gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,272
- 20,714
nilifikiri mbeba maboksi kumbe mwalimu wa lugha!!Ujue "mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba".Lakini pia,"tenda wema wende zako, usingoje shukurani" na ingawa "damu nzito kuliko maji" ukweli utabaki "chombo cha kuzama hakina usukani" ilhali "sikio la kufa halisikii dawa" na usishangae kabisa kupata "fadhila ya punda mateke". Ikiwa "jina jema hung'ara kizani" ujue pia "la kuvunda halina ubani".
Wasema "maji yakijaa hupwa" kama "mpanda ngazi hushuka" kwa vile "hakuna marefu yasiyo na tama"
"Mpanda farasi wawili hupasuka msamba" amua kama unataka kumsaidia umsaidie bila kero, na kama hutaki umuache bila kuona nuksani.
hahahahahahha!