Namfagilia mhe mama Salma Kikwete

ama kweli mmetuokota watanzania!!!

mbona miradi yote iko mkoa wa pwani anakotoka mumewe? sio ukanda huu??

au sio ufadhili unaofuata mkondo wa madaraka ya mumewe?

bila urais wa mumewe, WAMA itabaki kitu gani?

urais wa mkapa ulipoisha, EOTF ilibaki kitu gani?

wamekulipa kiasi gani kuja kuwavua magamba hapa JF?

Sijalipwa chochote na wala sio wa type hiyo kama nyinyi ambao mnalipwa na CDM ili hata pale mambo mazuri yanafanyika hamuoni , MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA. Nimejitokeza kusema ninayo yajua sio kwa Kuvua mtu gamba, hakuna mwenye magamba ndani ya WAMA, kwa uongo ukirudiwa mara kwa mara huwa ukweli .

Taasisi yoyote inapotaka kufanya uwekezaji lazima inafanya tathimini ya maeneo ya kufanya uwekezaji huo, na ndio maana kuna upembuzi yakinifu unafanyika na kwa kuzingatia vigezo vinavyotolewa na Wafadhili wa miradi hii. WAMA inaongozwa kwa taratibu hizo. kwa mazingira na vigezo hivyo Rufiji ikachaguliwa na sio kwa kuwa Mkoa anakotoka Mhe Rais kama hivyo ndivyo kwanini miradi isiwekezwe BAGAMOYO

Mlitaka miradi hiyo ipelekwe maeneo ambayo huduma hizo zipo ? Shule imejengwa Pwani sawa, lakini mbona wanaosoma pale ni watoto toka Mikoa yote Ishirini na Sita ya Tanzania na kwa makabila yote ? Kama anaefadhili ujenzi wa hiyo shule ameridhika inatosha ! Akija F/Lady mwengine atawekeza maeneo mengine baada ya miaka kadhaa Nchi yetu yote itakuwa imefikiwa Mdau .

Hoja hapa ilikuwa kutoa DATA za namna gani Mama Salma anachangia shughuli za jamii kupitia Taasisi ya WAMA na sio Taasisi ya Maulaji na HAKUNA UFISADI WOWOTE
 
uwakumbushe. Tunapoongelea WAMA hatumaanishi hawa wafanyakazi wadogo wanaochapa kazi ili kupata mkate wao. Tunamaanisha mapapa wake za wakubwa au wakubwa wenyewe hapa chini:

Mama. Salma Kikwete Chairaperson mke wa rais Jakaya Kikwete
Mama. Sophia Simba Chairperson of the Board waziri katika utawala wa Kikwete
Mama. Zakia Zamdan Meghji Board Member waziri wa zamani wa fedha aliyeondolewa kwa ufisadi
Amb. Mwanaidi Majaar Sinare Board Member balozi wa serikali ya Kikwete nchini Marekani anayedaiwa kusaini mikataba mingi ya kifisadi na asikanushe
Mama. Regina Lowassa Board Member mke wa waziri mkuu wa zamani aliyetimuliwa kwa ufisadi
Mama. Blandina Nyoni Board Member
Mama Hulda S. Kibacha Board Member
Kama kweli nia ya WAMA ni njema na si kutafuta kuchuma kwa kutumia matatizo ya akina mama, kwanini kwenye bodi ambayo ndiyo roho ya WAMA hakuna wanawake wa mashambani ambao ndiyo walengwa na waathirika? Bila kutoa jibu linaloingia akilini kuhusiana na NGO hii ya mke wa rais na mashoga zake bado umma utaendelea kuamini ni ya kiulaji kama ilivyokuwa EOTF ya Anna Mkapa.Mbona siku hizi imedoda? Simple. Mkapa si rais tena. Naandaa makala iitwayo WAMA ni wizara ya mambo yote. Je wizara husika zitafanya kazi gani? WAMA bado itaendelea kuwa kitendawili cha utawala wa kujuana na kuibiana hadi itakapotokomea baada ya Kikwete kuondoka madarakani hapa 2015. Tusiruhusu rais ajaye kuwa na NGO ya mkewe. Ni ufisadi wa kimfumo huu.:kev::kev::kev::kev::kev::kev::kev:

Hongera sana mkuu kwa useful taarifa,endelea kupayuka taarifa muhimu kuokoa taifa tajiri ila masikin wa fikra, ungekuwa hapa ningekupa glas ya wine au walau pepsi ya bariiidi! let him coment hapa,yeye ni kibaraka tuu!!
 
1. kungekuwa na dhambi gani kama angeendelea kufundisha hata baada ya mumewe kuwa rais?

2. je kazi pekee inayomfaa FL wa nchi kama yetu ni "kuongoza" NGO tu? tena yenye ofisi zake ikulu (au karibu na ikulu)?

umeona nchi gani first lady anafundisha jamani mbona mna chuki binafsi?olewa na wewe na j.k mke wa pili uwe second lady uanzishe wama B
 
uwakumbushe. Tunapoongelea WAMA hatumaanishi hawa wafanyakazi wadogo wanaochapa kazi ili kupata mkate wao. Tunamaanisha mapapa wake za wakubwa au wakubwa wenyewe hapa chini:

Mama. Salma Kikwete Chairaperson mke wa rais Jakaya Kikwete
Mama. Sophia Simba Chairperson of the Board waziri katika utawala wa Kikwete
Mama. Zakia Zamdan Meghji Board Member waziri wa zamani wa fedha aliyeondolewa kwa ufisadi
Amb. Mwanaidi Majaar Sinare Board Member balozi wa serikali ya Kikwete nchini Marekani anayedaiwa kusaini mikataba mingi ya kifisadi na asikanushe
Mama. Regina Lowassa Board Member mke wa waziri mkuu wa zamani aliyetimuliwa kwa ufisadi
Mama. Blandina Nyoni Board Member
Mama Hulda S. Kibacha Board Member
Kama kweli nia ya WAMA ni njema na si kutafuta kuchuma kwa kutumia matatizo ya akina mama, kwanini kwenye bodi ambayo ndiyo roho ya WAMA hakuna wanawake wa mashambani ambao ndiyo walengwa na waathirika? Bila kutoa jibu linaloingia akilini kuhusiana na NGO hii ya mke wa rais na mashoga zake bado umma utaendelea kuamini ni ya kiulaji kama ilivyokuwa EOTF ya Anna Mkapa.Mbona siku hizi imedoda? Simple. Mkapa si rais tena. Naandaa makala iitwayo WAMA ni wizara ya mambo yote. Je wizara husika zitafanya kazi gani? WAMA bado itaendelea kuwa kitendawili cha utawala wa kujuana na kuibiana hadi itakapotokomea baada ya Kikwete kuondoka madarakani hapa 2015. Tusiruhusu rais ajaye kuwa na NGO ya mkewe. Ni ufisadi wa kimfumo huu.:kev::kev::kev::kev::kev::kev::kev:

DUA la kuku Halimpati Mwewe , WAMA itaendelea hata Rais Kikwete atakapoondoka madarakani. Ni Taasisi inayoendeshwa kisomi ina mpango mkakati wake Strategic Plan ya miaka mitano mitano ( 2010-2015) ,inatumia MTEF kupanga mipango yake , inafanya SWOT analysis kila wakati . Hata EOTF inaendesha shughuli zake kama kawaida nenda kaitembelee Chang'ombe ipo imejaa tele.

Kuhusu wajumbe wa Bodi hapo juu, nashauri rudi darasani hususan fanya mapitio ya somo la Governance/ Organisation Development ukichukua MBA option yoyote utapitia hilo somo halafu jiridhishe na topic /sub topic inayohusu Roles za Board of Directors halafu utapata jibu la kwanini wameteuliwa watu wa kaliba tofauti wao sio watendaji Ufisadi huo wataufanyaje . Mmeshaona hoja yenu ya Mhe Mama Salma kwenye Taasisi yake ameweka ndugu zake ,n mkabila na mdini haina mshiko !


Na kwataarifa yenu Wajumbe hao wa Board wanafanya kwa kujitolea tu hawana hata Ada yoyote wanayolipwa hata sitting allowance hawalipwi kamwe . Waacheni wafanye kazi yao .HAKUNA UFISADI WAMA NA KAMWE HAUTATOKEA
 
Sijalipwa chochote na wala sio wa type hiyo kama nyinyi ambao mnalipwa na CDM ili hata pale mambo mazuri yanafanyika hamuoni , MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA. Nimejitokeza kusema ninayo yajua sio kwa Kuvua mtu gamba, hakuna mwenye magamba ndani ya WAMA, kwa uongo ukirudiwa mara kwa mara huwa ukweli .

