Mkuu Kabanga,
Nilipita Kibasika lakini ama hawajui kama yupo shule huko Tanga au walifanya makusudi ya kutoniambia. Lakini hiyo taarifa kwamba kwa sasa anafundisha shule moja mkoani Tanga niliipata hapo Kibasila.
Tiba
pole ni kibasila sec Tiba? umefika ofisi ya masijala? isije kuwa umemuuliza mlinzi getini....? ikiwa ni Sec, fanya hivyo nnilivyokueleza
Nilifika Kibasila Secondary kabisa nikakutana na mwanamke mmoja ambaye nadhani ni Mwalimu pale. Yeye nilipomweleza shida yangu, aliguna tu na kuniomba nimfuate. Akanipeleka kwa Mwalimu mwingine wa kike ambaye kutokana na maandishi kwenye mlango ni Mwalimu mkuu msaidizi. Yeye aliniuliza nina uhusiano gani na huyu ninayemtafuta, nikamweleza. Mwisho alinifahamisha kwa urahisi tu kwamba aliisha hama pale na kwa sasa kadiri anavyosikia anafundisha kwenye shule moja huko Tanga.
Nilihisi kuna kitu walikuwa hawataki kunieleza!!!!!!!!
Tiba
Duh,huyu atakuwa ndie mwenyewe,maana kajiunga leo na leo kamwaga number.mm namfahamu namba zangu hz 2wasiliane 0655080933 au 0755080933