Najuta kuoa mwanamke mlokole

Najuta kuoa mwanamke mlokole

Jaribu kumpa nafas nyingine kwanza huenda mambo yatakuwa kama utakavyo
 
Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa

Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.

Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.

Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi

Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.

Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu

Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana

Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.

Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao

Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa

Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena

Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.

Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?

Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?

Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense

Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.

Mi naona jaziba tu ndiyo zinazousumbua mkuu kwa kuwa anachokifanya hukipendi. Lakini ni bora mara mia afanyacho kuliko angekuwa anakuambia nipo nyumbani kumbe hayupo nyumbani au nipo kazini nimechelewa nivumilie kumbe yuko kwingine upande Fulani wa mji mkaao au nimesafiri leo nitarudi kesho kumbe yupo mahali furani ambako hawezi kukuambia na mengine na mengine (yote hayo mtoto atabaki na HG kumbuka!!!!).

Mi nakuomba ukubali kuwa umejaa jazba!!! kwa hiyo ili usaidike ondoa kwanza jazba na ufikiri vinginevyo utakuja kugundua kuwa umeoa mwanamke ambaye kwanza hukustahili kumuoa (yeye ameokoka wewe hujaokoka)na kumbe ni mke mzuri sana kwa mstakabali wa maisha yako na familia yako,

Mengine yote uliyosimulia hapa kama ni kweli yanazungumzika hasa ukiondoa jazba. Fikiria kidogo hapa kama kwa mfano asingezinduka kwa kipigo ulichokifanya kwake (pamoja na kujisifia kwako) ungekuwa jela na definitely ungefia hukohuko!!!! mwsho hivyo ulivyo ni matokeo ya yeye kuwa mke kwako kama utadhani natetea nisichokijua endelea na hako kamsimamo ulikoamua.

Muhimu sana msamehe halafu mshauriane kwa upole kwamba mfanyeje, nzuri Zaidi ni kwamba amekufuata na kutaka mazungumzo
 
Huyo kama ni kweli anafanya hivyo basi anahitaji kujifunza vizuri neno la Mungu
 
ndiyo mana mie siwezi kuoa mlokole maana walokole ndiyo malaya sana,,,,,,owa mwingine achana huyo

Completey rubbish. Walokole wa kweli, huwa wanajali familia na pia mambo ya Mungu pia. Yesu alisema, huwezi ukasema unampenda Mungu usie muona, wakati hauwajali wa nyumbani kwako. Asiye wajali wa nyumbani kwao ni mbaya na ameikana imani. Mungu ni wa utaratibu, kuna wakati wa kila jambo. Huyo mama itakuwa amepotoka na ahitaji msaada.

Lingine, unapaswa kuoa mtu mnafungamana imani, hilo lilikuwa kosa. Mngekuwa wa imani moja nafikiri ungeweza kumwelewa. Ninachokushauri, itisha kikao kati ya wewe, wazazi na pia mchungaji. Waeleze kila kitu, na mchungaji kama kweli ana hekima na ameitwa na Mungu atakuelewa. Haiwezakani kushinda kanisani kila siku asubuhi, mpaka jioni. Familia ndio kanisa la kwanza. Hii ndiyo torati ya kweli na manabii.Shalom
 
Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa

Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.

Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.

Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi

Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.

Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu

Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana

Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.

Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao

Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa

Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena

Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.

Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?

Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?

Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense

Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.

Kwanza pole! Neno la Mungu linasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa.... Huyo dada na Familia yake wamekukosea sana Lk km Mkristo hayna budi kuwasamehe na kuendelea mbele maana ameshajifunza isitoshe hakuwa akifanya usaliti... Mungu ni Mungu wa Utaratibu kuna muda maalumu kwa ajili ya Mungu na Muda uliobaki kwa ajili ya familia na Kazi
 
Kwa maelezo yako na uwelewa wangu nianze na jinsi ninavyo kuona:
  • Mosi, unaelekeakuwa una wivu wa kupindukia kiasi kuwa hupendi mkeo atoke nyumbani hata kwa kwenda kanisani.
  • Pili una udikiteta fulani, ndani mwako ni amri tu hakuna mjadala (negotiation), Unalotaka ndilo linakuwa.
  • Una mapenzi ya kizamani ya kikurya ambayo yanahusisha kupigana pigana.
Ulipaswa kabla ya kuoa, uchunguze kwanza: Unataka mke wa kushinda kwenye baa au saloon ama kitchen party, maana hawa nao wapo ni wewe tu na upendeleo wako. Si rahisi kumbadilisha mtu mlevi akawa mlokole na mlokole akawa mlevi hivyo ulipaswa upate ready made kuliko kutransform. Mkeo, licha ya mapenzi yako ya kizamani ya kupigana pigana, amekusamehe, anataka mrudiane wewe hutaki. Maana yake huna roho ya msamaha. Waswahili husema 'Asiye samehe haliwezi penzi.' Kumbe wewe huwezi penzi ingawa unaweza kupanda.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa uhuru wa kila mtu kuabudu imani aitakayo, lakini wewe unataka mkeo aabudu namna unavyotaka wewe, hivyo bila kujua, unataka kuwa juu ya Katiba ambayo ndiyo sheria mama ya sheria zote nchini. Masikini nduyu yangu hata hujui kuwa kuvunja Katiba ni kosa. Unaishi katika jamii ya watu wasiostarabika, wastaarabu huheshimu sheria zilizowekwa. Ni wanyama wa porini ndiyo wanaoishi kama unavyotaka wewe na mkeo muishi.
Sijazungumzia upande wa mkeo wala wazazi wake kwa sababu sijawasikia, lakini kubwa ni wewe uliyeomba ushauri na wao hawajaomba chochote. Ndoa ni taasisi inapaswa iheshimiwe na watu wote ukiwemo wewe mwenye ndoa. Mtu yeyote aliyemo kwenye ndoa hushawishiwa wakati wote na mtu mmoja mmoja vikundi vya watu marafiki mbalimbali wakike kwa wakiume, lakini wewe mwenye ndoa unapaswa kuwa na ushawishi mkubwa kushinda makundi yote. Tunapomshawishi mke hatumshawishi kwa mabavu, tunamshawishi kwa hoja huku ukinyunyiza juu yake UPENDO usiopatikana mahala pengine popote isipokuwa kwako tu
 
Asee umeeleza vizur sana ...wasiokuelewa nao watakuwa wametekwa akil Na pastor ...
 
Watu hawaoi wlokole wanaoa mke.ukioa ulokole fuata taratibu za ulokole ukioa mke pia fuata taratibu na makubaliano ya ndoa
 
Heheheee! Masimulizi yanahuzunisha ila presentation inafurahisha kwa kweli. Binafsi nahisi kama msipokua na mutual understanding baina yenu na maisha yenu, wewe ndio utakua kwenye upande wa kupoteza. Maana kupigana na mwanamke inaweza kukusababishia matatizo makubwa saana, unaweza ozea jela.

Maana hapo inaonesha kitu anachokifanya yeye na familia yake wanaona ni sawa tu, so kwa wewe kumbadilisha mawazo, kama hana akili ya kujiongeza, ni jambo gumu saana. Maana anaona wewe ndio umepotea.
 
Solution hawe pia kuwa mtu wa kanisa ndo mtaendana ila kama alikuwa hadanganyi hakuna haja ya kumfukuza mkeo rudiana na mkeo brada
 
Completey rubbish. Walokole wa kweli, huwa wanajali familia na pia mambo ya Mungu pia. Yesu alisema, huwezi ukasema unampenda Mungu usie muona, wakati hauwajali wa nyumbani kwako. Asiye wajali wa nyumbani kwao ni mbaya na ameikana imani. Mungu ni wa utaratibu, kuna wakati wa kila jambo. Huyo mama itakuwa amepotoka na ahitaji msaada.

Lingine, unapaswa kuoa mtu mnafungamana imani, hilo lilikuwa kosa. Mngekuwa wa imani moja nafikiri ungeweza kumwelewa. Ninachokushauri, itisha kikao kati ya wewe, wazazi na pia mchungaji. Waeleze kila kitu, na mchungaji kama kweli ana hekima na ameitwa na Mungu atakuelewa. Haiwezakani kushinda kanisani kila siku asubuhi, mpaka jioni. Familia ndio kanisa la kwanza. Hii ndiyo torati ya kweli na manabii.Shalom

mkuu lazima ukubali kuwa kuna wachungaji ni nguvu za giza tu.
we mchungaji anaomba mpaka salary slip yako ya nini?
si anataka kulinganisha mapato yako ili awe anakukamua zaidi?
lazima mujue kuwa sio kila anayehubiri katumwa na Mungu, kuna wengine wametumwa na matumbo yao.
 
mrudie keshajifunza huyo na ikiwezekana hameni mji am mtaaa. kaishi mbali na kwao!!!!!!!!!!
 
kama mama umemfungulia biashara,,na mchungaji awe kamshika,biashara inadumaa hata umuongeze mtaji wa bilioni yeye ataona maombi ya mchungaji ndo yameleta pesa na atazipeleka kwa mchungaji na biashara haiendi mbele

Kabisa usemalo hilo
 
ulokole bongo bhana, huyo dawa yake kumchukulia kifaa kingne then unampotezea hata asiporudi, mtu mzima na akili zake basi tu anakufanyia kusudi
 
Dah! Walokole weengi n kama wameshikiwa akili zao, manake wayafanyayo n tofaut na akili ya kawaida ya kufikiri, jamaa yangu flani pamoja na kupata zero form 6 pale kibaha baada ya kujaza vitu vya ajabu kwenye paper mpaka leo bado mlokole
Yaan kama vile wamemuazima mtu akili
 
Dah vaz la ulokole.......but ungemsamehe tu kwa kuwa hajachepuka ila kwa mashart mazito kuwa atabadilisha timetable za kanisa au ahame kanisa cos Mungu yuko pote na makanisa mazur yapo mengi tu
.Hata biblia imeandika mwanamke amtii na kumsikiliza mmewe sasa hilo kanisa linatumia biblia gani?na funzo kwa wakaka wengine mdada anakuvumilia weee wakat huna kitu halaf ukipata unajifanya oooh nataka mke mlokole.....mxuuuuuuuuu.....
 
Back
Top Bottom