Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

Mkuu, kuna kitu bado sijaelewa unamanisha nini hasa. Kwamba siyo vizuri kutotolesha mayai kwa kutumia kuku walio ya taga? If yes unadhani ni kwanini? Nahisi kuna point nzuri hapa ya kujifunza. Fafanua zaidi
kama hutojali.
 
Uzi wako mrefu Sana ola niliambiwa tu mayai yanayofaa kutotoleshea ni yale yaliyokaa sio zaidi ya siku 7 toka kutagwa. Hivyo ukizidisha mpaka siku 19 jua maya 30 yatakuwa jayana ubora hivyo hesabu yako hailipi
Nadhani hujasoma mpaka mwisho. Mayai yanaweza kukaa hata zaidi ya siku 30 Kama utakua unajua namna ya kuyahifadhi kwa kuzingatia joto stahiki na muelekeo wa mchongoko wa yai.

Na hesabu yangu inasema Kila baada ya siku kumi na sio kumi na Tisa.
 
Mkuu, kuna kitu bado sijaelewa unamanisha nini hasa. Kwamba siyo vizuri kutotolesha mayai kwa kutumia kuku walio ya taga? If yes unadhani ni kwanini? Nahisi kuna point nzuri hapa ya kujifunza. Fafanua zaidi
kama hutojali.
Huyu nadhani anaamisha uzao wa kuzaana kuku ndugu.

Wanashauri kuku wazaane angalau generation mbili tu. Baada ya hapo toa majogoo yote na utafute majogoo mengine ili kuondoa kizazi Cha kuku ndugu ambao Mara nyingi wanasumbuliwa Sana na magonjwa na wengi wanakufa wakiwa vifaranga.
 
Huyu nadhani anaamisha uzao wa kuzaana kuku ndugu.

Wanashauri kuku wazaane angalau generation mbili tu. Baada ya hapo toa majogoo yote na utafute majogoo mengine ili kuondoa kizazi Cha kuku ndugu ambao Mara nyingi wanasumbuliwa Sana na magonjwa na wengi wanakufa wakiwa vifaranga.
Yes mkuu, hili nalifahamu. Nilishangaa hapo kwenye kuatamia mayai yao, nikahisi kuna shida katika hilo. Nimemuelewa sasa, alimanisha kuchukua mayai pengine kwa sababu za kuondoa hiyo issue ya "inbreeding".
 
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne ( Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama.
Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo.
Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.
Nakaribisha maoni.
Nzuri but kuku 25 wanakula debe 1 kwa mwezi?? Unawapunja!!
 
Nzuri but kuku 25 wanakula debe 1 kwa mwezi?? Unawapunja!!
Siwapunji, baada ya kuchanganya chakula Chao kwa fumula elekezi naongeza na majani(mchicha au chines) au hydroponic folder au azola na funza (wa kutengeneza mwenyewe kupitia pumba na mbolea ya kuku). Kwahiyo sio debe moja tu la pumba ni pamoja na hivyo vi gine
 
Siwapunji, baada ya kuchanganya chakula Chao kwa fumula elekezi naongeza na majani(mchicha au chines) au hydroponic folder au azola na funza (wa kutengeneza mwenyewe kupitia pumba na mbolea ya kuku). Kwahiyo sio debe moja tu la pumba ni pamoja na hivyo vi gine
Uko vizuri. Nataka nijifunze hapo kwenye hydroponic folder na namna ya kutengenezs funza.
 
Uko vizuri. Nataka nijifunze hapo kwenye hydroponic folder na namna ya kutengenezs funza.
Kutengeneza funza ni rahisi

Chukua mbolea ya kuku iloweshe na maji weka kwenye ndoo au karai au chombo chochote chenye upana mzuri , chukua pumba za mahindi ziloweshe Kisha ziweke juu ya mbolea ya kuku iliyopo ndani ya chombo.

Then weka chombo chako eneo la wazi ili inzi waweze kufika kwa urahisi. Kila baada ya muda wa saa sita lowesha kwa maji na baada ya siku mbili mpaka nne utaanza kuona funza.
 
Uko vizuri. Nataka nijifunze hapo kwenye hydroponic folder na namna ya kutengenezs funza.
KUHUSU hydroponic ni shule ndefu kidogo jitahidi kutafuta Uzi humu unaelezea vizuri Sana kuhusu hiyo.

Jambo moja ambalo Uzi zote haujaeleza ni kwamba hydroponic folder kwa ajili ya kuku ni vizuri isizidi siku nne ili iweze kumeng'enywa kirahisi na kuleta matokeo chanya katika afya ya kuku.

Pia hydroponic kwa ajili ya kuku lazima ichukue nafasi isiyozidi 40% ya chakula chote cha Kila siku ili kuleta uzalishaji wenye tija kwa kuku wa mayai na nyama.
 
Kikubwa take action
Game inaendelea, sio maneno ni kazi juu ya Kaz.

IMG_20220107_181450_053.jpg
 
Nimefuga sasso 500 mwaka jana walikuwa wanakufa sana tofauti nanikifuga kroiler ilikuwa mara ya kwanza na ya mwisho.kila la kheri sasso mi mazuri kwa nyama siku kuhusu kutaga.sasso wanahitaji bio security yakutosha, hewa ya kutosha sio banda umetengeneza kama chumba cha kulala. Nasemea hao wengi maana 25 sio kaz kufuga.Dawa ya minyoo usisahau, Wape Newcastle wakifika minne.Ndui kama hawakuchanjwa watapukutika wote.muulize aliyekuuzia kama alichanja ndui.All the best
 
Hongera mkuu kwa hatua, ila hapo kwenye ratio ya mitetea na majogoo naona haiko sawa mayai yanaweza kosa mbegu. Majogoo ni mengi sana kwa idadi ya mitetea yako. Majogoo hapa yangekuwa matatu tu.
 
Hongera mkuu kwa hatua, ila hapo kwenye ratio ya mitetea na majogoo naona haiko sawa mayai yanaweza kosa mbegu. Majogoo ni mengi sana kwa idadi ya mitetea yako. Majogoo hapa yangekuwa matatu tu.
Hili nitalizingatia. Majogoo yatayoonekana afya yake hainishawishi nitayafanya kitowewo
 
Hongera sana Mkuu
Naomba nikukumbuashe kitu kimoja Cha muhimu ambacho ujapanga kukifanya

✓Ipo ivi Jogoo mmoja anaweza kumiliki/kumudu matetea kumi ivyo inabidi uwe na majogoo mawili tuu

✓ kwa sababu majogoo ya saso Yana kucha Kali ivyo kama yakiwa mengi huwa yanapelekea vidonda kwa matetea hasa upande wa ubavuni na mgongoni hivyo inaweza kupelekea kifo au ulemavu wa kudumu kwaiyo majogoo mawili yanatosha Mkuu nakufanya kuku wako kutaga vizuri

Kila lakheri Mkuu
 
Hongera sana Mkuu
Naomba nikukumbuashe kitu kimoja Cha muhimu ambacho ujapanga kukifanya

✓Ipo ivi Jogoo mmoja anaweza kumiliki/kumudu matetea kumi ivyo inabidi uwe na majogoo mawili tuu

✓ kwa sababu majogoo ya saso Yana kucha Kali ivyo kama yakiwa mengi huwa yanapelekea vidonda kwa matetea hasa upande wa ubavuni na mgongoni hivyo inaweza kupelekea kifo au ulemavu wa kudumu kwaiyo majogoo mawili yanatosha Mkuu nakufanya kuku wako kutaga vizuri

Kila lakheri Mkuu
With thanks
 
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne ( Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama.
Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo.
Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.
Nakaribisha maoni.
Mimi pia nafuga ninao Saso 100 now
Naweza sema wanahutaji full time care
 
Back
Top Bottom