Wana jf salaam,
leo najitokeza rasmi kumfagilia kwa sana f/lady wa tanzania mhe mama salma kikwete kwa utendaji wake wa kazi tangu ameingia madarakani mumewe mhe rais jakaya mrisho kikwete .
Wana jf nimekuwa nikosoma mara hapa jamvini. Kadhaa mada mbalimbali juu ya huyu mama nyingi zikionyesha kumshambulia pengine kwa kutojua kazi alizozifanya mpaka sasa. Pia baadhi ya magazeti hasa mwanahalisi na raia mwema zimekuwa zikiandika makala yenye mtizamo hasi juu ya f/lady na taasisi ya wama . Mwandishi mmoja nkwazi anaeishi kanada ktk makala zake nyingi juu ya f/l na wama ameonyesha waziwazi chuki binafsi juu ya wama na f/l
wana jf taasisi ya wama inafanya kazi kubwa ya kusaidia makundi maalum ya kijamii husasani wanawake na watoto wa kike walio katika mazingira hatarishi yaani yatima na familia duni kwa kuwapatia elimu itakayoweza kuwakuomboa .
Taasisi ya wama inayo bodi ya wakurugezi, timu ya menejimenti iliyopatikana kwa njia ya usaili wenye ushindani . Na katika timu ile mama salma hana ndugu hata mmoja aliemweka . Kuna wakati alituhumiwa kwa ukabila na udini katika taasisi yake ufuatao ni ukweli wa timu ya menejimenti ya wama ;
1. Daudi nasib- katibu mtendaji mpare muilslam
2. Neema mhada-afisa afya msukuma - mkiristo
3 gloria minja - afisa tathimini -mchaga-mkiristo
4 philomena marijani -afisa uraghibishi-mpare-mkiristo
5 john mataka -afisa elimu ya mtoto wa kike-mmakonde-mkiristo
6 tabu likoko- afisa uwezeshaji wanawake-mzigua -muislam
7 christina ngonyani(cpa)- mhasibu -mngoni -mkristo
8 subira mgalu(cpa) -mhasibu -mzaramo-muislam
9. Anande munuo -secretary f/l-mchaga-mkristo
10. Veronica -ngulupa -mhudumu-mnyasa-mkiristo
haya hoja ya ukabila na ukiristo ina mshiko ? Watanzania tumuogope molla wetu
hoja nyingine kwamba wama inapata fedha toka ikulu hii sio kweli tangu wama ianzishwe haijawahi kuchangiwa pesa yoyote toka ikulu wala mfuko mkuu wa hazina . Vyanzo vya mapato ni kutoka kwa wasamalia wema wenye kuguswa na shughuli zinazofanywa na f/l kupitia taasisi yake ya wama . Fedha zote zinazochangwa zinatumika kwa matumizi yaliyokusudiwa .
Kila mwaka taarifa hesabu za taasisi zinaandaliwa kwa viwango vya kimataifa na kuwasilishwa kwa mkaguzi wa nje kampuni ya kimataifa pkf iliyopo jengo la amani house floor ya tisa na zinapewa hati . Miaka mitatu mfululizo wama imepata hati safi .
Mafanikio ya wama inayoongozwa na mhe mama salma kikwete ni mengi sana na yameelezwa katika ripoti ya mwaka ya taasisi hasa 2006/2007 , 2007/2008 , 2008/2009.
Lakini jambo kubwa ni kwa mama salma kikwete kujenga shule ya kisasa ya mfano wa kuigwa wilayani rufiji mkoa wa pwani kwa mchango wa mfadhili hayao nakayama wa japan na wadau wa ndani ya nchi .shule hii mpaka sasa imegharimu zaidi ya billion 1.9 za kitanzania na inasomesha bure watoto yatima na wanaotoka kwenye familia duni toka mikoa yote ya tanzania bara na visiwani. Shule hii ina wanafunzi mpaka kidatio cha pili wapatao 272 na kati ya hao hakuna hata ndugu mmoja wa mama salma au mjumbe yoyote wa bodi au ndugu wa mfanyakazi wa wama
watoto hawa wanachaghuliwa na wizara ya tamisemi bila ya kujali dini,kabila , itikadi za wazazi wao,rangi n.k . Tunaomba wadau waendelee kumuunga mkono mhe mama salma kikwete kwa moyo wake huu wa kizalendo .kupitia shule hiyo taifa la tanzania litapata wataalamu wa kutosha katika maeneo mbalimbali . Shime wananchi/wadau/wahisani tuache kusikiliza maneneo ya mitaani , mhe mama salma ni mfano wa kluigwa .
