Nalivua pendo...

Nalivua pendo...

Dada Pole sana

Mapenzi ni matamu, Apendwae akifahamu.
Tena hayahishi hamu, Kwa yule alofahamu.
Haijalishi haramu, Bora alete Kayumu.

Mpende akupendae, Asiokupenda achana nae.
Mpe kila kimfahae, Moyoni mwako akae.
 
Dada Pole sana

Mapenzi ni matamu, Apendwae akifahamu.
Tena hayahishi hamu, Kwa yule alofahamu.
Haijalishi haramu, Bora alete Kayumu.

Mpende akupendae, Asiokupenda achana nae.
Mpe kila kimfahae, Moyoni mwako akae.

Abdallah,
maneno yako dawa...
Natumia simu,ila elewa
NIMEIPENDA
 
Nimepitwa na mengi mchana kutwa, lakini dada pole yako, wanaume wengine hatujui kupendwa, tunapenda tusipopendwa, tunapaacha tulipopendwa tunajitumbukiza pasipo na pendo.
Narudia tena dada pole, mungu atakujaalia utampata atakaejua nini thamani ya pendo.
 
Abdallah,
maneno yako dawa...
Natumia simu,ila elewa
NIMEIPENDA
Usijali!
Huyo mwanaume ni gumegume!

Wenzie wanakililia, Yeye anakichezea.
Bahati haitarudia, Pindi ikimpotea.
Atakuja ijutia, Na siku haitatokea.

Utakuwa umetuliia, Kwa raha zako ukijilia.
Kwa yule alieridhia, Moyo wako kuutibia.
Majeraha alokutia, Itabaki historia.
 
1.Unaweza kuvua baadae ukajakujuta na kusema bora ningebaki palepale UTAJIVUA MARA NGAPI??.
2. TAFAKARI kiini cha tatizo nini? je tatizo linaweza kurekebishika?
3. Uamuzi wowote unaotokana na hasira au jazba ni hasara maana imeandikwa hasira hukaa kifuani kwa mpumbavu.
 
Mi napenda pale anaposema "Nimefundwa kimitindo ya starehe za chumbani..."
 
Kulivua pendo si rahisi kivile
Kikubwa ni kutopoteza mwelekeo na kujipa muda.

Am telling you you are very very right.
Haikuwa rahisi kabisa but nimesonga mbele dadangu

(Haya irudishe upesi ulipoifukua hii thread)
 
Pole sana kwa yaliyoyo kukuta ni ngumu mtu mwingine kufeel kama ww kwa sasa , tafadhari kabla hujafanya uamuzi mgumu kiasi hicho jaribu kwenda vacation kwa muda take your tym fikiria vizuri tafakari kwa makini chanzo cha yote hayo then angalia kama kuna solution kwa ajili ya ku-
jenga. kumbuka relationship is very expensive you have to value it.lengo lisiwe kuvunja uhusiano wenu iwe ni kujenga. nina uhakika wewe ni mwanamke imara jenga mahusiano yako.
 
Safiiii!
Ndo ukubwa huo mama, ukianguka, unainuka, unajikung'uka vumbi then unasonga mbele

Am telling you you are very very right.
Haikuwa rahisi kabisa but nimesonga mbele dadangu

(Haya irudishe upesi ulipoifukua hii thread)
 
Ndahani nashukuru kwa kunipa moyo ila mh maana kama kuvumilia ni mwngi nimevumilia lakini mwishoni naona nashindwa. kwa nini mimi tu, mimi tu niwe nabembeleza kila siku hata kama makosa kafanya yeye?
mimi tu niwe naumia kwa sabau yake?... kwa nini mimi tu ndo niwe nahangaika to make it work? ... mimi tu why mimi tu? jamani ah

ushauri wangu kwa mwanaume unaempenda,usiendelee kumfuatafuata hasa pale ambapo hataki kuongea na wewe.muache fanya kama vile hujali .endelea na hamsini zako.Baada ya muda kuna kitu ataona kina miss atakutafuta. HAPO NDIO UTAMUONYESHA MSIMAMO WAKO.Nakushauri ujipumzishe kitandani, utahangaika sana, baadae utalala pasi kutegemea ,utakapoamka, walau utapata nguvu na mawazo mapya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom