Nani anakumbuka David Wakati?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,916
30,259
David Wakati alikuwa mzungumzaji wangu sana tukikutana. Nikipenda sana vipindi vyake hasa, "Nipe Habari."

Signature tune ya kiindi hiki ilikuwa nyimbo maarufu, ''South of the Border.''

Katika kipindi hiki cha kila Jumamosi usiku David Wakati alifanya kipindi kilichonigusa sana alipofariki Raymond Chihota Harare na pia alipofariki Mamboleo Rashid Makoko London.

Raymond Chihota alipata kuwa mtangazaji wa TBC katika miaka ya mwanzoni 1960s kabla ya kwenda Urusi kwa masomo ya juu.

Ray kama alivyojulikana alikuwa mmoja wa vijana wa Chipukizi Club pamoja na marehemu Henin Seif, Hussein Shebe, Salum Hiriz kwa kuwataja wachache wakiendesha kipindi kilichopendwa sana na vijana wakati ule wakiwa na bendi wakipiga muziki wa Kizungu wa akina Elvis Presley, Cliff Richard na Beatles.

Kipindi hiki kikirushwa Jumamosi mchana kwa jina la "Chipukizi Club."

David Wakati aliwatia moyo hawa vijana kufanya kipindi kile hadi kilipopigwa marufuku na Regional Commissioner wa Dar es Salaam Mustafa Songambele.

David Wakati alikuwa na kipaji cha hali ya juu cha kueleza mambo na alimweleza vyema Ray Chihota.

Halikadhalika alimweleza Mamboleo Rashid Makoko kwa ukarimu wake kwa Watanzania waliokuwa wanafika London.

Akiwaalika nyumbani kwake na kuwapa kila aina ya msaada.

Mamboleo Rashid Makoko aliondoka Tanganyika mwaka 1958 na hakutaka kurudi. Alirudishwa kwao Tanga kuzikwa.

Namkumbuka David Wakati mwaka wa 1991 wakati akiwa Mkurugenzi wa Radio Tanzania. Serikali ilijikuta ikipambana na Waislam katika suala la elimu.

Waislam waliigeuza Shule ya Muslim kuwa seminari Nyerere akatoa agizo shule irejeshwe katika hali yake ya zamani.

Ugomvi huu ulikuwa umetoka mbali.

Vijana wa Kiislam wakifahamika kama Warsha walikuwa wamejipenyeza ndani ya BAKWATA ili kuibadili. Jukumu lao la kwanza walilojipa ilikuwa kuboresha shule za Kiislam.

Hapa ndipo walipopambana na serikali.

Ili kupinga amri ile ya serikali Warsha ikaitisha mkutano Shule ya Kinondoni agenda kuu ikiwa hali ya elimu ya Waislam Tanganyika toka uhuru.

Mkurugenzi wa RTD David wakati ndiye aliyeingia studio kusoma tangazo la kuwaonya Waislam kutoitika mwito wa mkutano ulioitishwa na Warsha.

David Wakati kwa ile sauti yake nzito ya wastani alisema mkutano huo ni haramu na Waislam watakaohudhuria watakamatwa.

David Wakati akiupenda Ukristo wake na ukitaka kumfaidi ni pale RTD inaporusha matangazo ya moja kwa moja kutoka St. Joseph's Cathedral wakati wa Pasaka au Mkesha wa Christmas yeye akiwa mtangazaji.

Palitokea malalamiko kuwa David Wakati katika moja ya vipindi vyake kaweka ''signature tune,'' nyimbo ya kanisani, yaani ''hymn.''

Alilieleza hili katika kipindi akakana kuwa nyimbo ile ni ya kanisani na akaendelea kuitumia.

Picha: Chipukizi Club waliokaa kulia ni Henin Seif na kushoto ni Hussein Shebe. Kulia aliyesimama ni Raymond Chihota.

Mamboleo Rashid Makoko



 
Hii inaitwa "click bait", maudhui yanaashiria mlengo wako.

Na umesahau kuandika kuwa hicho kipindi kilikuwa kinaisha kwa wimbo mmoja maarufu wa "kila Mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe".....wimbo wa kwaya ya Arusha Mjini.
 
Sikuelewa historia uliyotaka kuleta hapa ila kweli mimi nilikuwa mfuasi sana wa David Wakati, na wakati bado nafundisha UDSM nilimfundisha mtoto wake mmoja aliyekuwa akiitwa Mandela Wakati na nilihudhuria graduation yake ambapo nilikaribishwa na Mandela mwenyewe na kunikutanisha na baba yake David.
 
Sikuelewa historia uliyotaka kuleta hapa ila kweli mimi nilikuwa mfuasi sana wa David Wakati, na wakati bado nafundisha UDSM nilimfundisha mtoto wake mmoja aliyekuwa akiitwa Mandela Wakati na nilihudhuria graduation yake ambapo nilikaribishwa na Mandela mwenyewe na kunikutanisha na bab yake David.
Sitaki kukoment maana Mzee Mohamed inaonekana ana yake ya kipekee.
 
Mzee lengo halisi haikuwa kuzungumzia mazuri ya David Wakati

Ulikusudia kusema Waislamu walibaguliwa na kunyimwa elimu kwa makusudi na Serikali

Ulikusudia kusema RTD ilishabikia udini hasa Ukiristo chini ya David Wakati wakati sio kweli

Hisia za udini ni sawasawa na maradhi sugu yasiyo na tiba
 
Sikuelewa historia uliyotaka kuleta hapa ila kweli mimi nilikuwa mfuasi sana wa David Wakati, na wakati bado nafundisha UDSM nilimfundisha mtoto wake mmoja aliyekuwa akiitwa Mandela Wakati na nilihudhuria graduation yake ambapo nilikaribishwa na Mandela mwenyewe na kunikutanisha na bab yake David.
Kichuguu,
Historia niliyokusudia ni vipi David Wakati nilimfahamu kwa yake mengi.

Nikianza kwa urafiki wetu na muingiliano wake na watu niliowafahamu mimi mfano wa Hussein Shebe kijana mdogo wakati ule hajazidi miaka 15 lakini kipaji chake cha kuimba kilikuwa kikubwa.

Hussein yuko Ulaya miaka mingi na aliposoma makala hii kaniletea ujumbe akimshukuru David Wakati kwa yale aliyowafanyia.

Nilitaka pia kumueleza David Wakati katika sakata la Shule ya Kinondoni 1991 mimi pia nikihusika jinsi lile tangazo alilosoma RTD nilivyotutia ari ya kupambananalo.

Hapa pana historia nzuri ukipenda nitaiweka hapa In Shaa Allah.

Kwa ufupi hupata, "inspiration," pale mtu anaponikumbusha yaliyopita na hapo ndipo nami huyaleta yote ya kipindi kile.

Picha hiyo hapo chini mimi na Hussein Shebe nyumbani kwangu.

Akija Dar tukikutana humuomba aniimbie tukikumbushana mengi.

Sisi sasa ni wazee.

20210530_121753.jpg
 
Sikuelewa historia uliyotaka kuleta hapa ila kweli mimi nilikuwa mfuasi sana wa David Wakati, na wakati bado nafundisha UDSM nilimfundisha mtoto wake mmoja aliyekuwa akiitwa Mandela Wakati na nilihudhuria graduation yake ambapo nilikaribishwa na Mandela mwenyewe na kunikutanisha na bab yake David.
Kichuguu,
Historia niliyokusudia ni vipi David Wakati nilimfahamu kwa yake mengi.

Nikianza kwa urafiki wetu na muingiliano wake na watu niliowafahamu mimi mfano wa Hussein Shebe kijana mdogo wakati ule hajazidi miaka 15 lakini kipaji chake cha kuimba kilikuwa kikubwa.

Hussein yuko Ulaya miaka mingi na aliposoma makala hii nakaniletea ujumbe akimshukuru David Wakati kwa yale aliyowafanyia.

Nilitaka pia kumueleza David Wakati katika sakata la Shule ya Kinondoni 1991 mimi pia nikihusika jinsi lile tangazo alilosoma RTD nilivyotutia ari ya kupambananalo.

Hapa pana historia nzuri ukipenda nitaiweka hapa In Shaa Allah.

Kwa ufupi hupata inspiration pale mtu anaponikumbusha yaliyopita na hapo ndipo nami huyaleta yote ya kipindi kile.
 
Sitaki kukoment maana Mzee Mohamed inaonekana ana yake yakipekee.
Idu...
Mimi nalichukulia hili baraza kama mahali pa kustarehe.

Sijui kwa nini wewe unatabika.

Lete comments uhangaishe kichwa changu nije na stori ambazo pengine hujazisikia.
 
Sitaki kukoment maana Mzee Mohamed inaonekana ana yake yakipekee.
Idu...
Mimi nalichukulia hili baraza kama mahali pa kustarehe.

Sijui kwa nini wewe unatabika.

Lete comments uhangaishe kichwa changu nije na stori ambazo pengine hujazisikia.
 
Hii inaitwa "click bait".....maudhui yanaashiria mlengo wako.

Na umesahau kipindi kilikuwa kinaisha kwa wimbo mmoja maarufu wa "kila Mtu atauchukua mzigo wake mwenyewe".....wimbo wa kwaya ya Arusha Mjini.
May Day,
Ahsante sana.
 
Idu...
Mimi nalichukulia hili baraza kama mahali pa kustarehe.

Sijui kwa nini wewe unatabika.

Lete comments uhangaishe kichwa changu nije na stori ambazo pengine hujazisikia.
Mzee Mohamed sio kama nahangaika, una hadithi nzuri sana lakini unaharibu...
 
Mzee lengo halisi haikuwa kuzungumzia mazuri ya David Wakati

Ulikusudia kusema Waislamu walibaguliwa na kunyimwa elimu kwa makusudi na Serikali

Ulikusudia kusema RTD ilishabikia udini hasa Ukiristo chini ya David Wakati wakati sio kweli

Hisia za udini ni sawasawa na maradhi sugu yasiyo na tiba
Uzalendo...

Mimi ni lazima niheshimu fikra zako.

Huo ndiyo ustaarabu wa mazungumzo.

Hilo la Waislam na ubaguzi wa elimu umelileta wewe na kwa kuwa umelileta naweza ukipenda kukuletea watu wakubwa waliopata kulieleza tena wengine ndani ya vyombo vya serikali: Aboud Jumbe, Prof. Malima, Kitwana Kondo.

Pia waandishi wasomi: P van Bergen, Hamza Njozi, John Sivalon.

Ndugu yangu kuna mengi usiyoyajua.

Vyombo vya habari hivi viwili RTD na The Nationalist na Uhuru chini ya Martin Kiama (RTD), Magazeti ya TANU chini ya Benjamin Mkapa nimekutananayo katika tafiti zangu.

Nayajua vyema.

Nina hakika nikikuwekea niyajuayo utastaajabu.

Nasubiri kauli yako niweke links.
 
Mzee Mohamed sio kama nahangaika, una hadithi nzuri sana lakini unaharibu...
Idu...
Usiogope ukweli.

Nikatalie pale una ushahidi kuwa mimi ni muongo.

Niliwahi kufanya mahojiano na Al Jazeera walikuja kunihoji nyumbani kwangu na walivuruga ukumbi wangu wote kwa kupanga sitting room yangu wapate picha na sauti vizuri.

Tanganyika's Independence Struggle topic yetu.

Swali la mwisho walinambia kesho wanakwenda Ikulu kumhoji Rais Kikwete wanaomba kufanya rejea ya maswali yao kutokana na niliyowaeleza na kutaja jina langu.

Niliwaruhusu.
Naamini katika ukweli na haki.

1622374815672.png


Mahojiano na Al Jazeera 2007

Idu,
Al Jazeera wakaja tena mwaka wa 2008 safari hii mahojiano yetu tulifanya Tanga.

