Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,916
- 30,259
David Wakati alikuwa mzungumzaji wangu sana tukikutana. Nikipenda sana vipindi vyake hasa, "Nipe Habari."
Signature tune ya kiindi hiki ilikuwa nyimbo maarufu, ''South of the Border.''
Katika kipindi hiki cha kila Jumamosi usiku David Wakati alifanya kipindi kilichonigusa sana alipofariki Raymond Chihota Harare na pia alipofariki Mamboleo Rashid Makoko London.
Raymond Chihota alipata kuwa mtangazaji wa TBC katika miaka ya mwanzoni 1960s kabla ya kwenda Urusi kwa masomo ya juu.
Ray kama alivyojulikana alikuwa mmoja wa vijana wa Chipukizi Club pamoja na marehemu Henin Seif, Hussein Shebe, Salum Hiriz kwa kuwataja wachache wakiendesha kipindi kilichopendwa sana na vijana wakati ule wakiwa na bendi wakipiga muziki wa Kizungu wa akina Elvis Presley, Cliff Richard na Beatles.
Kipindi hiki kikirushwa Jumamosi mchana kwa jina la "Chipukizi Club."
David Wakati aliwatia moyo hawa vijana kufanya kipindi kile hadi kilipopigwa marufuku na Regional Commissioner wa Dar es Salaam Mustafa Songambele.
David Wakati alikuwa na kipaji cha hali ya juu cha kueleza mambo na alimweleza vyema Ray Chihota.
Halikadhalika alimweleza Mamboleo Rashid Makoko kwa ukarimu wake kwa Watanzania waliokuwa wanafika London.
Akiwaalika nyumbani kwake na kuwapa kila aina ya msaada.
Mamboleo Rashid Makoko aliondoka Tanganyika mwaka 1958 na hakutaka kurudi. Alirudishwa kwao Tanga kuzikwa.
Namkumbuka David Wakati mwaka wa 1991 wakati akiwa Mkurugenzi wa Radio Tanzania. Serikali ilijikuta ikipambana na Waislam katika suala la elimu.
Waislam waliigeuza Shule ya Muslim kuwa seminari Nyerere akatoa agizo shule irejeshwe katika hali yake ya zamani.
Ugomvi huu ulikuwa umetoka mbali.
Vijana wa Kiislam wakifahamika kama Warsha walikuwa wamejipenyeza ndani ya BAKWATA ili kuibadili. Jukumu lao la kwanza walilojipa ilikuwa kuboresha shule za Kiislam.
Hapa ndipo walipopambana na serikali.
Ili kupinga amri ile ya serikali Warsha ikaitisha mkutano Shule ya Kinondoni agenda kuu ikiwa hali ya elimu ya Waislam Tanganyika toka uhuru.
Mkurugenzi wa RTD David wakati ndiye aliyeingia studio kusoma tangazo la kuwaonya Waislam kutoitika mwito wa mkutano ulioitishwa na Warsha.
David Wakati kwa ile sauti yake nzito ya wastani alisema mkutano huo ni haramu na Waislam watakaohudhuria watakamatwa.
David Wakati akiupenda Ukristo wake na ukitaka kumfaidi ni pale RTD inaporusha matangazo ya moja kwa moja kutoka St. Joseph's Cathedral wakati wa Pasaka au Mkesha wa Christmas yeye akiwa mtangazaji.
Palitokea malalamiko kuwa David Wakati katika moja ya vipindi vyake kaweka ''signature tune,'' nyimbo ya kanisani, yaani ''hymn.''
Alilieleza hili katika kipindi akakana kuwa nyimbo ile ni ya kanisani na akaendelea kuitumia.
Picha: Chipukizi Club waliokaa kulia ni Henin Seif na kushoto ni Hussein Shebe. Kulia aliyesimama ni Raymond Chihota.
Mamboleo Rashid Makoko
Signature tune ya kiindi hiki ilikuwa nyimbo maarufu, ''South of the Border.''
Katika kipindi hiki cha kila Jumamosi usiku David Wakati alifanya kipindi kilichonigusa sana alipofariki Raymond Chihota Harare na pia alipofariki Mamboleo Rashid Makoko London.
Raymond Chihota alipata kuwa mtangazaji wa TBC katika miaka ya mwanzoni 1960s kabla ya kwenda Urusi kwa masomo ya juu.
Ray kama alivyojulikana alikuwa mmoja wa vijana wa Chipukizi Club pamoja na marehemu Henin Seif, Hussein Shebe, Salum Hiriz kwa kuwataja wachache wakiendesha kipindi kilichopendwa sana na vijana wakati ule wakiwa na bendi wakipiga muziki wa Kizungu wa akina Elvis Presley, Cliff Richard na Beatles.
Kipindi hiki kikirushwa Jumamosi mchana kwa jina la "Chipukizi Club."
David Wakati aliwatia moyo hawa vijana kufanya kipindi kile hadi kilipopigwa marufuku na Regional Commissioner wa Dar es Salaam Mustafa Songambele.
David Wakati alikuwa na kipaji cha hali ya juu cha kueleza mambo na alimweleza vyema Ray Chihota.
Halikadhalika alimweleza Mamboleo Rashid Makoko kwa ukarimu wake kwa Watanzania waliokuwa wanafika London.
Akiwaalika nyumbani kwake na kuwapa kila aina ya msaada.
Mamboleo Rashid Makoko aliondoka Tanganyika mwaka 1958 na hakutaka kurudi. Alirudishwa kwao Tanga kuzikwa.
Namkumbuka David Wakati mwaka wa 1991 wakati akiwa Mkurugenzi wa Radio Tanzania. Serikali ilijikuta ikipambana na Waislam katika suala la elimu.
Waislam waliigeuza Shule ya Muslim kuwa seminari Nyerere akatoa agizo shule irejeshwe katika hali yake ya zamani.
Ugomvi huu ulikuwa umetoka mbali.
Vijana wa Kiislam wakifahamika kama Warsha walikuwa wamejipenyeza ndani ya BAKWATA ili kuibadili. Jukumu lao la kwanza walilojipa ilikuwa kuboresha shule za Kiislam.
Hapa ndipo walipopambana na serikali.
Ili kupinga amri ile ya serikali Warsha ikaitisha mkutano Shule ya Kinondoni agenda kuu ikiwa hali ya elimu ya Waislam Tanganyika toka uhuru.
Mkurugenzi wa RTD David wakati ndiye aliyeingia studio kusoma tangazo la kuwaonya Waislam kutoitika mwito wa mkutano ulioitishwa na Warsha.
David Wakati kwa ile sauti yake nzito ya wastani alisema mkutano huo ni haramu na Waislam watakaohudhuria watakamatwa.
David Wakati akiupenda Ukristo wake na ukitaka kumfaidi ni pale RTD inaporusha matangazo ya moja kwa moja kutoka St. Joseph's Cathedral wakati wa Pasaka au Mkesha wa Christmas yeye akiwa mtangazaji.
Palitokea malalamiko kuwa David Wakati katika moja ya vipindi vyake kaweka ''signature tune,'' nyimbo ya kanisani, yaani ''hymn.''
Alilieleza hili katika kipindi akakana kuwa nyimbo ile ni ya kanisani na akaendelea kuitumia.
Picha: Chipukizi Club waliokaa kulia ni Henin Seif na kushoto ni Hussein Shebe. Kulia aliyesimama ni Raymond Chihota.
Mamboleo Rashid Makoko