Naibu Waziri Elimu katika kashfa vyeti

Huu ni utani wakuu! kila taasisi za kiraia zisimame huyu afutwe kazi mara moja!
 
Wakuu sidhani kama kupata matokeo ya mtu ni issue,ukienda library vitabu vyote vya matokeo vipo,hata pale UDSM library vitabu vipo,pia Tanganyika Library vitabu vya matokeo vipo,kama ni member wa TLS ni free,ila kama sio member ni shs 500 unalipia kwa siku,sikumbuki kama wamepandisha gharama.
 
Nawahakikishia huyu hataguswa na hii si kashfa ya kwanza kwa mawaziri wa JK na wabunge wanaofoji vyeti,,,
 
Mtahangaika sana wana CDM.Hivi suala la Mulugo kuhusu jina liliisha tolewa maelezo lakini kwa sababu yeye ameahidi kumg'oa Sugu jimbol a mbeya 2015 mmeanza kutapata.Mwacheni apige kazi.Mbona jina la Wegesa tumeisha sahau?Fanyeni kazi acheni majungu.

Tunaomba utupe hayo maelezo!!!!!
 
Gazeti limechelewa kwa Habari kama hii
JF walishaeleza kwa undani juu ya ujanja
wa Hamimu lakini kama ana God father

Mpaka sasa Mzee wa Tanganyika&Zimbabwe anapeta tu na per diem za Serikali
Hivi JK kama jf haingii lakini gazeti nalo
halioni jamani.

Hamimu Hassan aachie ngazi japo itauma.
 
Swala la Mulugo limeletwa mara nyingi tu hapa jf.lakini vyombo vya usaama viko kimya tu wala hata kushituka hawashituki.Imeletwa video ya Lwakatare hapa vyombo vya usalama vimekimbizana harakaharaka kwenda kumdaka Lwakatare hata kabla ya kujiridhisha kuwa kitu kilicho wekwa jf kinaukweli wowote ule.utafikiri wanakwenda kumkamata OSAMA ili wapate dola ambazo wamarekani waliahidi kuzitowa kwa mtu yeyote atakaefanikiwa kumkamata Osama.
 
mwananchi wanasema wamefanya uchunguzi yeye analeta stori za maadui zake kisiasa, mwananchi msiishie hapo nendeni kule iramba kwa mwigulu nae aumbuke, kururdia la saba sheria hairuhusu!
 

“Kughushi vyeti ni kosa la jina siyo kwa walimu tu, hata waandishi wa habari,” aliongeza Bunyanzu.

Kwa upande wake, Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) halikuwa tayari kutoa matokeo ya mitihani ya Mulugo na badala yake msemaji wa baraza hilo John Nchimbi alisema matokeo hayo ni siri ya mtahiniwa na hawezi kupewa mtu mwingine.


Chanzo: Gazeti la Mwananchi, Machi 25, 2013

Hii ni habari inayoambatana na anguko la elimu nchini mwetu
Nimepitia Wasifu wake kwenye tovuti ya Bunge, jamaa inaelekea yupo smart na anafahamu anachofanya! Sizani kama unaweza kum-sue kwa kosa la kufoji vyeti. Sana sana labda kama unaweza kum-sue kwa hilo la kurudia darasa la saba, jambo ambalo sizani kama lina uzito hasa ukizingatia watu wengi wa zamani hizo ndo zilikuwa design zao kv hawakuwa na mbadala....kwamba, mtu akifeli darasa la saba, njia pekee ilikuwa ni kurudia darasa with exception of fews ambao wangeweza kwenda private schools ambazo zilikuwa chache na hazithaminiwi.

Na kama ni kumfungulia mashitaka ya kutumia cheti ambacho si chake, labda afunguliwe mashitaka ya kupata ajira Southern Highlands kwa cheti cha mtu mwingine....hakika haielekei hata kidogo kwamba hadi sasa Mulugo bado anatumia cheti cha Dick Mulungu. Baada ya kumaliza A-Level pale Songea Boys 1996, 2002 akaenda Open Univeristy....utamkamatia wapi?!
 
Hii nchi yetu ni ya ajabu! Elimu ya watu wengi walio kwenye majukumu muhimu ya kuhakikisha ustawi na maendeleo ya nchi hii ni ya mashaka. Tusishangae kkuwa mambo hayaendi vyema, toka juu huo mti unateremka hivyo hivyo...vilaza ndio tumewapa majukumu. Ninadhani wanachofanya ni kutukomoa kwa kuwa tuliwaburuza shule, na hawataki kusikia ushauri hata kidogo.
Hapa naomba na mimi niweke jambo, vijana wenzangu naona tumeingia kwenye mtego wa kulalamika kila siku juu na kuongozwa na watu/viongozi wasio na sifa. Napenda kuwakumbusha katika kuwa katika hili tunaopaswa kulaumiwa ni sisi wenyewe ambao tunajiona tunasifa za kuwa viongozi na kutoa meaningful contribution to our Nation ila tunajifungia makwetu au tunajifanya tunang'ang'ana na ajira na wakati wa uchaguzi au hatushiriki kwenye shughuli za siasa. Kwa kufanya hivyo tunawaachia watu wa design ya kina Mulugo na wengineo wenye sifa za kuungaunga na elimu za kuvundika kujipenyeza kwenye siasa as their fallback position na kutuongoza, wakati sisi wasomi tupo kwenye ajira zetu. Katika hili tukumbuke kuwa hata siasa ni ajira na tena ni high paying ajira kuliko hata huo uafisa uliong'ang'ana nao.

Ni kwamba hapa sisi watanzania wenyewe ndio la kulaumiwa maana tumeruhusu akili ndogo itawale akili kubwa. Wewe mwenye sifa za kutosha kuitoa Tanzania hapa ilipo huwezi kufwatwa nyumbani ili upewe Ubunge/Udiwani. Ni lazma uingie kikamilifu kwenye siasa. Tunao wasomi wenye sifa wachache walioingia kwenye siasa kwa lengo la kuisaidia nchi, hakika matunda ya wasomi hao kuingia kwenye siasa tunayaona, na pia tunao mamburula mengi yaliyoingia huko na adha za wao kuwa kwenye siasa hakika tunazion.

Ndugu zangu zipo options mbili tu katika maisha kuhusu uongozi, ni either uongoze au uongozwe. Usipokubali kuongoza na kuwa mmoja wa wafanya maamuzi katika Taifa lako basi jua wazi utakuwa, kwa hiari yako mwenyewe umechagua upande wa kuongozwa na kulalama kila kukicha kama mume mwenye gubu. Lets take actions now, ianze sasa safari ya kuelekea kwenye uongozi ili ushiriki kwenye maamuzi ya nchi yako, acha kulalamika. Hivi kuna ubaya gani kama 2015 nafasi za udiwani hata vijijini zikashikwa na watu wenye sifa stahiki?? Unadhan maamuzi yalokuwa influenced na wasomi yatakuwa ni maamuzi yaliyokuwa influenced na watu wasioenda shule kama haya tunayoyaona leo???

Siasa inaenfluence kubwa sana kwenye maendeleo ya taifa lolote duniani. Hivyo, kuna haja ya wasomi na wenye sifa stahiki kufikiria kuikaribia siasa badala ya kuwaachia wababaishaji kudominate huko. Kwa kufanya hivyo ni kuwa tunakuwa kwa hiari yetu wenyewe tumeruhusu akili kubwa zitawaliwe na akili ndogo, matokeo yake ndo hizi lawama zisizoisha na kama tukiendelea kuikimbia siasa, tutayaona ua ajabu kuliko haya. Kama wewe ni muajiriwa, ajira zetu zinautaratibu wa kumpa mwajiriwa likizo ya kutosha kwenda kugombea. So ajira sio excuse ya wewe kutoshiriki kwenye siasa/uchaguzi kama mgombea. Amka fanya uamuzi sasa.
 
Huu ni utani wakuu! kila taasisi za kiraia zisimame huyu afutwe kazi mara moja!



Hii sasa Mheshimiwa Mulugo achia mwenyewe la sivyo watakuwekea pingamizi Mahakamani ambapo utatoka kwa aibu...kumbuka ya Bwana Kihiyo walivyomnyofoa!!!
 
hatoki ng'o!!! labda maandamano ya leo yangefanyika. jk alikuwa anateua mawaziri kwa kubalance mikoa, umri na jinsia! pia hivyo vyeo vya kisiasa havina madhara km watendaji wa chini wako comptent.
 
Wizara ya elimu inahitaji mwalimu aliebobea na mwenye sifa sitahiki. Huku kucheza na watoto wetu kwa uteuzi wa watu tu pitiapitia ni hatari sana. Na kwa ufanisi wanaoelekea kustaafu hwastahili nyadhifa huko wizarani wala taasisi kubwa za kitaaluma kama vyuo vikuu
 
kazi ya wanasiasa ni kupiga domo tu na kila kitu kuandikiwa na wataalam pale wizarani, mawaziri uozo wapo wengi tu, sifa ya uwaziri ni ukada tu wa ccm mf.lukuvi
 
Kwa nini mwajiri wa Mulugo ndio wababaishaji kuliko hata Mulugo mwenyewe! Kwa nini boss wake hatoi tamko juu ya hii sintofahamu??????

Au Mulugo ana akili sana - taifa litakosa mchango wake kwenye wizara hii nyeti ya Elimu hasa kipindi hii ambacho wanahitaji mtu mwenye uwezo kama Mulugo kuweza kuwaondoa kwenye kitanzi cha kufeli!!!!!!!!1 Wizara ya Elimu ni kitovu cha Uzembe.
Katika hali ya mfumo wa Rais kuteua mawaziri kwa vigezo anavyojua yeye, sisi kama wananchi wa kawaida tunapaswa tu kujua hapo Mheshimwa Rais kuna fadhila anailipa kwa kumpa hiyo nafasi. Maana haingii akilini ni kwanini huyu bwana ha-step down au hasimiamishwi ili kupisha uchunguzi huru ufanyike kuhusu elimu yake. JK na Mulugo hawaoni ugumu uliopo katika kuupata ukweli iwapo Mulugo akiendelea kuwapo ofisini?? Je Mulugo haoni kama uwepo wake ofisin unawanyima nafasi watu walio chini ya ofisi yake hasa baraza la mitihani na wizara kwa ujumla kutoa ushirikiano wa kutosha katika kubaini ukweli. Yeye hatoona raha ukweli/utata juu ya elimu yake ukiwa cleared??

Aidha, nilitaka na yeye Mulugo afahamu kuwa muungwana msuli ukidondoka, hatimui mbio uchi. Badala yake anatakiwa kuchuchumaa na kuliokota. Anachokifanya sasa kulumbana kupitia magazeti ni kujichafua zaid, kama ana uhakika na elimu yake na mambo yake, si amuandikie tu Rais barua ya kumwomba akae nje ya huo unaibu waziri wa miezi kadhaa ili kupisha uchunguzi?? anaogopa nini kufanya hivyo?? si amesema anauhakika na mambo yake ya elimu???Haoni kuwa atapata credits zaid kama itakuwa proven yupo clean????? Haoni kuwa atafunga huu mjadala kwa mbwembwe???

Kumbukumbu zangu zinaniambia kuwa last time baada ya Sugu kuibua hili sakata, Naibu Waziri Philipo Augustine Mulugo, Hamimu Hassan, Hamimu Augustino, Dickson Mulungu (nadhan sijasahau jina) alipigiwa simu na mwandishi akasema kuwa yupo safarin na akifika ofisini basi atakuwa na wakati mzuri wa kulisemea hilo. Kwli hakujitokeza teeeeeeeeeeena hadi leo sakata hili lilipoibuka upya. Anavyosema kuwa ameshalijibia karibu mara 20, mbona kama napata shida kuelewa??? Kalijibu ndani ya mipaka ya nchi hii hii au kajibia wap na kamjibu nani?? Anadhan kama majibu yake yalieleweka kwann wananchi waendelee kumzonga???Lakini pia ubadilikaji wa hayo majina umeambatana na viapo vya mahakamani???

Kwako JK baada ya kuona mtu anaelimu ya kuvundika, kwann unamuacha aendelee kukaa katika wizara inayoongoza kwa kufanya vibaya??? Does it mean that huna uchungu na kuporomoka kwa kiwango cha Tanzania na kufail kwa watoto wetu wewe hakukuhusu?? Hivi kweli Mhe. hakuna mtu competent kuliko hawa waliorundikana kwenye hii wizara inayoongoza kwa ku underperform??? Nini mchango wa hawa mawaziri wako katika hii wizara??? Au huyu bwana ndiye mtaalamu na mshauri hadhimu wa Ndugu yako Kawambwa na bila huyu Kawambwa hawezi kukaa ofisin???

Maswali haya yakijibiwa na viongozi wa chama tawala ambao ni members humu yatanisaidia sana kuupa relief ubongo wangu kulingana na GB zilizobebwa na haya maswali in my brain/Hard Disk Drive.
 
Kama,
"TANGANYIKA+ZIMBABWE=TANZANIA"
Tume ya kuchunguza matokeo mabaya ni ya nini?.

Baba kilaza watoto je??????
 
Back
Top Bottom