Nakerwa na wananchi wa Kanda ya Ziwa

Nakerwa na wananchi wa Kanda ya Ziwa

wacha ukweli usemwe. Hajasema kabila lolote hapa. Viongozi na wabunge toka enzi za tanu na baadae ccm hawajawahi kutetea kanda ya ziwa ambapo idadi ya watanzania ni kubwa kuwarahisishia maendeleo yao kikanda. Tupo mbali na viwanda vya cement na vifaa vyakujengea lakini hata siku moja watu waccm hawajaona kama kuna haja ya serikali kuwapunguzia mzigo wakuvisafirisha ili vikapungua bei vifikapo huko. Usafiri wa gari moshi ulio kuwa nafuu matajiri waccm wameuangamiza ili watufikishie bidhaa kwa usafiri wa magari kwa faida kubwa, muone hata magufuli anakazana na kutengeneza barabara tu, je huwa akai katika baraza la mawaziri na akatetea train? Ili tukapata mizigo kanda ya ziwa ikiwa ina bei nafuu?(kila kitu bei ipo juu tofauti na dar, moro, tanga, dodoma, arusha, mbeya, zanzibar, nk kutokana na kusafirishwa mbali na viliko viwanda) wanaposhindwa kututolea ruzuku ya kuvisafirisha kwa nini hawaweki mkakati wa kuvijenga hukohuko kanda ya ziwa? (mwanza, musoma,kagera) au jirani na hapo (tabora, kigoma singida, nk)
kama sio kanisa la katoriki kutusaidia tukapata hospitali ya bugando na chuo kikuu cha sauti, pamoja na ukubwa wa kiuchumi ulioko huko kanda hii ingekuwaje sijui sisi ni watoto wa nani. Kwa kuwa sasa ccm imeshindikana kututoa katika karne ya 47, ngoja tuijaribu cdm huenda ikatuingiza katika ulimwengu wa digitali tukiwa salama. Mwanza, musoma wameishaliona hilo na shinyanga. Kagera wameanza hasa bukoba mjini na karagwe. Kigoma wao wana ngwe ya kwao ni safi kabisa. Jirani zetu tabora wamelala, sijui kwa nini hawalioni hili! Bado ninaamini ukombozi wa chi hii utaanzia kanda ya ziwa>


big like
 
Mtuwache tupumue, hatunaa akili za kushikiwa kama akina fulani.

Kuchochewa tu muandamane wee afu mnakufaa nyie wakati wenzenu wanakunywa kideri na lushoro.

Kama chuo st agustine ipo.
fikiri vizuri kama wewe si mwenyeji wa huko huna uchungu wowote wanaoupata vijana na wakazi wa kanda ya ziwa,hivyo unapochangia utumie akili badala ya kuropoka.
 
hapo heading inatoa picha ya ukabila na ukanda.mbona wapo wasomi wengi tu kutoka kanda ya ziwa kwani chuo kiki dsm ni kwa ajili ya wazaramo au hospital ya bugando ni kwa ajili ya wasukuma .wanao kwenda kusoma nje wanatakiwa waishi/kukulia air port
We unasema tu kama isingekuwa juhudi binafsi za vijana toka kanda ya ziwa kutafuta elimu kwa njia zozote hao unaosema wasomi wengi wasingekuwepo,Vyuo vikuu katika nchi hii,vinawachukia sana vijana toka kanda ya ziwa,kwani hata kama mgomo umeanzishwa na Mzaramo au Mgogo,vijana wanaosakwa ni kutoka kanda ya ziwa,sasa kama sisi ndiyo tunafujo kwanini serikali isitujengee chuo kikuu hata kimoja huko ili tusomee kwetu kuliko kusoma kwa vitisho? chukulia mfano tangu kuanzishwa chuo kikuu cha DODOMA ni wanafunzi wangapi kutoka kanda ya ziwa wamefukuzwa kimagumashi kutokana na migomo ya wanafunzi,tena wanafukuzwa na hawaruhusiwi kujitetea hata kama migomo imeanzishwa na mgogo.Vijana wa kanda ya ziwa tumekuwa tukinyanyaswa sana huko vyuo vikuu,utafikiri elimu kwetu hatupaswi kuipata au ni ujinga na mazoea ya wahadhiri na serikali.,,,,MIMI naona tujengewe vyuo vikuu vingi ili tutoe watu watakao hoji na kuthubutu kufanya maamuzi magumu kwa manufaa ya Taifa,kwani kwa asili huwa tumefunzwa kusimamia haki.
 
