Najuta kuoa mwanamke mlokole

Najuta kuoa mwanamke mlokole

Poleeee sana ndugu haya makanisa ya wachungaji kazi ni shida wanawajaribu akili watu
 
narudia tena mwanaume kamili na anayejiamini hpigi mke. mambo ya kupigana ni ya kinyama na hata wanyama hawapigi wanawake zao.huwezi kumrekebisha mtu kwakumpiga.unaonaje ukimpiga alafu ukamtia ulemavu.
kuna siku nilikuwa namwambia mtu pombe haifai.akasema hapana bwana inafaa ila usizidishe tu. nikamwambia tatizo la pombe ni pale ambapo unatakiwa kusema inatosha sasa.
mke sio mtu wa chini kiasi hicho. mbona wewe ukikosea hupigwi. huo ni mfumo kikurya ambao personally naudharau sana. wanaoongoza kwa mauza uza kwenye mahusiano mengi ni wanaume. wengi wanajisifia kufanya uzinzi ni uanaume na hata wanapofumania kuomba msamaha kwa mke wako unaona ni kujishusha. huo ni ujinga, upumbavu, ulimbukeni na ushenzi. mwanaume anayejitambua hawezi kuunda familia ya kupigana pigana. pia mambo ya kupigana sio ya kistaarabu wala kiungwana.
pia mke sio mtoto wa kuchapwa kiboko. mke ni patner. ana haki sawa kama wewe. watu wanaopenda kupiga ujue walikuwa abused wakati wa utoto wao.tabia ya kupiga ni tabia ya kinyama. ukishidwa kumrekebisha kwa vikao ujue umevamia ubavu wa mwenzakona sio wako huyo. sifa ya mchungaji mwema ni sauti yake kusikilizwa na kondoo wake. ukiona kondoo wako hasikilizi sauti yako ujue wewe sio mchungaji na hao au huyo sio kondoo wako
pia nakuona kama unahitaji msaada wakisaikolojia kwenye hili. am sure maafisa ustawi wa jamii wanaweza kusaidia na wanasaikolojia kama una hasira mbaya na tabia ya kupigamke. mtu anayemdharirisha mkewekwa kupiga ana chance kubwa pia kuwa huwa anabaka mkewe. hatuwezi kuunda taifa la wapigaji na wabakaji. lazima tabia hii ikome kabisa na ninasema ukweli nikikuta mtu anapiga mkewe barabarani lazima na yeye apigwe tu, maana hakuna namna nyingine na nasema apigwe tu apigaye mkewe
 
neno "MLOKOLE" ni neno TAKATIFU, mtu anaweza kujibebesha neno ulokole lakini yeye akawa siyo. ndivyo walokole weng wa miaka hii walivyo, wazee wengi wa zamani wamekuwa ni waadilifu na wapenda amani sana na sio kwamba wote walikuwa WALOKOLE, siku hizi mambo yapo kinyume xana huwez jua nini mwenzio anawaza juu yako. Mungu kwanza mambo mengne yafuate lakini neno linasema MWANAUME ampende mkewe na MKE amtii mumewe, kama kweli unampenda mke wako na yeye hakutii ww mumewe akumbuke kuwa BABA ni kichwa cha nyumba hata km kuna vitu kakuzidi hivyo inawezekana ww sio ubavu wake aliopangiwa na MUNGU, km ni ubavu wake na analeta ujuaji (bongo movie) basi na APIGWE TU!
 
Completey rubbish. Walokole wa kweli, huwa wanajali familia na pia mambo ya Mungu pia. Yesu alisema, huwezi ukasema unampenda Mungu usie muona, wakati hauwajali wa nyumbani kwako. Asiye wajali wa nyumbani kwao ni mbaya na ameikana imani. Mungu ni wa utaratibu, kuna wakati wa kila jambo. Huyo mama itakuwa amepotoka na ahitaji msaada.

Lingine, unapaswa kuoa mtu mnafungamana imani, hilo lilikuwa kosa. Mngekuwa wa imani moja nafikiri ungeweza kumwelewa. Ninachokushauri, itisha kikao kati ya wewe, wazazi na pia mchungaji. Waeleze kila kitu, na mchungaji kama kweli ana hekima na ameitwa na Mungu atakuelewa. Haiwezakani kushinda kanisani kila siku asubuhi, mpaka jioni. Familia ndio kanisa la kwanza. Hii ndiyo torati ya kweli na manabii.Shalom

Nashukuru umenena kwa busara ya hali ya juu.

Kwa maoni yangu hilo kanisa lina chembe chembe za cult. Cults huwa hazizingatii Biblia pamoja na kwamba zinaanza kana kwamba ni kanisa lenye msingi wa kiBiblia. Cult hizi huwa zinapindisha ukweli wa Mungu kidogo kidogo na hivyo kuwapotosha waumini taratibu, brainwashing. Mwishowe, muumini anakuwa hajitambui, haelewi na hataki kueleweshwa. Nia kuu ya waanzisha cults hizi ni kuwachomolea pesa, kuwadominate na to possess the members. Kibwetere ni mmojawapo alienzisha dini fake na kuishia kuwachomea kanisani waumini pamoja na kutoroka kusikojulikana na mali na fedha za hao marehemu. Pia Nkonyi nae wa huko huko Uganda, anaendesha vita na vitendo vya ukatili mkuu dhidi ya wananchi wa Uganda kwa kisingizio cha kuwa kiongozi wa The Lord's Resistance army. Anataka nchi iendeshwe kwa misingi ya amri kumi za Mungu ila at the same time anaua wasio na hatia pamoja na kubaka wanawake na watoto na kuwakata viungo.

Mwishowe, mtu alieokoka , kama alivyosema mkuu niliem quote, familia ni ya kujali maana 'asiewajali wa nyumbani mwake ameikana imani'.
 
Usije kuta mchungaji anakamua, maana dunia ya siku hizi imekuwa hovyo sana
 
Nadhani uende ukaongee na Baba Mchungaji kuna tatizo gani mke asahau majukumu ahudumu kanisa zaidi
 
Daaah!! Pengine unavua ulichokipanda kwa Rachel.

Ila ni kweli hata mimi nilishamshushia kipigo wife kwa ujinga huo.

Na hawa wanawake wa namna hii ndio hutufanya tuwe na michepuko aisee.
 
Kama amekuomba msamaha na kutaka kurudiana ina maana amegundua kosa lake na yuko tayari kubadilika. Nakushauri mkae chini muongee myamalize na umpe masharti yako. Siku zote kuna nafasi ya mkosaji kujirekebisha na wewe pia samehe mkeo. Kuoa mwingine naye atakuja na yake mwishowe utasema dunia imekupa kisogo. Mna mtoto tayari amka
 
Umenifurahisha uliposema "walipofika tu nikakamata wote wawili nikawapa kipigo kizito sana.."
 
Heri ukosee kushona suti, utashona nyingine kuliko ukosee mke au Mme...
 
" Waache wafu wazike wafu wenzao" njia iliyokuwa rahisi ni wewe kusoma sana maandiko ili uwe na uwezo wa kushirikiana naye na kumfafanulia baadhi ya mambo ikiwa na pamoja na kuwa na kiasi. Kumpiga ulikuwa hutatui bali ulikuwa unaendelea kumuongezea Muda wa kumlilia Mungu wake tena. Ulienda kanisa LA walokole ili upate mke mwenye hofu ya Mungu wakati wewe ukiwa huna Nuru hata punje hivyo haiwezekani Pepo akaenda kutembelea mbinguni hata siku moja hapo ilikuwa ni vita kati ya Nuru na Giza.
 
Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa

Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.

Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.

Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi

Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.

Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu

Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana

Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.

Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao

Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa

Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena

Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.

Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?

Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?

Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense

Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.
tupe mrejesho mkuu, kwa sasa imekuaje maana ni muda sasa umepita
 
Back
Top Bottom