Naitabiria Yanga mafanikio zaidi ya Simba msimu wa 2023-2024

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,151
7,918
Kuna dalili mbaya toka pre-season hadi jana kwenye Simba Day nimeshaaza kuziona zinazoashiria kuwa Simba inaenda kuwa na msimu mbaya sana.

1. Tukirudi nyuma mwishoni mwa msimu uliopita, kipa Aishi Manula aliumia na kwa sababu za kijinga kabisa Beno Kakolanya, kipa mwenye uwezo akawa anakaa benchi tena katika mechi kubwa na muhimu sana. Hili tumelizungumza sana na nadhani kuna uzi nilishawahi kuuleta. Cha ajabu zaidi, inaonyesha hakuna juhudi zilizokuwa zinafanyika kutafuta kipa mbadala ili kipindi cha usajili kikifika asajiliwe, matokeo yake tumekuja kuokota kipa wa KMC dakika za lala salama.

2. Pre-season baadhi ya wachezaji kucheleweshwa kupelekwa kambini bila sababu za msingi. Baadhi ya wachezaji wapya walikuwa wanazungushwa kwenye matukio hapo Dar wakati wenzao wako kambini na wengine kina Chama na Baleke walichelewa kupelekwa kambini bila sababu za kueleweka. Hapo hapo inasemekana kocha alienda kwenye kozi fupi kwao Brazil (na kama wiki moja kabla alikuwa huko huko Brazil). Kimsingi timu imefanya mazoezi ya pre-season ya pamoja ya labda wiki moja tu.

3. Kwanini timu imejaza mawinga na kuzembea kusajili kiungo mkabaji na beki wa kushoto mbadala wa Zimbwe? Msimu uliopita niliona Simba imefululiza kusajili wachezaji wafupi kwa mkupuo. Nilibaki najiuliza huyu anayefanya usajili ana nia gani, hili halioni au ni makusudi haya? Msimu huu tumebadili gia, tumejaza mawinga, unajiuliza nia ni nini? Ukiangalia mechi ya jana dhidi ya Power Dynamos, utaona shida ya toka msimu uliopita pale eneo la kati ipo pale pale na hili litaisumbua sana Simba. Kuna wakati nilishauri Israel Mwenda ajaribiwe beki wa kushoto na kweli Simba ikatembea na ushauri huo lakini ukiangalia zile mechi alizochezeshwa nafasi hiyo kama ile na Coastal Union bado hakuwa comfortable kucheza upande ule. Ni sawa kumtumia hivyo kwenye dharura ila kwenye dirisha la usajili kulikuwa na nafasi ya kusajili mtu ambaye anaweza kucheza hiyo nafasi kwa ufanisi.

4. Kuendelea kumkumbatia Bocco. Kama mpira ni burudani, mimi siburudiki nikimuona Bocco akiwa uwanjani anachezea Simba hasa ukizingatia wachezaji wenye viwango, uwezo na ambao uchezaji wao unavutia na wanakupa matokeo kama Moses Phiri wapo wanasugua benchi. Mimi naamini Robertinho bado ni kocha mzuri sana na siyo yeye anayemkumbatia Bocco, naamini anafuata amri anayopewa kutoka juu yanayombeba Bocco na yanayompiga pini Phiri. Simba isitegemee mafanikio yoyote ya ndani au nje kwa kumtumia Bocco katika zama hizi. Ni misimu mingapi Simba imekwama na kugotea Robo huko CAF kisa mapungufu ya hawa kina Bocco, kwa nini wahusika hawajifunzi?

Nadhani kuna watu pale kwenye uongozi ndani ya Simba hawana mapenzi ya dhati na timu. Wameshikilia dhamana ya kuwapa furaha wanasimba ila pia wamejiandaa kuitumia dhamana hiyo kuwaumiza kwa maksudi kabisa wanasimba kwa sababu wanazozijua wao wenyewe.

Yanga wana timu ya kawaida mno msimu huu ila pamoja na hilo kwa ninachokiona kinaendelea pale Simba, Yanga watakuwa na mafanikio msimu huu kuizidi Simba.

Nawasilisha.
 
Kuna dalili mbaya toka pre-season hadi jana kwenye Simba Day nimeshaaza kuziona zinazoashiria kuwa Simba inaenda kuwa na msimu mbaya sana.

1. Tukirudi nyuma mwishoni mwa msimu uliopita, kipa Aishi Manula aliumia na kwa sababu za kijinga kabisa Beno Kakolanya, kipa mwenye uwezo akawa anakaa benchi tena katika mechi kubwa na muhimu sana. Hili tumelizungumza sana na nadhani kuna uzi nilishawahi kuuleta. Cha ajabu zaidi, inaonyesha hakuna juhudi zilizokuwa zinafanyika kutafuta kipa mbadala ili kipindi cha usajili kikifika asajiliwe, matokeo yake tumekuja kuokota kipa wa KMC dakika za lala salama.

2. Pre-season baadhi ya wachezaji kucheleweshwa kupelekwa kambini bila sababu za msingi. Baadhi ya wachezaji wapya walikuwa wanazungushwa kwenye matukio hapo Dar wakati wenzao wako kambini na wengine kina Chama na Baleke walichelewa kupelekwa kambini bila sababu za kueleweka. Hapo hapo inasemekana kocha alienda kwenye kozi fupi kwao Brazil (na kama wiki moja kabla alikuwa huko huko Brazil). Kimsingi timu imefanya mazoezi ya pre-season ya pamoja ya labda wiki moja tu.

3. Kwanini timu imejaza mawinga na kuzembea kusajili kiungo mkabaji na beki wa kushoto mbadala wa Zimbwe? Msimu uliopita niliona Simba imefululiza kusajili wachezaji wafupi kwa mkupuo. Nilibaki najiuliza huyu anayefanya usajili ana nia gani, hili halioni au ni makusudi haya? Msimu huu tumebadili gia, tumejaza mawinga, unajiuliza nia ni nini? Ukiangalia mechi ya jana dhidi ya Power Dynamos, utaona shida ya toka msimu uliopita pale eneo la kati ipo pale pale na hili litaisumbua sana Simba. Kuna wakati nilishauri Israel Mwenda ajaribiwe beki wa kushoto na kweli Simba ikatembea na ushauri huo lakini ukiangalia zile mechi alizochezeshwa nafasi hiyo kama ile na Coastal Union bado hakuwa comfortable kucheza upande ule. Ni sawa kumtumia hivyo kwenye dharura ila kwenye dirisha la usajili kulikuwa na nafasi ya kusajili mtu ambaye anaweza kucheza hiyo nafasi kwa ufanisi.

4. Kuendelea kumkumbatia Bocco. Kama mpira ni burudani, mimi siburudiki nikimuona Bocco akiwa uwanjani anachezea Simba hasa ukizingatia wachezaji wenye viwango, uwezo na ambao uchezaji wao unavutia na wanakupa matokeo kama Moses Phiri wapo wanasugua benchi. Mimi naamini Robertinho bado ni kocha mzuri sana na siyo yeye anayemkumbatia Bocco, naamini anafuata amri anayopewa kutoka juu yanayombeba Bocco na yanayompiga pini Phiri. Simba isitegemee mafanikio yoyote ya ndani au nje kwa kumtumia Bocco katika zama hizi. Ni misimu mingapi Simba imekwama na kugotea Robo huko CAF kisa mapungufu ya hawa kina Bocco, kwa nini wahusika hawajifunzi?

Nadhani kuna watu pale kwenye uongozi ndani ya Simba hawana mapenzi ya dhati na timu. Wameshikilia dhamana ya kuwapa furaha wanasimba ila pia wamejiandaa kuitumia dhamana hiyo kuwaumiza kwa maksudi kabisa wanasimba kwa sababu wanazozijua wao wenyewe.

Yanga wana timu ya kawaida mno msimu huu ila pamoja na hilo kwa ninachokiona kinaendelea pale Simba, Yanga watakuwa na mafanikio msimu huu kuizidi Simba.

Nawasilisha.
Rudia tena mstari wa mwisho, eti umesema Yanga wana niniiii!!!!!
 
Kuhusu jipa kile chuma kilichosahiliwa linaenda kuchukua nafasi zaid ya hao waliokuwepo,.
Kuhusu Boko ni mchezaji mwandamizi , ni muhimu kua na wachezaji kama wale Kwa ajili ya kukijenga kikosi kisaikolojia na anajua mengi kuliko wageni hao.
Uwezo wake umepungua na Umri pia unachangia.
 
Hakuna kombe ambalo Yanga ataliacha mwaka huu ndani ya hii nchi, wanasimba tuambiane ukweli japo unauma. Nimewaangalia Yanga kwakweli hatuna uwezo wa kupambana nao hata robo.

Wenzetu wana vikosi vitatu tofauti na vyote kati ya hivyo hakuna hata kikosi kimoja ambacho timu yetu ya Simba inaweza kupambana nacho, ukweli usemwe.

Timu yetu inaendeshwa kiujanja ujanja tu na kuiga kila kitu wanachofanya wenzetu utopolo.
 
Ningeshangaa utopolo angeitabiriaje Mnyama mafanikio
Msifikie kukataana leo wakati huyo ni mwenzenu wa kila siku na humu anajulikana sana kwa mahaba na Simba. Yaani naona kwanzia jana watu akili haziwatulii kabisa maneno yamekuwa mengi kiasi kwamba Simba wenyewe kwa wenyewe mnapingana na kukataana. Mara hatumtaki kocha kwasababu hampangi Phiri, mara wengine kocha aachwe afanye anavyotaka ili mradi timu ishinde hata asipopangwa Phiri. Leo imeibuka mpya tena ya Simba kutopata mafanikio msimu huu. Sijui nini kimewakuta mashabiki wa Simba mpaka wenyewe kwa wenyewe mnashindwa kuongea lugha moja kabla hata mashindano hayajaanza.
 
Msifikie kukataana leo wakati huyo ni mwenzenu wa kila siku na humu anajulikana sana kwa mahaba na Simba. Yaani naona kwanzia jana watu akili haziwatulii kabisa maneno yamekuwa mengi kiasi kwamba Simba wenyewe kwa wenyewe mnapingana na kukataana. Mara hatumtaki kocha kwasababu hampangi Phiri, mara wengine kocha aachwe afanye anavyotaka ili mradi timu ishinde hata asipopangwa Phiri. Leo imeibuka mpya tena ya Simba kutopata mafanikio msimu huu. Sijui nini kimewakuta mashabiki wa Simba mpaka wenyewe kwa wenyewe mnashindwa kuongea lugha moja kabla hata mashindano hayajaanza.
Maendeleo ya haraka yanapatikana pale migongano ya hoja inaporuhusiwa. Inawafanya wahusika waache mambo yaliyopindapinda na wasijisahau
 
Lengo la Yanga kubeba makombe yote ni kuhakikisha wachezaji wa Simba wanasahau kabisa test ya sherehe ya kombe lolote! Hii ni psychological torture mbaya kuliko zote Kwa mchezaji! Hata wachezaji walipwe mishahara mikubwa kiasi Gani bila kombe misimu mitatu mfululizo hawatakuwa na morali inside! Hebu muangalie Kibwana akipangwa anavyojituma mlinganishe morali na Mzee Kapombe!

Upande wa mashabiki wa Simba , Yanga inabeba ndoo zote na kuhakikisha wanakuwa waropokaji na watukanaji grade one Dunia nzima! Bila kombe mshabiki huna cha kujivunia, unakuwa debe tupu haliachi kuvuma! Simba ni Debe Tupu fc linavuma! kolowizard mbumbumbu fc!

Kelele kibao ooh Mlete Phiri, hata wacheze Phiri hamsini uwanjani Simba itabaki kuwa timu mbovu, Haina mipango kama Yanga, Haina pesa kama Yanga, Haina uongozi kama Yanga ila pia Haina makombe kama Yanga, makombe ya Simba ni kuwa top ten CAF, kununua kibegi, kushindwa kiume na kujaza uwanja!
 
NAUNGA MKONO HOJA.

UAJIULIZA ANAYEFANYA USAJILI WA MAWINGA ANAAKILI TIMAMU KWELI?????????

Mawinga. 2023
1. Peter Banda.
2. Jimyson Mwinuke.
3. KIBU Denis.
4.Said Ntibazonkiza.
5. CLOTUS Chama 10-11.
6. Aubin Kramo.
7. Essomba Onana.
8. Luis Miquesson.

Hili KOSA lilifanyika 2020.
Mawinga walikuwa kumi, ukiunganisha idadi Yao mchango WAO MAGOLi hayafiki hata 10.

1 Bernald Morison.
2. Perfect CHIKWENDE.
3. Hassan Dilunga.
4. Ibrahim Ajibu.10--⁷
5.peter Banda.
6.pape sackho
7. Dunkan Nyoni
8. Valentine Muhilu.
9. KIBU Denis.
10. RALY BWALYA 8-10--11.

UNAJIULIZA HUU USAJILI UNAFANYWA NA MTU MWENYE AKILI TIMAMU KWELI.
 
Hakuna kombe ambalo Yanga ataliacha mwaka huu ndani ya hii nchi, wanasimba tuambiane ukweli japo unauma. Nimewaangalia Yanga kwakweli hatuna uwezo wa kupambana nao hata robo.

Wenzetu wana vikosi vitatu tofauti na vyote kati ya hivyo hakuna hata kikosi kimoja ambacho timu yetu ya Simba inaweza kupambana nacho, ukweli usemwe.

Timu yetu inaendeshwa kiujanja ujanja tu na kuiga kila kitu wanachofanya wenzetu utopolo.
Simba mbovu ilimfunga yanga imara bao 2 -0.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom