Nakata undugu huu wa mizinga....

Nakata undugu huu wa mizinga....

MadameX

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2009
Posts
7,792
Reaction score
3,859
Jamani huyu ni ndugu yangu tunashare mmoja wa wazazi, ni mtu wa matatizo sana. Mpaka leo hii yuko 40+ lakini ni mtu wa drama, from case to case za aina ya utapeli. Huwa pia anatabia ya uzushi na tabia nyingine nzito. Sasa naona umebaki undugu wa maslahi, kila siku ni mtu wa kutaka asaidiwe, yani hata changamoto za kupambana na maisha hana, siku akikujulia hali ujue kuna mzinga unakuja

Nimeamua kukata mahusiano sitaki zaidi ya salamu, naaanza na kublock number yake. Naombeni ushauri na busara zenu kwa uamuzi huu.
 
@MadameX pole sana,

Japo najua context zinaweza kuwa tofauti, I faced challenge similar to yours kutoka kwa uncle (mdogo wa mama yangu) ambaye naye ni something like 46 now lakini yuko hopeless sana. Ilikuwa kila nikiona simu yake au sms yake basi ujue ina mzinga juu yake

Wakati fulani akatoka kwa ndugu alipokuwa anakaa mwanzoni akaja kuishi nami na nilimvumilia kwa muda wa kama 5 to 6 months tukiwa tunasukumana kwani hata tabia zake was challenging

Good luck kijijini kuna mashamba na niliamua siku hiyo kumlia jiwe ngumu na nilipotoka kazini nilimwita nikamweka kikao nikamwambia sasa uncle inatosha na naomba sasa uone aibu hii haikubaliki. Nikamweka wazi (sijui kama niikuwa mkali sana but I think it was best option) kuwa nampa wiki moja tu kwangu aondoke na aende kijijini na msaada pekee nitakaompa ni gharama kidogo za kwenda kununulia pembejeo ili akaanze kilimo na mimi na yeye basi tena na kwa kweli sikuwa na huruma maana alipofika huko hakuweza kutulia kwenye kilimo na amekuwa mtu wa kuzurura na mii nimeamua kumpotezea, hata aombeje nimeamua siwezi kufuga ujinga kama ule

Nimemsaidia ajue kuwa na mimi nina malengo yangu ya maisha na nisingependa anilemee na kushindwa kujipanga kwa familia yangu binafsi

Mweke wazi na huo msimamo wako na sababu zako, ajue kabisa
 
..wiki takatifu hili.. Unatenda dhambi kubwa.

Kumbuka hujafa hujaumbika..

Usitukane mamba kabla hujavuka mto..
 
poleni sana ila msichoke kutenda mema,wapo wengi sana ndugu lawama na wengine ukimpa hela anaenda kujirusha baada ya kufanya mambo ya maana
 
Hiyo ndo hali halisi inayotupataga sisi wanaume kwa mademu.
 
Damu nzito kuliko maji! Na aliekupa wewe kiti ndo kamnyima nduguyo kiti na kumgea kumbi! Kutoa ni moyo wala si utajiri! Na mtu atoae huongezewa!

Hiyo mizinga kwani sh ngapi mpaka uvunje udugu yakheeeeeeee!!!!!!!! Pesa ngapi wazitapanya kwa lesswigs, mascara, viatu, maguo mipochi na ilhali si vitu vya kudumu watumia na kutupa ?????????

Huyo nduguyo hivo alivo anakeraa tena anakera haswaaaaaa ila bado ni kiumbe cha mola! Na yakupasa umpe zaidi kwa kumshukuru mola kuwa weye hukuwa kama huyo nduguyoooo!!!!!!

Itakufaa nini hata uwe na milki ya dunia nzima, majimali majimali ilhali wajua fika nduguyo analala na njaaa, au yupo polisi rumande na uwezo wa kumsaidia unao ila amekuchosha?

Kuna watu hawana ndugu kabisaaaaaaaaaa! Wakifa wazikwa na manispaaa bila ibada yoyote. Waomba mola hata wangempata ndugu kama huyo wako ila hakuwajaalia tena!

CHARITY BEGINS AT HOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mi nikiona mtu anataka avunje udugu kwa pesa ya mboga roho yaniuma sanaaaaa!
 
