Najuta kuoa mwanamke mlokole

Najuta kuoa mwanamke mlokole

Kwa maelezo yako na uwelewa wangu nianze na jinsi ninavyo kuona:
  • Mosi, unaelekeakuwa una wivu wa kupindukia kiasi kuwa hupendi mkeo atoke nyumbani hata kwa kwenda kanisani.
  • Pili una udikiteta fulani, ndani mwako ni amri tu hakuna mjadala (negotiation), Unalotaka ndilo linakuwa.
  • Una mapenzi ya kizamani ya kikurya ambayo yanahusisha kupigana pigana.
Ulipaswa kabla ya kuoa, uchunguze kwanza: Unataka mke wa kushinda kwenye baa au saloon ama kitchen party, maana hawa nao wapo ni wewe tu na upendeleo wako. Si rahisi kumbadilisha mtu mlevi akawa mlokole na mlokole akawa mlevi hivyo ulipaswa upate ready made kuliko kutransform. Mkeo, licha ya mapenzi yako ya kizamani ya kupigana pigana, amekusamehe, anataka mrudiane wewe hutaki. Maana yake huna roho ya msamaha. Waswahili husema 'Asiye samehe haliwezi penzi.' Kumbe wewe huwezi penzi ingawa unaweza kupanda.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa uhuru wa kila mtu kuabudu imani aitakayo, lakini wewe unataka mkeo aabudu namna unavyotaka wewe, hivyo bila kujua, unataka kuwa juu ya Katiba ambayo ndiyo sheria mama ya sheria zote nchini. Masikini nduyu yangu hata hujui kuwa kuvunja Katiba ni kosa. Unaishi katika jamii ya watu wasiostarabika, wastaarabu huheshimu sheria zilizowekwa. Ni wanyama wa porini ndiyo wanaoishi kama unavyotaka wewe na mkeo muishi.
Sijazungumzia upande wa mkeo wala wazazi wake kwa sababu sijawasikia, lakini kubwa ni wewe uliyeomba ushauri na wao hawajaomba chochote. Ndoa ni taasisi inapaswa iheshimiwe na watu wote ukiwemo wewe mwenye ndoa. Mtu yeyote aliyemo kwenye ndoa hushawishiwa wakati wote na mtu mmoja mmoja vikundi vya watu marafiki mbalimbali wakike kwa wakiume, lakini wewe mwenye ndoa unapaswa kuwa na ushawishi mkubwa kushinda makundi yote. Tunapomshawishi mke hatumshawishi kwa mabavu, tunamshawishi kwa hoja huku ukinyunyiza juu yake UPENDO usiopatikana mahala pengine popote isipokuwa kwako tu


Mleta Mada follow this advice .. Thanks..
 
Sijahalalisha, ila kinachotakiwa mume amshawishi mkewe kwa upendo. Mimi binafsi mke wangu alikuwa akisali kanisa fulani sitaki kulitaja, lilikuwa na ratiba kama ya mke wa mtoa uzi. Nilimwacha mke wangu akiendelea kusali kama kawaida huku nikimshawishi kujali familia yake kwa kutumia biblia ileile. Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa soma mwanzo. Mke anapaswa kumtii mumewe na mume anapaswa kumpenda mkewe kama mwili wake. Mtu amwenye upendo hawezi kuupiga mwili wake hadi kuutengua ubavu. Biblia inatuasa ' mke anayeishi na mume asiyeamini asimwache kwa maana mume aweza kuokoka kwa kuangalia matendo ya mkewe. Mke mwema ana wajibu wa kutunza familia yake kwa umahiri mkubwa.
Mwisho, kwa kuwa nilikuwa natumia pia mafundisho ya biblia, mke wangu akaona ni kweli. Dini inapswa iwe ile iletayo upendo katikati ya chuki, ilete faraja miungoni mwa wenye ndoa, ilete gundi ya kuwaunganisha badala ya kuwatenganisha, kwa maana imeandikwa 'alichokiunganisha Mungu mwanadamu asitenganishe. Biblia inasema tuonyane kwa upendo siyo kwa kutenguana mbavu. Shughuli nzima ya mapenzi ni ya kubembelezana, kama huwezi kubembeleza na kubembelezwa hakika huwezi mapenzi. Acha fanya kazi nyingine, lakini hakuna kazi nyingine mbala wa mapenzi

Very wise advice.. Mleta Mada again follow this advice.. Thanks.
 
Kanisa gani haijui kuna muda wa familia pia.....hawajui pia kuwa mama bora na kulea familia inavyotakikana pia ni moja ya uchamungu. zungumza na na mpe probation ya mabadiliko kwa ajili ya huyo mtoto
 
daaah Huuu ni usengerma kabisa had I Payslip yangu inamhusu nini sasa, Naunga mono kuachana na huyo mwanamke mtwange talaka 3 mchana kweupe halafu wazazi wake watamtafutia mlokole mwenzie huko haiwezekani mwanangu umuachishe kunyonya miezi 3 huumwi wala kisa kanisa daa amaizing.Makanisa sasa Hivi wanaanzisha Watu wao wanafanya ile Ndo kazi yao then wajinga sasa Ndo mtakuwa watumwa kupeleka sad aka na halambee za ila siku...piga chini
 
hivi hata hao wachungaji wa hilo kanisa hawasomi biblia au hata kujua haki ya mke kwa mumewe utadhani umewaolea wachungaji bwana hapo kuna vitu viwili sana akijirekebisha atapunguza ratiba za kanisani still bado kuna tatizo upande wa wazazi bado watakuendesha tu inshort hapo hakuna ndoa piga chini tu eti wazazi kama walikua wanataka kaa na binti yao wasingechukua mahari yako sasa hizi sio karne za kuendeshana ni wakati wa maamuzi magumu sasa rachel ameokota embe dodo kwenye mkorosho yeye aendele kuishi na
wazazi wake
 
Wapigwe tu maana hakuna namna ingine kama hashiki neno la Mungu kwamba mwanamke amtii mumewe basi apigwe enh kama hajui biblia inasema tuwe na kiasii yeye hana,kiasi anakaa kanisani 24/7 apigwe tu maana hataa kukuwekea vikao kila siku huku anayo makosa, ni kushindwa kutii maandiko yanayosema ndoa na iheshimiwe na watu wote! kwakweli mkuu huyo ni wakupiga mpige sana mpakaa atembee kwenye maandiko ila na wewe usiache maandiko :mkuu....yanasema hivi..mpende mkeo kama unavyojipenda wewe na sio umpende Rachel ambae sio mkeo.....angaliaa mwishoni msije kuonekana wabaya wote wewe tulia kaa mbali sana na Rachel nakuombaa mkuu nisikilize hutojuta
 
Mm demu akiniambia yeye ni mlokole...namgonga after ndo asinijue teeena... sitak tabu za hiv mm
 
Duh ama kweli mwanamke mpumbavu huvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe, mume hujali, hata mwanao pia hujali, wewe unaishi humu duniani kufanya nn kama watu wa muhimu kwako huwapi muda, huyu hata akifa kwenye hukumu kwa Mungu atachapwa vibao vitakatifu, na wazazi wake pumbaf kabisa, mtu ataavha wazazi wake ataambatana na mwenzie, sasa kama humsikizi mwenzio wewe baaaac, khalas
 
The red highlight is too wrong! Lengo la kuadhibu ni kurekebisha tabia-wanawake ni watoto wakubwa tu, so sometimes wanapaswa kurejeshwa kwenye njia sahihi!(kinachopaswa kuzingatiwa ni kiwango/ukubwa wa adhabu/kichapo). Binadamu tukiishi kwa kukatana/kuachana utahacha wangapi, na tutatengeneza jamii za aina gani? Naamini unaacha pale ambapo mazungumzo na adhabu zimeshindwa kufanya kazi!

Anyway, the "Rachel Gal" naona analeta balaaaaaaa! Mchepuko siyo dili japo njia kuu kuna foleni!


mwanaume kamili hapigi mke wala kulalamika. kama mtu anazingua unachukua njia yako. sioni hata haja ya kuwasema mabinti wa kilokole kwa sababu hukulazimishwa kuwa naye. kama na ameona mchungaji wake ni wa maana kuliko wewe chukua maamuzi magumu au mlowase. pia kuna ulokole na ugonjwa. ulokole hausemi mtu aharibu ndoa yake. hizo ni Imani za watu wasiojua wanachofanya. pia kisheria ukimuachisha mtoto maziwa kabla ya miezi sita unaharibu ubongo na kinga yake.
pia ungeenda kuongea na mchungaji wake. sio ustaarabu kupiga mke ambaye hulingani naye nguvu. pia hata wewe unaoneka una wenge jingi maana umempiga mke wako na kuja kumangaza hapa jf wakati yeye hawezi kujitetea. unapomsema mtu hakikisha naye yupo na anaweza kujitetea kama wewe. pia kwangu sioni tija ya ulichofanya hapa. mahusiano sio jela. mtu akizingua unajiachia kivyakooo
 
Mleta huu uzi nina mashaka na wewe kwa sababu kama kweli umemuoa mke mlokole basi ni lazima na wewe uwe mlokole vinginevyo ni udanganyifu unaleta hapa Jf. Swali kwako je wewe ni wa imani gani hasa?
 
The red highlight is too wrong! Lengo la kuadhibu ni kurekebisha tabia-wanawake ni watoto wakubwa tu, so sometimes wanapaswa kurejeshwa kwenye njia sahihi!(kinachopaswa kuzingatiwa ni kiwango/ukubwa wa adhabu/kichapo). Binadamu tukiishi kwa kukatana/kuachana utahacha wangapi, na tutatengeneza jamii za aina gani? Naamini unaacha pale ambapo mazungumzo na adhabu zimeshindwa kufanya kazi!

Anyway, the "Rachel Gal" naona analeta balaaaaaaa! Mchepuko siyo dili japo njia kuu kuna foleni!
tatizo sio Rachel,tatizo ni huyo mwanamke aliyemuoa hana akili, ni bora amuache kwani ipo siku atapata kesi ya kuua, sasa yote ya nn hayo ?
 
Mleta huu uzi nina mashaka na wewe kwa sababu kama kweli umemuoa mke mlokole basi ni lazima na wewe uwe mlokole vinginevyo ni udanganyifu unaleta hapa Jf. Swali kwako je wewe ni wa imani gani hasa?

mbona alishasema kuwa yy zamani alikuwa kwenye kanisa hilo lakini sasa amejitoa
 
kumbe ulimwacha Rache.... malipo ni hapahapa dunia... vumilia tuuuuu....
 
Pole sana ndugu; uliyetoa mada. Mkeo alishindwa tu kujielewa. Hakuna Mungu wa hivyo. Mungu mwenyewe alisema 'watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa' ona sasa! Mungu hafurahishwi na kushinda kwako kanisani au kutoa kila kitu na ndiyo maana pia akasema 'asiyewatunza wa nyumbani kwake ni mbaya kuliko yule asiyeamini! Binafsi nimetilia shaka imani ya kanisa hilo. Na lingine brother, 'Ulokoke' sio tatizo, tatiz makosa katika 'application' yake katika maisha yetu ya kila siku. Anyway nimekuunga mkono kwa msimamo wako ingawa mimi nisingempiga; angekutana na mizigo yake mlangoni na waraka mzito wa kwaheri ya kutoonana.
 
Ukisoma maamuzi ya "WAKWE TU" ukiunganisha na maamuzi ya "MKE" utajua ni watu wa aina gani... ningekuwa mimi nisingerudiana nae VILE VILE HAPO AWALI NISINGEMPIGA (UAMUZI NI WAKO NA MOYO UNAVYOKUTUMA).
 
Mzee umemtengua mtumishi wa Mungu mbavu subiri utatupwa kwenye lile ziwa la moto
 
Back
Top Bottom