Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

nimejifunza mengi sanaaa napenda kusema asante na tuendelee kupeana mrejeshoo hakuna kufanikiwa kwa muda mfupi katika haki wote tujifunze hiloo
 
Leo tarehe 18 mwezi wa 10, 2023.
Naendelea tena kutoa mrejesho wa awamu ya pili.

Kuku wanaendelea vizuri japo changamoto ya maginjwa haipukiki lakini cha msingi ni kuongeza juhudi na maarifa katika kukabiliana nayo na kuyadhibiti.
PXL_20231016_140132517.jpg
 
Malengo bado ni makubwa sana, mpaka mwisho wa mwaka ujao natarajia kuzalisha kuku wasiopungua 1000 kila baada ya miezi mitatu. Yaani niwe nnaweza kuuza kuku 1000 kila baada ya miezi mitatu, kwa tafsiri nyingine ni kuwa na uwezo wa kuuza kuku 300 kila mwezi.

Ili mipango iende sawa nimejenga cages za kulelea vifaranga ili kila mwezi niwe na uhakika wa kuweka vifaranga 300.
PXL_20230921_081015176.jpg
 
Malengo bado ni makubwa sana, mpaka mwisho wa mwaka ujao natarajia kuzalisha kuku wasiopungua 1000 kila baada ya miezi mitatu. Yaani niwe nnaweza kuuza kuku 1000 kila baada ya miezi mitatu, kwa tafsiri nyingine ni kuwa na uwezo wa kuuza kuku 300 kila mwezi.

Ili mipango iende sawa nimejenga cages za kulelea vifaranga ili kila mwezi niwe na uhakika wa kuweka vifaranga 300.View attachment 2785232
Congratulations mkuu
 
Kila la kheri mpambanaji. Nimemaliza kusoma andiko lako mwanzo mwisho pamoja na comment za wadau.
Wewe ni bonge ya mpambanaji.

Umenifanya nichukue kalamu na daftari kwa ajili ya kuandika.
 
Baada ya mwaka 2023 kuisha narudi tena na mrejesho mwingine.

December 2023 nilipata changamoto na kuamua kuuza kuku wote, nilitakiwa nisafiri na bahati mbaya sikuwa na mtu wa kunisaidia kuangalia kuku wangu ambao walikua takriban 100 na kidogo

Kwa sasa nimerudi tena na nna endelea mpaka kieleweke.

Tarehe 30 January nimeingiza vifaranga 100 aina ya sasso, ambavyo kwa sasa vinaelekea kumaliza wiki ya tatu, na tarehe 13 feb nimeingiza vifaranga 100 aina ya sasso vinakaribia kumaliza wiki ya kwanza.

Kwasasa malengo yamebadilika baada ya kuona kukaa na kuku muda mrefu ni gharama na haina tija. Ili upate faida kwenye kuku hawa wa chotara hakikisha unauza kuku wako ndani ya miezi mitatu tu. Ukizidisha unakua hauna uhakika wa kuipata faida kutokana na wanunuzi wengi wa kuku wanapenda kuku bei ya chini, sasa anavyokua zaidi ndio unavyopunguza idadi ya wanunuzi.

Ila unaweza ukachagua kwenye kila batch unayouza ukabakiza kuku 10 kwa ajili ya kuuzia wale wateja wasio na mawazo ya pesa, yaani wanaweza kununua kuku hata kwa 25,000 bila maneno mengi.

Malengo ya mwaka huu ni kuuza kuku sio chini ya 1000 au zaidi.
 
Wakiwa na siku moja
Wakiwa na wiki moja
Wakiwa na wiki mbili
 

Attachments

  • PXL_20240213_101155821.jpg
    PXL_20240213_101155821.jpg
    2 MB · Views: 9
  • PXL_20240207_123115474.jpg
    PXL_20240207_123115474.jpg
    2.6 MB · Views: 11
  • PXL_20240218_121407126.MP.jpg
    PXL_20240218_121407126.MP.jpg
    4.8 MB · Views: 9
Baada ya mwaka 2023 kuisha narudi tena na mrejesho mwingine.

December 2023 nilipata changamoto na kuamua kuuza kuku wote, nilitakiwa nisafiri na bahati mbaya sikuwa na mtu wa kunisaidia kuangalia kuku wangu ambao walikua takriban 100 na kidogo

Kwa sasa nimerudi tena na nna endelea mpaka kieleweke.

Tarehe 30 January nimeingiza vifaranga 100 aina ya sasso, ambavyo kwa sasa vinaelekea kumaliza wiki ya tatu, na tarehe 13 feb nimeingiza vifaranga 100 aina ya sasso vinakaribia kumaliza wiki ya kwanza.

Kwasasa malengo yamebadilika baada ya kuona kukaa na kuku muda mrefu ni gharama na haina tija. Ili upate faida kwenye kuku hawa wa chotara hakikisha unauza kuku wako ndani ya miezi mitatu tu. Ukizidisha unakua hauna uhakika wa kuipata faida kutokana na wanunuzi wengi wa kuku wanapenda kuku bei ya chini, sasa anavyokua zaidi ndio unavyopunguza idadi ya wanunuzi.

Ila unaweza ukachagua kwenye kila batch unayouza ukabakiza kuku 10 kwa ajili ya kuuzia wale wateja wasio na mawazo ya pesa, yaani wanaweza kununua kuku hata kwa 25,000 bila maneno mengi.

Malengo ya mwaka huu ni kuuza kuku sio chini ya 1000 au zaidi.

Mkuu nimekutext inbox
 
Kuna mtu kwenye uzi mmoja alikua anaomba ushauri kuhusu mradi wa kuku.
Nilimpa ushauri huu ambao nimeona niupost hapa huenda wanaofuatilia uzi huu wakapata kitu kidogo cha kujifunza.
👇👇👇
Mwaka 2019 nilikua nna wazo kama lako, na ni mawazo ya wafugaji wengi sana. Tofauti yangu na wewe ni idadi ya mifugo mi nilitamani nifikishe 1000 ndani ya mwaka mmoja we unahitaji kufikisha 5000 ndani ya mwaka na nusu.

Nilianza vizuri japo sikufikia malengo na nnaendelea kufuga mpaka leo lakini nilijifunza yafuatayo;

KWANZA
Kufuga kuku chotara ili umuuze kwa ajili ya nyama (kwa kutegemea soko la kawaida tofauti na special oder) zaidi ya miezi mitatu haitakulipa. Wanunuzi wengi wananunua kuku si zaidi ya 10,000 (ila inategemea na eneo ulipo hii ni kwa experience ya eneo nililopo.)

Hivyo basi hakikisha mipango na malengo yako yanachezea humo.

PILI
Hakuna tija(wala sio sifa) ya kuwa na kuku wa nyama 5000 kwa wakati mmoja ambao running cost inapanda kuliko selling price (mfano kuku 100 wanaweza wakala mfuko mmoja wa 80,000 lakini gharama yake ya kuuzwa ikalingana na kabla kula mfuko huo( labda wawe wa mayai ambao utakua unaokota mayai kila siku.

Hivyo basi ni bora ukawa na batch ya kuku wachache ambao watatoka kwa wakati tofauti tofauti ili kuepuka gharama za ziada ambazo zinapunguza faida. Mfano unaweza ukaamua kila wiki unauza kuku 100 au 200 au 300, so unakua unaingiza vifaranga 100 au 200 au 300 kila wiki wanaenda kwa mfululizo huo na idadi itaongezeka kila uhitaji wa soko utakavyoongezeka.

TATU
Chakula bora ni gharama sana hivyo unatakiwa kuanzisha mpango wa kutengeneza chakula mbadala kama vile hydroponic, azola na funza.

NNE
Ili kufikia malengo kwa wakati na kwa gharama nafuu fanya yafuatayo;

*Andaa kuku wazazi kwa ajili ya kutaga mayai ya kutotolesha kutokana na malengo yako ya mwezi. Kwa mfano unahitaji vifaranga 400 inahitaji kuku wazazi 100 tu.
Kuku hao watakua na uwezo wa kutaga sio chini ya tray 2(mayai 60)(za mayai yanayofaa kutotolesha) kwa siku na kwa siku 10 itakua una mayai 600. Kati ya mayai 600 huwezi kukosa kuku 400 kuanzia vifaranga mpaka kufikia kuku anaefaa kuuzwa. Hapa ni kwa malengo ya kuuza kuku 100 kila wiki, kwahiyo kwa mwezi kuku 400

Kumbuka idadi hii nnayokupa ni idadi ya chini kabisa ambayo hata zikitokea changamoto ni ngumu sana kushuka chini ya idadi hiyo.
Mfano kuku wazazi 100 wanaweza kuzalisha mpaka mayai 75 kwa siku, na mayai 600 yanaweza kutototewa mpaka vifaranga 500.

Hapo ukiangalia maelezo vizuri utagundua mayai ya kila mwezi wa kutotolesha yanapatikana ndani ya siku 10 tu, hizo siku zilizobaki utauza mayai ili kuendelea kupata hela ya kuhudumia kuku wazazi.

Biashara ikiwa nzuri utaongeza idadi ya kuku wazazi na mpango utakua kama hapo nilivyo eleza.

MWISHO
Kumbuka biashara ni hatua, so huwezi kuingia sokoni na kuku 1000, lazima uanze kuuza kidogo mpaka soko likutambue na upate wateja wa kutosha ili uuze mpaka zaidi ya idadi hiyo.
 
Back
Top Bottom