Namfagilia mhe mama Salma Kikwete

Mkufu

Member
May 6, 2009
32
5
Wana jf salaam,

leo najitokeza rasmi kumfagilia kwa sana f/lady wa tanzania mhe mama salma kikwete kwa utendaji wake wa kazi tangu ameingia madarakani mumewe mhe rais jakaya mrisho kikwete .

Wana jf nimekuwa nikosoma mara hapa jamvini. Kadhaa mada mbalimbali juu ya huyu mama nyingi zikionyesha kumshambulia pengine kwa kutojua kazi alizozifanya mpaka sasa. Pia baadhi ya magazeti hasa mwanahalisi na raia mwema zimekuwa zikiandika makala yenye mtizamo hasi juu ya f/lady na taasisi ya wama . Mwandishi mmoja nkwazi anaeishi kanada ktk makala zake nyingi juu ya f/l na wama ameonyesha waziwazi chuki binafsi juu ya wama na f/l

wana jf taasisi ya wama inafanya kazi kubwa ya kusaidia makundi maalum ya kijamii husasani wanawake na watoto wa kike walio katika mazingira hatarishi yaani yatima na familia duni kwa kuwapatia elimu itakayoweza kuwakuomboa .

Taasisi ya wama inayo bodi ya wakurugezi, timu ya menejimenti iliyopatikana kwa njia ya usaili wenye ushindani . Na katika timu ile mama salma hana ndugu hata mmoja aliemweka . Kuna wakati alituhumiwa kwa ukabila na udini katika taasisi yake ufuatao ni ukweli wa timu ya menejimenti ya wama ;

1. Daudi nasib- katibu mtendaji mpare muilslam
2. Neema mhada-afisa afya msukuma - mkiristo
3 gloria minja - afisa tathimini -mchaga-mkiristo
4 philomena marijani -afisa uraghibishi-mpare-mkiristo
5 john mataka -afisa elimu ya mtoto wa kike-mmakonde-mkiristo
6 tabu likoko- afisa uwezeshaji wanawake-mzigua -muislam
7 christina ngonyani(cpa)- mhasibu -mngoni -mkristo
8 subira mgalu(cpa) -mhasibu -mzaramo-muislam
9. Anande munuo -secretary f/l-mchaga-mkristo
10. Veronica -ngulupa -mhudumu-mnyasa-mkiristo

haya hoja ya ukabila na ukiristo ina mshiko ? Watanzania tumuogope molla wetu

hoja nyingine kwamba wama inapata fedha toka ikulu hii sio kweli tangu wama ianzishwe haijawahi kuchangiwa pesa yoyote toka ikulu wala mfuko mkuu wa hazina . Vyanzo vya mapato ni kutoka kwa wasamalia wema wenye kuguswa na shughuli zinazofanywa na f/l kupitia taasisi yake ya wama . Fedha zote zinazochangwa zinatumika kwa matumizi yaliyokusudiwa .

Kila mwaka taarifa hesabu za taasisi zinaandaliwa kwa viwango vya kimataifa na kuwasilishwa kwa mkaguzi wa nje kampuni ya kimataifa pkf iliyopo jengo la amani house floor ya tisa na zinapewa hati . Miaka mitatu mfululizo wama imepata hati safi .

Mafanikio ya wama inayoongozwa na mhe mama salma kikwete ni mengi sana na yameelezwa katika ripoti ya mwaka ya taasisi hasa 2006/2007 , 2007/2008 , 2008/2009.

Lakini jambo kubwa ni kwa mama salma kikwete kujenga shule ya kisasa ya mfano wa kuigwa wilayani rufiji mkoa wa pwani kwa mchango wa mfadhili hayao nakayama wa japan na wadau wa ndani ya nchi .shule hii mpaka sasa imegharimu zaidi ya billion 1.9 za kitanzania na inasomesha bure watoto yatima na wanaotoka kwenye familia duni toka mikoa yote ya tanzania bara na visiwani. Shule hii ina wanafunzi mpaka kidatio cha pili wapatao 272 na kati ya hao hakuna hata ndugu mmoja wa mama salma au mjumbe yoyote wa bodi au ndugu wa mfanyakazi wa wama

watoto hawa wanachaghuliwa na wizara ya tamisemi bila ya kujali dini,kabila , itikadi za wazazi wao,rangi n.k . Tunaomba wadau waendelee kumuunga mkono mhe mama salma kikwete kwa moyo wake huu wa kizalendo .kupitia shule hiyo taifa la tanzania litapata wataalamu wa kutosha katika maeneo mbalimbali . Shime wananchi/wadau/wahisani tuache kusikiliza maneneo ya mitaani , mhe mama salma ni mfano wa kluigwa .