Nawasilisha wada
leo najitokeza rasmi kumfagilia kwa sana f/lady wa tanzania mhe mama salma kikwete kwa utendaji wake wa kazi tangu ameingia madarakani mumewe mhe rais jakaya mrisho kikwete .
Wana jf nimekuwa nikosoma mara hapa jamvini. Kadhaa mada mbalimbali juu ya huyu mama nyingi zikionyesha kumshambulia pengine kwa kutojua kazi alizozifanya mpaka sasa. Pia baadhi ya magazeti hasa mwanahalisi na raia mwema zimekuwa zikiandika makala yenye mtizamo hasi juu ya f/lady na taasisi ya wama . Mwandishi mmoja nkwazi anaeishi kanada ktk makala zake nyingi juu ya f/l na wama ameonyesha waziwazi chuki binafsi juu ya wama na f/l
wana jf taasisi ya wama inafanya kazi kubwa ya kusaidia makundi maalum ya kijamii husasani wanawake na watoto wa kike walio katika mazingira hatarishi yaani yatima na familia duni kwa kuwapatia elimu itakayoweza kuwakuomboa .
Taasisi ya wama inayo bodi ya wakurugezi, timu ya menejimenti iliyopatikana kwa njia ya usaili wenye ushindani . Na katika timu ile mama salma hana ndugu hata mmoja aliemweka . Kuna wakati alituhumiwa kwa ukabila na udini katika taasisi yake ufuatao ni ukweli wa timu ya menejimenti ya wama ;
1. Daudi nasib- katibu mtendaji mpare muilslam
2. Neema mhada-afisa afya msukuma - mkiristo
3 gloria minja - afisa tathimini -mchaga-mkiristo
4 philomena marijani -afisa uraghibishi-mpare-mkiristo
5 john mataka -afisa elimu ya mtoto wa kike-mmakonde-mkiristo
6 tabu likoko- afisa uwezeshaji wanawake-mzigua -muislam
7 christina ngonyani(cpa)- mhasibu -mngoni -mkristo
8 subira mgalu(cpa) -mhasibu -mzaramo-muislam
9. Anande munuo -secretary f/l-mchaga-mkristo
10. Veronica -ngulupa -mhudumu-mnyasa-mkiristo
haya hoja ya ukabila na ukiristo ina mshiko ? Watanzania tumuogope molla wetu
hoja nyingine kwamba wama inapata fedha toka ikulu hii sio kweli tangu wama ianzishwe haijawahi kuchangiwa pesa yoyote toka ikulu wala mfuko mkuu wa hazina . Vyanzo vya mapato ni kutoka kwa wasamalia wema wenye kuguswa na shughuli zinazofanywa na f/l kupitia taasisi yake ya wama . Fedha zote zinazochangwa zinatumika kwa matumizi yaliyokusudiwa .
Kila mwaka taarifa hesabu za taasisi zinaandaliwa kwa viwango vya kimataifa na kuwasilishwa kwa mkaguzi wa nje kampuni ya kimataifa pkf iliyopo jengo la amani house floor ya tisa na zinapewa hati . Miaka mitatu mfululizo wama imepata hati safi .
Mafanikio ya wama inayoongozwa na mhe mama salma kikwete ni mengi sana na yameelezwa katika ripoti ya mwaka ya taasisi hasa 2006/2007 , 2007/2008 , 2008/2009.
Lakini jambo kubwa ni kwa mama salma kikwete kujenga shule ya kisasa ya mfano wa kuigwa wilayani rufiji mkoa wa pwani kwa mchango wa mfadhili hayao nakayama wa japan na wadau wa ndani ya nchi .shule hii mpaka sasa imegharimu zaidi ya billion 1.9 za kitanzania na inasomesha bure watoto yatima na wanaotoka kwenye familia duni toka mikoa yote ya tanzania bara na visiwani. Shule hii ina wanafunzi mpaka kidatio cha pili wapatao 272 na kati ya hao hakuna hata ndugu mmoja wa mama salma au mjumbe yoyote wa bodi au ndugu wa mfanyakazi wa wama
watoto hawa wanachaghuliwa na wizara ya tamisemi bila ya kujali dini,kabila , itikadi za wazazi wao,rangi n.k . Tunaomba wadau waendelee kumuunga mkono mhe mama salma kikwete kwa moyo wake huu wa kizalendo .kupitia shule hiyo taifa la tanzania litapata wataalamu wa kutosha katika maeneo mbalimbali . Shime wananchi/wadau/wahisani tuache kusikiliza maneneo ya mitaani , mhe mama salma ni mfano wa kluigwa .
Nawasilisha wada