uislam alikuwa hapati kibali cha utafiti.

Unawajua ni masheikh wangapi walikuwa mstari wa mbele katika TANU?
Hata mmoja hayuko katika historia ilyochapwa mwaka wa 1981 na Chuo Cha CCM Kivukoni.

Unajua historia ya Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika?

Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU, Sheikh Yusuf Badi wa Lindi, Sheikh Abdallah Rashid Sembe wa Tanga kwa kukutajia wachache.

Hii ndiyo sababu ya mimi kutafiti na kuandika kitabu cha Abdul Sykes.
Naomba ueleweshe umma wa watanzania ili tupate picha kamili
Hawa ndugu zetu walipigania uhuru walipigania uhuru kwa misingi ya dini? Au walishiriki kwa nia njema tupate uhuru?

Na kwa nini historia yao ifutwe?
 
Naomba ueleweshe umma wa watanzania ili tupate picha kamili
Hawa ndugu zetu walipigania uhuru walipigania uhuru kwa misingi ya dini? Au walishiriki kwa nia njema tupate uhuru?

Na kwa nini historia yao ifutwe?
Idu...
Labda ujiulize wewe mwenyewe.

Kimetokea nini nchi ikaaminishwa historia siyo?

Ukipata majibu hayo yaliyobakia yatakuwa mepesi kueleweka.
 
Idu...
Labda ujiulize wewe mwenyewe.

Kimetokea nini nchi ikaaminishwa historia siyo?

Ukipata majibu hayo yaliyobakia yatakuwa mepesi kueleweka.
Mzee Mohamed, kabla hatujapata ukweli halisi juu ya nchi kuaminishwa historia ambayo sio, tunatakiwa tujue ukweli. Je, hawa ndugu zetu ambao wengi walijitolea kupigania uhuru huku wakiwa na imani ya Kiislamu walipigania uhuru kwa misingi ya dini?

Mzee Mohamed pamoja kuwa unadai tumekaririshwa historia ambayo sio, lakini watanzania mpaka leo wanatambua ndio historia sahihi
 
Nakumbuka siku aliyomrithi mtangulizi na akiwa bosi wake Paulo Sozigwa ndiyo siku ambayo wanawake walianza kutangaza taarifa ya habari RTD.

Paulo Sozigwa hakutaka wanawake wasome taarifa ya habari.
 
Sikuelewa historia uliyotaka kuleta hapa ila kweli mimi nilikuwa mfuasi sana wa David Wakati, na wakati bado nafundisha UDSM nilimfundisha mtoto wake mmoja aliyekuwa akiitwa Mandela Wakati na nilihudhuria graduation yake ambapo nilikaribishwa na Mandela mwenyewe na kunikutanisha na bab yake David.

Mkuu ulifundisha UDSM miaka gani na idara ipi? Just out of interest!
 
Nilifundisha engineering kuanzia 1987 hadi 1994; mimi siyo mtoto wa jana!

Nimeamini wewe sio wa jana ulifundisha na professors Awadh Mawenya na Silas Lwakabanba!!!!
Afadhali, vijana watambue kuwa humu wako na babu zao!!!
 
Nimeamini wewe sio wa jana ulifundisha na professors Awadh Mawenya na Silas Lwakabanba!!!!
Afadhali, vijana watambue kuwa humu wako na babu zao!!!
Lwakabamba alikuwa anafundisha Thermodynamics wakati Mawenya alikuwa anafundisha Foundation Engineering; Lwakabamba wakati anaondoka kwenda Nigeria ndiye aliyemwachia Masuha (RIP) nafasi ya kuwa Dean wa FoE.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom