Nani aliyemuumba Mungu?

Nani aliyemuumba Mungu?

Sijakuelewa unapoandika "dhamira ya swali "nini" haikai katika Jina au Sifa ya chenye Elimu.
Hakuna sehemu niliyo andika "Dhamira". Ongeza umakini.

Tena ongeza katika kauli ya kitu chenye akili, au maarifa.
Swali lina dhamira au anayeuliza swali ndiye ana dhamira?
Sijakusudia "Dhamira" kwa maana ya lengo, nimeandika "Dhamiri".
Rekebisha kunitaka nirekebishe swali!
Naona unajitia ujuaji kwenye hakuna, hapo nimeandika "Dhamiri" na si "Dhamira". Ninayajia maneno haya kindakindaki, na nilichokiandika nina maanisha.

Nakuoa nafasi nyingine ya kuwa rekebisha swali lako, kisha nikujibu swali.

Nipo...
 
Waamuzi sura ya 13
Unakubali au unaamini vipi haya yaliyoandikwa humu ni ya kweli ?

Swali : Ni nani aliyeandika hizi habari ? Nipo katika msingi wa habari, ili tujue ni za kwelo au la, kisha tujadili matini sasa.
 
Sioni mantiki ya swali hili.

Kwa sababu jibu lolote nitakalolitoa, niwe nimepatia au nimekosea, niwe naweza kujibu swali au siwezi kujibu swali, halithibitishi uwepo wa Mungu.

Na kama halithibitishi uwepo wa Mungu, sioni mantiki ya swali hili.

Swali hili halina tofauti na mimi kukuuliza wewe, thibitisha 1 + 1 =2, halafu wewe uniulize, kabla ya yote, nieleze mimi ni nini.

Logical non sequitur.

Mimi nikiweza kueleza mimi ni nini, nikatoa jibu zuri kabisa, hilo litathibitishaje Mungu yupo?

Au, mimi nikishindwa kueleza mimi ni nini, hilo linathibitishaje Mungu yupo?

Lakini, kwanini upoteze muda wako kuchangia mawazo kuhusu 'kitu' ambacho wewe unaamini kuwa hakipo?
 
Hawezi kukujibu sana sana atakimbilia kwenye idea za watu wengine - zile logical fallacy
Hili ndiyo tatizo lao, hawawezi kufikiri nje ya mawazo ya Wakubwa zao, ambao no wajinga mno.

Pili, huyu yuko nyuma sana, leo hii bado anajifaragua na Logic/Ilm al Kalaam/Ilm Mantiq (Mantiki) ,elimu ambayo ni dhaifu na kwa yenyewe haiwezi kukupa ukweli.
 
Lakini, kwanini upoteze muda wako kuchangia mawazo kuhusu 'kitu' ambacho wewe unaamini kuwa hakipo?
Swali hili ni zuri sana.

Sipotezi muda, tunaelezana, tunajadiliana, tunaelimishana.

Ngoja niongee kwa mfano, labda utanielewa vizuri zaidi.

Tuchukulie kuna ugonjwa, mbaya sana , unaua. Hauna dawa wala kinga.

Ugonjwa huu unaenezwa kirahisi sana. Tuseme kwa kujamiiana bila kinga.

Halafu, wakaja watu wawili, mmoja tapeli, mwingine mjinga tu.

Yule tapeli anasema anayo dawa ya huo ugonjwa. Anawauzia watu miti tu ambayo si dawa, anapiga pesa ndefu.

Yule mjinga, yeye hapendi tu kuishi kwa hofu, anafuata upepo kusema ugonjwa una dawa, dawa ni ule mtishamba anaouza yule tapeli.

Sasa wewe daktari, umehakikisha kabisa ule mtishamba hautibu ugonjwa.

Na katika maadili yako ya kidaktari, una wajibu wa kuwaelimisha watu, kwamba jamani eeh, hiyo inayoitwa dawa si dawa, ni utapeli tu.

Sasa, katika habari hii, mimi ni kama huyo daktari, Mungu - dawa ya uongo- ni kama huo mtishamba, na hapa kuna matapeli wenye makanisa yao, viongozi wa kisiasa, mashehe etc, wanaouza hiyo dawa ya mtishamba kwa utapeli. Na kuna waumini wanaoamini tu kama bendera kufuata upepo, kwa ujinga.

Sasa, swali uliloniuliza ni sawa na umuulize yule daktari.

Wewe daktari, huamini hii dawa, unasema dawa haipo, sasa kwa nini unapoteza muda wako kupinga dawa ambayo haipo?

Ukweli ni kwamba, daktari huyu asipoelimisha wenzake, ile dawa feki itaua watu. Kutokuwepo kwa dawa maana yake si kwamba hakuna madhara.Watu watafanya ngono zembe, wakijua kuna dawa, tukiumwa tutapata dawa. Watu watapoteza hela zao nyingi kununua dawa isiyoponya kitu.

Hii habari ya dawa ya uongo, ni vizuri imulikwe ili watu wasipoteze maisha, wasipoteze mali zao, wasiishi maisha ya kufuata habari za uongo.

Kutokuwepo kwa Mungu kunaweza kuleta madhara kama watu wataaminishwa Mungu yupo, watafanywa waishi kwa kufuatisha imani ya uongo, watachukuliwa mali zao kwenye imani hiyo ya uongo. Wataishi kwa hofu ya kwenda motoni maisha yao yote, kwa kufuata imani hiyo ya uongo, watashindwa kujiamini wenyewe na kuchukua majukumu ya maisha yao wenyewe, kwa sababu ya imani ya uongo.

Sipingi Mungu ambaye hayupo.

Napinga imani potofu ya kuamini Mungu yupo, ambayo inaweza kuwa na madhara kama imani ya kuwa dawa ya uongo isiyoponya inaponya.
 
Hawezi kukujibu sana sana atakimbilia kwenye idea za watu wengine - zile logical fallacy
Mbona nishamjibu hapo juu, umesoma jibu langu?

Nikikuuliza bei ya kilo ya nguruwe China hapa unaweza kunijibu?
 
Unakubali au unaamini vipi haya yaliyoandikwa humu ni ya kweli ?

Swali : Ni nani aliyeandika hizi habari ? Nipo katika msingi wa habari, ili tujue ni za kwelo au la, kisha tujadili matini sasa.
Unataka emperical proof kwenye mambo ambayo ni spritual? Ulishawahi kuota ndoto? Kama ulishawahi kuota, mtu akija kwako leo halafu akakuambia kuwa unadanganya hujawahi kuota ndoto, wakati ukweli ni kuwa ulishawahi kuota na mpaka leo huwa unaota; katika hali kama hiyo how are you going to prove to the person kwamba ni kweli huwa unaota? So you want emperical scientific proof kwenye spritual science, si ndiyo? Umesoma? Uliwahi kusoma somo linaitwa reserach methodology? Huwa wanafanyaje watafiti, kulingana na mawaidha ya somo hili?
 
Nafikiri nimekujibu kuhusu Mungu ni nini. Ni wajibu wako kuchunguza jibu hilo, ili kujibu swali hili ulilouliza hapa.
Hujajibu swali hili.

"Kwa hiyo Mungu naye anafikiri, anathibitisha, anachunguza, anakataa?"
 
Unataka emperical proof kwenye mambo ambayo ni spritual?
Unauliza swali ambalo halilo. Jibu swali nililo kuuliza.
Ulishawahi kuota ndoto?
Ndiyo nimeota sana na nina endelea kuota.
Kama ulishawahi kuota, mtu akija kwako leo halafu akakuambia kuwa unadanganya hujawahi kuota ndoto, wakati ukweli ni kuwa ulishawahi kuota na mpaka leo huwa unaota;
Huu mfano wako ni mfano mfu, sababu suala la ndoto ni suala la kimaumbile na si la hiyari la mtu kuamua au kinyume chake. Bali suala hili wote tunakubaliana ya kuwa lipo. Ila suala ulilo longelea ni la watu fulani na ni wajibu wako kutupa ushahidi
katika hali kama hiyo how are you going to prove to the person kwamba ni kweli huwa unaota?
Jaribu kujenga hoja au kuuliza swali linalo endana na uhalisia. Kwanza huwezi kuulizwa swali la namna hiyo, sababu swali lako la uongo.
So you want emperical scientific proof kwenye spritual science, si ndiyo? Umesoma?
Mimi nataka ushahidi, na ninapo kuuliza au kutaka uniambia nani muandishi wa hizo habari ujue ya kuwa habari hizo hazijajiandika zenyewe bali yupo aliye andika, sasa uniambie ili tuanzie hapo kujua ukweli wa habari hizi.

