Nanasi Lililoozea Ndani...

Nanasi Lililoozea Ndani...

Last edited by a moderator:
Dah, ushaniharibia, nilikuwa na miadi leo. Ngoja nikabwie alter wine moja, maana ile makitu nikipata huwa ina deactivate kabisa hormone...

Hivi kumbe inasaidia? Itabidi niwe na chupa moja aisee. Itanisaidia kushinda majaribu.
 
Dah, ushaniharibia, nilikuwa na miadi leo. Ngoja nikabwie alter wine moja, maana ile makitu nikipata huwa ina deactivate kabisa hormone...

Hivi kumbe inasaidia? Itabidi niwe na chupa moja aisee. Itanisaidia kushinda majaribu.
 
nimejifunza kitu hiki nice things iz coming tomorrow asante kwa elimu nzur mtambuz
 
It's a lovely story na fundisho kwa maplayer wote na ving'ang'anizi wanaojifanya wao hakuna mwanamke anayewashinda.
 
Ushirika ni zaidi. Ya. Tuijuavyo mbe! Kontena la mama nanii lilivo kiwango kwa t.b.s ya macho ya nje ndani uozo,mungu tuepushe. Na hii dhahama
 
nimejifunza kitu hiki nice things iz coming tomorrow asante kwa elimu nzur mtambuz


Mkuu Mtambuzi ni baba yangu ndiyo lakini hadithi hii nimeiandika mimi!!!

It's a lovely story na fundisho kwa maplayer wote na ving'ang'anizi wanaojifanya wao hakuna mwanamke anayewashinda.
Crystal clear, na wewe ni mgumu kupatikana?

Cc: Asprin

Ushirika ni zaidi. Ya. Tuijuavyo mbe! Kontena la mama nanii lilivo kiwango kwa t.b.s ya macho ya nje ndani uozo,mungu tuepushe. Na hii dhahama

Kontena lipi mbe? Mimi nayajua mawili...

Huyu Mentor katuweka kundi la kifo...mbe

Jitetee mwenyewe mbe!
 
Last edited by a moderator:
Mbe" Mentor mananasi mengi mjini hapa yameoza kwa ndani ile nje mambo safi
Mbe" Hapana pima umbali kwa macho,
Ila mwambie Nicas anaweza kulala na bundi akaamka mwenye bahati..
Mbe ajali kazini mbe....leo nanasi linaweza kuwa safi kesho likaoza ndani kwa ndani
 

21[SUP]st[/SUP] November 2013, Alhamisi

Sifahamu usingizi ulinipitia saa ngapi ila nilishtushwa na sauti ya mtu akilia. Alikuwa ni Brenda ameamka. Alikuwa akilia kwa kwikwi. Sikuelewa ni kwa nini alikuwa akilia vile. Nilimbembeleza aniambie nini hasa kilichokuwa kikimliza. Nilimdanganya kwa ahadi nyingi za mapenzi na hata ndoa alimradi anyamaze. Lakini kadri nilivyotaja hizo ahadi ndipo alipozidi kulia. Baada ya muda alinyamaza na kunielezea.

Kumbe Brenda alizaliwa akiwa keshaathirika na virusi vya UKIMWI. Wazazi wake walifariki miaka mitano iliyopita kwa ugonjwa huo. Nakumbuka aliwahi kuniambia kuwa yeye ni yatima na kuwa alikuwa akilelewa na mjomba wake. Lakini kamwe hakuwahi kuniambia sababu za wazazi wake kufariki.

Hivyo Brenda alikuwa akiishi na virusi hivyo kwa muda wote huo. Mbe, nilianza kukumbuka kila kitu nilichokifanya usiku wa siku hiyo nikajua tu nimeshaupata. Nakumbuka mchana wa hiyo siku nilinyoa mavuzi na kwa hakika kuna sehemu mbili tatu nilijikata. Nilikumbuka kuwa pia sikutumia kinga yoyote na kwa vile alivyokuwa akikataa lazima kutakuwa na michubuko ambayo ama kwa hakika nisingeweza kuiona kwa macho lakini ipo.

Ghafla kichwani nilipata picha iliyonipagawisha. Nilijiona nikiwa nimekonda hadi mbavu zinaonekana huku nikiwa nimetuliwa na nzi kila mahali na sina mtu anayenihudumia kwani kila aliyepita alikuwa akisema yake; ‘Huyu alikuwa player sana’ ‘amevuna matunda ya uhuni wake’ Hata mama yangu nilimsikia akiniambia, ‘huyu ndo mjukuu uliyeniletea mwanangu? UKIMWI?’

Bila kujielewa nilijikuta nikienda kwenye kabati la dawa na sifahamu hata nilichukua nini na nini ila nilimeza vidonge vingi nikashushia na konyagi. Nahisi ni Brenda ndiye aliniwahi na kunileta hospitali la sivyo ningeshaondoka mbe.


Nilipata wazo la kumuuliza huyu Brenda yupo wapi lakini ghafla nikamuona mama yake akiingia wodini na nilipotupia macho saa yangu ya mkononi ndipo niligundua imeshafika saa sita za mchana na muda wa kuwaona wangojwa ulikuwa umewadia. Nilimsalimia na kuwaaga huku nikibaki na maswali mengi kichwani ya kumuuliza Nicas.

Kwa bahati mbaya nilitakiwa kupanda ndege ya jioni ile na kurudi Dar es salaam kuendelea na majukumu ya kujenga nchi. Nikiwa kwenye ndege niliwaza sana na kuogopa sana moyoni. Hakuna aliye salama tena katika nyakati hizi. Hata yale mananasi yaonekanayo masafi na mazima kwa nje kumbe yameozea kwa ndani.

Wasalaam wapendwa,
Mentor.

Wewe ni Mkare aisee....
Nimesoma na nimetamani tuitengenezee movie ili jamii ijifunze zaidi.
In serious note, naomba tuonane kesho hapo kwenye kijiwe changu cha kahawa ili tuandae huo mswada, nina mfadhili wa kutuwezesha.
Hii makitu inalipa aisee.
Mentor
 
Last edited by a moderator:
Mentor asante sana kwa kisa hiki ambacho kina ukweli na uhalisia ndani mwake. Hili ni janga na ni wachache wanachukua tahadhari ila kwa kweli hali ni mbaya sana
Mpigie Nicas aise ujue hata hali yake na status yake bana
 
Last edited by a moderator:
Wanaume wengi wakishajua msichana ni bikra swala la kupima kabla ya tendo linakuwa halipo....mana anamwamini msichana moja kwa moja sababu ya bikra yake...
 
It's a lovely story na fundisho kwa maplayer wote na ving'ang'anizi wanaojifanya wao hakuna mwanamke anayewashinda.

Mbe...kuna wanaume hawataki kushindwa....ndo wajifunze ukiona unakataliwa kila kukicha ujue unaepushwa na janga...mbe
 
Back
Top Bottom