Namna ya kutambua kama umeokoka au wewe ni Mkristo

Victor Mlaki

JF-Expert Member
May 1, 2016
3,564
3,472
Leo mtu akitokea na kuwauliza waumini wengi wa makanisa ya kiroho swali la Je! ni kweli tutakwenda mbinguni?.Bila shaka wengi watajibu ndiyo na sababu watakayoitoa kubwa ni kwamba wamempokea na kumkiri Yesu kama Bwana na Mwokozi. Lakini pamoja na jibu hilo bado siyo sababu kuu ingawa ni sehemu tu. Ipo namna ambayo Mungu ameifanya kwa watu kupata wokovu na kudumu katika wokovu.

Changamoto kubwa leo watu wengi wanakiri vitu wasivyovielewa Kwa mfano mtu akija akikuambia ipo jehanamu ya moto, jehanamu ni halisi, ukifa utaingia motoni unaweza kujenga hofu ila ukweli hatuingii mbinguni kwa sababu sababu ya kukwepa au kuogopa moto.

Wahubiri wengi leo wamesahau kabisa kufundisha juu ya misingi aliyoiweka Mungu inayowaunganisha wanadamu na wokovu. Wayahudi walipata nafasi ya kwanza ya wokovu kwa sababu ya misingi yao ya ufuasi na Mungu alijidhihirisha kwao kupitia utamaduni huo wa ufuasi. Mungu alijidhihirisha kwao kama Mungu wa Baba zao, waliishi katika misingi hiyo ya ufuasi kiasi kwamba walipoikiuka walipata mapigo.

Angalia jambo la hatari itakuwaje siku ya mwisho mtu anaambiwa na Mungu toka sikujui?.Unamueleza Mungu kuwa ukifanya unabii n.k Kwa kina lake halafu anasema hakujui!..Hii ina maanisha mtu anaweza kuwa muongofu wa imani na anajitoa sana katika masuala mbalimbali mahali anaposalia lakini yeye asitambuliwe na Mungu ila yule aliyewasaidia masikini Kwa kumpatia chakula, maji na mavazi, aliyewaona wafungwa Mungu akamwona ni mwenye heri kwa sababu alimsaidia alipokosa chakula, alimvisha alipokosa mavazi n.k.

Hii inaonesha yale unayowafanyia wengine ndiyo utamaduni uliojifungamanisha nao na ndiyo utakaokuwezesha kumuona Mungu ila siyo kukiri usiyoyafahamu. Hatutakiwi kukiri jambo tusiloliamini au tusilolifamu wala kuwa na uhakika nalo "you should not make confession to what you are not convicted by". Ibrahimu alihesabiwa haki sababu ya kuwa na imani thabiti "conviction".Uhakika wako ndiyo unaokupelekea wokovu.

Jiulize taratibu tu ni kwa nini leo nyumba za ibada zimejaa watu wanaosema wameokoka lakini wanatenda dhambi? Biblia inasema aliyeokolewa hatendi dhambi tena lakini ikitokea mtu anasema ameokoka na anaendelea kutenda dhambi kuna tatizo mahali. Inawezekana mtu huyo kuna hatua za mdsingi alizikosabna huenda aliyemuongoza mtu huyo alimwelekeza kufanya matamko tu ya kukiri na siyo katika uhakika wa mabadiliko ya mtindo wa maisha. Tunapoongoka sharti tupokee na mtindo wa maisha.

Hatupati wokovu Kwa kutamka tu 'tumeokoka' ila ni kwa kuwa na uhakika na imani dhabiti moyoni. Wokovu ni pale vitu vinavyoanza kubadilika ndani ya moyo wako na kuanza kufahamu maisha bila Yesu ni bure. Mtu huanza kutamani kuwa na Mungu, kumuona kuliko kitu chochote kile. Ila ukiona una mashaka mfano unajiuliza hivi Yesu akirudi mara ya pili nitanyakuliwa au la!.. ukiona una swali la aina hiyo elewa hautaiona pepo na haujaokoka au wewe siyo Mkristo bado.
 
Hata walio okoka wanateleza na kutenda dhambi ndio maana kuna msalaba na kuomba toba kila siku.

