Namuheshimu mama yangu lakini simpendi


episodes pole sana kwa kweli ni maisha magumu haya ila mshukuru MUNGU kwa yote. ... chukulia ni kitu cha kawaida .(Si nasikia wachaga wanahusudu sana wenye pesa hadi wanawaamkia..shikamoo mwanangu!!- kama ni kweli ). Hii post yako imenigusa sana but amini unapoweka 'grudges' juu ya mama yako Moyoni mwako ndivyo unavyozizuia baraka za Mwenyezi Mungu katika maisha yako. Tumeambiwa tuwaheshimu wazazi wetu ili siku zetu zipate kuwa nyingi humu duniani lakini pia ziwe za mafanikio. Huwezisema unamheshimu wakati unamchukia!! hebu kaa na utafakari hiyo heshima yako ikoje----- heshima ni zaidi ya shikamoo mama; aksante mama e.t.c. Heshima ni ule m-package mzima wa shukrani, thamani na appreciation- Sasa kama unasema unamheshimu lakini humpendi- kutokumpenda kunawezakukuzuia kumthamini na hata kuappreciate anayokufanyia au malezi alokupa.

Funguka..........kama unaweza jenga ukaribu naye kisha mweleze..Mama najua sina uwezo kiasi cha kukuriddhisha, but mama jinsi unavyotutreat mimi na mdpgp wangu nakwazika..............mweleze unavyojisikia pengine ye anafikiri hujagundua au hujui. Mweleze kuwa unajua, wamama tuna huruma na huumia sana pale tunapowakosea wenetu (hatunaga ile pride ya mimi ni mzazi wako -so sistahili kukuomba msamaha) unawezashangaa akawa karibu nawe zaidi.

Funguka moyo ili upate kuachia baraka za MUNGU zimiminike kwenye maisha yako na kuyafungua madirisha ya baraka na mafanikio nyumbani kwako. Kila la khheri
 
Kuna somo moja alifundisha alifundisha Mwalimu wa neno la Mungu Mwakasege, linalosema LANGO LA MZALIWA WA KWANZA, ungepata kitabu au CD, ungejifunza kitu kikubwa. Hata hivyo kaka huna option, nikunyenyekea tu, kutubu kwa Mungu, nakuomba hicho kiambaza kiondoke kati yako na mama yako.
 
Pole kwa yote yanayokukuta.......
Ila kama ni mkristo naomba zingatia amri ya Mungu isamayo...."waheshimu baba na mama yako siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na bwana MUNGU wako.". Muache akufanyie ubaya usilipize, mpende na msikilize...just do your part.
 

Kweli kabisa LD..nimekisoma kitabu chake.
 
Reactions: LD
Mungu hawezi kukunyima vyote, Yeye ni mwaminifu kwao wamchao na hakika siku moja atasikia sala yako atakuinua kwa wakati wake

Jina la Bwana lihimidiwe

Pengine nisingeweza kutoa ushauri mzuri zaidi ya wa Miss Judith!
Labda kwa nyongeza tu ni kuwa MAMA hata waweje, hata wawe na tabia gani, bado watabaki kuwa ni mama zetu, tuwapende na tuwaheshimu.
Kupenda kwake kwa wanawe walio na uwezo kusikufanye wewe usimpende yeye kwani "Ukweli ni kuwa na wewe anakupenda". Kama angelikuwa hakupendi, sidhani kama angejisumbua kubeba ujauzito wako na kukulea hadi umefika ulipo.

Kitu kinachokusumbua ni kukosa kwako mali, kwa maneno mengine, chuki zako kwa mama yako zimeanzia kwa kaka zako walio na uwezo, na kuanzia hapo kila analofanya mama au ndugu zako unahisi ni manyanyaso kwako. Sio hivyo. Ikiwa wamepata kwa juhudi zao, nawe fanya juhudi kutafuta chako. Ikiwa Mungu amewapa na wewe kukunyima, uelewe kuwa Mungu humpa na kumnyima amtakaye, hugawa kwa mujibu wa kiasi na stahili zetu. Kama ushauri, "Usitumai cha ndugu".

Nisingependa kutumia maneno "wivu na choyo" lakini kumbuka kuwa vitu hivi ni kama kensa katika nafsi zetu. Nina wasiwasi kuwa hata hii hali ulinayo inaweza kutokana na wivu na choyo chako. Natamani niwe nimekosea kufikiri hivi na ninakuomba samahani ikiwa nmekosea. Kumbuka tu kuwa "Anayejitahidi hufanikiwa". Nawe Jitahidi!

Kama neno la mwisho nikitilia mkazo yale ya mwanzo, MPENDE NA MHESHIMU MAMA YAKO. Hili si ombi, ni amri toka kwa Mungu kwani ni wajibu wako.
Kila la Heri Mkuu!
 
<br />
<br />
Nahisi huu ndo ukweli, wachaga walio wengi huwa hawana mapenzi ya utu, bali wana mapenzi ya pesa. Pole sana.
 
&lt;br /&gt;<br />
<br />
<br />


UMEJAA HEKIMA NA UZOEFU WA MAISHA MISS JUDITH,ANA HERI YEYE ALALAYE AU ATAKAYELALA KWENYE KIFUA CHAKO!!<br />
Such a Wonderful Woman!!
 
Mkuu hilo ni kwa watu wengi sana na hii ni kwa sababu wazazi wanathamin pesa kuliko ki2 kingine ....La muhimu msamehe bure coz hajui alitendalo
 
<br />
<br />



Hakika hizi ni Hekima za Suleiman,Episode,sikikia sauti hii ya Mtu aliye nyikani,ukasawazishe hicho kilima kati yako na Mama yako!!
Be Strong,Inawezekana kabisa akawa na yeye anaugua Moyoni mwake Juu yako,go speak to her!! Inawezekana Mazingira aliyokulia hayakumfunda kusema hisia zake!!
Mara chache sana akina Mama kuwa vichaa,tatizo huwa ni sisi akina Baba!!
 
<br />





Sawasawa Kaka,na kwa kawaida mtu hawezi kutoa kitu ambacho hana,atatoa alichonacho tu!! Kama amekulia katika familia ambayo thamani ya mtu hupimwa kwa Fedha ni dhahari na yeye atatoa hichohicho kwa Watoto wake!!!
 
watanzania ni watu wenye upendo sana
nashukuru wote mnaochangia hili,na kila wakati ninapata kitu kipya kutoka hapa
nilimtembelea rafiki yangu mmoja na kuona jinsi mama yao anavyoongea nao vizuri japo wao sio matajiri nikatamani ningekuwa ni mimi
ndugu zangu elimu niliyo nayo inanisaidia sana kwenye kazi zangu lakini mimi ni mtu mwenye maisha ya kawaida kabisa na sina mpango wowote wa kutafuta utajiri ili mzazi wangu aniheshimu
mimi namwamini mungu mkuu na ninaamini ninaishi na kumtegemea yeye
huyu mungu akipenda kunipa mali atanipa na hakuna wa kupinga
kila nikisoma comment zenu ninalia machozi
nimeamua kuchukua likizo labda kwenye mwezi wa kumi na nitakwenda kukaa na mama yangu nione kama naweza hili
 
Reactions: Mbu

Episode, Pole sana ndugu yangu.

Kuna msemo mapenzi ya pesa si mapenzi, ila mapenzi ya roho ni ya maisha.
Ninalokushauri, mweke mama yako kwenye maombi. Mkumbuke kwenye dua zako.
Mama yako anakupenda, ila labda hajaweza kukupa mapenzi vile weye unavyoyatafsiri.
Kumbuka, miezi tisa tumboni, ukazaliwa akakulea tangu ukiwa huna uwezo wa kujifanyia lolote mpaka
pale ulipokuwa na mamuzi yako.

Hakuna kama mama, iwe tulizaliwa mmoja au zaidi ya mmoja.
Endelea kumuombea kila lililo na heri mama yako.
Upendo unazaa upendo, na utu ni bora kuliko mali.
Hakuna haja ya kushindania Upendo wa mama.
Nyote mnapendwa, kila mtu kwa nafasi yake.

Ni yangu hayo machache, kila la heri.
 
Mzazi ni mzazi tu naye shida zake ndo zilimfanya ajisahau aegemee upande mmoja, mpe heshima yake kwani maisha ya duniani ni mafupi, ogopa adhabu utakayoikuta kutokanana kuvunja amri ya MUNGU ya kutokuwaheshimu wazazi.
 
mpendwa nimekutafutia huu wimbo ukusaidie kutafakati ukuu wa Mungu maishani mwako. i hope utaupenda:


wimbo wenyewe unapatikana hapa:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...-ya-siku-chozi-la-damu-lilipochuruzika-2.html

ni vizuri ukisoma na ushuhuda wa yule kaka ili uone Mungu anavyotupenda.

ubarikiwe sana mpendwa

Glory to God!
 
mkuu mimi ni mwanaume na ni wa kwanza kuzaliwa,wadogo zangu wana uwezo lakini mimi sina uwezo sana ila mungu amenisaidia kuridhika na hali niliyo nayo

Hutakiwi kuridhika ili uendelee, u have to fight ili ufike pale panapostahili. pole sanan haya ndo maisha ya mwisho wa dunia, vituko kila kukicha. Mungu ni mwema atakuinua ukikazana.
 
Wapo wamama wa hivyo, i hate them kwa tabia kama hiyo, wote ni watoto wake, kama hawana uwezo yeye kama mama anatakiwa kuwaombea ili wafanikiwe na kuwahimiza watoto wake wenye uwezo wamsaidie mwanzao ambaye uwezo wake ni mdogo! Ila msamehe kwani ibilisi anaweza kumtumia mtu yeyote ili kukufarakanisha na ndugu na hatimaye ukose amani maishani mwako
 
Hebu kajifunze upya tafsiri na maana ya usemi huu.............what goes around comes around!
 

Haya mambo yapo sana tuu mkuu na sidhani suluhisho kwako ni kumchukia mama yako kw aaliyokutendea na anayokutendea. Nafikiri suluhisho kwako ingekuwa kumuonyesha mama kuwa wewe ni mpambanaji na unapambana na bado hutaki hali uliyo nayo iendelee hata kwa watoto wako. Nafikiri Mama akishaona hayo atafurahi sana maana nafikiri kama wachangiaji wengine walivyosema inawezekana mama alinyanyaswa sana na jamii kutokana na umaskini wake so hataki mtoto wake awe maskini au anyanyasike kama yeye. Kaa na mama wala usiwe na ile hali ya kinyongo na mwambie wazi malengo yako na mategemeo yako na tekeleza hayo malengo yako kwa kiwango na kiasi then muonyeshe mama na mama akiona hayo atajua kuwa unafight kutoka katika hali uliyo nayo. Usiridhike wala usimwonyeshe mama kuwa umeridhika na hali uliyo nayo maana wewe ni mwanaume onyesha mapambano na onyesha kuwa wewe ni mtoto wa kwanza kwa kuontgoza mapambano ya kuistawisha familia yako.
 
Na mimi nakubaliana na maneno ya wahenga kuwa hilo kabila wengi wana roho za kipalestina. I wish angekuziba pua zako kwa manyonyo yake wakati uko kachanga ndo ingekuwa suluhu ya upuuzi wako.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…