Nakerwa na wananchi wa Kanda ya Ziwa

Nakerwa na wananchi wa Kanda ya Ziwa

Kanda ya ziwa imekuwa na watu wasio na njozi zozote.Imebaki ni kutahiri mabinti, UCHAWI, KUTETEMEKEA VIONGOZI WANAFIKI, na kula mabaki ya samaki achilia mbali wazungu kuua wana mara wanapokatiza mbugani.ITS SHAME KWA KWELI-UMEFIKA WAKATI WA KUAMKA SASA,AMKENI WANA KANDA YA ZIWA.
HATA WABUNGE WETU NI WALE WANAOSINZIA SINZIA BUNGENI. LOO,MUNGU ATUREHEMU WANA KANDA YA ZIWA victoria.

Akurehemu mwenyewe mp...mbaaa mkubwa weye.
 
Nendeni huko kwa wachaga ndo mkapeleke huo ukinga wenu...huku hatuchagui chama..tunamchagua mtu..
 
Kanda ya Ziwa sio Mwanza.....na Kanda ya Ziwa has nothing to do with Nyanza....au hujui Kagera walikuwa na yao...pia shinyanga walikuwa SHIRECU!
Tuambie mwana Mwanza gani alihujumu public university kujengwa Mwanza????

Basi wakulaumiwa ni Nyerere kwa nini akujenga chuo kikuu Mwanza.
 
Tuko mikoa zaidi ya sita yenye watu wengi,madini,samaki,mazao ya biashara hivi kwanini tusijitoe Tanzania tuanzishe nchi yetu? Tuna uwanja wa ndege mwanza tunaweza wasitufanye wapuuzi kwamba wao ndio wajanja saa hivi wanajenga bandari kwao kwa pesa za wananchi lakini Ziwa hamna kitu huu ni upuuzi
Yes to Lake Zone.Ipo siku kanda ya ziwa itaanza harakati za kujitenga, kwa yaendeleayo. Jiji la Mwanza kuwa ndio KITOVu.
 
Mleta hoja umenena. Napenda kuunga mkono hoja kwa aslimia 100+!Ni dhahiri kuwa kanda ya Ziwa inayojumuisha mikoa ya Mwanza,Mara,Shinyanga,Tabora,Kagera,Kigoma na mkoa mpya wa Simiyu imeonewa,iimepuuzwa,imenyonywa na imenyanyaswa kiasi cha kutosha tangu enzi za Mwalimu Nyerere.Ujinga,Unyonge na Upole wa watu hawa ndiyo umewafanya waonewe,wanyonywe na wanyanyaswa kiasi cha kutosha.Ukweli na Uwazi! Kijiografia Mikoa hii ina utajiri wa raslimali za asili ambazo Mwenye enzi Mungu aliziweka kwa maksudi maalumu. Lakini kutokana na wajanja wachache,waroho na wenye tamaa ya madaraka katika nchi hii Mikoa ya Kanda ya Ziwa ndiyo imeendelea kushikilia mkia katika nyaza za Kielimu,Kiuchumi na Kiutawala!!! Mpaka leo huwa najiuliza kwanini Mwalimu J.K.Nyerere(RIP) akiwa mwasisi wa Taifa hili alishindwa kuchukua hatua za maksudi za kuiendeleza Kanda hii kuanzia Kielimu,Kiuchumi na Kiutawala.Badala yake aliamua kuwaweka pembeni ndugu zake wa Kanda ya Ziwa na kuelekeza nguvu zake kwa kanda zingine kama Pwani,Kaskazini,Kusini na Nyanda za Juu.Niliwahi kuambiwa na wazee wa kisukuma kuwa Washashi(Jamii ya Wazanaki,Wailkizu,Wakurya n.k.)wana kawaida ya choyo. Hivyo Nyerere akiwa Mzanaki alichukua asili ya uchoyo na kuamua kuwanyanyasa Wasukuma ambalo ndilo kabila kubwa kuliko yote Kanda ya Ziwa na Tanzania yote kwa ujumla. Niliambiwa kwamba Nyerere alikuwa anajua nguvu ya kabila ya Wasukuma kama kabila kuwa wakielemika na kuwa na nguvu ya Kiuchumi basi utawala wake ungelikuwa mashakani! Kwa hiyo Nyerere akaamua kutumia njia chafu za KIKOLONI za DEVIDE&RULE na DO NOT EDUCATE THEM yaani wagawanye uwatawale na uwanyima elimu!!Hakika Nyerere alifanikiwa katika hilo maana Mzanaki huyu alihakikisha shule za sekondari zinajengwa chache sana na hakukuwa na Chuo Kikuu hata kimoja mpaka Nyerere alipoiaga dunia. Shule za sekondari Kanda ya Ziwa zilikuwa za kuhesabu moja moja ukilinganisha na kanda zingine kama Kaskazini. Nakumbuka kulikuwa na sekondari chache kama Kahororo, Bwiru Boys& Girls,Shybush/com,Tabora Boys,Mara Sek,Musoma Alliance na Tarime Girls, basi!!Ilhali ukilinganisha na Kanda kama Kasakazini mkoa wa Kilimanjaro peke yake ulikuwa na zaidi ya sekondari 50!Kwa kweli hapa Nyerere hakuwatendea haki watu wa Kanda ya Ziwa na alijua kile alichokuwa amekipanga.Kuna viongozi muhimu waliokuwa wanainukia toka Kanda ya Ziwa lakini Nyerere alihakikisha hao jamaa hawafurukuti na mara nyingi alitumia mbinu za kuwaweka ndani au kuwapeleka nje ya nchi kuwa mabalozi wa kudumu. Kuna mifano hai kama kina Bomanis Family:Marehemu Paulo Bomani,Emanuel Bomani,Judge Mark Bomani. Paulo Bomani akiwa kiongozi wa chama cha Wakulima chenye nguvu-Nyanza Federation alijikuta akipewa Ubalozi wa kudumu huko Marekani mpaka watu wakamsahau. Jaji Mark Bomani alianza kama Mwanasheria Mkuu wa Tanzania miaka ya 1960s lakini Nyerere alipoona anaanza ku-gain popularity akampemperusha kwenye Ubalozi cjui nchi gani mpaka anarudi Tanzania watu walishamsahau.Mbali na kina Bomani kulikuwa na kina Kasela Bantu,kina Abdulla Fundikira na waliokuwa watemi(wafalme) enzi za mkoloni,Nyerere alihakikisha wananyamazishwa kwa hila au kwa kupewa ubalozi au kazi ambazo hazina exposure kwa Watanzania hasa Wana Kanda wenzao wa Ziwa. Mpaka leo hii more than 50yrs of independence watu wa Kanda ya Ziwa hawana mbele wala nyuma. Pamoja na kugunduliwa kwa madini ya thamani kama Almasi za Mwadui,Dhahabu za Kahama,Geita, Ulyanhulu, Tulawaka na maeneo mengine bado mikoa ya Kanda ya Ziwa inaoneka iko nyuma vibaya sana kimaendeleo. Almasi na Dhahabu kutoka mikoa hii zinavunwa na majamazi wanaojiita wawekezaji baada ya sera ya ugenishaji wa migodi yote! Bado mikoa hii na wilaya zake hazina BARABARA ZA LAMI kwa sehemu kubwa! Bado wakulima wa Pamba,Kahawa,Mahindi,Karanga n.k. wameendelea kuwa fukara.Ukija kwa wavuvi hali ni hiyo hiyo. Masoko yote ya mazao ya Kilimo yamevamiwa na matapeli wanaoshrikiana na serikali kununua mazao ya wakulima kwa bei za kutupa huku wao wakijipatia faida nono. Bado elimu katika mikoa hii ni duni sana. Hakuna Chuo Kikuu cha serikali hata kimoja. Pongezi zieende kwa taasisi za kidini kwa kuanzisha chuo Kikuu cha St. Augustine pale Mwanza vinginevyo watu wa Kanda hii wangelishia kusikia tu kuwa kuna vyuo vikuu vya UDSM,Sokoine,UDOM,Mzumbe n.k. Inasikitisha kuona kwamba upuuzi huu bado umeendelezwa na awamu zote chini ya CCM kuidhulumu mikoa ya Kanda ya ziwa. Wito wangu kwa Watanzania wa Kanda ya Ziwa ni kwamba sasa TUSEME BASI INATOSHA! Kwamba tumeonewa kiasi cha kutosha,tumenyonywa kiasi cha kutosha na tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Ujinga wetu,Unyonge wetu na Upole wetu ndiyo umesababisha haya yote. Adui mkuu wa watu wa Kanda ya ziwa ni chama Twawala CCM kwa hiyo basi dawa ni kuking'oa chama cha CCM kutoka kwenye uongozi hapo mwaka 2015. Naamini hili litawezekana kwa vile sasa tupo kwenye mchakato wa Katiba mpya ambayo itapatikana mapema kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2015. Lazima Watanzania wa Kanda ya Ziwa washikane kwa hali na mali ili kukitupilia mbali chama dhalimu cha CCM ili kuweza kujikomboa.Nina amini kuna maeneo ambayo yameonyesha nia ya kutaka mabadiliko katika Uchaguzi Mkuu uliopita wa 2010. Mkoa wa Mwanza na hasa Jiji la Mwanza walionyesha kuwa hawataki tena kuburuzwa na chama cha Mafisadi wa CCM. Lakini pia UK(Ukerewe) hawakubaki nyuma. Shinyanga hali kadhalika walionyesha cheche zao pamoja na hila na mbinu chafu za kuchakachua matokeo kama Shinyanga Mjini bado CHADEMA ilichukua majimbo ya Meatu na Maswa Magharibi. Kigoma, Musoma?Mara na Kagera CDM walipata Ubunge.Tunaomba mwaka 2015 kasi ya kuiondoa CCM kwa kutumia Katiba Mpya ifikie aslimia 99.999 kama siyo 100.Mungu Ibariki Tanzania,Mungu Ibariki Kanda ya Ziwa na watu wake.Ng'wabeja sana.
Mimi ndio maana sahihi yangu itasalia hivyo-hivyo, ninayo maana pana sana tangu nilipoamua kuiweka saini hiyo ambayo inazidi na itazidi kuwa ni maarufu. Lake zone tunanyanyaswa na kuachanizwa saana. Lake zone ina kila kitu, tatizo hatujapata strong figure to be promotted for presidency. Aliibuka Lipumba akaishia njiani, labda Zitto akienda vema na aitumie vema karata ya lake zone. Bado hajapatikana kiranja wa kumfata.Japo airport ndege zatua muda wowote, lakini Mwanza airport bado haina hadhi ya international. Mwanza ni jiji la pili hapa Tanzania, lakini tunayofanyiwa ni hovyoooo.Nitaendelea kuitumia sahihi yangu na werevu watabaini. Tumechoka.
 
