Hbr wadau baada ya kupata mafunzo ya driving pale Mabibo Nina wiki nmebahatika kazi namuendesha Dada mmoja Wa shirika Fulani la Wajerumani.
Tatizo vijana wenzangu wakiniona nawahi kushuka namfungulia mlango yule Dada ashuke jamaa wanamaindi.Yule Dada kweli pia hupenda kufungua mlango mwenyewe Bali nimemkataza nikamwambia nitakuwa namfungulia.
Akishuka nambebea begi lake mpaka ofisini wakati Wa kutoka nambebea mpaka kwenye gari.Jamaa wanachukia eti najishusha.
Chuoni nimefundishwa kumkarimu abiria wangu ambae ni bosi kiumri nimemzidi kidogo japo kimo tunalingana namnyenyekea jamani nimesota sana mtaani.
Jamaa mpaka wananitenga sijui nifanyaje yule Dada nafaidi vingi Kwa ukarimu wangu.Keep change za kutosha.Nishaurini kitu.