Taasisi yoyote inapotaka kufanya uwekezaji lazima inafanya tathimini ya maeneo ya kufanya uwekezaji huo, na ndio maana kuna upembuzi yakinifu unafanyika na kwa kuzingatia vigezo vinavyotolewa na Wafadhili wa miradi hii. WAMA inaongozwa kwa taratibu hizo. kwa mazingira na vigezo hivyo Rufiji ikachaguliwa na sio kwa kuwa Mkoa anakotoka Mhe Rais kama hivyo ndivyo kwanini miradi isiwekezwe BAGAMOYO

Mlitaka miradi hiyo ipelekwe maeneo ambayo huduma hizo zipo ? Shule imejengwa Pwani sawa, lakini mbona wanaosoma pale ni watoto toka Mikoa yote Ishirini na Sita ya Tanzania na kwa makabila yote ? Kama anaefadhili ujenzi wa hiyo shule ameridhika inatosha ! Akija F/Lady mwengine atawekeza maeneo mengine baada ya miaka kadhaa Nchi yetu yote itakuwa imefikiwa Mdau .

Hoja hapa ilikuwa kutoa DATA za namna gani Mama Salma anachangia shughuli za jamii kupitia Taasisi ya WAMA na sio Taasisi ya Maulaji na HAKUNA UFISADI WOWOTE

hakuna shida, nimekusamehe kujibu maswali mengine baada ya kuhisi kuwa kuna mambo mawili:

1. hapo ndipo upeo wako ulipoishia

2. unajitahidi kubaki within your terms of reference!

jitahidi uvue magamba, WAMA = EOTF = kisu kikali cha first lady kwenye keki ya taifa = ujasirimali wa kisasa ndani ya ikulu!

amini usiamini, WAMA haiwezi ku-survive hata kwa sekunde mbili ikiwa nje ya ikulu!!

kama uko timamu upstairs umeelewa.

happy Easter!
 
umeona nchi gani first lady anafundisha jamani mbona mna chuki binafsi?olewa na wewe na j.k mke wa pili uwe second lady uanzishe wama B

unapaswa kuwaomba radhi walimu wote duniani kwa kauli yao hii!!!

kama kuolewa dili, olewa wewe. kwa upande wangu kama ni kukaa ikulu naweza hata kugombea urais wenyewe miaka ijayo, wewe usiyeamini kuwa ikulu ni haki ya kila mtanzania kufanya kazi kajichekeshe kwa mmkwere uolewe!

samahani kama nimekukwaza.
 
Mkufu,
Hata mimi nina admire kazi anayofanya Bi. Salma Kikwete. Lakini nina swali dogo tu. What happens to WAMA when her term in the ikulu is kwishney? Ataendelea na usimamizi wa NGO hiyo au atampisha atakayechukua nafasi yake? Au itaishia kimya kimya kama ilivyotokea kwa ile ya Mama Mkapa? Asante.
 
Sijalipwa chochote na wala sio wa type hiyo kama nyinyi ambao mnalipwa na CDM ili hata pale mambo mazuri yanafanyika hamuoni , MWENYE MACHO HAAMBIWI TAZAMA. Nimejitokeza kusema ninayo yajua sio kwa Kuvua mtu gamba, hakuna mwenye magamba ndani ya WAMA, kwa uongo ukirudiwa mara kwa mara huwa ukweli .

Taasisi yoyote inapotaka kufanya uwekezaji lazima inafanya tathimini ya maeneo ya kufanya uwekezaji huo, na ndio maana kuna upembuzi yakinifu unafanyika na kwa kuzingatia vigezo vinavyotolewa na Wafadhili wa miradi hii. WAMA inaongozwa kwa taratibu hizo. kwa mazingira na vigezo hivyo Rufiji ikachaguliwa na sio kwa kuwa Mkoa anakotoka Mhe Rais kama hivyo ndivyo kwanini miradi isiwekezwe BAGAMOYO

Mlitaka miradi hiyo ipelekwe maeneo ambayo huduma hizo zipo ? Shule imejengwa Pwani sawa, lakini mbona wanaosoma pale ni watoto toka Mikoa yote Ishirini na Sita ya Tanzania na kwa makabila yote ? Kama anaefadhili ujenzi wa hiyo shule ameridhika inatosha ! Akija F/Lady mwengine atawekeza maeneo mengine baada ya miaka kadhaa Nchi yetu yote itakuwa imefikiwa Mdau .

