Mtahangaika sana wana CDM.Hivi suala la Mulugo kuhusu jina liliisha tolewa maelezo lakini kwa sababu yeye ameahidi kumg'oa Sugu jimbol a mbeya 2015 mmeanza kutapata.Mwacheni apige kazi.Mbona jina la Wegesa tumeisha sahau?Fanyeni kazi acheni majungu.
hakuna anayekosa maadui, hata wewe unaoEti ni janja ya maadui zake kisiasa, hivi nae ana maadui?? Kazi kweli kweli
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Nimepitia Wasifu wake kwenye tovuti ya Bunge, jamaa inaelekea yupo smart na anafahamu anachofanya! Sizani kama unaweza kum-sue kwa kosa la kufoji vyeti. Sana sana labda kama unaweza kum-sue kwa hilo la kurudia darasa la saba, jambo ambalo sizani kama lina uzito hasa ukizingatia watu wengi wa zamani hizo ndo zilikuwa design zao kv hawakuwa na mbadala....kwamba, mtu akifeli darasa la saba, njia pekee ilikuwa ni kurudia darasa with exception of fews ambao wangeweza kwenda private schools ambazo zilikuwa chache na hazithaminiwi.
Kughushi vyeti ni kosa la jina siyo kwa walimu tu, hata waandishi wa habari, aliongeza Bunyanzu.
Kwa upande wake, Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) halikuwa tayari kutoa matokeo ya mitihani ya Mulugo na badala yake msemaji wa baraza hilo John Nchimbi alisema matokeo hayo ni siri ya mtahiniwa na hawezi kupewa mtu mwingine.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi, Machi 25, 2013
Hii ni habari inayoambatana na anguko la elimu nchini mwetu
Hapa naomba na mimi niweke jambo, vijana wenzangu naona tumeingia kwenye mtego wa kulalamika kila siku juu na kuongozwa na watu/viongozi wasio na sifa. Napenda kuwakumbusha katika kuwa katika hili tunaopaswa kulaumiwa ni sisi wenyewe ambao tunajiona tunasifa za kuwa viongozi na kutoa meaningful contribution to our Nation ila tunajifungia makwetu au tunajifanya tunang'ang'ana na ajira na wakati wa uchaguzi au hatushiriki kwenye shughuli za siasa. Kwa kufanya hivyo tunawaachia watu wa design ya kina Mulugo na wengineo wenye sifa za kuungaunga na elimu za kuvundika kujipenyeza kwenye siasa as their fallback position na kutuongoza, wakati sisi wasomi tupo kwenye ajira zetu. Katika hili tukumbuke kuwa hata siasa ni ajira na tena ni high paying ajira kuliko hata huo uafisa uliong'ang'ana nao.Hii nchi yetu ni ya ajabu! Elimu ya watu wengi walio kwenye majukumu muhimu ya kuhakikisha ustawi na maendeleo ya nchi hii ni ya mashaka. Tusishangae kkuwa mambo hayaendi vyema, toka juu huo mti unateremka hivyo hivyo...vilaza ndio tumewapa majukumu. Ninadhani wanachofanya ni kutukomoa kwa kuwa tuliwaburuza shule, na hawataki kusikia ushauri hata kidogo.
Huu ni utani wakuu! kila taasisi za kiraia zisimame huyu afutwe kazi mara moja!
Katika hali ya mfumo wa Rais kuteua mawaziri kwa vigezo anavyojua yeye, sisi kama wananchi wa kawaida tunapaswa tu kujua hapo Mheshimwa Rais kuna fadhila anailipa kwa kumpa hiyo nafasi. Maana haingii akilini ni kwanini huyu bwana ha-step down au hasimiamishwi ili kupisha uchunguzi huru ufanyike kuhusu elimu yake. JK na Mulugo hawaoni ugumu uliopo katika kuupata ukweli iwapo Mulugo akiendelea kuwapo ofisini?? Je Mulugo haoni kama uwepo wake ofisin unawanyima nafasi watu walio chini ya ofisi yake hasa baraza la mitihani na wizara kwa ujumla kutoa ushirikiano wa kutosha katika kubaini ukweli. Yeye hatoona raha ukweli/utata juu ya elimu yake ukiwa cleared??Kwa nini mwajiri wa Mulugo ndio wababaishaji kuliko hata Mulugo mwenyewe! Kwa nini boss wake hatoi tamko juu ya hii sintofahamu??????
Au Mulugo ana akili sana - taifa litakosa mchango wake kwenye wizara hii nyeti ya Elimu hasa kipindi hii ambacho wanahitaji mtu mwenye uwezo kama Mulugo kuweza kuwaondoa kwenye kitanzi cha kufeli!!!!!!!!1 Wizara ya Elimu ni kitovu cha Uzembe.