Naibu Waziri Elimu katika kashfa vyeti

Naibu Waziri Elimu katika kashfa vyeti

Hii ni hatari sana kwa taifa, haina tofauti na form IV/VI Div 0 ndiyo anakwenda kusomea ualimu tena wa vodafasta nini kitatokea hapo. . . .
 
Kauli ya huyu mtu aliyejitambulisha kama mwalim wake alipokuwa mbeya sekondari inaendena kabisa na kauli ya jinambunge wa chadema joseph mbilinyi maarufu kama sugu kuwa dick mulugo lake alipokuwa sekondari hiyo ya mbeya alitumia jina la hamim augustino ..
 
Hivi hili lijitu inakuwaje linaachiwa achiwa tu.....hivi kweli sisi Watanzania wote tumekuwa Mipumbavu kiasi cha kuachia UOZO ulio wazi kama huu wa "Mulugo"............halafu anajigamba kuwa na "vyeti".......hivi watu wote wenye bongo zao wenye jukumu la kucheck hivyo vyeti........bado mmekaa kimya tu..........

Mpuuzi mwingine kutoka NECTA eti anasema matokeo ni siri ya mtahiniwa........shame on you.....hili lijitu limepewa Public Office.....kwa nini iwe siri.........hivi kwanini sisi wabongo tunaendekeza UPUUZI.......maneno meeengi.....kila kukicha......unasikia upuuzi tu.........can someone out there put STOP to these stupid things...........damn!
 
Hivi hili lijitu inakuwaje linaachiwa achiwa tu.....hivi kweli sisi Watanzania wote tumekuwa Mipumbavu kiasi cha kuachia UOZO ulio wazi kama huu wa "Mulugo"............halafu anajigamba kuwa na "vyeti".......hivi watu wote wenye bongo zao wenye jukumu la kucheck hivyo vyeti........bado mmekaa kimya tu..........

Mpuuzi mwingine kutoka NECTA eti anasema matokeo ni siri ya mtahiniwa........shame on you.....hili lijitu limepewa Public Office.....kwa nini iwe siri.........hivi kwanini sisi wabongo tunaendekeza UPUUZI.......maneno meeengi.....kila kukicha......unasikia upuuzi tu.........can someone out there put STOP to these stupid things...........damn!

thank you kwa kuonyesha uchungu mkubwa na mapenzi kwa nchi yako. yaani inashngaza mulugo anadai kuwa ili kuwaonyesha kuwa yeye ni mkweli eti amekuwa akiwaonyesha vyeti vyake jamani mtu kuwa na vyeti feki ni rahisi tu na kuonyesha vyeti sio kuthibitisha kuwa unayoyasema ni ya ukweli jamani hii ni ajabu na kweli
 
Naomba Nimfanyie Booking Waziri Muluo kwenye Serikali ya 2015 maana jamaa ana Roho ya Paka eti ukibisha anakuletea vyeti anatembea navyo kama silaha yake, jamaa alikuwa anapenda sana shule sema shule haikumpenda majina yanabadilika kama kinyonga, akitoka kwenye Wizara akatafute Cheti cha Hayati Rugakingira akapige dili la uwakili mahakamani.Huyu ni Assad wa Tz kwa 'misimamo'
 
001amulugo.jpg

Mmoja wa wakuregenzi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (jina tunalihifadhi) alisema: "Ili mwalimu wa sekondari awe headmaster (mkuu wa shule) ni lazima awe na shahada ya kwanza kutoka kwenye chuo kikuu kinachotambulika. Anatakiwa pia kuwa na uzoefu wa kazi wa miaka isiyopungua minane."

Kuhusu kughushi vyeti mkurugenzi huyo alisema, ikigundulika kuwa mwalimu ameghushi cheti anafukuzwa kazi mara moja, lakini alikiri kwamba katika shule binafsi inawezekana walimu wasio na sifa wakapenya, lakini wakaguzi wakibaini hutoa maelekezo wafukuzwe.

"Kwanza siku hizi ili mwalimu aajiriwe ni lazima akabidhi vyeti vyake wizarani na hupelekwa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) ili kuhakikiwa. Zamani ukaguzi haukuwa makini kwa hiyo inawezekana kuna watu wasio na sifa walipenya," alisema.

Kuhusu kurudia darasa la saba, alisema sheria haijawahi kuruhusu watu kurudia darasa la saba na kwamba wale waliorudia hutumia mbinu zao kufanya hivyo.

"Sheria haijawahi kuruhusu watu kurudia darasa la saba. Ni kweli wengi wamerudia sijui wanatumia mbinu gani, lakini hairuhusiwi. Ukishafanya mtihani wa darasa la saba mara moja ndiyo basi," alisema mkurugenzi huyo.

Mkurugenzi wizara ya elimu mwongo sheria iliruhusu kukariri darasa la 7 kwa jina na namba ile ile
Siku za nyuma ninavyofahamu sheria iliruhusu kurudia darasa la saba kwa jina na namba ile ile ya usajili. Watu walikuwa wanakwepa kufanya hivyo kwa sababu ya sheria ya kurudia darasa la saba ilitaka waliorudia katika matokeo ya mitihani yao ya kuhitimu punguzo la asilimia fulani kitu ambacho kilichangia wengi kuangukia pua maana akifaulu wastani sawa na asiyerudia darasa anaweza asichaguliwe kwa sababu atakapopata rungu la punguzo la asilimia hatafaulu, ndo maana walitumia janja ya kuridhi jina na namba ya wale ambao wameacha chule bila kuhitimu, na hivyo walimu kufanya janja ya kuingiza maendeleo ya wongo kwa kipindi ambacho aliyeacha hakuwepo shuleni.

Walimu wa shule za msingi wamekuwa na mazoea ya kutumia majina na namba za usajili za wanafunzi ambao ni non-attendance na hivyo kuwarithisha wale walioshindwa mitihani ya darasa la saba ambao wanaonyesha uwezo mzuri darasani. Jambo hilo limezoeleka pia katika baadhi ya shule za sekondari.

Kosa la wazi hapa kwa Waziri Mulugo ni kama ifuatavyo:
  1. Kurudia darasa la saba kwa kutumia jina la mtu mwingine katika usajili badala ya jina lake halisi kukwepa lungu la kupokonywa asilimia kadhaa za ufaulu kwa sababu ya kukariri darasa la kuhitimu shule ya msingi baada ya kushindwa mithani ya taifa kumaliza elimu ya msingi.
  2. Kughushe vyeti vya ualimu kwa ajili ya kutafuta ajira kinyume cha sheria
  3. Kuidanganya serikali katika ufaulu na vyeti faki wake kwa nafasi mbalimbali alizoshika kama ualimu, ubunge na uwaziri
  4. Kubadili majina kwa nafasi mbalimbali bila kufuata utaratibu wa kisheria na kabisa kuvunja sheria za wizara ya elimu na baraza la Mitihani Tanzania.
  5. Kuendelea kuidanganya serikali na wananchi kuhusiana na tuhuma hizo wakati kuna ushahidi wa wazi kutoka hata kwa watu waliosoma naye shule mmoja na walimu waliomfundisha.

Makosa haya ni mazito kwa kiongozi wa umma, kwa ajili ya kulinda heshima yake anatakiwa achukua hatua za makusudi za mara moja kujiuzuru:
  1. Uwaziri wa Elimu
  2. Ubunge
  3. Nafasi nyingine anazoshika kichama
Sababu nafasi zote amepata kupitia udangayifu huo.

