- Thread starter
- #61
Nashukuru ndugu ila naona kama jamii imenitenga ninapofanyia kazi imenitenga hata zuri linageuzwa kuwa baya,sina tena ujasiri wa kuthubutu kama ilivyokuwa awali ndg
Endelea katika njia njema bro wangu. Wakati upo katika shida ndipo Mungu yupo nawe karibu. Usipoteze matumaini wala usirudi tena kwa waganga unapoteza tu fedha na zaidi ni kama unakataa kuwa Mungu hawezi kukusaidia.
Nakuombea pia huku nilipo. Shetani hana mamlaka na roho yako. Ataathiri mwili tu kupitia hayo majaribu ila zaidi ya hapo hana la zaidi. Jichanganye na watu na ikibidi kuwa karibu na mkeo kwani kumrudisha kwao kutakuongezea madhara ya upweke. Na zaidi mliapa kuwa wote katika shida na raha hapo ndipo utaujua upendo wake.
Usipoteze matumaini, amini kuwa una nguvu kuliko yote unayopitia. Sali sana nguvu ya kushinda hiyo hali ipo ndani yako na si kwa waganga wala kwa wachungaji japo ni vizuri kujadiliana na wachungaji wako, kumbuka maneno ya Yesu kama (wewe ni Mkristu) kuwa "imani yako imekuponya". Usiache kuamini nguvu za Mungu.
Sent using Jamii Forums mobile app