Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,646
Habari wakuu,
Kama mtakumbuka mnamo tarehe 10 mwezi mei mwaka huu mnamo saa tisa na dakika 50 nilipost thread ya kutafuta mchumba. Ingawa zoezi lilikuwa gumu sana lakini napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatie mchumba bora. Taratibu zote kwa mujibu wa mila nimezifuata na napenda kusema kuwa tutafunga ndoa katika kipindi cha miezi sita ijayo.
Napenda kuishukuru JF kwa kuniwezesha kupata mchumba bora ambaye natarajia atakuwa mke bora.
Nawashukuru wadau wote walionipa ushauri kupitia jamvini humu na wale waliojitokeza kutaka niwe mume mtarajiwa wao.
Mwisho: Mitandao ya kijamii ni mitandao inayoweza kuleta mapinduzi makubwa sana katika nchi yetu. Tuitumie vema ili tupate maendeleo na tupinge kwa nguvu zetu zote ubeberu wa aina yoyote wenye lengo la kuifungia au kuiwekea vikwazo mitandao ya kijamii, na hapa nazungumzia JAMII FORUM.
Nawasilisha.
Kama mtakumbuka mnamo tarehe 10 mwezi mei mwaka huu mnamo saa tisa na dakika 50 nilipost thread ya kutafuta mchumba. Ingawa zoezi lilikuwa gumu sana lakini napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipatie mchumba bora. Taratibu zote kwa mujibu wa mila nimezifuata na napenda kusema kuwa tutafunga ndoa katika kipindi cha miezi sita ijayo.
Napenda kuishukuru JF kwa kuniwezesha kupata mchumba bora ambaye natarajia atakuwa mke bora.
Nawashukuru wadau wote walionipa ushauri kupitia jamvini humu na wale waliojitokeza kutaka niwe mume mtarajiwa wao.
Mwisho: Mitandao ya kijamii ni mitandao inayoweza kuleta mapinduzi makubwa sana katika nchi yetu. Tuitumie vema ili tupate maendeleo na tupinge kwa nguvu zetu zote ubeberu wa aina yoyote wenye lengo la kuifungia au kuiwekea vikwazo mitandao ya kijamii, na hapa nazungumzia JAMII FORUM.
Nawasilisha.