Damu nzito kuliko maji! Na aliekupa wewe kiti ndo kamnyima nduguyo kiti na kumgea kumbi! Kutoa ni moyo wala si utajiri! Na mtu atoae huongezewa!

Hiyo mizinga kwani sh ngapi mpaka uvunje udugu yakheeeeeeee!!!!!!!! Pesa ngapi wazitapanya kwa lesswigs, mascara, viatu, maguo mipochi na ilhali si vitu vya kudumu watumia na kutupa ?????????

Huyo nduguyo hivo alivo anakeraa tena anakera haswaaaaaa ila bado ni kiumbe cha mola! Na yakupasa umpe zaidi kwa kumshukuru mola kuwa weye hukuwa kama huyo nduguyoooo!!!!!!

Itakufaa nini hata uwe na milki ya dunia nzima, majimali majimali ilhali wajua fika nduguyo analala na njaaa, au yupo polisi rumande na uwezo wa kumsaidia unao ila amekuchosha?

Kuna watu hawana ndugu kabisaaaaaaaaaa! Wakifa wazikwa na manispaaa bila ibada yoyote. Waomba mola hata wangempata ndugu kama huyo wako ila hakuwajaalia tena!

CHARITY BEGINS AT HOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mi nikiona mtu anataka avunje udugu kwa pesa ya mboga roho yaniuma sanaaaaa!

@Lara1 unachoongea ni sahihi kabisa dada yangu,

Personally ni mtu ninaependa kusaidia kila ambae nitaona yuko katika uhitaji na mimi niko kwenye position ya kuweza kufanya hivyo...

Lakini je, unaweza kukubaliana na mimi kwamba kuna watu wengine wanajidekeza and they have decided to be beggars?

Yaani kwa mfano case yako hapo juu mpaka mtu nachukua hatua ya kumfanyia mpango apate pembejeo zote muhimu na kwa kuwa nguvu ipo na kilimo alishakifanya muda mrefu lakini matokeo yake vile vifaa vyote kaenda kuviweka tu huko anakazi ya kuzurura from one place to another na kuomba tu watu pesa bila kujishughulisha .....and at the age of 46...hana ulemavu wala nin...a very energetic...na ukiangalia kuan vibibi huko vinapiga jembe au kufanya vitu vya maendeleo??

Unamuuliza anakuambia sitaki jembe litanizeesha labda unifungulie duka...nyambaaaafu, me mwenyewe hata duka la kuuza pipi na bazoka sina
 
Damu nzito kuliko maji! Na aliekupa wewe kiti ndo kamnyima nduguyo kiti na kumgea kumbi! Kutoa ni moyo wala si utajiri! Na mtu atoae huongezewa!

Hiyo mizinga kwani sh ngapi mpaka uvunje udugu yakheeeeeeee!!!!!!!! Pesa ngapi wazitapanya kwa lesswigs, mascara, viatu, maguo mipochi na ilhali si vitu vya kudumu watumia na kutupa ?????????

Huyo nduguyo hivo alivo anakeraa tena anakera haswaaaaaa ila bado ni kiumbe cha mola! Na yakupasa umpe zaidi kwa kumshukuru mola kuwa weye hukuwa kama huyo nduguyoooo!!!!!!

Itakufaa nini hata uwe na milki ya dunia nzima, majimali majimali ilhali wajua fika nduguyo analala na njaaa, au yupo polisi rumande na uwezo wa kumsaidia unao ila amekuchosha?

Kuna watu hawana ndugu kabisaaaaaaaaaa! Wakifa wazikwa na manispaaa bila ibada yoyote. Waomba mola hata wangempata ndugu kama huyo wako ila hakuwajaalia tena!

CHARITY BEGINS AT HOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mi nikiona mtu anataka avunje udugu kwa pesa ya mboga roho yaniuma sanaaaaa!

Ushauri mzuri huu_though doesnt work in the real world.
 
@MadameX pole sana,

Japo najua context zinaweza kuwa tofauti, I faced challenge similar to yours kutoka kwa uncle (mdogo wa mama yangu) ambaye naye ni something like 46 now lakini yuko hopeless sana. Ilikuwa kila nikiona simu yake au sms yake basi ujue ina mzinga juu yake

Wakati fulani akatoka kwa ndugu alipokuwa anakaa mwanzoni akaja kuishi nami na nilimvumilia kwa muda wa kama 5 to 6 months tukiwa tunasukumana kwani hata tabia zake was challenging

Good luck kijijini kuna mashamba na niliamua siku hiyo kumlia jiwe ngumu na nilipotoka kazini nilimwita nikamweka kikao nikamwambia sasa uncle inatosha na naomba sasa uone aibu hii haikubaliki. Nikamweka wazi (sijui kama niikuwa mkali sana but I think it was best option) kuwa nampa wiki moja tu kwangu aondoke na aende kijijini na msaada pekee nitakaompa ni gharama kidogo za kwenda kununulia pembejeo ili akaanze kilimo na mimi na yeye basi tena na kwa kweli sikuwa na huruma maana alipofika huko hakuweza kutulia kwenye kilimo na amekuwa mtu wa kuzurura na mii nimeamua kumpotezea, hata aombeje nimeamua siwezi kufuga ujinga kama ule

Nimemsaidia ajue kuwa na mimi nina malengo yangu ya maisha na nisingependa anilemee na kushindwa kujipanga kwa familia yangu binafsi

Mweke wazi na huo msimamo wako na sababu zako, ajue kabisa

Ni uamuzi mzuri maana hata Yeremia 17:5 inasema amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake... tena kama akiwa hana matatizo ya kiafya au ulemavu wa kumfanya ashindwe kufanya kazi.
 
Ujue "mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba".Lakini pia,"tenda wema wende zako, usingoje shukurani" na ingawa "damu nzito kuliko maji" ukweli utabaki "chombo cha kuzama hakina usukani" ilhali "sikio la kufa halisikii dawa" na usishangae kabisa kupata "fadhila ya punda mateke". Ikiwa "jina jema hung'ara kizani" ujue pia "la kuvunda halina ubani".

Wasema "maji yakijaa hupwa" kama "mpanda ngazi hushuka" kwa vile "hakuna marefu yasiyo na tama"

"Mpanda farasi wawili hupasuka msamba" amua kama unataka kumsaidia umsaidie bila kero, na kama hutaki umuache bila kuona nuksani.
 
Damu nzito kuliko maji! Na aliekupa wewe kiti ndo kamnyima nduguyo kiti na kumgea kumbi! Kutoa ni moyo wala si utajiri! Na mtu atoae huongezewa!

Hiyo mizinga kwani sh ngapi mpaka uvunje udugu yakheeeeeeee!!!!!!!! Pesa ngapi wazitapanya kwa lesswigs, mascara, viatu, maguo mipochi na ilhali si vitu vya kudumu watumia na kutupa ?????????

Huyo nduguyo hivo alivo anakeraa tena anakera haswaaaaaa ila bado ni kiumbe cha mola! Na yakupasa umpe zaidi kwa kumshukuru mola kuwa weye hukuwa kama huyo nduguyoooo!!!!!!

Itakufaa nini hata uwe na milki ya dunia nzima, majimali majimali ilhali wajua fika nduguyo analala na njaaa, au yupo polisi rumande na uwezo wa kumsaidia unao ila amekuchosha?

Kuna watu hawana ndugu kabisaaaaaaaaaa! Wakifa wazikwa na manispaaa bila ibada yoyote. Waomba mola hata wangempata ndugu kama huyo wako ila hakuwajaalia tena!

CHARITY BEGINS AT HOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mi nikiona mtu anataka avunje udugu kwa pesa ya mboga roho yaniuma sanaaaaa!

Umeongea yote sina hata kuongeza umenifanya nitafakari sana.
Nina ndugu yangu ana pesa si mchezo yani nikisema ana pesa namaanisha ana pesa sana. Lakini ana mtoto he is 27 hamsaidii, ana ndugu zake pia wapo madereva daladala hawasaidii hadi uwa najiuliza hizo pesa zake zina maana gani yani sioni hata sababu ya kuwa nazo.
He got plenty of cars, hotels, maduka lakini what for if they cannot help your people pesa sio za kufuga ni za kutumia na katika kutumia ni kusaidia watu.
 