Hoja hapa ilikuwa kutoa DATA za namna gani Mama Salma anachangia shughuli za jamii kupitia Taasisi ya WAMA na sio Taasisi ya Maulaji na HAKUNA UFISADI WOWOTE


hapo kwenye nyekundu ndio pamejibu maswali niliyokua najiuliza... mtateseka sana
 
hakuna shida, nimekusamehe kujibu maswali mengine baada ya kuhisi kuwa kuna mambo mawili:

1. hapo ndipo upeo wako ulipoishia

2. unajitahidi kubaki within your terms of reference!

jitahidi uvue magamba, WAMA = EOTF = kisu kikali cha first lady kwenye keki ya taifa = ujasirimali wa kisasa ndani ya ikulu!

amini usiamini, WAMA haiwezi ku-survive hata kwa sekunde mbili ikiwa nje ya ikulu!!

kama uko timamu upstairs umeelewa.

happy Easter!

Happy Easter nawe Mdau hakuna swali ambalo sikulijibu. Upeo wangu mi mkubwa sana kuliko unavyofikiri ! WAMA itaendelea kuwepo Daima kwani ilipokuwa inawekeza na inaendelea kuwekeza hawakukurupuka tu, imetumia Consultant anaeijua kazi yake . Hata hivyo kwenye Elimu shule iliyojengwa itadumu zaidi ya miaka mia sasa utasemaje WAMA haitakuwepo Mhe JK akiondoka Ikulu . Hata hivyo Mfadhili aliesaidia kujenga hiyo shule Bw Nakayama yupo na ana obligation ya kusaidia WAMA Forever nyie vipi ? Subirini muone misaada yake kwa watoto yatima itakavyomiminika kwani huyu Mfadhili ameridhika na matumizi ya Pesa zake hazikuchakachuliwa !

WAMA itaendelea kudumu kwenye mioyo ya watoto wanaotoka kwenye mazingira hatarishi na yatima wanaofaidika na udhamini wa Elimu kwa kadiri mungu atakavyowawezesha . Na kwa vile wanatoka Mikoa yote hapa Tanzania hawa ni MABALOZI WA WAMA DAIMA DAWAMU NA INATOSHA KABISA . Ni hivyo tu we mdau hutokani na mazingira magumu lakini ungeikubali kazi ya mama salma kama ungeonja mazingira hayo bila ya kujali Bodi yake ina wajumbe wa aina gani .
 
]
Muda wake wa kukaa madarakani utakwisha
[/COLOR] l

Mkufu, naomba ufafanuzi hivyo mama Salma ana muda wa kukaa madarakani?

Awali ya yote, ni madaraka gani hayo aliyo nayo mke wa rais, na madaraka hayo yametolewa na sheria gani naomba utueleze kuhusu hili maana hii ni mara ya kwanza kusikia na kwa kiasi imenistua sana.
 
hapo kwenye nyekundu ndio pamejibu maswali niliyokua najiuliza... mtateseka sana

Wala hakuna anaeteseka , Kelele za Mlango hazimnyimi mwenye nyumba usingizi ! Mnasema weeeee lakini Taasisi za nje zinazidi kumfagilia F/L wa Ukweli Mhe Mama Salma Kikwete na juzi tu mlimuona kwenye Fund raising ya kuchangisha pesa za kusafirisha vifaa vya kutolea huduma ya afya na watu zaidi 1200 walihudhuria toka Taasisi mbalimbali USA zilihudhuria na Tanzania imesaidiwa vifaa vya afya vyenye thamani ya bilioni 45 kupitia F/L wetu Hongera mama Salma mwendo mdundo. Waache Waseme Mchana Usiku Watalala
 
Mkufu, naomba ufafanuzi hivyo mama Salma ana muda wa kukaa madarakani?

Awali ya yote, ni madaraka gani hayo aliyo nayo mke wa rais, na madaraka hayo yametolewa na sheria gani naomba utueleze kuhusu hili maana hii ni mara ya kwanza kusikia na kwa kiasi imenistua sana.

Mdau naamaanisha muda wa kukaa madarakani mumewe Mhe Rais utakapoisha na yeye U F/Lady nao unaisha
 
DUA la kuku Halimpati Mwewe , WAMA itaendelea hata Rais Kikwete atakapoondoka madarakani. Ni Taasisi inayoendeshwa kisomi ina mpango mkakati wake Strategic Plan ya miaka mitano mitano ( 2010-2015) ,inatumia MTEF kupanga mipango yake , inafanya SWOT analysis kila wakati . Hata EOTF inaendesha shughuli zake kama kawaida nenda kaitembelee Chang'ombe ipo imejaa tele.

Kuhusu wajumbe wa Bodi hapo juu, nashauri rudi darasani hususan fanya mapitio ya somo la Governance/ Organisation Development ukichukua MBA option yoyote utapitia hilo somo halafu jiridhishe na topic /sub topic inayohusu Roles za Board of Directors halafu utapata jibu la kwanini wameteuliwa watu wa kaliba tofauti wao sio watendaji Ufisadi huo wataufanyaje . Mmeshaona hoja yenu ya Mhe Mama Salma kwenye Taasisi yake ameweka ndugu zake ,n mkabila na mdini haina mshiko !


Na kwataarifa yenu Wajumbe hao wa Board wanafanya kwa kujitolea tu hawana hata Ada yoyote wanayolipwa hata sitting allowance hawalipwi kamwe . Waacheni wafanye kazi yao .HAKUNA UFISADI WAMA NA KAMWE HAUTATOKEA
We jamaa unaonekana umekaa mkao wa kujikomba komba ili mama salma akuone na kukukomboa. Lakini kamwe hautapanda kwa kutumia migongo ya wana JF. Upuuzi huu ambao we unadhani ni mafanikio bila ya kutueleza kama wamama yako ina sustainability yoyote baada ya JK kutoka ikulu, ujinga mtupu. Nyie ndo zama za utumwa zikirudishwa leo mtajipeleka wenyewe utumwani. We tangu lini mwalimu wa chekechea akawa na maarifa ya kutoa kitu chenye akili wakati yeye hana. Si angetumia hizo akili kujiendeleza kuwa mwalimu wa shule ya msingi
 
Mkufu,
Hata mimi nina admire kazi anayofanya Bi. Salma Kikwete. Lakini nina swali dogo tu. What happens to WAMA when her term in the ikulu is kwishney? Ataendelea na usimamizi wa NGO hiyo au atampisha atakayechukua nafasi yake? Au itaishia kimya kimya kama ilivyotokea kwa ile ya Mama Mkapa? Asante.

Ukiisha muda wake wa kuwa F/L Taasisi itaendelewa kustawi, kwa kuwa madhumuni ya kuundwa kwake yapo kwenye MEMARTS yake, waweza tembelea WAMA watakupa nakala . Pia Bodi ya wakurugenzi ipo itaendelea kuisimamia Taasisi si mama salma mwenye jukumu la kuisimamia peke yake La hasha ni la Bodi nzima na wapo makini sana na jukumu hilo. Nakutoa wasiwasi Mdau WAMA itakuwepo na Mama Salma taendelea ku shine kama KAWA
 
unapaswa kuwaomba radhi walimu wote duniani kwa kauli yao hii!!!

kama kuolewa dili, olewa wewe. kwa upande wangu kama ni kukaa ikulu naweza hata kugombea urais wenyewe miaka ijayo, wewe usiyeamini kuwa ikulu ni haki ya kila mtanzania kufanya kazi kajichekeshe kwa mmkwere uolewe!

samahani kama nimekukwaza.[

hahaha!
nawaheshimu walimu sana ila sio mama salma aendelee kufundisha na u first lady hata kama ualimu ni wito......uraisi mwema mama ila usimwonee gere mama salma
 
Mkufu,
Hata mimi nina admire kazi anayofanya Bi. Salma Kikwete. Lakini nina swali dogo tu. What happens to WAMA when her term in the ikulu is kwishney? Ataendelea na usimamizi wa NGO hiyo au atampisha atakayechukua nafasi yake? Au itaishia kimya kimya kama ilivyotokea kwa ile ya Mama Mkapa? Asante.