Kwa nini walirudi mara ya pili?

Ukiniuliza nitakujibu In Shaa Allah.

1622375049868.png
 
Idu...
Usiogope ukweli.

Nikatalie pale una ushahidi kuwa mimi ni muongo.

Niliwahi kufanya mahojiano na Al Jazeera walikuja kunihoji nyumbani kwangu na walivuruga ukumbi wangu wote kwa kupanga sitting room yangu wapate picha na sauti vizuri.

Tanganyika's Independence Struggle topic yetu.

Swali la mwisho walinambia kesho wanakwenda Ikulu kumhoji Rais Kikwete wanaomba kufanya rejea ya maswali yao kutokana na niliyowaeleza na kutaja jina langu.

Niliwaruhusu.
Naamini katika ukweli na haki.
Ingekuwa kipindi cha Magufuli ungewaruhusu wakutaje,kuwa mkweli hapo
 
Uzalendo...
Mimi ni lazima niheshimu fikra zako.
Huo ndiyo ustaarabu wa mazungumzo.

Hilo la Waislam na ubaguzi wa elimu umelileta wewe na kwa kuwa umelileta naweza ukipenda kukuletea watu wakubwa waliopata kulieleza tena wengine ndani ya vyombo vya serikali: Aboud Jumbe, Prof. Malima, Kitwana Kondo.

Pia waandishi wasomi: P van Bergen, Hamza Njozi, John Sivalon.

Ndugu yangu kuna mengi usiyoyajua.

Vyombo vya habari hivi viwili RTD na The Nationalist na Uhuru chini ya Martin Kiama (RTD), Magazeti ya TANU chini ya Benjamin Mkapa nimekutananayo katika tafiti zangu.

Nayajua vyema.

Nina hakika nikikuwekea niyajuayo utastaajabu.

Nasubiri kauli yako niweke links.
Itakuwa vema ukiweka hadharani hayo uyajuayo ili tupate jua yaliyojificha kama kweli yapo
 
Ingekuwa kipindi cha Magufuli ungewaruhusu wakutaje,kuwa mkweli hapo
Mdukuzi,
Kwa nini unaniuliza swali hilo?
Una maana kuwa ningeogopa?

Sasa labda mimi si wa kulijibu swali hilo.
Fikra uliyojenga ni kuwa mimi ni muoga.

Acha wengine wanijibie.
 
Mdukuzi,
Kwa nini unaniuliza swali hilo?
Una maana kuwa ningeogopa?

Sasa labda mimi si wa kulijibu swali hilo.
Fikra uliyojenga ni kuwa mimi ni muoga.

Acha wengine wanijibie.
Sio wewe tu watanzania wote tulinyamazishwa kipindi cha jpm kasoro mtu mmoja tu.
 
Sio wewe tu watanzania wote tulinyamazishwa kipindi chaA
Mimi katika maisha yangu yote nimekuwa ni mtu wa kuandika na ninapoombwa huzungumza katika hadhira tofauti iwe radio au TV.

Hapo chini ni kipindi katika vipindi vingi nilivyofanya na Azam TV:


file:///C:/Users/yemen/Pictures/Mohamed%20Said_%20AZAM%20TV%20KIPINDI%20MAALUM%20CHA%20MASHUJAA%20WA%20UHURU%20WA%20TANGANYIKA.html

Nilikuwa na blog: mohamedsaidsalum.blogspot unaweza kutembelea na kuangalia kama nilisimama kuandika na kuzugumza.


 
Itakuwa vema ukiweka hadharani hayo uyajuayo ili tupate jua yaliyojificha kama kweli yapo
Uzalendo,
Naweka baadhi:


''Lakini tuende kielimu. Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine. Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe. Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79. Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21.

Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu. Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga. Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha. Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini.''

(Hotuba ya Mh. Kitwana Kondo (MB) aliyoitoa Bungeni Dodoma, 1999)


Mohamed Said: ABOUD JUMBE ALIPOZUNGUMZA TATIZO LA UDINI TANZANIA 1992
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom