Namuheshimu mama yangu lakini simpendi

Namuheshimu mama yangu lakini simpendi

Kuwa mkubwa kwenye familia haimaanishi ku take responsibility. Kuna watu wengine wazito kama mawe, tena baadhi ya wanamme mkiona ndio hovyo kabisa. Mtu anasubiri asukumwe hata kutoa mchango wa rambirambi, nani akushirikishe sasa?


Mnakuwa active ukweni kwenu, mie mtu nikiona analalamika hashirikishwi kwao namwona pun.guani tu, kwa nini asi-take initiative za kuanzisha jambo na yeye ndio ashirikishe watu? Huoni aibu kaka mkubwa kila siku unashirikishwa badala ya kuwashirikisha wewe wadogo zako?

Ni rahisi sana ku judge kama hayajakutokea au kushuhudia nimeshaona kaka mkubwa hashirikishwi vikao vya maamuzi ya family na hata kwenye msiba wanaitana pembeni wadogo na wazazi then jamaa anatumwa tu nenda sokoni kalete hiki na young brother kisa yeye hana kitu
 
Mwanamme unajiita jina hili? It speaks volume.

mkuu mimi ni mwanaume na ni wa kwanza kuzaliwa,wadogo zangu wana uwezo lakini mimi sina uwezo sana ila mungu amenisaidia kuridhika na hali niliyo nayo
 
Pole sana ndugu, Hebu chukulia hali hiyo kama challenge kwako ujitume na ikufanye ufikie malengo. Muda mwingine si dhambi kuwa na wivu. Bali ni nguvu inayotufanya tufikie hali fulani.
Nakuaminia kakangu toka moshi nyie huwaga ma faita sana. Hebu chukua changamoto hizo kutoka kwa mama ahalafu zifanyie kazi. Na hakika siku moja utakuja kumkumbusha (Kwa utani) kua 'mama ulikua hunipendi kipindi kile nilivokua sina kitu'.
 
mkuu mimi ni mwanaume na ni wa kwanza kuzaliwa,wadogo zangu wana uwezo lakini mimi sina uwezo sana ila mungu amenisaidia kuridhika na hali niliyo nayo

Duuh! Nilishaingia chaka nikidhani wewe ni "she" kwa hilo jina lako ulilochagua yaani rosemarie.
 
Ama hamjamwelewa mtoa mada au mu sehemu ya watumwa wa Mali. "Mali ipatikanayo haraka huondoka haraka" Ushauri wangu naiona imani thabiti ndani yako. Endelea kuomba ulinzi wa MUNGU,samehe ,mwombee anayekuudhi, mmbariki anayekulaani,utainuliwa. Tatizo ni asili ya jamii(shina analotoka mama) Wanathamini fedha kuliko utu. Haijalishi unazipataje. Simamia imani yako. Kati ya fedha na MUNGU utachagua nini ? Nina uhakika unaandaa kesho njema kwa uzao wako. Omba toba kuondoa chuki yako kwa mama. Ukiona giza nene usiku tambua asubuhi ikaribu
 
mkuu nafikiri mimi ni mtu mwenye moyo laini sana
mtu akishaniudhi inakuwa tabu sana kusahau,lakini nafikiri uwezo nilio nao ni mungu peke yake anaweza kuniongezea
namtegemea muumba wangu najua siku moja nitakuwa na mali kama wanavyotaka lakini kamwe sitaweza kulazimisha hilo

we una kila dalili ya kuwa na 'low self esteem". Kila wakati unahisi unaonewa tu. Unajiona dhaifu usiyestahili na unafikri kila mtu anakuona kama unavyojiona wewe. Hata unavyoonyesha unamtegemea mungu sana, sijui una moyo laini ni dalili za kutokujiamini. Ukijiona unafaa utahisi kila mtu anakuona unafaa hata kama hawakuoni hivyo. Anza mchakato wa kujiamini. Acha kujitiisha huruma kwa mungu.
 
mkuu baba yangu hakuwa tajiri,tuliishi maisha ya kawaida kabisa,lakini waliweza kutulea
kwa kweli jambo la kusema tulazimishe kupata mali mimi nipo kinyume kabisa
naishi maisha ya kawaida nina nyumba,kazi na kausafiri,na nina watoto wangu wazuri sana
jamani nifanye nini mimi ili niheshimike?

ufanye nini ili uheshimike? jiheshimu mwenyewe kwanza. Heshimu utu wako kwamba wewe ni mtu kamili, kwamba huhitaji mtu akunyenyekee au kukupapatikia ndo ujiskie amani. Ukijitosheleza ndani mwako hutahitaji mtu wa nje akukamilishe. Tabia ya mtu asiyejiamini ya kuwatuhumu wenzie huwa inakera sana na hufanya watu wakae nae mbali ili kukwepa lawama na manung'uniko.
 
Back
Top Bottom