Namna bora ya kukata roho

Namna bora ya kukata roho

Mshana nipo China kwa sasa, nitaishi huku miaka mitatu, naweza kupata sehemu ya kufundishwa hayo mambo unayoyajua?
Maana huku naona karibu kila kitu ukitaka unapata.
Inaitwaje/ niulizeje nijiunge hata kwa kulipia
Elimu yako imekuongezea hekima nyingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana nipo China kwa sasa, nitaishi huku miaka mitatu, naweza kupata sehemu ya kufundishwa hayo mambo unayoyajua?
Maana huku naona karibu kila kitu ukitaka unapata.
Inaitwaje/ niulizeje nijiunge hata kwa kulipia
Elimu yako imekuongezea hekima nyingi

Sent using Jamii Forums mobile app
Safi kabisa huko soma Taoisim, Confucius au Analects

Jr
 
mshana jr kuna kisa nimekutana nacho siku chache zilizopita kuna mzee aligoma kufa ikafika hatua wakawa wanamuombea afe...yaani yuko kitandani muda mrefu..wakimpeleka hospital wanaambiwa mrudisheni tu nyumbani..

Kilichonishangaza ni kwamba eti hawa wazee wa zamani kuna vitu walikua wanameza ambavyo vinawafanya hii process unayoizungumzia hapa kuwa ngumu kwao..hii imekaaje..
 
Si kweli huu ni upotoshaji wa shetani ili watu wengi wapotee na wasiende mbinguni na wasimtumainie Mungu

Duniani kuna nguvu mbili tu ya Mungu na ya shetani yaani ya wema au ubaya

Ili kwenda mbinguni inakubidi uwe chini ya nguvu ya Mungu na hakuna yeyote anaeweza kwenda kwa Mungu bila kujitoa kikamilifu kwake na haikuhitaji kufanya chochote cha ziada ili kuwa kwake ila kila kitu kimeshaandaliwa kwa wote wanaokubali kumtii

Hayo mengine ni mbinu za shetani kuwapa watu matumaini ya uongo ili waweze kujitumainia wenyewe na mwisho wafe ktk dhambi zao na kuangamia ktk moto siku ya hukumu

Kwa mujibu wa biblia mtu anapokufa anarudi ktk hali aliyokuwa nayo ya kutojifahamu kabla hajazaliwa hadi atakapofufuliwa tena kwa ajili ya hukumu ndipo atakapopata tena fahamu na kwenda motoni au mbinguni kupo chini ya Mungu yaani siku ya hukumu tambua hakuna binadamu ama roho yoyote inayoweza isaidia roho nyingine kwenda popote pale mbinguni ama motoni hizo ni porojo za shetani
Nami ntatoa ushuhuda wa meditation hii kitu ni kweli aisee ila sio hii ya mshana jr, hii inatisha
 
Muda wote huo niliona alivyokuwa akipambana roho isimuache. Niliingia ulimwengu wa roho kimyakimya kumsaidia uhai, mapambano. Ni kupitia huko nilimuona akielea mbali kabisa na mimi. Alikuwa mwepesi na mwenye kasi ya ajabu. Nilirudi kimwili na kumuona akijaribu kupepesa macho huku madaktari kwa juhudi kubwa wakifanya hand pumping, mashine ilikuwa imeshashindwa kazi.

Duuuuhh katika siku ambazo hujaeleweka na SIJAKUELEWA KABISA ni leo,


1. kumsaidiaje? kuifukuzia roho irudi? kuikamata? napata maswali mengi yasiyo na majibu kabisaa, HOW?
2. Kama ndi hivyo hata roho ya TAL unaweza kuiona saiv inafanyaje
yaana yanakuja maswali mengi yasiyo na majibu

Muhubiri 8:8
8 Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho;
Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa;
Wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile;
Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.
 
Kwa mujibu wa biblia mtu anapokufa anarudi ktk hali aliyokuwa nayo ya kutojifahamu kabla hajazaliwa hadi atakapofufuliwa tena kwa ajili ya hukumu ndipo atakapopata tena fahamu

Hapo napingana na wewe Kabisa, Nioneshe hilo andiko, navyojua na kuelewa mtu akifa anakua na fahamu zake zilezile tena zinakua MORE ACTIVE kuliko alivyokua, tena anajua na kuwakumbuka aliowaacha duniani kama ni ndugu,watoto,wazazi, marafiki, mali, heshima,cheo, hadi ugonjwa uliomuua anaujua mpk matendo alokua anaishi toka alivyozaliwa hadfi alivyokufa, kwa hapo tusidanganyane

N.B kumbuka TAJIRI NA MASKINI
 
Kwa muktadha wa Bible takatifu uko sahihi kabisa na nakubaliana nawe kwa asilimia mia moja lakini dunia hii ni zaidi ya uijuavyo
Kuna imani nyingi kuna dini nyingi na nyingine ni za ajabu hasa.... Nakushauri jifunze tu ujue lakini si lazima uamini au u practice... Mungu akurehemu

Jr
Mungu anamrehemu MAREHEMU tu bwana mshana usitake kumzika mtu bado yupo nyuma ya key-pard/board.
 
Mkuu mshana wewe siku hizi umekuwa msaidizi au aide de camp wa Israel mtpa roho..? Maana kuna sehemu umesema ulimsaidia kukata roho.
 
Back
Top Bottom