Namna ya kusafisha pasi yako

Namna ya kusafisha pasi yako

Chukua pasi yako toka nayo nje, angalia sehemu yenye mchanga mzuri na msafi (sio udongo) isugue hapo mara kadhaa utaiona inang'aa kama ndio inatoka Kwa shop
 
Habari wana JF
Nimekumbwa na changamoto moja ya kupasi nguo zangu mwenyewe zoezi nililoliacha miaka thelathini iliyopita, nimeshika pasi naona ni chafu sana. Huko zamani kuna dawa tulikua tunaiweka alafu uchafu unatoka na yenyewe inatoa moshi mkali, sijui ni panadol au septrin ila nimesahau na ni muda mrefu. Naomba kujuzwa njia nyepesi ili nisiunguze nguo zangu na kuzichafua, Asanteni.
 
Habari wana JF
Nimekumbwa na changamoto moja ya kupasi nguo zangu mwenyewe zoezi nililoliacha miaka thelathini iliyopita, nimeshika pasi naona ni chafu sana. Huko zamani kuna dawa tulikua tunaiweka alafu uchafu unatoka na yenyewe inatoa moshi mkali, sijui ni panadol au septrin ila nimesahau na ni muda mrefu. Naomba kujuzwa njia nyepesi ili niunguze nguo zangu na kuzichafua, Asanteni.
iwashe then ikichemka pangusa na kidonge cha panadal, alafu futa na kitambaa chochote baada ya kidonge kuyeyuka, it wil be very fine
 
Washa pasi yako (iweke kwenye umeme), ikipata moto, sugua au safisha kwa panadol/paracetamol/ sina uhakika kama kila kidonge kinafaa.
Baada ya hapo kidonge kitakua kama kinayeyuka kikitoa moshi, pangusa kwa kitamaa kuondoa huo uchafu, utaiacha pasi yako ikiwa safi.

Kwa hisani ya wahenga!
 
Washa pasi yako (iweke kwenye umeme), ikipata moto, sugua au safisha kwa panadol/paracetamol/ sina uhakika kama kila kidonge kinafaa.
Baada ya hapo kidonge kitakua kama kinayeyuka kikitoa moshi, pangusa kwa kitamaa kuondoa huo uchafu, utaiacha pasi yako ikiwa safi.

Kwa hisani ya wahenga!
Asante sana Mkuu
 
Paracetamol au panadol.....unawasha pasi iache ipate joto la kutosha kisha chukua kidonge kishikilie kwa kitu kama katasi then unasugua mkuu
 
Back
Top Bottom