Namna ya kusafisha pasi yako

Namna ya kusafisha pasi yako

Habari wana JF
Nimekumbwa na changamoto moja ya kupasi nguo zangu mwenyewe zoezi nililoliacha miaka thelathini iliyopita, nimeshika pasi naona ni chafu sana. Huko zamani kuna dawa tulikua tunaiweka alafu uchafu unatoka na yenyewe inatoa moshi mkali, sijui ni panadol au septrin ila nimesahau na ni muda mrefu. Naomba kujuzwa njia nyepesi ili niunguze nguo zangu na kuzichafua, Asanteni.

Washa pasi moto mzur sugua na panadol then futia tissue za maji I mean wipes
 
Paracetamol au panadol.....unawasha pasi iache ipate joto la kutosha kisha chukua kidonge kishikilie kwa kitu kama katasi then unasugua mkuu
Sijajua mnaosema panadol au paracetamol mmefanya utafiti wa madhara ya moshi utoakanao na kuungua kwa kemikali hiyo ikiingia kwenye mapafu ina madhara gani? halafu kwa pasi zenye matundu ya kutolea maji chini uchafu ukishayeyushwa na kidonge hicho unajificha kwenye matundu hayo je inasaidia?
 
Sijajua mnaosema panadol au paracetamol mmefanya utafiti wa madhara ya moshi utoakanao na kuungua kwa kemikali hiyo ikiingia kwenye mapafu ina madhara gani? halafu kwa pasi zenye matundu ya kutolea maji chini uchafu ukishayeyushwa na kidonge hicho unajificha kwenye matundu hayo je inasaidia?
Nini kifanyike?Anunue pasi mpya ama?
 
Sijajua mnaosema panadol au paracetamol mmefanya utafiti wa madhara ya moshi utoakanao na kuungua kwa kemikali hiyo ikiingia kwenye mapafu ina madhara gani? halafu kwa pasi zenye matundu ya kutolea maji chini uchafu ukishayeyushwa na kidonge hicho unajificha kwenye matundu hayo je inasaidia?
Swali zuri sana, maaana ndiyo nataka nianze kutafuta hizo pain killers
 
Habari wana JF
Nimekumbwa na changamoto moja ya kupasi nguo zangu mwenyewe zoezi nililoliacha miaka thelathini iliyopita, nimeshika pasi naona ni chafu sana. Huko zamani kuna dawa tulikua tunaiweka alafu uchafu unatoka na yenyewe inatoa moshi mkali, sijui ni panadol au septrin ila nimesahau na ni muda mrefu. Naomba kujuzwa njia nyepesi ili nisiunguze nguo zangu na kuzichafua, Asanteni.
Hiyo dawa uliyoisahau ni kidonge cha ASPIRIN. Njia nyingine ni kwa kutumia chaki nyeupe (hizi hizi za kuandikia ubaoni).

Set pasi yako ya umeme kwenye Maximum Temperature kisha isubiri ichemke. Ikikata moto sababu ya joto, anza kukwangua uchafu kwa kutumia chaki. Uchafu unaondoka wote. Ukishamaliza, iache ipoe kisha ifute kwa kitambaa kilicholowekwa kwenye maji kuondoa vumbi la chaki. YOU ARE DONE.....
 
Unaweza kutumia chumvi pia. Unaiweka chumvi kwenye karatasi nzito kama rim paper then pasi iliyo kwenye umeme unaisugulia kwenye chumvi.
Inakua safiiii
 
wenzetu wameweka kiwango cha moto na aina ya nguo sie kwa haraka ama kujisahau tunakiuka miongozo hiyooo

panadol huwa inaharibu sanaaa tu...tabaka (layer) lililowekwa kwenye pasi likishaharibiwa kidogo ubora wa pasi wapungua
 
Panadol inaharibu sanaa ipi? uchoraji,uimbaji,uchongaji?
wenzetu wameweka kiwango cha moto na aina ya nguo sie kwa haraka ama kujisahau tunakiuka miongozo hiyooo

panadol huwa inaharibu sanaaa tu...tabaka (layer) lililowekwa kwenye pasi likishaharibiwa kidogo ubora wa pasi wapungua
 
Nimejaribu baking powder ina work.Unaimiminia eneo lenye uchafu then pasi ikikolea joto sugua na karatasi ngumu inatoa vzur kweli
 
Back
Top Bottom