Inakuwaje Mwanahistoria Anapokutana Njiani na Kizazi Cha Chief Marealle na Chief Maruma Wote Kwa Wakati Mmoja?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,264
INAKUWAJE MWANAHISTORIA ANAPOKUTANA NJIANI NA KIZAZI CHA CHIEF MAREALLE NA CHIEF MARUMA WOTE KWA WAKATI MMOJA?

Kuna mengi yasiyofahamika katika historia ya uhusiano waliokuwanao machifu wa Tanganyika na raia wa kawaida.

Halikadhalika na viongozi waliokuwa katika harakati za TANU za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Bahati mbaya sana machifu wenyewe wamekuwa kimya sana kusema lolote kuhusi kipindi hiki cha historia hata pale wanaposingiziwa yale ambayo hawakufanya.

Inawezekana hii ni kwa sababu za adabu za watawala kuwa kwa hadhi zao na kulinda heshima zao hawawezi kujiingiza katika ubishi.

Nimebahatika kusoma barua za Paramount Chief Thomas Marealle alizokuwa akiandikiana na Ally Sykes katika Nyaraka za Sykes na vilevile kuelezwa urafiki uliokuwapo baina ya Chief Thomas Marealle na Abdul Sykes na mdogo wake Ally katika miaka ya 1950.

Barua hizi zinasisimua.
Naamini iko siku watafiti watazifikia na kuandika.

Nimeelezwa habari za Chief Thomas Marealle na Ally Sykes na pia na Mwalimu Sakina bint Arab.

Mwalimu Sakina anasema kuwa kuwa siku zote Abdul akikutana na Marealle, Abdul akimwambia Marealle kuwa yeye ni ''King'' si Chief lakini Waingereza hawataki kumwita hivyo kwa kuwa wakifanya hivyo King George mfalme wao watamwitaje?

Mimi katika nikiishi jirani na David Marealle, Masaki lakini hatukupata kufahamiana kwa karibu.

Siku moja Abbas Sykes alikuja nyumbani kwangu na akaniomba nimsindikize nyumbani kwa David Marealle.

David Marealle alikuwa na nyumba nzuri sana katika nyumba zilizojengwa Masaki miaka ile.

David Marealle akaniambia kuwa mara yake ya kwanza kufika Dar es Salaam katika miaka ya mwishoni 1940 au mapema 1950 alifikia nyumbani kwa Abdul Sykes na hapo ndipo alipofahamiana na Abbas Sykes ambae umri wao ulikuwa umelingana.

Urafiki wao ulianza hapo.

David Marealle alipofariki Abbas Sykes alihudhuria mazishi yake halikadhalika alipofariki Chief Thomas Marealle.

Nakumbuka aliporudi kutoka maziko ya Chief Thomas Marealle aliniambia kuwa kakutana na David Marealle lakini afya yake si njema.

Leo nimekutana na Peter Marealle na yeye akanisalimia na akajitambulisha.

Mimi nilikuwa natoka benki na yeye ndiyo anaingia.
Tumekutana mlangoni.

Wakati tunasalimian mara akawa anakuja Harold Maruma akanitambulisha kwake na kumwambia kuwa mimi nina mengi niyajuayo kuhusu wao.

Hivi ndivyo mazungumzo yetu yalivyoanza.

Hii ilikuwa bahati kubwa sana kwangu.

Nikawafahamisha kuwa nina mengi ya wazee wao na nimefahamiana na ndugu zao wengine hapa Dar es Salaam sote tukiwa wanafunzi sekondari na wengine Chuo Kikuu: Philip Marealle, Kibo Marealle, Janet Marealle na Winston Maruma.

Historia ina kawaida ya kujirudia.

Kibo Marealle alikuja nyumbani kwangu Tanga ameongozana na Abraham Sykes na ndiyo siku tukafahamiana.

Nikawapiga picha hiyo hapo chini.

Baba zao walikuwa marafiki na wao watoto wamekuja kuwa marafiki.

Kibo alipofariki ni Abraham ndiye aliyenipa taarifa ya msiba.

Winston Maruma yeye alikuwa rubani.

Nilikutananae Maputo mwaka wa 1990, Ujamaa House baada ya kupoteana.

