Naingia kwenye kufuga kuku chotara (Saso)

CoderM

Senior Member
Jun 15, 2015
102
272
Baada ya mvua za msimu huu kuwa za kusita na kupoteza mbegu kwa kupanda zaidi ya Mara mbili na kuungua na jua, huku nyanya nazo zikiwa zinachechemea, nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara Aina ya sasso wakati tunaendelea kusubiri neema ya mvua Kama itatuwezesha kuvuna.

Mpango ni kufikisha kuku 1000 na zaidi mpaka mwisho wa mwaka huu 2022.

Kwa Sasa nimeanza na kuku 25 (mitetea 20 na majogoo 5) ambao nimewanunua December 26 wakiwa na miezi miwili.

Malengo makuu ni kusubiri kuku wafike umri wa kutaga kuanzia march 2022 (wakiwa wamefikisha miezi 5) ili nitotoleshe mayai.

Kuku wakianza kutaga nategemea kupata wastani wa mayai 10 kwa siku (kwa uchache) sawa na mayai 100 Kila baada ya siku 10. Hii inamaana Kila baada ya siku 10 nitapeleka mayai 100 kutotolesha.

Baada ya siku 120 ambayo ni wastani wa miezi 4 kuanzia mwezi March sawa na mwezi July 22 nitakuwa nimetotolesha mayai 1200 ambayo kwa wastani nitapata vifaranga 1000 na kidogo (hayo mayai 200) naasume baadhi yatakuwa hayajatotoleshwa au vifaranga watakaoshindwa kuvuka nursery stage.

Kwahiyo mpaka inafika December 2022(insha_Allah) nitakuwa na kuku 1000 ambao ukiachana na parent 25 nilionza nao kutakua na wakubwa wenye miezi 6,5,4(watakua wameanza kutaga) size ya Kati na wadogo kabisa batch ya mwisho miezi miwili.

Baada ya kufikisha idadi hiyo nitaanza kuuza mayai au kutotolesha vifaranga kwa ajili kuuza au kwa ajili kufuga wa nyama.

KUHUSU GHARAMA
Kuku nimenunu 8000 Kila mmoja sawa na 200,000 kwa kuku wote.

Banda lilikuwepo linalowatosha kuku hao 25.

Kwa kuku watarajiwa Banda lao natarajia kuanza kuhangaika nalo baada ya kuku kuanza kutaga. Ambalo nitalijenga kwa awamu nne (Kila awamu nitakamilisha sehemu ya kuku 300) makisio ya gharama za ufundi kwa Banda la kisasala kuku 1000 na zaidi ambalo nimeandaa eneo la (20x10)m nimepata ni shilling 3.5M kwa materia ya eneo nililokuwepo.

KUHUSU CHAKULA
Kutokana nimewanunua wakiwa wakubwa nimetengeneza mchanganyiko wangu wa chakula ili kupunguza gharama. Ambapo gharama za debe moja(baada ya kuchanganya) ni chini ya 3000 na kuku wote 25 wanakula debe 1 na nusu kwa mwezi. Na nimeanza mchakato wa kutengeneza funza na hydroponic folders na baadae nitaandaa bwawa la azola.

Baada ya kufikisha kuku 1000 makadirio ya chakula kwa siku ni kilo 130 ambazo ni sawa kwa mchanganyo wangu wa chakula + hydroponic ni 500 kwa kilo. Sawa na sh 65,000 kwa siku

KUHUSU MATARAJIO YA FAIDA
kwa mwaka huu wote wa 2022 silengi kupata faida, nahitaji mradi ujisogeze na uwe stable. Kwa maana mpaka inafika December 2022 mradi uwe umerudisha gharama zangu japo kwa uchache na uwe inaweza kujiendesha kwa kuuza mayai au kuku.

Baadaya ya mwaka huu nategemea kupata faida Kama ifuatavyo.

1. Kwa kuwa natarajia kwenye kuku 1000 kuwe na mitetea isiyopungua 800 hivyo nategemea kukusanya mayai yasiopungua 510 kwa siku(kwa makadirio ya chini. Sawa na tray 17 kwa siku .

Tray 1ni sawa na tsh10,000 kwa mayai ya chotara (Bei za nilipo) sawa na tsh 170,000 kwa siku

NB: Mradi huu nitausimamia mwenyewe kwa asilimia 100 hivyo hakuta kuwa na gharama za ziada za mfanyakazi.

Hivyo ndivyo nitavyoiishi 2022.

Nakaribisha maoni.
 
Umesema umewanunua wakiwa na miezi 2 na March wataanza kutaga

Ila bei mbona kubwa sana kwa kuku wa miezi 2? 8000/- au sijaelewa hapo

Nilifuga kuku kama utani yaani sukuwa na nia ya kuwa mfugaji bali niliona kuna chakula kingi hiyo sehemu kama pumba na majani

Walifika mpaka 100 ila walikufa na kubaki 40 baada ya hapo nikauza wote

Ila hongera sana kwa hilo

Kuhusu kilimo kwa mvua ni kazi sana
 
Umesema umewanunua wakiwa na miezi 2 na March wataanza kutaga

Ila bei mbona kubwa sana kwa kuku wa miezi 2? 8000/- au sijaelewa hapo

Nilifuga kuku kama utani yaani sukuwa na nia ya kuwa mfugaji bali niliona kuna chakula kingi hiyo sehemu kama pumba na majani

Walifika mpaka 100 ila walikufa na kubaki 40 baada ya hapo nikauza wote

Ila hongera sana kwa hilo

Kuhusu kilimo kwa mvua ni kazi sana
Ni kuku wakubwa wanakua haraka, ukiwaangalia ni Kama wa kienyeji aliyeanza kutaga

16415668703941778633666562687362.jpg
 
Hongera sana mkuu. Ni mawazo mazuri sana. Kwa kusimamia mwenyewe hakika utafanikisha malengo yako na Mungu wetu wa mbinguni akutangulie. Ulishawahi kufuga before? Mimi pia hadi sasa nafanya kama unachofanya, nimeanza mwaka jana September na maendeleo siyo haba. Mimi ninafuga almost ndege (Wafugwao) wote wanaopatikana mazingira ya Tz.

Sasa nina haya machache nadhani yanaweza kukufaa;
1. Kwa idadi ya hao matetea unaweza kukomaa ukatotolesha kwa kutumia kuku wenyewe (sina hakika kama sasso wanaatamia). Kwa maoni yangu ni bora kuliko mashine. Ndicho nachofanya. Nilishawauzia watu mashin sana kabla sijaamua kuanza kufiga. Mashine zina changamoto sana ya efficiency. Unaweza peleka mayai 100 ukaambiwa yametotolewa 15. Unaweza zimia au ukahisi umeibiwa. Kuku ukimwekea mayai 13 atakupa walau vifaranga 10. Kuna maelezo mengi sana hapa ya kuelezea. Tuishie hapa kwa sasa.

2. Vifaranga wakitotolewa hakikisha wanakaa juu na poop inadondoka chini. Yaani jenga kitu kama chanja hivi ili huduma zao zote wapate wakiwa juu. Ukifuga hii staili ya siku zote vifaranga wakakaa chini/kwenye maranda utaumia sana. Utachukia ufugaji. Ukifanya hii staili nakuhakikishia hatakufa kofaranga yeyote kwa ugonjwa.

3. Hakikisha unajipanga kwa chanjo zote za muhimu za kuku. Japo kwa hiyo staili ya ukaaji hapo juu (2) niliyosema hata ukiamua usichanje watakua vizuri tu. But no need to risk kwa project kubwa. Wapige chanjo zote muhimu.

4. Hakikisha maji na chakula wanapata ipasavyo na kwa wakati. Bila kusahau usafi wa vyombo. Usicheze na usafi kabisa.

5. Jipe muda wa kukaa na kuku bandani na kiwaangalia, wasome tabia zao. Hii itakusaidia kujua kama kuku anaumwa au la. Kuna muda ugonjwa unaweza ingia usifahamu ukachelewa kuwapa dawa halafu ukakuumiza.

6. Vifaranga hakikisha wanakula super starter (pellet) kwa wiki 2 za mwanzo. Pia katika wiki hizi mbili za mwanzo ukiweza wanyweshe maji yenye multvitamin, OTC 20, Trimazine, Amplorium.

7. Hakikisha hizo dawa hapo juu plus fluban muda wote uko nazo ndani.

8. USAFI wa banda ni muhimu muda wote kama kuku wenyewe walivyo muhimu!

Anyway, yapo mengi ya kuelezea. Muhimu FOCUS.

Kila la heri mkuu!

Dongbei.


*
 
Hongera sana mkuu. Ni mawazo mazuri sana. Kwa kusimamia mwenyewe hakika utafanikisha malengo yako na Mungu wetu wa mbinguni akutangulie. Ulishawahi kufuga before? Mimi pia hadi sasa nafanya kama unachofanya, nimeanza mwaka jana September na maendeleo siyo haba. Mimi ninafuga almost ndege (Wafugwao) wote wanaopatikana mazingira ya Tz.

Sasa nina haya machache nadhani yanaweza kukufaa;
1. Kwa idadi ya hao matetea unaweza kukomaa ukatotolesha kwa kutumia kuku wenyewe (sina hakika kama sasso wanaatamia). Kwa maoni yangu ni bora kuliko mashine. Ndicho nachofanya. Nilishawauzia watu mashin sana kabla sijaamua kuanza kufiga. Mashine zina changamoto sana ya efficiency. Unaweza peleka mayai 100 ukaambiwa yametotolewa 15. Unaweza zimia au ukahisi umeibiwa. Kuku ukimwekea mayai 13 atakupa walau vifaranga 10. Kuna maelezo mengi sana hapa ya kuelezea. Tuishie hapa kwa sasa.

2. Vifaranga wakitotolewa hakikisha wanakaa juu na poop inadondoka chini. Yaani jenga kitu kama chanja hivi ili huduma zao zote wapate wakiwa juu. Ukifuga hii staili ya siku zote vifaranga wakakaa chini/kwenye maranda utaumia sana. Utachukia ufugaji. Ukifanya hii staili nakuhakikishia hatakufa kofaranga yeyote kwa ugonjwa.

3. Hakikisha unajipanga kwa chanjo zote za muhimu za kuku. Japo kwa hiyo staili ya ukaaji hapo juu (2) niliyosema hata ukiamua usichanje watakua vizuri tu. But no need to risk kwa project kubwa. Wapige chanjo zote muhimu.

4. Hakikisha maji na chakula wanapata ipasavyo na kwa wakati. Bila kusahau usafi wa vyombo. Usicheze na usafi kabisa.

5. Jipe muda wa kukaa na kuku bandani na kiwaangalia, wasome tabia zao. Hii itakusaidia kujua kama kuku anaumwa au la. Kuna muda ugonjwa unaweza ingia usifahamu ukachelewa kuwapa dawa halafu ukakuumiza.

6. Vifaranga hakikisha wanakula super starter (pellet) kwa wiki 2 za mwanzo. Pia katika wiki hizi mbili za mwanzo ukiweza wanyweshe maji yenye multvitamin, OTC 20, Trimazine, Amplorium.

7. Hakikisha hizo dawa hapo juu plus fluban muda wote uko nazo ndani.

8. USAFI wa banda ni muhimu muda wote kama kuku wenyewe walivyo muhimu!

Anyway, yapo mengi ya kuelezea. Muhimu FOCUS.

Kila la heri mkuu!

Dongbei.


*
Asante Sana kwa ushauri wenye nyama nyingi. Suala la kutotolesha kwa kuku wa kienyeji nitalifanyia kazi.
 
Uzi wako mrefu Sana ola niliambiwa tu mayai yanayofaa kutotoleshea ni yale yaliyokaa sio zaidi ya siku 7 toka kutagwa. Hivyo ukizidisha mpaka siku 19 jua maya 30 yatakuwa jayana ubora hivyo hesabu yako hailipi
 
Sina uzoefu/elimu sana na ufugaji wa kuku niliwahi kufuga zaidi ya mwaka siku za nyuma kabla sijaacha usimamizi kwa mtu wa familia.. Changamoto moja hasa kwenye utotoleshaji ni kama mkuu mmoja alivyochangia hapo juu, lakini hata ukitumia kuku wenyewe kutotolesha kuna ishu ya ubora wa mayai, wanasema kizazi husika cha mayai yaani kuku ulio nao kinakua si chema sana kutotolesha ndio maana baadhi ya watu huwa wanachukua mayai toka kwa wafugaji wengine ingawa napo changamoto ni uaminifu maana mayai yaliyokaa muda mrefu hayafai, hivyo kama ukitumia mayai ya kuku ulionao ni bora ufuatae utaalamu zaidi ya uchaguzi wa mayai.
 
Back
Top Bottom