Kwa Afrika ... It's not the vote that count ... It's who count the votes ... Hata Kama watachagua CDM 2015 , kkama Hakuna Tume Huru ya Uchaguzi ... Tegemea Maumivu na kukereka zaidi ... Mark my word!!!

Dalili zinaonesha kuwa itakuwa kama kenya! System ita-crash, kisha watahesabu manual, kisha ataapishwa mgombea wa CCM!...
 
Acheni ukabila Mwanza kuna St Agustine, CBE wana Campus yao, kuna Chuo cha Ualimu Nyegezi, kuna Chuo cha Kilimo, Bungando Hostpital kuna Chuo.

Sasa sijui unataka Mwanza wafanyie nini tofauti na mikoa mingine.
 
Pamoja na ukweli kwamba kwa miaka yote tangu uhuru mpaka sasa watu ya kanda ya ziwa wamekuwa wakikandamizwa na kunyimwa elimu, bado kundi hili kubwa limeendelea kukumbatia chama ambacho kimekuwa sababu ya umasikini mkubwa kwa wengi katika eneo hilo.
- Kwa miaka yote Serikali ilihakikisha kuwa shule za Sekondari zinabakia chache ili vijana wasipate elimu
- Serikali ikaweka mkakati wa makusudi ili eneo hilo lisipewe Chuo Kikuu cha Serikali.....
Palikuwa na sababu gani kuvipanga Vyuo Vikuu.. Dar... Morogoro... Dodoma? Kwa nini kimoja kisingekwenda kanda Ya ziwa?
- Kwa makusudi Serikali ikaweka mikakati kuhakikisha mazao ya biashara kanda ya ziwa yanapata bei za kusuasua ili wananchi wawe hoi kiuchumi....

Imefika wakati wa kila mtu kutumia alicho nacho. Kanda ya ziwa amkeni sasa na mtumie wingi wenu kwa maslahi yenu.
Anayekuja huko kutaka uraisi, kwanza ajibu swali ataifanyia nini kanda hiyo inayoibiwa mali kila kukicha na wajanja janja wanaocheka cheka tu....?
Zungusha macho na uone ni mali kiasi gani zinatoka Kanda ya ziwa na manufaa yake ni nini?

KWA KWELI NINYI WA KANDA YA ZIWA MNANIKERA....

Hivi mtachezewa chezewa mpaka lini? Mtakanyagwa kanyagwa mpaka lini? Mtaibiwa ibiwa mpaka lini? Mtadanganywa danganywa mpaka lini?
NASEMA TENA: MNANIKERA.......................EBOOOOOOO....

Ahsante kwa kutufumbua macho. Umetusaidia kutambua kwamba kwa sababu ya ujinga wetu tuliwanyamazia wakati mnahamisha raslimali za nchi kupeleka kwenu ambazo mlitumia kujengea mahekalu migombani, mashule ya sekondari kila kijiji, umeme kila kaya, barabara za lami kila Kata ilhali huku kwetu tukiwa hatuna barabara hata mkoa hadi mkoa achilia mbali umeme ambao tuliuona kama anasa. Ahsante sana mkuu.
 
Tuko mikoa zaidi ya sita yenye watu wengi,madini,samaki,mazao ya biashara hivi kwanini tusijitoe Tanzania tuanzishe nchi yetu? Tuna uwanja wa ndege mwanza tunaweza wasitufanye wapuuzi kwamba wao ndio wajanja saa hivi wanajenga bandari kwao kwa pesa za wananchi lakini Ziwa hamna kitu huu ni upuuzi

nimeambiwa eti huko kanda ya ziwa kuna mkoa mmoja una shule ya HIGH SCHOOL MOJA tu hivi ni kweli tena ya wasichana tu wakati wenzenu tunaingia kwenye high school moja kila tarafa sijui nyie mtafika lini huko!
 
Achana nao, waache waendelee kuumia tu. Nawashukuru TEC kwa kuleta SAUT!!!!
 
Acheni ukabila Mwanza kuna St Agustine, CBE wana Campus yao, kuna Chuo cha Ualimu Nyegezi, kuna Chuo cha Kilimo, Bungando Hostpital kuna Chuo.

Sasa sijui unataka Mwanza wafanyie nini tofauti na mikoa mingine.

sitaki kuamini kwamba hujui ukabila ni nini labda umeteleza,kanda ya ziwa inakaliwa na watu wa makabila ya aina zote yaliyopo Tanzania hii,labda kama unawashauri waanze kubaguana kwa kufuata ukabila wa mtu.
 
Acheni ukabila Mwanza kuna St Agustine, CBE wana Campus yao, kuna Chuo cha Ualimu Nyegezi, kuna Chuo cha Kilimo, Bungando Hostpital kuna Chuo.

Sasa sijui unataka Mwanza wafanyie nini tofauti na mikoa mingine.

Acha akili ndogo St Augustine ni cha Serikali? Mbona mnakurupuka kujibu,soma polepole ndipo ujibu ndio maana ziro nyingi

Tumehoji chuo cha serikali,unasema Cbe wana miaka miwili tu,wataweza kuwaacommodate wanafunzi wote wa kanda ya Ziwa? Unahesabu na chuo cha ualimu hauko serious ndio moto umeshaanza hivyo tunataka uwepo mgawanyo sawa wa mali za serikali sio wananufaika wengine

Bugando nayo unahesabu ni ya serikali? Boya kweli wewe
 
Acheni ukabila Mwanza kuna St Agustine, CBE wana Campus yao, kuna Chuo cha Ualimu Nyegezi, kuna Chuo cha Kilimo, Bungando Hostpital kuna Chuo.

Sasa sijui unataka Mwanza wafanyie nini tofauti na mikoa mingine.


Ndugu kwani ni lazima kuchangia kila mada?
 
Tanzania inazungumzia ukanda. Leo. Kanda ya ziwa: Butimba, kizumbi,buhare, bunda ttc,tarime ttc katoke ttc, tabora ttc, shy com,uhaziri tbr. Govt institutions. Ukiriguru, nyegezi fisheries.
Nn kingine lake zone.?
 
Me nadhani tungefanya mchakato,twende UN tukaombe kujitenga,tuwe na nchi yetu ya Lake zone.wao tuwaache na dar es salaam yao huko.
 
Southern highlanders: mbeya tech, ruaha cdti, what else? Msiifanye tz ikawa USSR 1996. Huku siberia, chechinia, Russia, kanda ya ziwa wasomi kibao.
Nyerere, warioba sinde, nyirabu kasanga tumbo, nyalali, boman, maprofesa usiseme.
Kanda ya ziwaaa. Danganyikeni.
 
acha 2015 ndo CCM itajua heshima ni nini na thamani yake ikoje ..kwanza tunajiweza na tunaweza kufanya..
 
hakuna cha ukabila wala nn,message sent,2015 mwendo wa....
 
Kwa ishu hii naunga mkono hoja. Hebu fikiria hiyo barabara wameipata lini? Ni majuzi tu, ilikuwa ili ufike mapema Mwanza na Mara hadi upite nchi jirani ya Kenya, waliachwa nyuma mno Kanda ya Ziwa. Kama vipi jiungeni daini state yenu bana mbona mnaweza tu, medhulumiwa sana, mmeonewa sana, mmetumika sana, huu ni wakati wenu wa kudai mabadiliko, it's your time guys wake up now na tutawaunga mkono:
 
Back
Top Bottom