Nawasilisha wada
 
Mungu amzidishie nguvu kwa haya anayoyafanya, kwani kila mtenda wema si lazima alipwe jema, watu humu JF hata kama ni ya wema kama afanyayo huyu mama , wao huona ni mabaya tu
 
Mwache achape kazi!
Lakini huu utaratibu wa tz kutegemea NGO badala ya kuwa na taasisi na serikali responsible utaisha lini?
Nimemsikia Prime Minister anaomba ardhi Arusha naye anataka kuanzisha taasisi ya kansa na masuala ya albino. Kwa mwendo huu zile taasisi za serikali zitatoa huduma iliyotukuka kweli!
Ninawaza kwa sauti iliyokuu! Ukitilia maanani shule za sirikali sasa zimetelekezwa na zile za St ....... zinachana mbuga kwa kuwahudumia watoto wa familia bora ili hali watoto wa bora famili wakichota ujinga wa kumwaga kutoka St government primary and sec school.
Anyway, huenda ndo falsafa mpya ya afrika na hasa hasa tz.
 
Vibaraka mna kazi kweli...hivi si mna gazeti lenu la uhuru au wavuti ya wama ndo muende mkaandike haya mautumbo yenu huko...mbona mnahangaika sana
 
mkufu usemayo ni sahihi lakini lengo walilonalo wasemaji a.k.a wapayukaji...a.k.a over intelligence wa hapa jf sio kukosoa serikali ili irekebishe pale penye mapungufu bali ni kukosoa kila kitakachofanyika kwenye serikali hii iliyopo madarakani na ukitaka kuwa member mpendwa basi shiriki kikamilifu katika ukosoaji hata kwa jema tafuta kasoro otherwise jiandae kujiongezea idadi ya maadui!
 
Vibaraka mna kazi kweli...hivi si mna gazeti lenu la uhuru au wavuti ya wama ndo muende mkaandike haya mautumbo yenu huko...mbona mnahangaika sana

Nilijua baadhi ya Vibaraka mtakosa la kujibu. Kwa kuwa mnatumia jf hii nami nimeamua kutoa Data kupitia jamvi hilihili, TUTABANANA HAPA HAPA ! Na kwa taarifa yenu Mama Salma yupo makini hana tuhuma za kujilimbikizia mali ! resources zote za WAMA hahusiki nazo kabisa , kuna menejimenti iliyoenda shule na ikabobea ndio inaratibu shughuli zote .

Huo ni wivu tu unaokusumbua . Muda wake wa kukaa madarakani utakwisha lakini ataacha LEGACY na atakumbukwa na mamia ya watoto wa kike yatima na mazingira duni watakaokuwa wamefanikiwa kupitia mkono wake

Hakuna ukibaraka, penye ukweli lazima tuseme kwa bahati nzuri ni watu wachache wanaomchukia mama salma ukiwemo wewe , mama salma mungu anampenda zaidi idumu Taasisi ya WAMA

Wadau tunaikubali.Wenye wivu wajinyonge! Wamoja Havai Mbili !
 
la kujiuliza:

1. kabla mumewe hajawa rais wa JMT alikuwa na mchango gani na alionyesha umahiri gani wa utendaji?

2. kwanini huo "umahiri wake wa utendaji" ulisubiri mumewe apate urais wa JMT?

akili za mbayuwayu.... changanya na zako!!
 
Mkufu, tunaomba utuwekee hizo ripoti zake ya mwaka

Ripoti hazina shida zitawekwa hapa jamvini, ila pia sio mbaya ukiwa mtanzania ukatembelea WAMA ambapo pia utapewa copy ya hizo ripoti . Lakini ripoti peke yake hazisaidii kama Mtanzania mwenye mapenzi ya dhati basi tembelea kwenye miradi mikubwa ya WAMA kama ifuatavyo

1. Kijijini Nyamisati njia panda ya Bungu wilayani Rufiji -kuna shule ya vipaji maalum ya wasichani ni uwekezaji wa 1.9 Billion, utakuta Mkandarasi na mshauri kazi inaendelea. Utakuta wanafunzi 172 yatima na wanaotoka familia duni watakupa ushuhuda

2.Kijiji cha Hoyoyo Mkuranga ujenzi wa Kituo cha Afya unaogharimu milioni 145, ujenzi unaendelea na utamkuta Mkandarasi yupo site anakamilisha kazi.

3.Nyamisati ujenzi wa shule ya kata ya salale ambapo kulikuwa hakuna sekondari na kata hii imezungukwa na visiwa ujenzi huu umegharimu Milioni Hamsini,kwa sasa zaidi ya wanafunzi 400 wapo hapo wanasoma.