Dar viwanda vya cement vitatu, Pwani kipo! Kanda yote ya ziwa hola! CCM ni mashetani
 
Wewe mkwapua simu, kwani bungando ni ya serikali? wasukuma wameonewa sana ifike wakati waseme basi yatosha...maji ya kunywa shida, usafiri shida, shule shida, wakilima vipamba vyao mnawapangia bei bila kujari gharama walizotumia, dawa za mifugo tabu tupu, aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaagh!!!!! wasukuma wenzangu amkeni acheni upimbi
Mkuu,Ndio tunaamka sasa, wabheja sana nkoi.
 
Pamoja na ukweli kwamba kwa miaka yote tangu uhuru mpaka sasa watu ya kanda ya ziwa wamekuwa wakikandamizwa na kunyimwa elimu, bado kundi hili kubwa limeendelea kukumbatia chama ambacho kimekuwa sababu ya umasikini mkubwa kwa wengi katika eneo hilo.- Kwa miaka yote Serikali ilihakikisha kuwa shule za Sekondari zinabakia chache ili vijana wasipate elimu- Serikali ikaweka mkakati wa makusudi ili eneo hilo lisipewe Chuo Kikuu cha Serikali.....Palikuwa na sababu gani kuvipanga Vyuo Vikuu.. Dar... Morogoro... Dodoma? Kwa nini kimoja kisingekwenda kanda Ya ziwa?- Kwa makusudi Serikali ikaweka mikakati kuhakikisha mazao ya biashara kanda ya ziwa yanapata bei za kusuasua ili wananchi wawe hoi kiuchumi....Imefika wakati wa kila mtu kutumia alicho nacho. Kanda ya ziwa amkeni sasa na mtumie wingi wenu kwa maslahi yenu.Anayekuja huko kutaka uraisi, kwanza ajibu swali ataifanyia nini kanda hiyo inayoibiwa mali kila kukicha na wajanja janja wanaocheka cheka tu....?Zungusha macho na uone ni mali kiasi gani zinatoka Kanda ya ziwa na manufaa yake ni nini?KWA KWELI NINYI WA KANDA YA ZIWA MNANIKERA....Hivi mtachezewa chezewa mpaka lini? Mtakanyagwa kanyagwa mpaka lini? Mtaibiwa ibiwa mpaka lini? Mtadanganywa danganywa mpaka lini?NASEMA TENA: MNANIKERA.......................EBOOOOOOO....
Mwanza first...Tanzania BAADAE.
 
