Nakusudia kumshtaki baba yangu

Nakusudia kumshtaki baba yangu

Msukuma Original, Nimepitia machungu mengi sana ingawaje sijafikisha hata 37 years, Mungu alinifanya nikaajiriwa nikiwa na miaka 24 nilithaminiwa, nikapoteza ajira, yaliyonikuta sitoyasahau kamwe kwani nishatukanwa tusi zito huku mama mzazi akiangalia mwanawe akinitukana.

Nimeapa kutosaidia ndugu msaada wa kumtoa kimaisha zaidi ya kinafiki, marafiki ndio wananipigania, nakula kwao, Nalala, ninaumia maana sina ajira kwa sasa ila wameniambia nisikate tamaa yataisha. Mungu kunionesha mapema adui zangu kanisaidia sana, ashukuriwe Mungu!

Hapa napoandika huu ujumbe ni kuwa hao ndugu hawajui nipo wapi wala nakula nini ila utashangaa mzazi anakuambia nipe mchango wa ndoa! Kaka hiyo siku bila kuwa mzazi wangu wa kunizaa basi tusi ambalo nilitaka kumpatia sidhani kama angenitafuta tena. Hii dunia sio kabisa ndugu yangu, kwani ndugu utasikia wanakuambia kuwa sisi nduguzo kisa unazo mali, fulia ujue rangi zao.

Ilifikia hatua nilianza michakato ya kutafuta scholarship nikasome nje nipate uraia huko kwani hapa sina msaidizi au ndugu but sijakata tamaa, nikipata chance hiyo nasepa jumla...
 
kidambinya,
Mkuu historia yako inafanana na yangu 100%. Mie nilikuwa nawathamini sana wazazi wangu, wadogo zangu na ndugu wote kwa ujumla. Nilianza harakati za kuwasaidia wadogo zangu kabla hata maisha yangu mwenyewe hayajasimama maana nilikuwa very naive. Niliamini kumsaidia mdogo wako au ndugu ni wajibu wangu na watakuja kunithamini au wananithamini kama ninavyowathamini.

Nilipata bahati ya kuishi nje ya nchi hivyo nilijitahidi kujinyima nilichokuwa nakipata na kukituma nyumbani kwa wazazi na shuleni kuwasaidia wadogo zangu issue za ada na mambo mengine. Niliporudi nchini nikabahatika nikapata kazi yenye hela nzuri. Nilizidisha kutoa misaada kwa wazazi na kwa kila ndugu aliyeniomba sikusita kumsaidia. Hamadi!!!! Siku hazilingani.

Kazini mambo yakaharibika, nikaachishwa kazi, nikafulia kinoma. Wadogo zangu washamaliza vyuo na mambo yao yapo juu ya mstari. Nilidhani watanisaidia, bwanaee hakuna hata mmoja aliyekumbuka wema wangu. Hadi wazazi wangu wakanigeuka, sikuamini. Nilitokea kumchukia kila mtu. Nilihangaika peke yangu, mke wangu alikuwa mjamzito na nilikuwa na mtoto wa darasa la kwanza, nilipata tabu sana.

Niliapa sitasaidia mbwa yoyote kwenye maisha yangu. Nimekaa karibia miaka miwili nahangaika bila msaada kutoka kwa ndugu. Marafiki pekee ndio walikuwa wananisaidia. Mungu ni mwema, tayari nimeshaanza kuyarudisha tena maisha yangu kwenye mstari.

Na tayari nishaanza kuwaona washaanza kujipendekeza. Kama ulivyosema hata mimi namshukuru Mungu amenisaidia kuwajua ndugu zangu walivyo. Sasa hivi ndugu zangu ni mke wangu na watoto wangu basi.
 
Msukuma Original, Alafu kuna mabwege yanajifanya kuthamini ndugu na kuwaamini 100% sio mimi nasema, Kuna siku niliwahi kumwambia rafiki yangu kuwa laiti kama wangejua navyowachukulia hawa ndugu, sidhani kama kuna ambaye angethubutu kunisogelea hata kama ni mita moja.
 
Baba yako ametekwa ufahamu, tumia njia mbili tu zinaweza kukusaidia,ungana na familia yako mfunge siku tatu au zaidi kwa ajili ya kumuombea afunguke.

Njia ya pili nenda kwa nabii yoyote unaemfahamu,manabii wanajua yajayo na yaliyopita watakusaidia,kwa sababu nabii ni kama waganga tuu,tofauti yao ni ndogo Sana.

Kama ukienda mahakamani nakwambia utapoteza tena helaa kwa sababu unadili na kitu kisichoonekana kwa hiyo kipambanishe na kisichoonekana chenzake.Wakati unafanya hayo hakikisha wewe na mzee mpo fresh.Pole Sana.

Wanaume wanapenda wake zao japo wanakuwa na vimada,tatizo kimada hata mkubaliane kwamba asiisumbue familia lazima tuu atachonganisha mwanaume aichukie familia yake yeye apendwe zaidi matokeo yake ndo anaharibu kama hivi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ningekuwa ndiyo wewe ningemsamehe nikafanya maisha yangu. Over 6 years umehudumia familia hesabu baraka zako endelea na maisha penye kufaa msaada toa pasipofaa acha.

Neema za Mungu huja kwa nyakati, Kuna kipindi anakubariki ili na wengine wabarikiwe kupitia wewe, dont spoil the chain hakuna lenye mwanzo likakosa mwisho

I've been into problems with my mum ila katika sala huwa namwambia Mungu if it takes me to love any woman better not even myself I should love this mama.

Kwenye shida namsaidia kama uwezo upo then nakaa mbali kuna muda yeye mwenyewe unajishtukia but mimi natulia for I know what I'm doing.

Kuna wakati hutakiwi kufanya maamuzi ni hekima kidogo tuu, hakuna jaribu unapewa ushindwe kulivuka and at the end richness and wealth of the world will remain on earth.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Manzile,
Pamoja na Maumivu lakin mfanyie ihsan achana na masuala ya mahakaman. Huyo ndio Babako na hutapata mwingine, chukua hiyo kama lesson.

Fanya mambo kwa umakini sasa usioneshe dharau ila waweza fnya mishe zako kwa tahadhar sasa
 
Mambo ya kifamilia ni magumu sana kuyaingilia.

Ni bora kuyaacha, wayamalize wenyewe.

Hatujasikia maelezo kutoka kwa Baba wa muhusika.

Unaweza kupata maelezo kutoka kwa Baba wa muhusika, maelezo yake ukakuta tofauti sana na haya yaliyotolewa hapa
 
Kesi yako haitakuwa ya kwanza, kuna ambayo naifahamu, watoto wanashindana na baba yao ambaye baada ya mama yao kufariki kaamua kuuza mali za mama yao ambazo wao ni warithi.
 
Manzile,
Hii ni ngumu kuvumilia. Lazima ifanyike namna ya kumstopisha ili asiendeleze ujinga
 
Back
Top Bottom