Warumi 3:23-25

Jambo la pili tukifuata biblia hayo uliyo yasema ni mambo mazuri kufanywa lakini mtu hawezi kuokolewa kwa matendo peke yake (mfano unasema mimi nina vituo vya watoto yatima vingi so hiyo ndo price yangu ya kununua wokovu)

Kulea yatima na kusaidia watu ni jambo zuri lakini wokovu tunaupata kwa neema na kujinyenyekeza katika Jina lipitalo majina yote
 
Hata walio okoka wanateleza na kutenda dhambi ndio maana kuna msalaba na kuomba toba kila siku.

Warumi 3:23-25

Jambo la pili tukifuata biblia hayo uliyo yasema ni mambo mazuri kufanywa lakini mtu hawezi kuokolewa kwa matendo peke yake (mfano unasema mimi nina vituo vya watoto yatima vingi so hiyo ndo price yangu ya kununua wokovu)

Kulea yatima na kusaidia watu ni jambo zuri lakini wokovu tunaupata kwa neema na kujinyenyekeza katika Jina lipitalo majina yote
Haswaa!..
Aliyeokoka hatendi dhambi ila hufanya makosa. Biblia inatuonesha hayupo mteule wa Mungu hata mmoja ambaye hakukosea hivyo inawezekana kuwa mteule na ukakosea pia .
 
Leo mtu akitokea na kuwauliza waumini wengi wa makanisa ya kiroho swali la Je! ni kweli tutakwenda mbinguni?.Bila shaka wengi watajibu ndiyo na sababu watakayoitoa kubwa ni kwamba wamempokea na kumkiti Yesu kama Mwokozi. Lakini pamoja na jibu hilo bado siyo sababu kuu ingawa ni sehemu tu. Ipo namna ambayo Mungu ameifanya kwa watu kupata wokovu na kudumu katika wokovu.

Changamoto kubwa leo watu wengi wanakiribvitu wasivyovielewa Kwa mfano mtu akija akikuambia ipo jehanamu ya moto, jehanamu ni halisi, ukifavutaingia motoni unaweza kujenga hofu ila ukweli hatuingii mbinguni kwa sababu sababu ya kukwepa au kuogopa moto.

Wahubiri wengi leo wamesahau kabisa kufundisha juu ya misingi aliyoiweka Mungu inayowaunganisha wanadamu na wokovu. Wayahudi walipata nafasi ya kwanza ya wokovu Kwa sababu ya misingi yao ya ufuasi na Mungu alijidhihirisha kwao kupitia utamaduni huo wa ufuasi. Mungu alijidhihirisha kwao kama Mungu wa Baba zao, waliishi katika misingi hiyo ya ufuasi kiasi kwamba wakipoikiuka walipata mapigo.

Angalia jambo la hatari itakuwaje siku ya mwisho mtu anaambiwa na Mungu toka sikujui?.Unamueleza Mungu kuwa ukifanya unabii n.k Kwa kina lake halafu anasema hakujui!..Hii ina maanidha mtu anaweza kuwa muongofu wa imani na anajitoa sana katika masuala mbalimbali mahali anaposalia lakini yeye asitambuliwe na Mungu ila yule aliyewasaidia masikini Kwa kumpatia chakula, maji na mavazi, aliyewaona wafungwa Mungu akamwona ni mwenye heri kwa sababu alimsaidia alipokosa chakula, alimvisha alipokosa mavazi n.k.

Hii inaonesha yale unayowafanyia wengine ndiyo had utamaduni uliojifungamanisha nao na ndiyo utakaokuwezesha kumuona Mungu ila siyo kukiri usiyoyafahamu. Hatutakiwi kukiri jambo tusiloliamini au tusilolifamu wala kuwa na uhakika nalo "you should not make confession to what you are not convicted by". Ibrahimu alihesabiwa haki sababu ya kuwa na imani thabiti "conviction".Uhakika wako ndiyo unaokupelekea wokovu.

Jiulize taratibu tu ni kwa nini Leo nyumba za ibada zimejaa watu wanaosema wameokoka lakini wanatenda dhambi? Biblia inasema aliyeokolewa hatendi dhambi tena lakini ikitokea mtu anasema ameokoka na anaendelea kutenda dhambi kuna tatizo mahali. Inawezekana mtu huyo kuna hatua za mdsingi alizikosabna huenda aliyemuongoza mtu huyo alimwelekeza kufanya matamko tu ya kukiri na siyo katika uhakika wa mabadiliko ya mtindo wa maisha. Tunapoongoka sharti tupokee na mtindo wa maisha.

Hatupati wokovu Kwa kutamka tu 'tumeokoka' ila ni kwa kuwa na uhakika na imani dhabiti moyoni. Wokovu ni pale vitu vinavyoanza kubadilika ndani ya moyo wako na kuanza kufahamu maisha bila Yesu ni bure. Mtu huanza kutanani kuwa na Mungu, kumuona kuliko kitu chochote kile. Ila ukiona una mashaka mfano unajiuliza hivi Yesu akirudi mara ya pili nitantakuliwa au la!.. ukiona una swali la aina hiyo elewa hautaiona pepo na haujaokoka bado.
Mpotoshaji mkubwa.

Wokovu unapatikana kwa kumkiri Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wako, kuwa Yeye alikufa kwa niaba yako ili wewe usamehewe dhambi zako zote - ulizowahi kuzifanya, unazofanya sasa, na utakazofanya mbeleni. Na si vinginevyo.
 
Samahani ila niulize tu, Hivi neno kuokoka aga mnalichukuliaje nyie watu? Ndo ile kujiona huna dhambi tena hukosei na yesu akija tu 💯 pepo ni yako?
Hapana, mtu anaweza kuokoka na akakosea pia.
Hili halizuii kuwa mteule( Ibrahimu, Daudi, Ayubu, Enoka, Musa , Petro....n.k walikosea ila haiondoi uteule wao.
 
Mpotoshaji mkubwa.

Wokovu unapatikana kwa kumkiri Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wako, kuwa Yeye alikufa kwa niaba yako ili wewe usamehewe dhambi zako zote - ulizowahi kuzifanya, unazofanya sasa, na utakazofanya mbeleni. Na si vinginevyo.
Kama ni hivyo tu wanaomkiri ni wengi mno hata wewe ila suala ni kuwa mfuasi wake, kuishi ukristo. Jaribu kuelewa kwanza kuna jambo wengi hatuelewi kuhusi wokovu.
Yesu aliwaelekeza wanafunzi wake kuenenda na kuwafanya watu kuwa wafuasi, unaelewa maana ya kuwa wafuasi nukta.
 
Kama ni hivyo tu wanaomkiri ni wengi mno hata wewe ila suala ni kuwa mfuasi wake, kuishi ukristo. Karibu kuelewa kwanza kuna jambo wengi hatuelewi kuhusi wokovu.
Yesu aliwaelekeza wanafunzi wake kuenenda na kuwafanya watu kuwa wafuasi, unaelewa maana ya kuwa wafuasi nukta.
Kama wanamkiri, wameokoka. Ufuasi - matendo na tabia njema ni matunda ya wokovu. Tabia njema au matendo mema havimwokoi mtu.
 
Kama wanamkiri, wameokoka. Ufuasi - matendo na tabia njema ni matunda ya wokovu. Tabia njema au matendo mema havimwokoi mtu.
Naam, wokovu ni mtindo wa maisha " life style" na unaanzia moyoni , huwezi kusema umeokoka halafu unaishi maishha yaleyale" there must be transformations".
 
Naam, wokovu ni mtindo wa maisha " life style" na unaanzia moyoni , huwezi kusema umeokoka halafu unaishi maishha yaleyale" there must be transformations".
Soma hapa kwa kutulia na soma hizo nukuu zote kutoka Biblia:

Wokovu ni nini ? Mtu anapataje wokovu ?


Mtu anakuwaje mkristo ? Mkristo ni nani ?

 
Samahani ila niulize tu, Hivi neno kuokoka aga mnalichukuliaje nyie watu? Ndo ile kujiona huna dhambi tena hukosei na yesu akija tu pepo ni yako?
Kuokoka nikujionyesha kwa watu hauna dhambi na kuonyesha watu haupendi dhambi ,na kuonyesha watu unasal sala ndefu, na kufunga kila kila mara .
 
S
Soma hapa kwa kutulia na soma hizo nukuu zote kutoka Biblia:

Wokovu ni nini ? Mtu anapataje wokovu ?


Mtu anakuwaje mkristo ? Mkristo ni nani ?

Shukrani nitapitia kwa utaratibu kabisa Mkuu
 
Back
Top Bottom