Nahodha - Marufuku majeshi yetu kuajiri raia

Nahodha - Marufuku majeshi yetu kuajiri raia

Huyu Mzanzibari atueleze ni waru wa aina gani wanjiunga na mafunzo ya kujitolea ya JKT na wanapatikana vipi?.. Wengi wa vijana waliokimbilia JKT kwa sasa ukitoa wale wa kwa mujibu wa sharia ni form failures...sasa jeshi na polisi waingie failrues tu?
 
Samahani wote, hivi kujiunga na jeshi ni umri wa miaka mingapi? Nataka kujiunga ila nashaka na umri.
 
Huyu Mzanzibari atueleze ni waru wa aina gani wanjiunga na mafunzo ya kujitolea ya JKT na wanapatikana vipi?.. Wengi wa vijana waliokimbilia JKT kwa sasa ukitoa wale wa kwa mujibu wa sharia ni form failures...sasa jeshi na polisi waingie failrues tu?

Kwani kuna mtu alishajiunga na JkT mwenye div.1????
 
Huu ni utaratibu mzuri na ni maono yanayohitaji pongezi.

Kama ilivyokuwa kipindi cha utawala wa Mwl. Nyerere ambapo ilikuwa lazima upitie JKT kujiunga na masomo ya juu.

Kwa maana nyingine, wale wanaotegemea kupata ajira kwenye majeshi katika maeneo yanayohitaji technical skills lazima kwanza wakapige kwata.
 
kabwebwe acheni,njooni mpewe ukakamavu na uzalendo wa nchi yetu.Wenzetu wa ujamaa jeshi ni lazima.
eg Park wa arsenal anatakiwa akatumikie jeshi la kwao ndio aludi kazini pale emirate stadium
 
Mchungaji Msigwa alikuwa sahihi aliposema akili ndogo kuongoza akili kubwa.
Ajira za raia katika sekta za jeshi haziepukiki kwa sabaubu wanajeshi kazi yao ni ile waliyochukulia mafunzo. Papo hapo jeshi linahitaji makarani, wataaalamu mbalimbali katika fani ambazo si zautendaji wa kijeshi bali wa kiofi na utal;amu mwingine katika ofisi za jeshi. Hilo lipo po pote vinginevyo huyu waziri ni mzuzu anayeongea kisiasa zaidi. Ukichukulia jambo lenyewe lilivyo haliepukiki.

Wenzetu utaona jeshi la polisi ofisi za record, na shughuli nyingine wamejaa raia wa kawaida ambao wamesomea mambo ya uhaziri na sheria. Polis ni kwenye majukumu yao huko.

Tuache siasa, tuje kwenye hali halisi ya maisha na utendaji.

yule mchunga ngurue alionyoa kiduku ndio alisema hivo
 
Lugha iliyotumika ina kejeli raia, "raia marufuku..." kama vile raia wamekosea kitu fulani. Hakuna vita, jeshi halina kazi, ndo maana lina luxury ya ku cherry pick waajiriwa.

Pia Waziri anapata wapi madaraka ya kuamua nani anaajiriwa wapi? Katiba na sheria zetu mbovu, lazima tuogope kuwapa watu madaraka kama haya. Kesho kutwa atakuja dikteta na utaratibu wa "kuanzia leo jeshini marufuku kuajiri mtu zaidi ya wanaume wakurya wenye misuli ya shingo." Such arbitrary powers.

Wanajeshi wa Tanzani hawapigani vita, rahi ndio maana waziri anaweza kutumia lugha za
 
upuuzi tu!hivi mimi nikija na utaalamu wangu wa kipekee utanitaka niende JKT kupoteza muda ndio uniajiri?
hizi ni mbwembwe tu zilizokosa mashiko.....sijui tunataka kuachieve nini?wenzetu wanaimarisha weledi wa kijeshi sisi tunaongeza miguvu isiyokuwa na tija.

Naunga mkono hoja hii hapa nahodha kama kawaida yake amekurupuka kutafuta umaarufu wa kisiasa mara zote husema bila kuwaza, Jeshi letu linahitaji utaalamu sio maguvu, kama tunahitaji askari wa miguu wa mstari wa mbele sawa, lakini kapa tunahitaji utaalamu ndani ya jeshi, basi majeshi yetu pamoja na polisi waajiri kutoka kwenye soko kulingana na na utaalamu uhaohitajika, si wanafanyiwa vetting kabla ya kuajiriwa sasa wasi wasi wake nini, au ndio kuingiza siasa katika majeshi, basi anaonaje turejeshe makamisaa jeshini, kuzaa second version ya akina JK, Kinana, Ngwilizi, Nnauye, na wenzao.

Usiwe mvivu wa kufikiri Nahodha, najua unataka uwe kwenye chati kama akina Mwakyembe na Mangufuli, fanya kazi sio maneno yatakuweka katika chati, nakutabiria uhamisho mwengine JK akipangua baraza la mawaziri huna uliwezalo, sasa ndio inaonyesha wazi Karume alikuwa akikubeba tu, na Dr. Shein hakukosea kukutupa nje ni mzigo tu ndani ya serikali.

Zama za siasa za fitna zimepitwa nawakati sasa ni jinsi utakavyo perform sio kuleta chuki za kisiasa, majeshi yetu yanahitaji utaalamu wa aina mbali mbali sio kufunga na kufungua tuu, unafahamu nini wewe kuhusu jeshi hujawahi kuwa hata mgambo au valantia kule kwenu, na kama unazungumzia uzalendo ulikushinda TVZ ukaenda Arusha kufanyakazi na peace corps, so shut up.
 
upuuzi tu!hivi mimi nikija na utaalamu wangu wa kipekee utanitaka niende JKT kupoteza muda ndio uniajiri?
hizi ni mbwembwe tu zilizokosa mashiko.....sijui tunataka kuachieve nini?wenzetu wanaimarisha weledi wa kijeshi sisi tunaongeza miguvu isiyokuwa na tija.

Wenzenu kina nani? Utaalamu wako hauhitajiki jeshini. Watanzania hakika yatupasa tupigane na common enermy, ARROGANCE!
 
Ata USA ambapo wametuzidi kwa mengi raia wamejaa kibaondani ya majeshi yao!why viongozi wetu ni waropokaji hivi?
 
Wewe na UTAALAMU wako kaa nao chumbani kwako ujiajiri ila ukitaka ajira serikalini lazima upitie JKT hii ni nzuri sana
 
Back
Top Bottom