Safari hii unaweza kuifanya kwa siku moja kwenda na kurudi ili ujiridhishe na thamani ya fedha yaani Value for Money !
 
Ripoti hazina shida zitawekwa hapa jamvini, ila pia sio mbaya ukiwa mtanzania ukatembelea WAMA ambapo pia utapewa copy ya hizo ripoti . Lakini ripoti peke yake hazisaidii kama Mtanzania mwenye mapenzi ya dhati basi tembelea kwenye miradi mikubwa ya WAMA kama ifuatavyo

1. Kijijini Nyamisati njia panda ya Bungu wilayani Rufiji -kuna shule ya vipaji maalum ya wasichani ni uwekezaji wa 1.9 Billion, utakuta Mkandarasi na mshauri kazi inaendelea. Utakuta wanafunzi 172 yatima na wanaotoka familia duni watakupa ushuhuda

2.Kijiji cha Hoyoyo Mkuranga ujenzi wa Kituo cha Afya unaogharimu milioni 145, ujenzi unaendelea na utamkuta Mkandarasi yupo site anakamilisha kazi.

3.Nyamisati ujenzi wa shule ya kata ya salale ambapo kulikuwa hakuna sekondari na kata hii imezungukwa na visiwa ujenzi huu umegharimu Milioni Hamsini,kwa sasa zaidi ya wanafunzi 400 wapo hapo wanasoma.

Safari hii unaweza kuifanya kwa siku moja kwenda na kurudi ili ujiridhishe na thamani ya fedha yaani Value for Money !


ama kweli mmetuokota watanzania!!!

mbona miradi yote iko mkoa wa pwani anakotoka mumewe? sio ukanda huu??

au sio ufadhili unaofuata mkondo wa madaraka ya mumewe?

bila urais wa mumewe, WAMA itabaki kitu gani?

urais wa mkapa ulipoisha, EOTF ilibaki kitu gani?

wamekulipa kiasi gani kuja kuwavua magamba hapa JF?
 
duh .. kumbe Salma ni mhe.? Nielimisheni .. kwa k(v)igezo gani?
 
la kujiuliza:

1. kabla mumewe hajawa rais wa JMT alikuwa na mchango gani na alionyesha umahiri gani wa utendaji?

2. kwanini huo "umahiri wake wa utendaji" ulisubiri mumewe apate urais wa JMT?

akili za mbayuwayu.... changanya na zako!!


Kabla mumewe hajawa Rais alitumia kipaji chake kwa kufundisha kwa miaka 17, na ndio maana mumewe alipoingia madarakani aliendelea kutumia kipaji hicho kuwekeza katika Elimu ya Mtoto wa Kike kwa kuwaomba Wasamaria wema kuchangia uwekezaji huo. Wadau hao hawaladhimishwa, lakini Wamesalute kwa ushupavu wa F/Lady na uthubutu wake.Wajapan wametembelea miradi hiyo na wameahidi kuzidi kuichangia WAMA, WAMA inapaa katika Anga za Kitaifa .Hata kwenye mikutano ya kimataifa Mama Salma yupo JUU, Taasisi za Mataifa mbalimbali yana appreciate kazi za WAMA kimsingi Ipo juu najua baadhi ya Wana JF mnakerekwa sana na hili tuvumiliane ila Penye Ukweli Uwongo Hujitenga !
 
Mama Salma poa sana, mi nampenda sana, ni mchapa kazi.
Serikali iunde taasisi za kusimamia mambo yote ili zi chape kazi harakaharaka kwani mawazi ni wawakilishi tu kwenye cabinet.
 
Kabla mumewe hajawa Rais alitumia kipaji chake kwa kufundisha kwa miaka 17, na ndio maana mumewe alipoingia madarakani aliendelea kutumia kipaji hicho kuwekeza katika Elimu ya Mtoto wa Kike kwa kuwaomba Wasamaria wema kuchangia uwekezaji huo. Wadau hao hawaladhimishwa, lakini Wamesalute kwa ushupavu wa F/Lady na uthubutu wake.Wajapan wametembelea miradi hiyo na wameahidi kuzidi kuichangia WAMA, WAMA inapaa katika Anga za Kitaifa .Hata kwenye mikutano ya kimataifa Mama Salma yupo JUU, Taasisi za Mataifa mbalimbali yana appreciate kazi za WAMA kimsingi Ipo juu najua baadhi ya Wana JF mnakerekwa sana na hili tuvumiliane ila Penye Ukweli Uwongo Hujitenga !

1. kungekuwa na dhambi gani kama angeendelea kufundisha hata baada ya mumewe kuwa rais?

2. je kazi pekee inayomfaa FL wa nchi kama yetu ni "kuongoza" NGO tu? tena yenye ofisi zake ikulu (au karibu na ikulu)?
 
uwakumbushe. Tunapoongelea WAMA hatumaanishi hawa wafanyakazi wadogo wanaochapa kazi ili kupata mkate wao. Tunamaanisha mapapa wake za wakubwa au wakubwa wenyewe hapa chini:

Mama. Salma Kikwete Chairaperson mke wa rais Jakaya Kikwete
Mama. Sophia Simba Chairperson of the Board waziri katika utawala wa Kikwete
Mama. Zakia Zamdan Meghji Board Member waziri wa zamani wa fedha aliyeondolewa kwa ufisadi
Amb. Mwanaidi Majaar Sinare Board Member balozi wa serikali ya Kikwete nchini Marekani anayedaiwa kusaini mikataba mingi ya kifisadi na asikanushe
Mama. Regina Lowassa Board Member mke wa waziri mkuu wa zamani aliyetimuliwa kwa ufisadi
Mama. Blandina Nyoni Board Member
Mama Hulda S. Kibacha Board Member
Kama kweli nia ya WAMA ni njema na si kutafuta kuchuma kwa kutumia matatizo ya akina mama, kwanini kwenye bodi ambayo ndiyo roho ya WAMA hakuna wanawake wa mashambani ambao ndiyo walengwa na waathirika? Bila kutoa jibu linaloingia akilini kuhusiana na NGO hii ya mke wa rais na mashoga zake bado umma utaendelea kuamini ni ya kiulaji kama ilivyokuwa EOTF ya Anna Mkapa.Mbona siku hizi imedoda? Simple. Mkapa si rais tena. Naandaa makala iitwayo WAMA ni wizara ya mambo yote. Je wizara husika zitafanya kazi gani? WAMA bado itaendelea kuwa kitendawili cha utawala wa kujuana na kuibiana hadi itakapotokomea baada ya Kikwete kuondoka madarakani hapa 2015. Tusiruhusu rais ajaye kuwa na NGO ya mkewe. Ni ufisadi wa kimfumo huu.:kev::kev::kev::kev::kev::kev::kev:
 
uwakumbushe. Tunapoongelea WAMA hatumaanishi hawa wafanyakazi wadogo wanaochapa kazi ili kupata mkate wao. Tunamaanisha mapapa wake za wakubwa au wakubwa wenyewe hapa chini:

Mama. Salma Kikwete Chairaperson mke wa rais Jakaya Kikwete
Mama. Sophia Simba Chairperson of the Board waziri katika utawala wa Kikwete
Mama. Zakia Zamdan Meghji Board Member waziri wa zamani wa fedha aliyeondolewa kwa ufisadi
Amb. Mwanaidi Majaar Sinare Board Member balozi wa serikali ya Kikwete nchini Marekani anayedaiwa kusaini mikataba mingi ya kifisadi na asikanushe
Mama. Regina Lowassa Board Member mke wa waziri mkuu wa zamani aliyetimuliwa kwa ufisadi
Mama. Blandina Nyoni Board Member
Mama Hulda S. Kibacha Board Member
Kama kweli nia ya WAMA ni njema na si kutafuta kuchuma kwa kutumia matatizo ya akina mama, kwanini kwenye bodi ambayo ndiyo roho ya WAMA hakuna wanawake wa mashambani ambao ndiyo walengwa na waathirika? Bila kutoa jibu linaloingia akilini kuhusiana na NGO hii ya mke wa rais na mashoga zake bado umma utaendelea kuamini ni ya kiulaji kama ilivyokuwa EOTF ya Anna Mkapa.Mbona siku hizi imedoda? Simple. Mkapa si rais tena. Naandaa makala iitwayo WAMA ni wizara ya mambo yote. Je wizara husika zitafanya kazi gani? WAMA bado itaendelea kuwa kitendawili cha utawala wa kujuana na kuibiana hadi itakapotokomea baada ya Kikwete kuondoka madarakani hapa 2015. Tusiruhusu rais ajaye kuwa na NGO ya mkewe. Ni ufisadi wa kimfumo huu.:kev::kev::kev::kev::kev::kev::kev:

asante mkuu... watu wanafikiri Jf ni global publishers ambapo unaweza kuandika upuuzi kwenye magazeti ya risasi na ijumaa
 
Wana jf salaam,

leo najitokeza rasmi kumfagilia kwa sana f/lady wa tanzania mhe mama salma kikwete kwa utendaji wake wa kazi tangu ameingia madarakani mumewe mhe rais jakaya mrisho kikwete .

Wana jf nimekuwa nikosoma mara hapa jamvini. Kadhaa mada mbalimbali juu ya huyu mama nyingi zikionyesha kumshambulia pengine kwa kutojua kazi alizozifanya mpaka sasa. Pia baadhi ya magazeti hasa mwanahalisi na raia mwema zimekuwa zikiandika makala yenye mtizamo hasi juu ya f/lady na taasisi ya wama . Mwandishi mmoja nkwazi anaeishi kanada ktk makala zake nyingi juu ya f/l na wama ameonyesha waziwazi chuki binafsi juu ya wama na f/l

wana jf taasisi ya wama inafanya kazi kubwa ya kusaidia makundi maalum ya kijamii husasani wanawake na watoto wa kike walio katika mazingira hatarishi yaani yatima na familia duni kwa kuwapatia elimu itakayoweza kuwakuomboa .

Taasisi ya wama inayo bodi ya wakurugezi, timu ya menejimenti iliyopatikana kwa njia ya usaili wenye ushindani . Na katika timu ile mama salma hana ndugu hata mmoja aliemweka . Kuna wakati alituhumiwa kwa ukabila na udini katika taasisi yake ufuatao ni ukweli wa timu ya menejimenti ya wama ;

1. Daudi nasib- katibu mtendaji mpare muilslam
2. Neema mhada-afisa afya msukuma - mkiristo
3 gloria minja - afisa tathimini -mchaga-mkiristo
4 philomena marijani -afisa uraghibishi-mpare-mkiristo
5 john mataka -afisa elimu ya mtoto wa kike-mmakonde-mkiristo
6 tabu likoko- afisa uwezeshaji wanawake-mzigua -muislam
7 christina ngonyani(cpa)- mhasibu -mngoni -mkristo
8 subira mgalu(cpa) -mhasibu -mzaramo-muislam
9. Anande munuo -secretary f/l-mchaga-mkristo
10. Veronica -ngulupa -mhudumu-mnyasa-mkiristo

haya hoja ya ukabila na ukiristo ina mshiko ? Watanzania tumuogope molla wetu

hoja nyingine kwamba wama inapata fedha toka ikulu hii sio kweli tangu wama ianzishwe haijawahi kuchangiwa pesa yoyote toka ikulu wala mfuko mkuu wa hazina . Vyanzo vya mapato ni kutoka kwa wasamalia wema wenye kuguswa na shughuli zinazofanywa na f/l kupitia taasisi yake ya wama . Fedha zote zinazochangwa zinatumika kwa matumizi yaliyokusudiwa .

Kila mwaka taarifa hesabu za taasisi zinaandaliwa kwa viwango vya kimataifa na kuwasilishwa kwa mkaguzi wa nje kampuni ya kimataifa pkf iliyopo jengo la amani house floor ya tisa na zinapewa hati . Miaka mitatu mfululizo wama imepata hati safi .

Mafanikio ya wama inayoongozwa na mhe mama salma kikwete ni mengi sana na yameelezwa katika ripoti ya mwaka ya taasisi hasa 2006/2007 , 2007/2008 , 2008/2009.

Lakini jambo kubwa ni kwa mama salma kikwete kujenga shule ya kisasa ya mfano wa kuigwa wilayani rufiji mkoa wa pwani kwa mchango wa mfadhili hayao nakayama wa japan na wadau wa ndani ya nchi .shule hii mpaka sasa imegharimu zaidi ya billion 1.9 za kitanzania na inasomesha bure watoto yatima na wanaotoka kwenye familia duni toka mikoa yote ya tanzania bara na visiwani. Shule hii ina wanafunzi mpaka kidatio cha pili wapatao 272 na kati ya hao hakuna hata ndugu mmoja wa mama salma au mjumbe yoyote wa bodi au ndugu wa mfanyakazi wa wama

watoto hawa wanachaghuliwa na wizara ya tamisemi bila ya kujali dini,kabila , itikadi za wazazi wao,rangi n.k . Tunaomba wadau waendelee kumuunga mkono mhe mama salma kikwete kwa moyo wake huu wa kizalendo .kupitia shule hiyo taifa la tanzania litapata wataalamu wa kutosha katika maeneo mbalimbali . Shime wananchi/wadau/wahisani tuache kusikiliza maneneo ya mitaani , mhe mama salma ni mfano wa kluigwa .

Nawasilisha wada


huu upuuzi ungepeleka kwenye magazeti ya uhuru, mzalendo au global publishers wangekuelewa sio humu
 
Back
Top Bottom