Wizara ya utumishi ilaumiwe
Ajira huhakikiwa na wizara ya utumishi. Nafasi zote ambazo amezishika tukiondoa ile aliyokuwa anafanya kwa mwajiri binafsi wizara ilipaswa kuhakiki mwenyendo wa elimu, utumishi na vyeti alivyo navyo. Kama hilo halikuwa wazi kwa wizara ya utumishi, lakini kumekuwepo na malalamiko mengi hadharani na hata kwenye vyombo vya habari juu ya tuhuma hizo, jambo la kushangaza wizara ya utumishi imekuwa bubu hadi sasa gazeti la Mwananchi limeanika mambo hadharani.

Hii ni penati kick, kama ni kipa hodari kweli kudaka combola la penati ambalo mpiga mpira anaonekana kujaza misuli haswa anahitaji ziada ambayo ni sawa na ngamia kupenya tundu la sindano.

Athari za kutumia majina ya watu wengine na Vitambulisho vya Taifa
Zoezi la sasa la kupata vitambulisho vya taifa ambavyo huhitaji nakala za vyeti vya kuzaliwa vyenye kuonyesha jina halisi na wazazi itakuja kuwakumba vigogo wengi walio katika utumishi wa umma. Wengi wamepita kwa ujanja huo, sasa linapokuja suala la usajiri wa kupata kitambulisho cha kitaifa wanaweza kupenya kwa ujanja, lakini itakapofika wenye majina nao kutaka kujisajili ili kupata kitambulisho cha taifa ndipo sokomoko litakapowakumba baadhi ya watumishi wa umma.

CC;
alles, acheche, politiki, acheche, Kiranga, acheche, Mfamaj, kitalekwa, MpigaFilimbi, tetere,, Songoro, Ogah
 
No wonder watoto full division 0. Kikwete alimteuaje mtu kama huyu. Full forgery.
 
Sasa nimeamini ni kweli "Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zimbabwe".
Pia nitumie nafasi hii kumbumbusha bosi wa Mulugo Rais Kikwete. Mwezi uliyopita Mwakyembe aliwafukuza /kuwasimamisha kazi wafanyakazi 11 wa bandari ya Tanga kwa kosa la kufoji au kutumia vyeti visivyo vyao kupata hajira Bandari ya Tanga (Kama aliyofanya Bwana Mulugo kutumia cheti cha Dick Mulungu). Kosa hilo linafanana kabisa la Naibu waziri wako Philipo Mulugo ambaye pia anafahamika kwa majina mengine kama Hamimu Augustino/Philipo Hamimu/ Dick Augustino/ Mulugo EDM na pia kama Mulugo D.Philip. Usipomfukuza uyu kazi means wale wote waliofukuzwa huko nyuma kwa kuwa na vyeti bandia warudishwe kazini.

Nape na secretariat yako pia inawahusu: mkimwacha uyu mtu aendelee na ubunge na vyeo vingine vya CCM means mnabariki vyeti bandia. Hiki ni kipimo kizuri cha ccm. Wazee wa TISS pia hii ni haibu yenu, je uwa hampitii mafaili/profile ya wateuliwa wa rais kwa ngazi za juu kama hizi kabla hawajateuliwa?.
 
Nitumie nafasi hii kumbumbusha bosi wa Mulugo Rais Kikwete. Mwezi uliyopita Mwakyembe aliwafukuza /kuwasimamisha kazi wafanyakazi 11 wa bandari ya Tanga kwa kosa la kufoji au kutumia vyeti visivyo vyao kupata hajira Bandari ya Tanga (Kama aliyofanya Bwana Mulugo kutumia cheti cha Dick Mulungu). Kosa hilo linafanana kabisa la Naibu waziri wako Philipo Mulugo ambaye pia anafahamika kwa majina mengine kama Hamimu Augustino/ Hamimu Augustino/ Philipo Hamimu/ Dick Augustino/ Mulugo EDM na pia kama Mulugo D. Philip. Usipomfukuza uyu kazi means wale wote waliofukuzwa huko nyuma kwa kuwa na vyeti bandia warudishwe kazini.

Nape na secretariat yako pia inawahusu: mkimwacha uyu mtu aendelee na ubunge na vyeo vingine vya CCM means mnabariki vyeti bandia. Hiki ni kipimo kizuri cha ccm. Wazee wa TISS pia hii ni haibu yenu, je uwa hampitii mafaili/profile ya wateuliwa wa rais kwa ngazi za juu kama hizi kabla hawajateuliwa?.

Nakubaliana nawe kwa asili mia. Hoja ya kukariri darasa la saba siku za nyuma ilikuwaliwa kwa kutumia jina na namba ile ile, kosa kubadili jina. Angalia post yangu # 26 hapo juu. Thanks.
 
Eti ni janja ya maadui zake kisiasa, hivi nae ana maadui?? Kazi kweli kweli

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Chezea kusoma wewe kulivyo kugumu, sasa raha ni pale kilaza anapotaka aingie kundi la wasomi..... Shida tupuuuu•••••
 
Hastahili kuwa waziri huyu mtu kwanza hata upeo wake wa kufikiria ni mdogo baaaah.....tuliona hadi english yke!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mtahangaika sana wana CDM.Hivi suala la Mulugo kuhusu jina liliisha tolewa maelezo lakini kwa sababu yeye ameahidi kumg'oa Sugu jimbol a mbeya 2015 mmeanza kutapata.Mwacheni apige kazi.Mbona jina la Wegesa tumeisha sahau?Fanyeni kazi acheni majungu.
 
Wanabodi turejea kumbukumbu zetu hapa chini:

ARCHIVES/KUMBUKUMBU ZA JAMIIFORUMS 27/December/2012 source: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/374832-waziri-mulugo-aumbuliwa-na-sugu-7.html

icon1.png
Waziri Mulugo aumbuliwa na Sugu
na Asha Bani

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (CHADEMA), amemuumbua Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo, akidai hatishwi na kauli zake kwani ana elimu ya kuungaunga akiwa ametumia jina la mtu mwingine. Kauli ya Mbilinyi maarufu kama Sugu, inakuja siku chache tangu Mulugo atangaze kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kitayarejesha majimbo yaliyoko mikononi mwa CHADEMA mkoani Mbeya, likiwemo la Mbeya Mjini.

Akizungumza jana kwa simu na Tanzania Daima, Mbilinyi alisema anamshangaa Mulugo kwa kauli hiyo wakati akiwa na hali mbaya kisiasa jimboni kwake Songwe, kiasi cha walimu kulalamika kukosa hata chaki shuleni. "Mimi Mulugo hanitishi hata kidogo maana mambo yake yote ni ya kuungaunga, kuanzia elimu yake hadi siasa jimboni. Huyu nimesoma naye Sekondari ya Mbeya Day nikiwa namtangulia, na jina lake alikuwa akiitwa Amim si hili la Philip Mulugo," alisema.

Mbilinyi aliongeza kuwa amefanya ziara jimboni kwa Mulugo na kuelezwa matatizo mengi yanayowakabili wapiga kura wake, na kwamba alishangazwa na hatua ya kuona walimu wakilalamika kukosa chaki wakati mbunge wao ni naibu waziri wa elimu.
"Haya mambo hatuyasemi kwa sababu ya kuwachukia CCM, bali wanatuletea wenyewe malalamiko wakitaka tuwasaidie kusema. Sasa Mulugo kashindwa kwake anakuja Mbeya Mjini kujitapa kuwa wataning'oa," alisema.

Aliongeza kuwa, kutokana na ubabaishaji wa Mulugo, kuanzia sasa ataanza kumuita jina lake halali la Amim ili watu wafahamu kuwa hata kweli elimu aliunga licha ya kuteuliwa kuwa naibu waziri. "Kila mtu anakuwa na ndoto, haikataliwi, hata yeye alipotoka hadi kuwa Naibu Waziri wa Elimu ni ndoto pia, hakutegemea kutokana na kusoma kwa kuungaunga kwa kutumia jina na cheti cha mtu, hakuwa na uwezo," alisema.