Scientific Proof ni kwa mambo ya Sayansi, na ushahidi wa kidini ni ithibati ya hakika na uhalisia, bali shahidi za kidini huwa madhubuti mno kuzidi shahidi za kisayansi kwa mambo ya kisayansi. Kwahiyo usichanganye mambo ya Kisayansi na kuyapa hadhi ya ithibati kuliko mengine, huu ni ufinyu wa maarifa.
Uliwahi kusoma somo linaitwa reserach methodology?
Somo hili nililisoma, na miongoni mwa vitabu nilivyo soma ni "The Etiquette of Research and Debate"
Huwa wanafanyaje watafiti, kulingana na mawaidha ya somo hili?
Hili swali sijaona umuhimu wake wala haja ya kulijibu.
 
Huu mfano wako ni mfano mfu, sababu suala la ndoto ni suala la kimaumbile na si la hiyari la mtu kuamua au kinyume chake. Bali suala hili wote tunakubaliana ya kuwa lipo. Ila suala ulilo longelea ni la watu fulani na ni wajibu wako kutupa ushahidi
Hujanielewa. Sala hapa nilikuwa nataka kukuthibitishia kuwa swala la kuota huwa linafanyika kwenye ulimwengu wa roho, kiasi kwamba huwezi uka-prove kwa mtu mwingine kwamba huwa unaota, kwa kutumia empirical tools, kwa sababu they (emperical) do not work in the spritual world, so are spritual tools in the empirical realm
 
Kabla hufajika huko jiulize huu ulimwengu na sayari zote zimetokea wapi? eti ziko hewani tu zinazunguka jua na hazigongani zenyewe kwa zenyewe miaka mabillion kwa mabillion.... eti jua nalo limetegenezwa kwa madini gani ambayo yanatoa joto kali bila madini hayo kuisha miaka mabillion kwa mabillion..
 
Majibu yapo katika vitabu vyake..... Wewe unakuja kutuuliza upuuzi gani hapa....?!

Matoto ya siku hizi laana mnazitafuta katika umri mdogo sana. Na hapo unakuta mahudhurio ya nyumba za ibada ni zero tupu...
 
Unauliza swali ambalo halilo. Jibu swali nililo kuuliza.

Ndiyo nimeota sana na nina endelea kuota.

Huu mfano wako ni mfano mfu, sababu suala la ndoto ni suala la kimaumbile na si la hiyari la mtu kuamua au kinyume chake. Bali suala hili wote tunakubaliana ya kuwa lipo. Ila suala ulilo longelea ni la watu fulani na ni wajibu wako kutupa ushahidi

Jaribu kujenga hoja au kuuliza swali linalo endana na uhalisia. Kwanza huwezi kuulizwa swali la namna hiyo, sababu swali lako la uongo.

Mimi nataka ushahidi, na ninapo kuuliza au kutaka uniambia nani muandishi wa hizo habari ujue ya kuwa habari hizo hazijajiandika zenyewe bali yupo aliye andika, sasa uniambie ili tuanzie hapo kujua ukweli wa habari hizi.

Scientific Proof ni kwa mambo ya Sayansi, na ushahidi wa kidini ni ithibati ya hakika na uhalisia, bali shahidi za kidini huwa madhubuti mno kuzidi shahidi za kisayansi kwa mambo ya kisayansi. Kwahiyo usichanganye mambo ya Kisayansi na kuyapa hadhi ya ithibati kuliko mengine, huu ni ufinyu wa maarifa.

Somo hili nililisoma, na miongoni mwa vitabu nilivyo soma ni "The Etiquette of Research and Debate"

Hili swali sijaona umuhimu wake wala haja ya kulijibu.
Ndoto huwa inatokea kwenye ulimwengu wa roho, na ndiyo maana mtu hawezi akaota ndoto akiwa yuko macho, lazima uwe umesinzia. Unaweza ukasinzia dakika tano lakini ukaota ndoto yenye mambo ambayo unaweza ukachukua siku nzima kuyaelezea; umetembea kote duniani mabara yote ambayo umeshawahi kufika, in just within 5 minutes!
 
Back
Top Bottom