(Niliambiwa kuwa jumba hili refu Samora Machel aliwapa Tanzania siku Msumbiji ilipopata uhuru kwa kuiambia Tanzania wachague jengo lolote yeye atawapa bure na hapa Ujamaa House ndipo ulipo ubalozi wa Tanzania, Msumbiji).

Ilikuwa wakati wa Kombe la Dunia na Watanzania wengi walikuwa pale wanatazama mpira.

Winston Maruma tukakutana tena siku moja mwaka wa 2004 uwanja wa ndege wa zamani mimi nikitafuta ndege ya haraka kwenda Zanzibar.

Bahati mbaya sana nilikutana na mabwana Marealle na Maruma wao wakiingia benki mimi natoka.

Hatukuwa na muda wa kuongea sana.

''They made my day,'' kama wasemavyo Waingereza.

PICHA: Picha ya kwanza machifu watatu na majina yao.

Picha ya pili kulia ni Peter Marealle kushoto ni Harold Maruma na picha ya tatu kulia ni Abraham Sykes na Kibo Marealle.

Picha ya nne ni Mangi Mkuu Thomas Marealle.

1708035436328.png

1708035482742.png

1708035513734.png

1708035572532.jpeg



 
Usisahau siku nyingine uje na habari za Mangi maarufu kuliko wote Chief Mwamba wa miamba yote Mangi Sina wa Kibosho
 
Usisahau siku nyingine uje na habari za Mangi maarufu kuliko wote Chief Mwamba wa miamba yote Mangi Sina wa Kibosho
Wadiz,
Nimeandika kitabu: ''Rajabu Ibrahim Kirama Jemedari wa Vita Kuwa Jemedari wa Uislamu,'' (2020).

Katika kitabu hiki nimemtaja Mangi Sina mara 37 katika kitabu cha kurasa 104.

Siwezi kuandika habari zake zote hapa kwani makala itakuwa ndefu sana lakini nitakuwekea baadhi ya vipande vya matukio muhimu yanayomuhusu Mangi Sina ambae wewe umemwita ''Mangi Maarufu kuliko wote.''

''Mtoto Sina alitekwa katika vita lakini askari kwa huruma ya kuona ule umri wake; inakisiwa alikuwa hajafika hata miaka kumi; walishindwa kunyanyua sime kumtumbukiza tumboni kumuua.

Waliamua kumchukua hadi kwa Mangi Ndeseruo ili hayo mauaji ikiwa atapenda ayafanye yeye mwenyewe kwa mikono yake.

Mangi Ndeseruo hakumuua Sina alimpenda sana huyu mtoto na akaishi nae ndani ya nyumba yake kama mwanaye.

Sina akaja kuwa Jemadari wa Vita katika utawala wa Mangi Ndeseruo na yaliyotokea baadaye sasa ni historia ya kusisimua kwani alipopata umri alimtawaza kuwa Mangi wa Kibosho na akampa jukumu la kuhakikisha kuwa atakapokufa ahakikishe kuwa mwanaye wa pili Shangali ndiye anakuwa Mangi wa Machame badala ya kaka yake mkubwa Ngamini...

Mangi Sina aliingiza jeshi lake kushambulia Machame akidai kuwa Shangali atawazwe kuwa Mangi.

Abisai Temba katika kitabu chake ‘Three Hundred Years On Kilimanjaro Mountain Area’, Juzuu ya 1 anaeleza kuwa Ngamini aliuawa katika vita hivi.

Lakini mjukuu wa Ngamini, Mama Ali anasema babu yake alikwenda uhamishoni Old Moshi pamoja na Jemadari wake wa Vita, Muro Mboyo.

Taarifa nyingine zinaeleza kuwa Mangi Sina alipovamia Machame, Ngamini yeye mwenyewe aliamua kuachia madaraka na kuondoka Machame.

Waandishi wengi wa historia ya vita hii, hawamtaji Muro Mboyo kama mtu muhimu kwa Ngamini na mtu aliyenusuru maisha yake.

Kama itakavyokuwa Mangi Ngamini na Jemadari wake waliwafanikiwa kuondoka Machame na wakafika Old Moshi kwa Mangi Rindi Mandara salama salimini.

Mangi Mandara aliwapokea vyema Ngamini na Muro Mboyo na akawakatia ardhi ili waanze maisha mapya.

Ngamini akapewa ardhi Mbokomu na Muro Mboyo alibakia Old Moshi sehemu inayojulikana kama Tela. Mangi Renguo na Mangi Rindi walikuwa na uhusiano mzuri na huko nyuma walipigana vita vingi na nchi nyingine kwa kuunganisha majeshi yao.

Ikumbukwe kuwa Mangi Renguo alikuwa mtawala wa mwanzo kabisa kupokea fikra na mpango wa Sisya Mshau Nkya wa kuunganisha majeshi ya watawala wote wa Uchaggani kwa ajili ya kujihami na maadui.

Hii inaonesha kuwa Mangi Rindi alikuwa anatambua nguvu ya umoja na bila shaka aliwapokea viongozi hawa wawili kwa msimamo wake uleule kuwa viongozi wale huenda iko siku wakaja kumfaa.

Baada ya vita, Shangali akatawazwa mwaka wa 1890, kama alivyotaka baba yake Mangi Ndeseruo na kuwa Mangi akiwa mtoto mdogo kabisa wa umri wa miaka 13.

Mama Ali anaeleza kuwa baada ya vita hii Ngulelo mdogo wake Ngamini akapelekwa Kismayu na Wajerumani kwa kusudio la kunyongwa lakini hili halikufanyika na alirejea Machame Muislam baada ya kusilimu akiwa huko na akachagua jina la Selemani.

Taarifa nyingine zinasema kuwa Ngulelo hakupelekwa Kismayu bali alipelekwa kifungoni Lamu na haikuwa kwa kusudio la kunyongwa bali kifungoni na huko ndiko alikosilimu na kuwa Muislam.

Vita viliendelea kwingi Uchaggani na hili liliwaudhi sana Wajerumani na wakaamua kuwakamata viongozi wote isipokuwa wachache na kuwanyonga hadharani.

Shangali aliponea chupuchupu baada ya kuombewa na Mmishionari Emil Muller ambaye utetezi wake kwa Mangi Shangali ilikuwa alitoa msaada mkubwa kwa Wamishionari wa Liepzig Mission.

Tutakuja kuona hapo baadaye jinsi mwanaye Mangi Shangali, Abdiel Shangali atakavyokuja kupambana na mtoto wa Muro Mboyo, Rajabu Ibrahim Kirama pale atakapoingiza Uislamu Machame bila shaka akikumbuka hisani ambayo Wamishionari walimfanyia baba yake kumuokoa kwenye kitanzi cha Wajerumani...''
(Kutoka kitabu cha Rajabu Ibrahim Kirama)

1708054770988.png

 
Wadiz,
Nimeandika kitabu: ''Rajabu Ibrahim Kirama Jemedari wa Vita Kuwa Jemedari wa Uislamu,'' (2020).

Katika kitabu hiki nimemtaja Mangi Sina mara 37 katika kitabu cha kurasa 104.

Siwezi kuandika habari zake zote hapa kwani makala itakuwa ndefu sana lakini nitakuwekea baadhi ya vipande vya matukio muhimu yanayomuhusu Mangi Sina ambae wewe umemwita ''Mangi Maarufu kuliko wote.''

''Mtoto Sina alitekwa katika vita lakini askari kwa huruma ya kuona ule umri wake; inakisiwa alikuwa hajafika hata miaka kumi; walishindwa kunyanyua sime kumtumbukiza tumboni kumuua.

Waliamua kumchukua hadi kwa Mangi Ndeseruo ili hayo mauaji ikiwa atapenda ayafanye yeye mwenyewe kwa mikono yake.

Mangi Ndeseruo hakumuua Sina alimpenda sana huyu mtoto na akaishi nae ndani ya nyumba yake kama mwanaye.

Sina akaja kuwa Jemadari wa Vita katika utawala wa Mangi Ndeseruo na yaliyotokea baadaye sasa ni historia ya kusisimua kwani alipopata umri alimtawaza kuwa Mangi wa Kibosho na akampa jukumu la kuhakikisha kuwa atakapokufa ahakikishe kuwa mwanaye wa pili Shangali ndiye anakuwa Mangi wa Machame badala ya kaka yake mkubwa Ngamini...

Mangi Sina aliingiza jeshi lake kushambulia Machame akidai kuwa Shangali atawazwe kuwa Mangi.

Abisai Temba katika kitabu chake ‘Three Hundred Years On Kilimanjaro Mountain Area’, Juzuu ya 1 anaeleza kuwa Ngamini aliuawa katika vita hivi.

Lakini mjukuu wa Ngamini, Mama Ali anasema babu yake alikwenda uhamishoni Old Moshi pamoja na Jemadari wake wa Vita, Muro Mboyo.

Taarifa nyingine zinaeleza kuwa Mangi Sina alipovamia Machame, Ngamini yeye mwenyewe aliamua kuachia madaraka na kuondoka Machame.

Waandishi wengi wa historia ya vita hii, hawamtaji Muro Mboyo kama mtu muhimu kwa Ngamini na mtu aliyenusuru maisha yake.

Kama itakavyokuwa Mangi Ngamini na Jemadari wake waliwafanikiwa kuondoka Machame na wakafika Old Moshi kwa Mangi Rindi Mandara salama salimini.

Mangi Mandara aliwapokea vyema Ngamini na Muro Mboyo na akawakatia ardhi ili waanze maisha mapya.

Ngamini akapewa ardhi Mbokomu na Muro Mboyo alibakia Old Moshi sehemu inayojulikana kama Tela. Mangi Renguo na Mangi Rindi walikuwa na uhusiano mzuri na huko nyuma walipigana vita vingi na nchi nyingine kwa kuunganisha majeshi yao.

Ikumbukwe kuwa Mangi Renguo alikuwa mtawala wa mwanzo kabisa kupokea fikra na mpango wa Sisya Mshau Nkya wa kuunganisha majeshi ya watawala wote wa Uchaggani kwa ajili ya kujihami na maadui.

Hii inaonesha kuwa Mangi Rindi alikuwa anatambua nguvu ya umoja na bila shaka aliwapokea viongozi hawa wawili kwa msimamo wake uleule kuwa viongozi wale huenda iko siku wakaja kumfaa.

Baada ya vita, Shangali akatawazwa mwaka wa 1890, kama alivyotaka baba yake Mangi Ndeseruo na kuwa Mangi akiwa mtoto mdogo kabisa wa umri wa miaka 13.

Mama Ali anaeleza kuwa baada ya vita hii Ngulelo mdogo wake Ngamini akapelekwa Kismayu na Wajerumani kwa kusudio la kunyongwa lakini hili halikufanyika na alirejea Machame Muislam baada ya kusilimu akiwa huko na akachagua jina la Selemani.

Taarifa nyingine zinasema kuwa Ngulelo hakupelekwa Kismayu bali alipelekwa kifungoni Lamu na haikuwa kwa kusudio la kunyongwa bali kifungoni na huko ndiko alikosilimu na kuwa Muislam.

Vita viliendelea kwingi Uchaggani na hili liliwaudhi sana Wajerumani na wakaamua kuwakamata viongozi wote isipokuwa wachache na kuwanyonga hadharani.

Shangali aliponea chupuchupu baada ya kuombewa na Mmishionari Emil Muller ambaye utetezi wake kwa Mangi Shangali ilikuwa alitoa msaada mkubwa kwa Wamishionari wa Liepzig Mission.

Tutakuja kuona hapo baadaye jinsi mwanaye Mangi Shangali, Abdiel Shangali atakavyokuja kupambana na mtoto wa Muro Mboyo, Rajabu Ibrahim Kirama pale atakapoingiza Uislamu Machame bila shaka akikumbuka hisani ambayo Wamishionari walimfanyia baba yake kumuokoa kwenye kitanzi cha Wajerumani...''
(Kutoka kitabu cha Rajabu Ibrahim Kirama)

Hakika umenena historia njema kabisa thanks, at some stage I will be buying such books for my library
 
Braza...
Jaribu kuuliza kwenye maduka ya vitabu.
sawa.

Hiyo system ya uchifu mimi naona ni afadhali mzee Nyerere alivoamua kuifutilia mbali yaani mtu anachaguliwa kuwaongoza eti tu kwa sababu tu ya kuzaliwa kwa ukoo wa chifu hata kama ni bogus amejaza maji kichwani mwake. huyu mzee
Nyerere ana makosa yake lakini kwa jambo hili aliwatendea haki pakubwa sana watzania.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom