Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu watanzania,
Kuna kipindi kulikuwa Kuna washangaza wazalendo wengi Sana juu ya Uvujaji na usambaaji wa Siri na Nyaraka za Siri za serikali, watu walikuwa wanaona fahari kuvujisha Siri za serikali na Nyaraka za serikali, ilikuwa Ni kawaida kukuta na kuona mitandaoni habari nyeti za serikali. Nilikuwa najiuliza ujasiri huo ulikuwa unatoka wapi wa kufanya hayo mambo pasipo kuhukumiwa na dhamira zao juu ya viapo vyao.vikali kimaneno.
Ndugu zangu Ili ushinde Vita ya aina yoyote Ile Ni lazima uwe msiri wa mambo yako,mipango yako,mikakati yako na mbinu zako za kimedani. Huwezi ukaishinda Vita kwa kuandika Siri za jeshi lako hadharani utafikiri pumba za mashineni, mataifa yaliyoendelea na yenye nguvu za kijeshi, kiuchumi, kisayansi, kiteknolojia, kijasusi na kiinterejensia yamefanikiwa katika suala la utunzaji wa Siri na kuzilinda Siri za mafanikio Yao kwa jasho na Damu, hawana mchezo katika suala la Siri za Taifa na Nyaraka za serikali au vyombo vya ulinzi na usalama na mipango yake.
Ifahamike kuwa kuvujisha Siri na Nyaraka za serikali ni hatari kiusalama. Ni kulivua Nguo Taifa kwa kuwa inatoa mwanya kwa maadui zetu na wapinzani wetu wa kiuchumi na hata maadui zetu kiusalama kuweza kupata mahali pa kuanzia na kujuwa udhaifu wetu ulipo, wanapata kujuwa udhaifu wetu wa kutunza mambo yenye maslahi kwa Taifa letu na hivyo kuwa Rahisi kutuhujumu kiuchumi na hata kiusalama.
Kwa bahati nzuri Tangia ameingia madarakani mama yetu mpendwa kipenzi Cha watanzania, mama imara na shupavu. Jasiri na mzalendo wa kweli Mama Samia Suluhu Hassan kumeonekana kupatiwa dawa kwa Tabia hii mbaya iliyokuwa inataka kumea hapa nchini kwa baadhi ya watumishi, kwa Sasa watu wanashindwa hata kubashiri ni nani anaweza kuteuliwa katika nafasi fulani hata Kama mh Rais akisema kuwa anataka kufanya mabadiliko mahali fulani kwa wasaidizi wake, iwe Ni kwenye chama aliko Kama Mwenyekiti au serikalini ambako Ni Rais na Amiri Jeshi mkuu amedhibiti Sana Uvujaji Wa Siri za serikali Hali iliyoleta utulivu serikalini na kuondoa Taharuki kwa wananchi, imeondoa presha na hata sintofahamu iliyokuwa ikitokea na maneno maneno.
Mimi Mwashambwa nikiwa Kama mzalendo na mpenda nchi yangu nawapongeza Sana wale wote waliokula viapo vya kutunza Siri mahali pa kazi kwa kuwa waadilifu na wenye kuzingatia viapo vyao, Nawasihi Kuendelea na moyo huo kwa maslahi mapana ya Taifa letu, kila mmoja wetu aliyepewa dhamana ahakikishe anatunza Siri za serikali kwa Kiwango Cha juu, kusiwepo kuishiwa uvumilivu katika suala la kiapo, Taifa letu Ni muhimu kuliko kitu kingine chochote, Na kila mtu ajione mwenye hatia inayostahili adhabu Kali ya majuto na majonzi avujishapo Siri za serikali.
Rai yangu kwa wahusika Ni kuhakikisha kuwa maafisa wote serikalini wanazingatia viapo vyao, isitokee hata kwa bahati mbaya mambo ya serikali yanatoka nje na kuleta Taharuki na kutetemesha usalama wetu, kila mmoja aliyepewa dhamani Ahakikishe anakuwa msiri ikiwezekana hata kufa kwa ajili ya kulinda maslahi ya Taifa letu kwa maslahi mapana ya vizazi vijavyo.
Hongera Sana Rais wangu, Umethibitisha uimara na ushupavu wako, umetoa dira na muelekeo wa serikali yako, mausia na maonyo uliyoyatoa hadharani yamezingatiwa na sisi watanzania Tumeona matokeo yake. Tunakuamini sana Rais wetu, tunakuunga mkono, tupo bega kwa bega na wewe, tunakupigania mitaani na kukusemea kila mahali.
Tunaendelea kukuombea afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia wananchi wako, Songa mbele kwa nguvu maana tulio upande wako Ni wengi zaidi ya wale walio kinyume na wewe kwa maslahi yao binafsi, umefanikiwa Kuiteka na kuitawala mioyo ya watanzania kwa uchapa kazi wako, ndio maana unaona utulivu na Amani ukiwa umetamalaki hapa nchini.
Kazi Iendeleee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627
Kuna kipindi kulikuwa Kuna washangaza wazalendo wengi Sana juu ya Uvujaji na usambaaji wa Siri na Nyaraka za Siri za serikali, watu walikuwa wanaona fahari kuvujisha Siri za serikali na Nyaraka za serikali, ilikuwa Ni kawaida kukuta na kuona mitandaoni habari nyeti za serikali. Nilikuwa najiuliza ujasiri huo ulikuwa unatoka wapi wa kufanya hayo mambo pasipo kuhukumiwa na dhamira zao juu ya viapo vyao.vikali kimaneno.
Ndugu zangu Ili ushinde Vita ya aina yoyote Ile Ni lazima uwe msiri wa mambo yako,mipango yako,mikakati yako na mbinu zako za kimedani. Huwezi ukaishinda Vita kwa kuandika Siri za jeshi lako hadharani utafikiri pumba za mashineni, mataifa yaliyoendelea na yenye nguvu za kijeshi, kiuchumi, kisayansi, kiteknolojia, kijasusi na kiinterejensia yamefanikiwa katika suala la utunzaji wa Siri na kuzilinda Siri za mafanikio Yao kwa jasho na Damu, hawana mchezo katika suala la Siri za Taifa na Nyaraka za serikali au vyombo vya ulinzi na usalama na mipango yake.
Ifahamike kuwa kuvujisha Siri na Nyaraka za serikali ni hatari kiusalama. Ni kulivua Nguo Taifa kwa kuwa inatoa mwanya kwa maadui zetu na wapinzani wetu wa kiuchumi na hata maadui zetu kiusalama kuweza kupata mahali pa kuanzia na kujuwa udhaifu wetu ulipo, wanapata kujuwa udhaifu wetu wa kutunza mambo yenye maslahi kwa Taifa letu na hivyo kuwa Rahisi kutuhujumu kiuchumi na hata kiusalama.
Kwa bahati nzuri Tangia ameingia madarakani mama yetu mpendwa kipenzi Cha watanzania, mama imara na shupavu. Jasiri na mzalendo wa kweli Mama Samia Suluhu Hassan kumeonekana kupatiwa dawa kwa Tabia hii mbaya iliyokuwa inataka kumea hapa nchini kwa baadhi ya watumishi, kwa Sasa watu wanashindwa hata kubashiri ni nani anaweza kuteuliwa katika nafasi fulani hata Kama mh Rais akisema kuwa anataka kufanya mabadiliko mahali fulani kwa wasaidizi wake, iwe Ni kwenye chama aliko Kama Mwenyekiti au serikalini ambako Ni Rais na Amiri Jeshi mkuu amedhibiti Sana Uvujaji Wa Siri za serikali Hali iliyoleta utulivu serikalini na kuondoa Taharuki kwa wananchi, imeondoa presha na hata sintofahamu iliyokuwa ikitokea na maneno maneno.
Mimi Mwashambwa nikiwa Kama mzalendo na mpenda nchi yangu nawapongeza Sana wale wote waliokula viapo vya kutunza Siri mahali pa kazi kwa kuwa waadilifu na wenye kuzingatia viapo vyao, Nawasihi Kuendelea na moyo huo kwa maslahi mapana ya Taifa letu, kila mmoja wetu aliyepewa dhamana ahakikishe anatunza Siri za serikali kwa Kiwango Cha juu, kusiwepo kuishiwa uvumilivu katika suala la kiapo, Taifa letu Ni muhimu kuliko kitu kingine chochote, Na kila mtu ajione mwenye hatia inayostahili adhabu Kali ya majuto na majonzi avujishapo Siri za serikali.
Rai yangu kwa wahusika Ni kuhakikisha kuwa maafisa wote serikalini wanazingatia viapo vyao, isitokee hata kwa bahati mbaya mambo ya serikali yanatoka nje na kuleta Taharuki na kutetemesha usalama wetu, kila mmoja aliyepewa dhamani Ahakikishe anakuwa msiri ikiwezekana hata kufa kwa ajili ya kulinda maslahi ya Taifa letu kwa maslahi mapana ya vizazi vijavyo.
Hongera Sana Rais wangu, Umethibitisha uimara na ushupavu wako, umetoa dira na muelekeo wa serikali yako, mausia na maonyo uliyoyatoa hadharani yamezingatiwa na sisi watanzania Tumeona matokeo yake. Tunakuamini sana Rais wetu, tunakuunga mkono, tupo bega kwa bega na wewe, tunakupigania mitaani na kukusemea kila mahali.
Tunaendelea kukuombea afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia wananchi wako, Songa mbele kwa nguvu maana tulio upande wako Ni wengi zaidi ya wale walio kinyume na wewe kwa maslahi yao binafsi, umefanikiwa Kuiteka na kuitawala mioyo ya watanzania kwa uchapa kazi wako, ndio maana unaona utulivu na Amani ukiwa umetamalaki hapa nchini.
Kazi Iendeleee, mama ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627