Siku wananchi wote wa Tanzania watakapotambua thamani ya kura zao basi ndio siku vyama vya siasa pamoja na wanasiasa wataacha kufanya siasa za hadaa na ghilba.

Kwa wakati huu kanda ya ziwa ndio wakati wake kuamka toka usingizini kwakuwa kutokana na rasilimali za asili zilizopo kulipaswa kuwa na vyuo vikuu vya umma pamoja na viwanda vya uhakika vya pamba na samaki.

Nakumbuka watu wa Mbeya waliamua kuishika shati serikali hadi ikakipandisha hadhi chuo cha ufundi Mbeya (MTC) kuwa chuo kikuu cha sayansi na teknolojia Mbeya (MUST).
 
Pamoja na ukweli kwamba kwa miaka yote tangu uhuru mpaka sasa watu ya kanda ya ziwa wamekuwa wakikandamizwa na kunyimwa elimu, bado kundi hili kubwa limeendelea kukumbatia chama ambacho kimekuwa sababu ya umasikini mkubwa kwa wengi katika eneo hilo.
- Kwa miaka yote Serikali ilihakikisha kuwa shule za Sekondari zinabakia chache ili vijana wasipate elimu
- Serikali ikaweka mkakati wa makusudi ili eneo hilo lisipewe Chuo Kikuu cha Serikali.....
Palikuwa na sababu gani kuvipanga Vyuo Vikuu.. Dar... Morogoro... Dodoma? Kwa nini kimoja kisingekwenda kanda Ya ziwa?
- Kwa makusudi Serikali ikaweka mikakati kuhakikisha mazao ya biashara kanda ya ziwa yanapata bei za kusuasua ili wananchi wawe hoi kiuchumi....

Imefika wakati wa kila mtu kutumia alicho nacho. Kanda ya ziwa amkeni sasa na mtumie wingi wenu kwa maslahi yenu.
Anayekuja huko kutaka uraisi, kwanza ajibu swali ataifanyia nini kanda hiyo inayoibiwa mali kila kukicha na wajanja janja wanaocheka cheka tu....?
Zungusha macho na uone ni mali kiasi gani zinatoka Kanda ya ziwa na manufaa yake ni nini?

KWA KWELI NINYI WA KANDA YA ZIWA MNANIKERA....

Hivi mtachezewa chezewa mpaka lini? Mtakanyagwa kanyagwa mpaka lini? Mtaibiwa ibiwa mpaka lini? Mtadanganywa danganywa mpaka lini?
NASEMA TENA: MNANIKERA.......................EBOOOOOOO....

Sio hao tu, kanda ya kati nayo inaongoza kwa kuipigia ccm.
Cha kutambua ni kuwa Tairi isumbuayo ndiyo hufanyiwa matengenezo. Wa tz tuamke
 
Umenena kweli kamanda! inatia hasira sana! Ebu tubadilike kanda ya ziwa. haiwezekani tudharirishwe hivyo. angalia safu za viongozi wa serikali na vyama vya siasa km utaona kanda ya ziwa imetendewa haki! hii ndoho taabu imepitwa na wakati, ebu tuaamke sasa kanda ya ziwa. Uongozi wa nchi hii uko mikononi mwetu! ewe mwanakanda ya ziwa amka na useme big no kuwekwa njia ya kupitiwa na kunufaisha wengine.
 
Kwa Afrika ... It's not the vote that count ... It's who count the votes ... Hata Kama watachagua CDM 2015 , kkama Hakuna Tume Huru ya Uchaguzi ... Tegemea Maumivu na kukereka zaidi ... Mark my word!!!

Hilo lina uhalisia, lakini kuna mfano toka uchaguzi uliopita endapo wapiga kura watasimamia vizuri kura zao haki itatendeka.
 
Kanda ya ziwa ndio yenye ushawishi , lazima ukombozi uanzie lakezone kwa kishindo

Waacheni waendelee kulala tu, Minofu ya samaki inaondoka kwa ndege wao waokoteza mabaki, Pia madini yaondoka wao wakiachiwa mashimo na sumu katika maji. Wamekuwa ni zaidi ya tomaso
 
Pamoja na ukweli kwamba kwa miaka yote tangu uhuru mpaka sasa watu ya kanda ya ziwa wamekuwa wakikandamizwa na kunyimwa elimu, bado kundi hili kubwa limeendelea kukumbatia chama ambacho kimekuwa sababu ya umasikini mkubwa kwa wengi katika eneo hilo.
- Kwa miaka yote Serikali ilihakikisha kuwa shule za Sekondari zinabakia chache ili vijana wasipate elimu
- Serikali ikaweka mkakati wa makusudi ili eneo hilo lisipewe Chuo Kikuu cha Serikali.....
Palikuwa na sababu gani kuvipanga Vyuo Vikuu.. Dar... Morogoro... Dodoma? Kwa nini kimoja kisingekwenda kanda Ya ziwa?
- Kwa makusudi Serikali ikaweka mikakati kuhakikisha mazao ya biashara kanda ya ziwa yanapata bei za kusuasua ili wananchi wawe hoi kiuchumi....

Imefika wakati wa kila mtu kutumia alicho nacho. Kanda ya ziwa amkeni sasa na mtumie wingi wenu kwa maslahi yenu.
Anayekuja huko kutaka uraisi, kwanza ajibu swali ataifanyia nini kanda hiyo inayoibiwa mali kila kukicha na wajanja janja wanaocheka cheka tu....?
Zungusha macho na uone ni mali kiasi gani zinatoka Kanda ya ziwa na manufaa yake ni nini?

KWA KWELI NINYI WA KANDA YA ZIWA MNANIKERA....

Hivi mtachezewa chezewa mpaka lini? Mtakanyagwa kanyagwa mpaka lini? Mtaibiwa ibiwa mpaka lini? Mtadanganywa danganywa mpaka lini?
NASEMA TENA: MNANIKERA.......................EBOOOOOOO....
hatudanganyiki, kunywa maji ukalale, kama unapatamani hamia huko
 
Hii ni ishara kwamba sasa chadema wameshaanza kupoteza matumaini ya kutwaa dola kama walivyokuwa wakiota ndoto zao za alinacha. Sasa wanataka kuigawa nchi. Tanzania itabakia kama ilivyo na siijui sana mwanza na shinyanga lakini tabora na kigoma nazijua vizuri sana. Tabora na kigoma haziwezi kuwa siyo sehemu ya tanzania. Infwakti, sisi wanadarisalama tuna historia na Kigoma na Tabora ya zaidi ya miaka 300. Historia yetu na ukanda wa chadema haifiki hata miaka 70. Hivi mnasubiri nini kujiunga na wakikuyu wenzenu? Rais wenu Uhuru juzi ameshinda uchaguzi kwenu huko...
 
Kanda ya ziwa imekuwa na watu wasio na njozi zozote.Imebaki ni kutahiri mabinti, UCHAWI, KUTETEMEKEA VIONGOZI WANAFIKI, na kula mabaki ya samaki achilia mbali wazungu kuua wana mara wanapokatiza mbugani.ITS SHAME KWA KWELI-UMEFIKA WAKATI WA KUAMKA SASA,AMKENI WANA KANDA YA ZIWA.
HATA WABUNGE WETU NI WALE WANAOSINZIA SINZIA BUNGENI. LOO,MUNGU ATUREHEMU WANA KANDA YA ZIWA victoria.


Mtu unampa ubunge Wasira sura tu utafikiria sokwe unategemea akupe maendeleo gani?

Mtu malaya wa kichama ashatembea vyama zaidi ya vitatu lakini hamna anaeuliza kadi zake zingine ziko wapi,lakini angekuwa wa Cdm tayari TISS na polisi wangeshasema ni kesi ya ugaidi

Polisi wenyewe taabu mwanajeshi yeyote akistaafu jeshini akirudi anagombea vyeo ccm si walishaambiwa hawaruhusiwa kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa kaanza lini kuwa mwanansiasa kama si maigizo hayaa?
 
Waacheni waendelee kulala tu, Minofu ya samaki inaondoka kwa ndege wao waokoteza mabaki, Pia madini yaondoka wao wakiachiwa mashimo na sumu katika maji. Wamekuwa ni zaidi ya tomaso

pale geita pana vijana wanaendesha basikeli wenyewe wanaita daladala hawana matumaini ya maisha wazungu wanabeba dhahabu wenyewe wanaendesha basikeli route sh mia mbili, inatia huruma sana, vijana wamepigika katikati ya utajiri wanatakiwa kuongozwa wafanye maamuzi magumu wachukue utajiri wao waondokane na barabara za vumbi, maji machafu ya kunywana kuoga na pia wapate elimu bora kabisa toka katika utajiri ulio katika ardhi yao.
 
Back
Top Bottom