Nani aliyemuumba Mungu?

Nani aliyemuumba Mungu?

Kwanza ulithibitisha ya kuwa huyo aliyemtokea ni Malaika ?

Habari hizi tunazipata katika kitabu gani ?
Hakuwa Malaika perce, alikuwa Malaika kwenye umbile la binadamu. Ni kwenye Kitabu cha Waamuzi sura ya 13


Kuzaliwa kwa Samsoni


1Waisraeli walitenda tena uovu mbele ya Mwenyezi-Mungu, naye akawaacha watawaliwe na Wafilisti kwa miaka arubaini.
2Kulikuwa na mtu mmoja huko Sora, wa kabila la Dani, jina lake Manoa. Mke wake alikuwa tasa. 3Siku moja, malaika wa Mwenyezi-Mungu akamtokea huyo mwanamke, akamwambia, “Wewe ni tasa, huna watoto. Lakini utapata mimba na kumzaa mtoto wa kiume. 4Kwa hiyo uwe mwangalifu, usinywe divai au kileo wala usile kitu chochote kilicho najisi, 5kwa maana utachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume. Nywele za mtoto huyo kamwe zisinyolewe, maana atakuwa amewekwa wakfu kwa Mungu tangu kuzaliwa kwake. Naye ataanza kuwakomboa Waisraeli mikononi mwa Wafilisti.” 6Mwanamke huyo akaenda kumwambia mume wake, “Mtu wa Mungu ambaye sura yake ilikuwa kama ya malaika wa Mungu alinijia. Sikumwuliza alikotoka wala hakuniambia jina lake. 7Lakini aliniambia kwamba nitachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume. Aliniamuru nisinywe divai au kileo wala kula chochote kilicho najisi, maana mtoto huyo atakuwa amewekwa wakfu kwa Mungu tangu kuzaliwa kwake mpaka atakapokufa.”
8Kisha Manoa akamwomba Mwenyezi-Mungu, akisema, “Nakuomba ee Mwenyezi-Mungu, umtume tena yule mtu wako uliyemtuma ili atufundishe mambo tunayopaswa kumtendea huyo mtoto atakayezaliwa.” 9Mwenyezi-Mungu akalisikia ombi la Manoa, na yule malaika wa Mungu akamwendea tena yule mwanamke alipokuwa ameketi shambani. Lakini mumewe, Manoa, hakuwa pamoja naye. 10Mwanamke akakimbia upesi, akamwambia mumewe, “Tazama! Yule mtu aliyenijia siku ile amenitokea tena.” 11Manoa akafuatana naye mpaka kwa mtu huyo, akamwuliza, “Je, wewe ni yule mtu aliyezungumza na mwanamke huyu?” Yule mtu akamjibu, “Ni mimi.” 12Kisha Manoa akasema, “Sasa maneno yako yatakapotimia ni mambo gani tutakayofuata kwa ajili ya huyo mtoto? Tutafanya nini kwa ajili yake?” 13Malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwambia Manoa, “Mkeo atapaswa kushika yote niliyomwambia: 14Asionje mazao yoyote ya mzabibu, wala asinywe divai au kileo wala kula chochote kilicho najisi. Yote niliyomwamuru, ayafuate.”
15Manoa akamwambia huyo malaika wa Mwenyezi-Mungu, “Tafadhali, ukae kidogo tukutayarishie mwanambuzi.” 16Yule malaika wa Mwenyezi-Mungu akamwambia Manoa, “Hata kama mkinilazimisha kukaa sitakula chakula chenu. Lakini kama ukipenda, tayarisha sadaka ya kuteketezwa, mtolee Mwenyezi-Mungu.” Manoa hakujua kuwa huyo alikuwa malaika wa Mwenyezi-Mungu. 17Basi, Manoa akamwambia huyo malaika wa Mwenyezi-Mungu, “Tuambie jina lako ili tukuheshimu wakati maneno yako yatakapotimia.” 18Malaika wa Mwenyezi-Mungu akamjibu, “Kwa nini unataka kujua jina langu, kwa kuwa jina langu ni la ajabu?” 19Hapo Manoa akatayarisha mwanambuzi na tambiko, akaviweka juu ya mwamba amtolee Mwenyezi-Mungu afanyaye maajabu. 20Basi, wakati Manoa na mkewe walipokuwa wanatazama miali ya moto ikipanda juu mbinguni kutoka madhabahuni, walimwona malaika katika miali hiyo akipanda kwenda mbinguni. Basi Manoa na mkewe wakasujudu. 21Manoa akajua kuwa huyo alikuwa malaika wa Mwenyezi-Mungu. Malaika hakumtokea tena Manoa na mkewe.
22Basi, Manoa akamwambia mkewe, “Hakika tutakufa, maana tumemwona Mungu.” 23Lakini mkewe akamjibu, “Kama Mwenyezi-Mungu angetaka kutuua hangepokea sadaka yetu ya kuteketezwa na ya nafaka; wala hangetuonesha mambo hayo wala kutuambia maagizo.”
24Kisha mkewe Manoa akajifungua mtoto wa kiume, naye Manoa akampa jina Samsoni. Mtoto huyo akakua naye Mwenyezi-Mungu akambariki. 25Roho ya Mwenyezi-Mungu ikaanza kumsukuma akiwa huko Mahane-dani, kati ya Sora na Eshtaoli.
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Jifunze Mengi Kuhusu Biblia Habari Njema
 
Mtawala anayeweza kuwatawala watu milioni sitini na kuwatuliza kwa kuua wengi ana akili kwa sababu kaweza kuwatawala? Au hana akili kwa sababu anawaua raia wake?
Kibailojia mtu anatawaliwa na mfumo wa kati wa fahamu ndiyo ubongo na uti wa mgongo.
Ubongo unahusu akili na uti wa mgongo unahusu hisia. Kwahiyo, baiolojia inakubali kwamba mtu yeyote awaye ana akili.
Sasa inawezekakanaje mtawala anayetawala watu, ambaye naye ni mtu asiwe na Akili? Labda, kama unasema mwenendo wake.
Hayo unayoyasema hapo ni majeraha ya akili; amejeruhiwa kiakili.
 
The question: "If God is the creator, then who created the creator?" is illegitimate because by definition, the Creator is uncreated. He is eternal, without beginning, without end and all affairs return back to Him: (وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلْمُنتَهَىٰ) "And that to your Lord is the return (of all beings and affairs) (and of all perfections in attributes)." (53:42).

Thus to ask who or what created something that is uncreated is the way of:
a) an ignorant person devoid of intellect,
b) a lying deceiver, a sophist.

Note : Maelezo haya mafupi nime "copy" na ku "paste" toka kwenye tovuti iitwayo "www.aboutatheism.net", mnaweza tembelea huko mpate faida.

Tujadili hili, kwa wale wote ambao huuliza swali hilo, waje watuambie kwanini wanauliza swali hilo.

Ahsante.

Jurjani (Zurri)
Mungu anatengenezwa kifra sio kitu halisi ndo mana hakipo wala akionekani na wala hakisemi mungu anatengenezwa kwenye Ubongo
 
Sijakuelewa unapoandika "dhamira ya swali "nini" haikai katika Jina au Sifa ya chenye Elimu.

Swali lina dhamira au anayeuliza swali ndiye ana dhamira?

Rekebisha kunitaka nirekebishe swali!
"Rekebisha kunitaka nirekebishe swali!"

Hahahaha ila nimecheka sio siri
 
Kufikiri, kuthibitisha, kuchunguza, kukataa ndiyo huitwa akili.
Hivi yule msichana aliyenikataa kipindi kile hivi kumbe ana akili.!

Kabisa alikaa akachunguza akathibitisha sitompata wa zaidi yake

Mimi leo nalea ndoa yangu_yeye kawa ngoma ya mtaa kila muhuni anapiga tu.!

Mkuu labda nimeelewa vibaya ngoja nisikilize maoni kiranga katika hili..nilikua napita tu ila ukimya umenishinda
 
Hivi yule msichana aliyenikataa kipindi kile hivi kumbe ana akili.!

Kabisa alikaa akachunguza akathibitisha sitompata wa zaidi yake
Huyo msichana hakukukataa kwa sababu kwamba alichunguza akathibitisha kwamba hutapata mwingine zaidi yake.

Hayo ulioeleza hapo ni fikiri yako kumuhusu huyo msichana alivyokutendea na sio fikiri ya msichana.

Kwa sababu yeye hakuwa msichana peke yake; hivyo wengine zaidi yake walikuwepo na wapo.

Ni mara ngapi umesikia, umeona, umehisi au umeambiwa taarifa au jambo, lakini ukaacha kulitekeleza au kulipokea? Ni nini hicho kinakufanya ufanye hivyo; na kwa nini?
 
Huyo msichana hakukukataa kwa sababu kwamba alichunguza akathibitisha kwamba hutapata mwingine zaidi yake.

Hayo ulioeleza hapo ni fikiri yako kumuhusu huyo msichana alivyokutendea na sio fikiri ya msichana.

Kwa sababu yeye hakuwa msichana peke yake; hivyo wengine zaidi yake walikuwepo na wapo.

Ni mara ngapi umesikia, umeona, umehisi au umeambiwa taarifa au jambo, lakini ukaacha kulitekeleza au kulipokea? Ni nini hicho kinakufanya ufanye hivyo; na kwa nini?
Kwaiyo hayo maamuzi aliyoyachukua huyo msichana ndio Akili yenyewe.?
 
"Rekebisha kunitaka nirekebishe swali!"

Hahahaha ila nimecheka sio siri
Anachekesha.

Ameshindwa kujibu swali, analeta figisu za mikingamo, na huko anajikuta kashindwa.
 
Unataka uthibitisho wa kuwepo Mungu kwa wenye kuamini Mungu?
Kutoka kwa yeyote yule, hususan asiyeamini ila anayejua.

Anayeamini kuthibitisha, kimantiki, hawezi, ndiyo maana anaamini.Kuamini ni kukubali kitu bila uthibitisho.

Ukiweza kuthibitisha, umeondoka kwenye kuamini, uthibitisho wako unasema kwamba wewe unajua.

Ila hata anayeamini anaruhusiwa kujaribu kuthibitisha.

Na asipoweza kuthibitisha, habari ya kuwepo kwa Mungu inakuwa imani tu kama imani nyingine ambazo hazina uthibitisho.
 
Kabla ya yote ueleze wewe ni nini
Sioni mantiki ya swali hili.

Kwa sababu jibu lolote nitakalolitoa, niwe nimepatia au nimekosea, niwe naweza kujibu swali au siwezi kujibu swali, halithibitishi uwepo wa Mungu.

Na kama halithibitishi uwepo wa Mungu, sioni mantiki ya swali hili.

Swali hili halina tofauti na mimi kukuuliza wewe, thibitisha 1 + 1 =2, halafu wewe uniulize, kabla ya yote, nieleze mimi ni nini.

Logical non sequitur.

Mimi nikiweza kueleza mimi ni nini, nikatoa jibu zuri kabisa, hilo litathibitishaje Mungu yupo?

Au, mimi nikishindwa kueleza mimi ni nini, hilo linathibitishaje Mungu yupo?
 
Tueleze Mungu ni nini na thibitisha Mungu yupo kweli.
Naona unaendelea kukosea. Huwa nawaambia silei ujinga.

1. Hiki ni nini ? (Katika lugha kuna dhamiri za hayawani kitu kisicho ba akili na maarifa na kitu chenye maarifa uliza swali sahihi)

2. Huyu ni nani ?Dhamira ya swali inampelekea au inarudi kwa mwenye akilo na si hayawani (Yaani wanyama au miti au mfano wake).

Nasisitiza tena, rekebisha kiti chako kisha ukitie nakshi.
 
Kabla ya yote ueleze wewe ni nini
Hawezi kujibu swali hilo sababu anajua siyo sahihi, na kama hajui,tutamuuliza kwanini anajadili juu ya jambo usilolijua ?

Akijibu swali hilo kwa dhamiri hiyo, nitaomba hui uzi ufutwe.
 
Logical non sequitur.
Hii elimu ya Mantiki inaonekana uliivamia na hujui kama inazidi kukufanya uwe dhaifu katika kujenga hoja na kufikiri mambo katika uhalisia.
 
Back
Top Bottom