Naliona anguko la Kibanda


Kibanda to be honest wengi hatujapendezwa na makala yako, si kwamba hatuna uwezo wa kuchambua mambo. Kwanza uliandika kwa hasira na kuonyesha kuwa ni wewe tu ndio mwenye mtazamo sahihi kiasi cha kusema wote wanaomuunga mkono Sitta ni mazuzu(ingawa hukutumia neno zuzu).

Katika makala yako, tofauti kabisa na makala za wapambanaji wengi unaonekana kabisa kutokuchukizwa na malipo ya dowans bali wanaopinga ndio hutaki hata kuwasikia. Hiyo imewapa wasiwasi watu wengi sana wanaofuatilia makala zako na especially ile ya jumatano.

To me naona TZ Daima polepole limeanza kuchukua direction tofauti kidogo na hasa makala zako, ushauri wangu kwako ni kuwa jitathmini upo wapi kwa sasa vinginevyo ukiendelea hivi hilo gazeti la TZ Daima hasa la j5 tutaliweka pembeni tutaendelea na Mwanahalisi na Raia Mwema. Don't say i didn't warn you!
 
Pole sana Kibanda! Umesahau kitu kimoja... Kusoma ni jambo moja na kuelewa ni jambo jengine! Baadhi ya wasomi wetu wa kileo, upeo wao ni mdogo sana, kwa sababu wao wanataka kuamini kile walichokwishaamini hivyo basi anaweza kusoma paragraph moja tu, akahitimisha habari nzima na kutoa hukumu zake. Hapo ndipo wanapozusha na hawaambiliki!!

Hivi kama wao ni wakweli na wana-kumbukumbu basi watuambie ni KWANINI MWALIMU ALIKUWA HAMTAKI SS? Na kama SS si mbinafsi na mwenye kupenda kujitenga alikuwamo katika G55!! Na kama kweli yeye SS ni mwenye uchungu na nchi na hana uchu wa madaraka na kupenda sifa KWANINI JENGO LA SPIKA LIJENGWE JIMBONI MWAKE NA SI DODOMA ina maana alitaka USPIKA - UKAMUZU BANDA!?)
 


Nakushukuru kwa uvumilivu wako na kwa uzito wa maelezo yako. Nilikaribia kuiweka hapa lakini nimeogopa kuwakera wengi kwa uurefu wake
 
Thubutu... afanyeje??? Kule ndiko anakojua kwamba angalau angali na chochote na anaheshimika labda hamumjui mzee yule! Ulizeni wanaojaribu kugombea nae ubunge kule jimboni kwake mtapata habari zake. Mnadhani jimboni kwake wanamtaka! Ila wale wapinzani halisi huwa anawawahi kimtindo wa kutumia dola biashara inaisha anabaki na mngombea dhaifu. Akitoka huko na kuja mjengoni anaonekana shujaa! Lakini kwa akili zetu wacha na tumuone shujaa kwa muda, wakati utafika kila ukweli utajulikana... kama mjuavyo media zikikubeba utaonekana na siku zikikuacha ndio mporomoko na mengineyo yanajulikana
 
Nakushukuru kwa uvumilivu wako na kwa uzito wa maelezo yako. Nilikaribia kuiweka hapa lakini nimeogopa kuwakera wengi kwa uurefu wake
Mkuu, Kila mtu anao uhuru wa kutoa maoni yake na hatoi maoni kwa sababu ya kumfurahisha mtu bali kutoa ukweli uliomo ndani ya nafsi yake. Mzigo wa moyo hautuliwi kwa kuwafurahisha watu, Koti la mfalme likiwa na mawaa aambiwe... ili asiaibike. Lakini tukitaka kufurahishana (si ni heri tununuliane chai na vitafinwa) sio katika mambo na mustakabali wa Nchi. Hii ni Nchi yetu sote lazime tuwe na muono tofauti ili tupate kilicho bora. Tukiwa na mawazo ya aina moja basi itakuwa Nchi ya wendawazimu na tusio na fikra bali kufatana kama mchwa hata kama tunatumbukia mtoni!!

Usife moyo, UKWELI SIKU ZOTE HAUTAKIWI KWA MAANA NI MCHUNGU, BALI UONGO HUTHAMINIWA KWA MAANA UNAFURAHISHA MIOYO!
 

Bro/sister kama ndio great thinkers tumekwisha. Wape pole.
 
Kabanda, Balile, Kibonde deserve a place in CCM's propaganda newspaper Uhuru and not progressive and highly respected papers like Tanzania Daima.
Hawa ni waandishi wajinga, waganga njaa ambao muda si mrefu sana wataaibishwa na matendo yao dhidi ya umma wa watanzania. Ama sasa nimeamini methali ya kiingereza isemayo 'a hungry stomach knows no discipline'' Ndiyo maana tunawashuhudia sasa waandishi hawa na wengine tuliodhani wana weledi kununuliwa kwa bei poa kulingana na saizi ya njaa katika matumbo yao! Ni nani alimtazamia Salva Rweyemamu kuangukia ikulu kwenye lambalamba ya 'Sultani' Kikwete? Historia itawahukumu.
 
Kama kweli kibanda umesema ivo,ebu piga moyo konde. Mi namheshimu sana mzee6.
 
Safi sana Mkembe 2010! Umechambua vizuri makala ya Kibanda na ni ukweli mtupu! Nadhani wako wengi wameahidiwa na hao mafisadi tunda la mtu wa kati ukiachia Kibanda na Fungamtama ili Dowans ilipwe! Ninachotaka kuwakumbusha hao waahidiwa na ambao tayari wameshafungasha mtama wao kibindoni waangalie kitu kimoja, upande huo waliopo (wa mafisadi) ni waovu na wako tayari kupoteza reputations zao ili mradi hela ipatikane, kwahiyo kama na wao wako tayari historia iwakumbukwe kwa hayo basi waendelee ila sisi wananchi (wajinga na vipofu) hatutakubali na tutambana mpaka dakika ya mwisho!!
 
Wakuu siwezi kuwasemea wengine, lakini yeyote aliyesoma mada yote na michango yote anabakia na kiu ya makala ya kesho. Tunawaomba walioko nchini na wenye uwezo watuletee hapa kesho tena yote nzima. Kuna kitu nahisi kinafichwa kwa ustadi mkubwa. Msisahau humu tuko wengi na wenye fani mbali mbali licha ya tofauti za umri na "level of exposure". Msomi hafichwi maana kama lugha anaijua.
 
Kibanda kuna kitu kinaitwa jf public opinion kwenye issues mbali mbali. Ukitofautiana na public opinion hizi tegemea matukano.

Kuhusu Sitta ile siku anahitimisha mjadala wa Richmond pale Dodoma kwa mtindo wa fumika kombe, nilitoa maoni yangu humu na nilishambuliwa.

Juzi baada ya hukumu ya ICC nilitoa maoni kuhusu mkataba ile ulivyo mbovu tumeshikwa pabaya. Nikasema kauli za Sitta na Mwakiembe ni furahisha genge. Wakunishukia walinishukia.

Kwa upande wangu nakukubali japo kuna pengi natofautiana na wewe na wengi kuhusu baadhi ya issues zikiwemo zihusuzo Chadema.
 
Kwanza kabisa nampongeza mkuu mkembe kwa analysis yake nzuri, hata kama ilishajadiliwa but yeye ameipresent kivingine and bcaz we are great thinkers hatuchoki kujadili hot topics kama hizi..!

Mwisho kabisa niseme tu huyu bwana ametuchosha..! hamna ubishi ameshachakachuliwa tena to the maximum, sioni sababu ya kamanda mbowe kuendelea kumkip this chap, hata kama alisema nini bila kutetereka against Jk he is nat da same chap nowdays!

I THINKS ITS A HIGH TIME NOW HE DECIDES IF HE IS WITH US OR AGAINST US ILI TUJUE ASIJIDAI YE NI MTU WA KATI WKT UPANDE WAKE UNJIDHIHIRISHA...! SO KAMA ATAENDELEA KUBAKI TANZANIA DAIMA AACHE KUANDIKA UOZO WAKE ATHER WISE AHAMIE UHURU AMA RAI..!:frusty:
 
KIBANDA KWA HILI TUKO PAMOJA ! sema tu, nimekuelewa na ninatayarisha nakala ya kutetea na kuuelewesha umma unamaanisha nini! just simple logic is needed!
 
Kibanda ni yule nilimfahamu chuo kikuu cha dsm aliyemaliza 1994 au mwingine. Maaana sitegemei kama anaweza kuwatetea mafisadi
 

Acha uvivu kipindupindu. Hoja zimepangwa na zinaeleweka vyema. Namuunga mkonn kuwa Kibanda ameanza kutumiwa na mafisadi. And they pay him good ndo maana anakubali kuharibu reputation yake but aonekane mzuri kwa kina EL+RA.
 
Hicho kibanda kimeshaungua kimenunuliwa zamani sana na hao Mafisi kumbe hamjui!! tatizo hawafanyi tathimini kama wakifanya tathimini hilo gazeti limepungua wasomaji kwa asilimia zaidi ya kumi tokea hicho kibanda kiungua na moto wa pesa za Rushwa.
 
KIBANDA KWA HILI TUKO PAMOJA ! sema tu, nimekuelewa na ninatayarisha nakala ya kutetea na kuuelewesha umma unamaanisha nini! just simple logic is needed!

Tunasubiri makala yako bwana wakili a.k.a mtetezi wa wanyonge.

Hapa tunahitaji facts sio utetezi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…