Mbilinyi alifafanua kuwa Mulugo amemchokoza mwenyewe na kumtaka atambue kuwa yeye si wa kuchezea wala chama chake cha CHADEMA, na kwamba chama hicho chini yake au mtu mwingine kuliacha Jimbo la Mbeya Mjini ni baada ya miaka 25 ijayo. Alisema kutokana na kupendwa na watu na kuwapa changamoto katika halmashauri licha ya kwamba CCM wana madiwani 22 na CHADEMA 14, anaamini kabisa kwa sasa atajipanga kugombea umeya badala ya ubunge.

"Yaani Mulugo amechemsha, hakuna namna ya kumtoa Sugu wala chama chake, na sasa itafika wakati nitakuwa meya, tena pale ndio wamechemsha kabisa kumweka mwenyekiti asiyekubalika, na sasa wakifanya mikutano yao hawapati watu. "Mulugo ndiyo maana hata historia ya nchi haijui kwa kuwa elimu yake yenyewe ina utata, aanze kuchunguzwa, mtaniambia kafanya jambo la ajabu sana, mwenzake alifaulu, lakini kutokana na kutokuwa na uwezo wa kuendelea na shule yeye akanunua jina lake," alisema.
Mbilinyi alisema kama Mulugo anahitaji kuendelea na siasa, basi aende Mbeya Mjini ili wamfundishe jinsi ya kuishi na watu jimboni kwake na kujua kero zao.

Hata hivyo, Mulugo alipotafutwa kufafanua madai hayo, alikwepa kulisemea sakata la kutumia jina lingine wakati akisoma sekondari, akisema kuna vitu ni stori, lakini fitina hizo za kisiasa ni majungu ya mtu na mtu. Aliongeza kuwa, Mbilinyi aliwahi kwenda jimboni kwake Songwe na kusema madai hayo pamoja na kumtukana, lakini wananchi walimzomea wakisema wao ndio wanamfahamu mbunge wao kuanzia elimu ya msingi mpaka shahada.

"Matusi yale yalisababisha vurugu mpaka CHADEMA wakapata kura 19 dhidi ya kura 365 za CCM. Nilichokisema kwenye mkutano wa Mbeya ni jambo la kawaida kwa mwanasiasa yeyote aliye makini, tena mjumbe wa NEC. "Nilisema majimbo yote ya CHADEMA Mkoa wa Mbeya tutayarudisha. Sasa kwani mbona wao kila siku wanasema watachukua majimbo yote ya Mkoa wa Mbeya?" alisema Mulugo kupitia ujumbe mfupi wa sms.

Hizi tuhuma dhini ya Mh. Mulugo zinaonekana kuna ka-ukweli ndani yake, yaani watu wote wamsingizie, Mh. Mulugo hebu jitokeze utueleze ukweli maana katika 'public office' vyeti vyako vyote umma unastahili kupata ukweli hutakiwi kujitetea ktk 'vikao vya ndani' au 'kupitia wizara elimu ambapo pia wewe ni boss', jitokeze Mheshimiwa uueleze umma kuhusu mtiririko wa vyeti vyako.
 
Jamani kwani Southern Highlands sasa nayo ni shule ya kutoa elimu kwa watoto?
 
Wadau tujaribu ku Google hayo majina ya Mulugo yamkini tutabaini kitu hapo.
 
KHAAA....Kwa mtaji huu kwa nini watoto wetu wasifaulu kwa kiwango cha negative 60%!!! Nashauri hiyo Tume iliyoundwa kuchunguza sababu za ufaulu wa negative 60% ianzie kwa huyo MLUGO...MLUGU...MLUNGU...eehe..nani tena vile.. maana ana majina mengi!
 
Halafu inaundwa tume ya kuchunguza mass failure F4 huku NaibuWaziri ni kihiyo.
 
Back
Top Bottom