Nakusudia kumshtaki baba yangu

Nakusudia kumshtaki baba yangu

Manzile,
Mkuu pole Sana kwa hayo ya mzazi wetu. Nikuombe tu huyo Ni mzazi wako hata Kama atakuwa amekukera na kukuumiza kwa kiasi gani. Kumbuka pia kila mafanikio Yana changamoto zake huenda hili nijaribu kwako ili kukufanya uwe imara zaidi.

Achana na kumuita mpumbavu huyo mzazi tafuta kajikwaa wapi mpk anafanya hayo km aliweza kukutengenezea misingi mizuri na Leo uko hivilazima Kuna uzuri wake mwingi na mkubwa. Haya maisha Yana mambo mengi Sana mkuu ikiwezekana ongea naye au ongea na rafiki yake wa karibu atakupa Mwanga juu ya kinachomsibu mshua then kuanzia hapo utapata wapi pa kuanzia.

Achana na kumuita mpumbavu mzee wako, bila huyo usingekuwepo duniani hata ungekuwepo si kwa jina la manzile Mali zinatafutwa tu boss wangu
 
Manzile,
Cha kwanza Kama kumbukumbu zangu zipo fresh sio Mara ya kwanza kuleta hichi kitu. Je, Mara ya kwanza ulimalizana nae vipi?
 
Mkuu mzee wako katekwa kiakili
Akili yake haipo sawa
Hapa ndgu siwezi kuwa mpumbavu namna hii, katelekeza familia miaka zaidi ya 6 nahangaika kusomesha watoto wake bado kuna mengi nimesahe yeye ameenda kuchukua mwanamke ana watoto wakubwa wa wanaume wenzake kamjengea nyumba nzuri kwa jasho langu na miradi huku wanae, nimuache Mali zangu zifaidishe ukoo mwingine huku wadogo zangu wanateseka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshua karogwa kawekwa sawa na huyo kimada hapo hajielewi ukute ni chapombe balaa tupu kwa imani yako you can solve this, ishu za kifamilia ni very complicated kushauri Ila haitakiwi kumuacha hata kama ni baba solve tatizo Fanya kumfungulia kesi aliyenunua
kiwanja baba ataungwa kwenye hiyo chain komaa nae usimchekee kashakuona boya na huwezi mfanya chochote alivyofanya ni vituko ase pia jaribu kuchunguza mahusiano yao na mama before upate picha kamili ukute baba alikuwa baharia kitambo
 
Manzile, Iyo bunduki irudishe ulikoitoa la sivyo utaua kweli nimekufuatilia Sana unataja taja kuua.Si unafamilia tayari?usije fungwa wakana teseka Sana
Kwanza pole sana.

Wazee wa hivyo wapo.The best thing epukana naye mwa kumuweka mbali
Hilo ni tatizo.

Kesi samehe utaona Mibaraka tele baada ya nisamehe
I'm talking this according to my experience

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzazi mtu wa kuheshimika sana, ujue hata ukimkosea mama akipiga ziwa chini chako kimeisha,

Waheshimuni tu as siku wanaondoka unabaki huru.

Sent using Jamii Forums mobile app
Africa wazazi ndio wanaosababisha watoto wao kufa masikini kwa sababu ya vinyongo, mali ya mtoto wanaamini ni ya wazazi. Mungu kaniumba tofauti sana.... Hao watoto wangu (not more than two) watakapozaliwa wataenjoy sana maana mshua najielewa.
Nimeshuhudia Mzazi kavua nguo na kuwa uchi wa mnyama, akimlaani mwanae kwa sababu hamjali. Mzazi alisema hadharani kuwa nimeshakuharibia hivyo, kwisha sasa huna jipya.
Ilikuwa aibu sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzazi mtu wa kuheshimika sana, ujue hata ukimkosea mama akipiga ziwa chini chako kimeisha,

Waheshimuni tu as siku wanaondoka unabaki huru.

Sent using Jamii Forums mobile app
Akipiga hilo ziwa atakuwa amepata nini?
Itamsaidia nini?
Alibeba mimba ili apige ziwa chini?
So what?
Wazazi wengi wanalewa hadhi yao kwa watoto.
Kwa niliyopitia mimi, huwa sipendi kukaa karibu na hawa watu maana ni kweli unayosema kuwa wanaweza kukuharibia muda wowote ule.
Wazazi wengi wamezaa watoto kwa ajili yao na sio kwa ajili ya maisha ya hao watoto. Why, ifike kipindi Watoto wafurahie moyoni kifo cha mzazi kisa tabia zake?
Ni hatari sana na mtihani sana kuishi na wazazi wa aina hii!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa ndgu siwezi kuwa mpumbavu namna hii, katelekeza familia miaka zaidi ya 6 nahangaika kusomesha watoto wake bado kuna mengi nimesahe yeye ameenda kuchukua mwanamke ana watoto wakubwa wa wanaume wenzake kamjengea nyumba nzuri kwa jasho langu na miradi huku wanae, nimuache Mali zangu zifaidishe ukoo mwingine huku wadogo zangu wanateseka

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata hao ndugu zako ni wanawe pia kaka, achana nao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kesi yako haitakuwa ya kwanza, kuna ambayo naifahamu, watoto wanashindana na baba yao ambaye baada ya mama yao kufariki kaamua kuuza mali za mama yao ambazo wao ni warithi.
Mkuu imekaaje hiyo?

Kuna mali ya mke kisheria ambayo haimuhusu mume?

Naomba ufafanuzi kidogo ili niunganishe dots.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna baadhi ya madingi wazinguaji saana...

Haturuhusiwi tu ki imani kulipiza ila hata mboko inatakiwa walambwe ...maana wengi wao ndiyo wamesababisha familia kuwa kwenye lindi la umaskini wakati wao wanaishia ishia yaani age za 70 na kuendelea.

Unafika age hiyo kaoukutisha pea zake kwa anasa, anaumwa, hana bima inabidi uhangaike kuhakikisha chakula, matibabu ba malazi..

Sisi ma dingi watarajiwa tusirudie mambo haya ya kishamba..!!
 
Back
Top Bottom