Binadamu ukichagua kuwa mnafiki bana ni chaguo baya sana, wewe unachotaka ni kuona hiyo NGO inasurvive baada ya urais wa waume zao au unataka kuona matokeo mazuri ya kazi zao?. Kwani wama ikifa wakati shule zimejengwa na vimwana wamesomeshwa kuna ubaya gani aise?. Kuhusu matumizi ya ya jina jina la ikulu au matumizi ya wadhifa wa mkumewe kufanya fundrising na kupata pesa za kusaidia jamii nadhani hiyo ni faida kwetu kama angeitwa First lady kisha Akajiketia tu mbuzini akikuna nazi we ungejisikiaje?.
 
Rais Salma, Rahma na Kikwete na walamba viatu wao



Kwa wanaojua urais barani Afrika ulivyo mtaji mkubwa kwa familia na waramba viatu wa kwenye kuwa nao, watakubaliana nasi kitu kimoja. Chunguza picha hiyo hapo juu ambapo Rais wa WAMA, Salma Kikwete yuko ziarani nchini Marekani.
Je Salma amekuwa rais lini zaidi ya baada ya mumewe kuwa rais? Kabla hapo rais wa kutumia NGO hakuwa mwingine bali Anna Mkapa ambaye alitimka baada ya mumewe kuutema ulaji.

Je rais Salma ameandamana na nani? Kwenye picha anaonekana Zakhia Meghji aliyekuwa waziri wa fedha wa mumewe kabla ya kuondolewa kwa kashfa mbali mbali za wizi wa mabilioni ya fedha za umma.

Anayefuata nani? Mwanaidi Maajar ambaye ni balozi wa mumewe nchini Marekani anayetuhumiwa kusaini nyaraka za baadhi ufisadi wa kutisha na mwisho wa yote kuzawadiwa ubalozi. Je aliteuliwa kuwa balozi kutokana na merit au kuwa karibu na bwana au bi mkubwa kama anavyooneka? Je ni wangapi wamo kwenye ofisi za umma kupitia mgongoni mwa ufisadi huu wa kunuka unaoendelea kuvumiliwa? Tuliwahi kuandika makala ya Hidden Presidents of Africa.

Wanaoikumbuka wanaweza kujua ni marais wangapi Afrika inao nyuma ya pazia. Wa mwisho mkumbuke Simone Gbagbo na alivyoisha kabla ya Suzana Mubarak na Leila Trebelsi wa Tunisia. Wakumbuke marais hawa waliopata urais kutokana na kulala kitanda kimoja na rais wako wakati ukiangalia picha ya rais huyo wa WAMA.

Bado rais Rahma al Kharoos Kasiga wa RBP Group ambayo imeota baada ya Kikwete kuingia madarakani.
 
We jamaa unaonekana umekaa mkao wa kujikomba komba ili mama salma akuone na kukukomboa. Lakini kamwe hautapanda kwa kutumia migongo ya wana JF. Upuuzi huu ambao we unadhani ni mafanikio bila ya kutueleza kama wamama yako ina sustainability yoyote baada ya JK kutoka ikulu, ujinga mtupu. Nyie ndo zama za utumwa zikirudishwa leo mtajipeleka wenyewe utumwani. We tangu lini mwalimu wa chekechea akawa na maarifa ya kutoa kitu chenye akili wakati yeye hana. Si angetumia hizo akili kujiendeleza kuwa mwalimu wa shule ya msingi

Kweli humu Jamvini kumbe kuna watu wanaendekeza ushabiki , Mama Salma humjui hajapata kuwa Mwalimu wa Chekechea ingawa si dhambi kuwa mwalimu wa Chekechea kwani mwanzo wa Hesabu ni Moja ! N i mwalimu wa shule ya Msingi ana elimu yake nzuri tu na vipaji lukuki , kwani Rais Zuma wa Afrika kusini ana elimu ya Level gani ? Mbona anafanya wonders huko ? sustainability ya WAMA inakuhusu nini ? nilikuwa natoa data kukanusha ufisadi katika Taasisi ya WAMA na kueleza hapa Jamvini ambapo kuna watu wanajitokeza na kujifanya vipofu kutoona WAMA imewafanyia nini wanajamii wenye mahitaji . Ukitaka kujua sustainability ya WAMA jongea tu ofisini kwao utakuta watendaji watakupatia mpango mkakati wa WAMA

Sina sababu ya kujikomba , wakati mnabeza juhudi za F/L nanyi mnakuwa mnajikomba kwanani au kwa F/L wenu wa Kusadikika ? Pole sana
 
Rais Salma, Rahma na Kikwete na walamba viatu wao



Kwa wanaojua urais barani Afrika ulivyo mtaji mkubwa kwa familia na waramba viatu wa kwenye kuwa nao, watakubaliana nasi kitu kimoja. Chunguza picha hiyo hapo juu ambapo Rais wa WAMA, Salma Kikwete yuko ziarani nchini Marekani.
Je Salma amekuwa rais lini zaidi ya baada ya mumewe kuwa rais? Kabla hapo rais wa kutumia NGO hakuwa mwingine bali Anna Mkapa ambaye alitimka baada ya mumewe kuutema ulaji.

Je rais Salma ameandamana na nani? Kwenye picha anaonekana Zakhia Meghji aliyekuwa waziri wa fedha wa mumewe kabla ya kuondolewa kwa kashfa mbali mbali za wizi wa mabilioni ya fedha za umma.

Anayefuata nani? Mwanaidi Maajar ambaye ni balozi wa mumewe nchini Marekani anayetuhumiwa kusaini nyaraka za baadhi ufisadi wa kutisha na mwisho wa yote kuzawadiwa ubalozi. Je aliteuliwa kuwa balozi kutokana na merit au kuwa karibu na bwana au bi mkubwa kama anavyooneka? Je ni wangapi wamo kwenye ofisi za umma kupitia mgongoni mwa ufisadi huu wa kunuka unaoendelea kuvumiliwa? Tuliwahi kuandika makala ya Hidden Presidents of Africa.

Wanaoikumbuka wanaweza kujua ni marais wangapi Afrika inao nyuma ya pazia. Wa mwisho mkumbuke Simone Gbagbo na alivyoisha kabla ya Suzana Mubarak na Leila Trebelsi wa Tunisia. Wakumbuke marais hawa waliopata urais kutokana na kulala kitanda kimoja na rais wako wakati ukiangalia picha ya rais huyo wa WAMA.

Bado rais Rahma al Kharoos Kasiga wa RBP Group ambayo imeota baada ya Kikwete kuingia madarakani.

Mhe F/L alienda Marekani kikazi ameiwakilisha nchi, nadhani unafahamu kazi iliyofanyika huko sasa ulitaka Balozi wakati nchi inapewa msaada wa vifaa vya bilioni 45 asiwepo ? Mbona umechukua picha tu hukuchukua na maelezo hiyo kweli chuki binafsi na kweli umerathimisha jina lako la UPAYUKAJI .

Mama Meghji ameenda kama mjumbe wa Bodi ya WAMA . Huo mualiko mama salma hakuuomba ni Taasisi yenyewe ndio imeamua kumualika mwaka huu F/L wa Tanzania baada ya kuridhika na jitihada zake za kuisaidia Serikali kupunguza vifo vya kina mama na watoto . Kupitia Taasisi anayoiongoza mwaka jana tu aliweza kutoa msaada wa vifaa vya kuboresha huduma ya afya ya kina mama na watoto vyenye thamani ya milioni 300 kwa kununua MSD na kuvigawa kwenye vituo vya afya vya kata 66 hapa nchi Jambo dogo hili acheni ushabiki .Hao kina simone ,leila na wengineo hawafanani na F/L wa ukweli wa Tanzania mbona hawajawahi hata kualikwa huko Marekani kuchangishiwa vifaa vya afya ! Walijulikana ni Mafisadi, kamwe yaliyowakuta hao role modals wako uliowataja hayatamkuta F/L Mama Salma Kikwete ambae sio Rais ni M/k wa Bodi ya WAMA na F/L

Huyo rais Rahma mnamjua nyinyi jamvini mbona haalikwi,mbona hana title ya U F/L endeleeni kumpa na matumaini hewa lakini hana nafasi .
 
Back
Top Bottom