@Lara 1 unachoongea ni sahihi kabisa dada yangu,

Personally ni mtu ninaependa kusaidia kila ambae nitaona yuko katika uhitaji na mimi niko kwenye position ya kuweza kufanya hivyo...

Lakini je, unaweza kukubaliana na mimi kwamba kuna watu wengine wanajidekeza and they have decided to be beggars?

Yaani kwa mfano case yako hapo juu mpaka mtu nachukua hatua ya kumfanyia mpango apate pembejeo zote muhimu na kwa kuwa nguvu ipo na kilimo alishakifanya muda mrefu lakini matokeo yake vile vifaa vyote kaenda kuviweka tu huko anakazi ya kuzurura from one place to another na kuomba tu watu pesa bila kujishughulisha .....and at the age of 46...??

Mimi bwana nachoamini ni kuwa Aliekupa wewe upeo na akili nyingi za maisha na kutafuta pesa ndo kamnyima huyoo ndugu yako upeo mkubwa na kumpa ule alionao!

Na yule ni mtihani wako wa maisha! Mungu anakupima tu kwa yule kiumbe wake. Kakupa uwezo wa kumsaidia kwa makusudi kabisaa, na hakuna mzinga atakaokupiga uncle ulio nje ya uwezo wako! La hasha uwezo wa kumsaidia unao labda tu ni priority ndo inagomba!

Binadamu tujifunze kuishi na mitihani yetu, misalaba yetu tusichoke kuibeba asilani. Ukishajua flani ni msalaba wangu basi wajitahidi usikerekwe nae, na kumzoea kumsaidia na kumfanya part ya maisha yako. Kwani pesa ngapi twalewea bar na hazituumi? na zaidi tunaunguza maini tu?

Mimi nina ndugu zangu wasumbufu ila nimewazoea na namshukuru sanaaa Mola, tena sanaaa kwa kunipa msalaba mwepesi, kuna watu ndugu zao Vichaaa kabisa, wengine walemavu, wengine wagonjwa! Mungu tuipushie mbali ila kumkimbia ndugu yako anaejielewa, hakuaibishi, anaenda chooni mwenyewe anachokubebesha mzigo ni pesa ndogo ndogo tu?????????? Ni kumkufuru Mungu kulaumu kwa na ndugu kama huyo!

So find uncle, be nice to him, na umpe uwezacho Gog will bless your hustles kila anachopunguza uncle atakurudishia mara 10. Uncle ile ndo destiny yake alio andikiwa!
 
Ujue "mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba".Lakini pia,"tenda wema wende zako, usingoje shukurani" na ingawa "damu nzito kuliko maji" ukweli utabaki "chombo cha kuzama hakina usukani" ilhali "sikio la kufa halisikii dawa" na usishangae kabisa kupata "fadhila ya punda mateke". Ikiwa "jina jema hung'ara kizani" ujue pia "la kuvunda halina ubani".

Wasema "maji yakijaa hupwa" kama "mpanda ngazi hushuka" kwa vile "hakuna marefu yasiyo na tama"

"Mpanda farasi wawili hupasuka msamba" amua kama unataka kumsaidia umsaidie bila kero, na kama hutaki umuache bila kuona nuksani.

Hhaaaaa, Mkuu Kiranga you said it all....hekima hizi
 
Ujue "mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba".Lakini pia,"tenda wema wende zako, usingoje shukurani" na ingawa "damu nzito kuliko maji" ukweli utabaki "chombo cha kuzama hakina usukani" ilhali "sikio la kufa halisikii dawa" na usishangae kabisa kupata "fadhila ya punda mateke". Ikiwa "jina jema hung'ara kizani" ujue pia "la kuvunda halina ubani".

Wasema "maji yakijaa hupwa" kama "mpanda ngazi hushuka" kwa vile "hakuna marefu yasiyo na tama"

"Mpanda farasi wawili hupasuka msamba" amua kama unataka kumsaidia umsaidie bila kero, na kama hutaki umuache bila kuona nuksani.

Hahahaaaaaaaa! Yakheeeeeee umenikumbusha mbali sanaaa na ufasaaa wa hii lugha! Umenikumbusha methali za Mwenda tezi na omo marejeo ngamani! Mgaa na upwa hali wali mkavu, Ikivumaa sanaaa ujue yakaribia kupasuka hiyo! Na kila mwamba ngoma huvutia kwakee!

Hivi vitu kuvisikia karne hii vikitamkwa kiufasahaa ni ndara sanaa labda kwenye kipindi cha Kiswahili radio 1 jumamosi majira asubuhi!
 
Mimi bwana nachoamini ni kuwa Aliekupa wewe upeo na akili nyingi za maisha na kutafuta pesa ndo kamnyima huyoo ndugu yako upeo mkubwa na kumpa ule alionao!

Na yule ni mtihani wako wa maisha! Mungu anakupima tu kwa yule kiumbe wake. Kakupa uwezo wa kumsaidia kwa makusudi kabisaa, na hakuna mzinga atakaokupiga uncle ulio nje ya uwezo wako! La hasha uwezo wa kumsaidia unao labda tu ni priority ndo inagomba!

Binadamu tujifunze kuishi na mitihani yetu, misalaba yetu tusichoke kuibeba asilani. Ukishajua flani ni msalaba wangu basi wajitahidi usikerekwe nae, na kumzoea kumsaidia na kumfanya part ya maisha yako. Kwani pesa ngapi twalewea bar na hazituumi? na zaidi tunaunguza maini tu?

Mimi nina ndugu zangu wasumbufu ila nimewazoea na namshukuru sanaaa Mola, tena sanaaa kwa kunipa msalaba mwepesi, kuna watu ndugu zao Vichaaa kabisa, wengine walemavu, wengine wagonjwa! Mungu tuipushie mbali ila kumkimbia ndugu yako anaejielewa, hakuaibishi, anaenda chooni mwenyewe anachokubebesha mzigo ni pesa ndogo ndogo tu?????????? Ni kumkufuru Mungu kulaumu kwa na ndugu kama huyo!

So find uncle, be nice to him, na umpe uwezacho Gog will bless your hustles kila anachopunguza uncle atakurudishia mara 10. Uncle ile ndo destiny yake alio andikiwa!

Lara ushauri wako uko sawa kabisa lakini kuna mazingira mengine no,

I will not believe over 1000 years kwamba this is kind of life uncle ameandikiwa, no bana...at 46 maisha ya kutanga tanga, mtu anaamua kuwa tayari kukusaidia kwenye eneo ambalo life can be something ppositive kwako lakini bado hutaki we unachotaka ni kukata miguu kwenye nyumba moja baada ya nyingine ya ndugu ili "ulelewe" ilhali u mzima kabisa na nguvu zako zote ni umeamua tu kufunga utashi wako kuishi hivyo

Ana mtoto mmoja wa kike ambae anashindwa kumhudumia kwa sababu ya maisha ya kutanga tanga....nimeona kuliko kupoteza resources zangu kwa uncle bora nizitumie kuhakikisha mtoto wake (mdongo wangu) anapata fursa ya kusoma mpaka atakapofikia kuwa na miguu yake

Ni kweli kwa tunaoamini katika Biblie (na hata Waislamu pia) asietunza watu wa kwao ni mbaya kabisa na ni mbaya kuliko hata asiyeamini....lakini katika kesi kama hii ya uncle kwa kweli no na naamini kama ungekuwa unamfahamu vizuri (maana kuhadithiwa sio sawa na uhalisia halisi) ungeona nilichofanya ni sahihi maana sasa ndugu wote ni kama tunaelekea kukubaliana sasa huyu mtu namna pekee ya kumchangisha akili ni kuahca ujinga wa kumlea na ujinga wake

Kuna ile ya mara moja chache mtu anakuambia ana tatizo umsaidie, lakini sio hiyo ya kuwa 100% dependant.........akuuuu, ngoja hiyo hela ambayo ningempa iende imsaidie binti yake ajikwamue kimaisha
 
Damu nzito kuliko maji! Na aliekupa wewe kiti ndo kamnyima nduguyo kiti na kumgea kumbi! Kutoa ni moyo wala si utajiri! Na mtu atoae huongezewa!

Hiyo mizinga kwani sh ngapi mpaka uvunje udugu yakheeeeeeee!!!!!!!! Pesa ngapi wazitapanya kwa lesswigs, mascara, viatu, maguo mipochi na ilhali si vitu vya kudumu watumia na kutupa ?????????

Huyo nduguyo hivo alivo anakeraa tena anakera haswaaaaaa ila bado ni kiumbe cha mola! Na yakupasa umpe zaidi kwa kumshukuru mola kuwa weye hukuwa kama huyo nduguyoooo!!!!!!

Itakufaa nini hata uwe na milki ya dunia nzima, majimali majimali ilhali wajua fika nduguyo analala na njaaa, au yupo polisi rumande na uwezo wa kumsaidia unao ila amekuchosha?

Kuna watu hawana ndugu kabisaaaaaaaaaa! Wakifa wazikwa na manispaaa bila ibada yoyote. Waomba mola hata wangempata ndugu kama huyo wako ila hakuwajaalia tena!

CHARITY BEGINS AT HOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mi nikiona mtu anataka avunje udugu kwa pesa ya mboga roho yaniuma sanaaaaa!

Chukua tano lara1
 
Ushauri mzuri huu_though doesnt work in the real world.

Binadamu tu mmekuwa na roho nzito na za kwanini! Kweli kwa wengi Udugu umebakia majina tu, ila kama huna kitu basi husaminiwi kabisaaa!

Mi naomba Mola aniepushie roho ya kwanini na dharau na dhihaka kwa ndugu zangu na viumbe wake kwa ujumla wao.
 
Ujue "mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba".Lakini pia,"tenda wema wende zako, usingoje shukurani" na ingawa "damu nzito kuliko maji" ukweli utabaki "chombo cha kuzama hakina usukani" ilhali "sikio la kufa halisikii dawa" na usishangae kabisa kupata "fadhila ya punda mateke". Ikiwa "jina jema hung'ara kizani" ujue pia "la kuvunda halina ubani".

Wasema "maji yakijaa hupwa" kama "mpanda ngazi hushuka" kwa vile "hakuna marefu yasiyo na tama"

"Mpanda farasi wawili hupasuka msamba" amua kama unataka kumsaidia umsaidie bila kero, na kama hutaki umuache bila kuona nuksani.
santeee!
na hiki cha BAKITA kumbe mkali hv!
napenda ujuzi wako wa lugha ndugu yangu!
:yo:
:yo::yo::yo:
 
Damu nzito kuliko maji! Na aliekupa wewe kiti ndo kamnyima nduguyo kiti na kumgea kumbi! Kutoa ni moyo wala si utajiri! Na mtu atoae huongezewa!

Hiyo mizinga kwani sh ngapi mpaka uvunje udugu yakheeeeeeee!!!!!!!! Pesa ngapi wazitapanya kwa lesswigs, mascara, viatu, maguo mipochi na ilhali si vitu vya kudumu watumia na kutupa ?????????

Huyo nduguyo hivo alivo anakeraa tena anakera haswaaaaaa ila bado ni kiumbe cha mola! Na yakupasa umpe zaidi kwa kumshukuru mola kuwa weye hukuwa kama huyo nduguyoooo!!!!!!

Itakufaa nini hata uwe na milki ya dunia nzima, majimali majimali ilhali wajua fika nduguyo analala na njaaa, au yupo polisi rumande na uwezo wa kumsaidia unao ila amekuchosha?

Kuna watu hawana ndugu kabisaaaaaaaaaa! Wakifa wazikwa na manispaaa bila ibada yoyote. Waomba mola hata wangempata ndugu kama huyo wako ila hakuwajaalia tena!

CHARITY BEGINS AT HOME!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mi nikiona mtu anataka avunje udugu kwa pesa ya mboga roho yaniuma sanaaaaa!
kuna mahali nilikuwa nakufyagilia haiba yako watu wala hawakunielewa!nazidi kuamini nilichokiamini the very day i set my eyes on lara 1
remember?
WEWE NI WA AINA YAKO!
 
Last edited by a moderator:
Imeandikwa heri mkono wa kutoa kuliko upokeao, na tenda wema uende zako.
ujionavyo nafsini ndivyo ulivyo, ukiona tashwishwi nafsini mwako jua una choyo la ukiona furaha jua u mwema. heri kutoa kwa wema kuliko kwa kutoa kwa tashwishwi. na wahenga walisema tamu ya muwa kifundoo.
 
Back
Top Bottom