Nahitaji kupata Majarida ya "Sani"

Nahitaji kupata Majarida ya "Sani"

Nico ye Mbajo ni Muasisi mwenza wa gazeti la Sani - Yeye na rafikiye Said M. M. Bawji Walianzisha Gazetila Sani lililokuwa maarufu tokea Miaka hiyo ya 1980
. Sani ni muunganiko wa silabi za mwanzo za majina yao - 'SA' kutoka kwenye Said na 'NI' kutoka kwenye Nicco. Ndiye aliyewabuni wahusika wakongwei wa gazeti la Sani: Kipepe, Ndumilakuwili...huyu ni mkongwe asiyevuma lakini mwenye mchango mkubwa sana kwenye fasihi simulizi kupitia utunzi, uandishi na uchoraji. Inasemekana baada ya kutofautiana na Bawji ndiyo alianzisha jarida lake la 'Mcheshi'.

Kumbuka kuwa Miaka ile Ya Nyuma Majarida Vitabu na Michezo ya Redio ilitumika sana kuelimisha Jamii yetu ...Burudani ilikua kubwa sana kupitia Fasihi Andishi



Nico mwenyewe huyo hapo chini.

Chanzo: fesibuku

IMG_20200901_194857.jpg
 
Nico ye Mbajo ni Muasisi mwenza wa gazeti la Sani - Yeye na rafikiye Said M. M. Bawji Walianzisha Gazetila Sani lililokuwa maarufu tokea Miaka hiyo ya 1980
. Sani ni muunganiko wa silabi za mwanzo za majina yao - 'SA' kutoka kwenye Said na 'NI' kutoka kwenye Nicco. Ndiye aliyewabuni wahusika wakongwei wa gazeti la Sani: Kipepe, Ndumilakuwili...huyu ni mkongwe asiyevuma lakini mwenye mchango mkubwa sana kwenye fasihi simulizi kupitia utunzi, uandishi na uchoraji. Inasemekana baada ya kutofautiana na Bawji ndiyo alianzisha jarida lake la 'Mcheshi'.

Kumbuka kuwa Miaka ile Ya Nyuma Majarida Vitabu na Michezo ya Redio ilitumika sana kuelimisha Jamii yetu ...Burudani ilikua kubwa sana kupitia Fasihi Andishi



Nico mwenyewe huyo hapo chini.

Chanzo: fesibuku

View attachment 1555689
Mkuu. Asante sana kwa maelezo haya, nadhani wengi wetu tulikuwa hatufahamu chanzo/mwanzo wa jarida hili! Asante sana
 
Hahahaha kuna wale mabush star wanaonekana watu wa mikoani wale sio dar madenge kipepe Mzee meko bob mazishi ndumilakuwili sokomoko lodi lofa pimbi betina Zena wengine nimewasahau lakin hao walikuwa mastaa kinoma na kuna hadithi zao zina maneno ukisoma inakuwa kama unaangalia video za ngono unakuwa umetulia enzi hizo movie za Kiswahili ni hizo na kibisa yaan makundi ya Ngoma kama muungano Mandela ddc kibisa tot n.k ilikuwa raha sana Kwa kweli kipindi kwenda majumba ya sinema ujipange Kwanza ujipange
Tena hukoooo Dar!
 
Hapa sasa naona tunaanza kuongea lugha moja! mkuu tunapataje hayo mambo. hahahahahaha
Mi nipo Mwanza, ila haya magazeti yapo Nyumbani Chunya. Bwana mdogo nimemuomba anipigie picha na kunitumia. Nakumbuka, hilo gazeti la TABASAMU ninalo kuanzia toleo namba 1 mpaka la mwisho. Bongo kuanzia namba 5. Ambha ninalo namba 1 mpaka la mwisho. Sani sina uhakika kuanzia namba ngapi!
Kuna sehemu nimeyahifadhi. Bado mapyaaa!
 
Mi nipo Mwanza, ila haya magazeti yapo Nyumbani Chunya. Bwana mdogo nimemuomba anipigie picha na kunitumia. Nakumbuka, hilo gazeti la TABASAMU ninalo kuanzia toleo namba 1 mpaka la mwisho. Bongo kuanzia namba 5. Ambha ninalo namba 1 mpaka la mwisho. Sani sina uhakika kuanzia namba ngapi!
Kuna sehemu nimeyahifadhi. Bado mapyaaa!
Safi sana! hiyo imekaa vizuri! hayo ni kuyazalisha tu. hakuna namna
 
Kaduma alipokufa au kufariki kila kitu kilipotea Sani
Mchoraji wa kwanza alikuwa Nico Ye Mbajo (kama ilivyoelezwa hapo juu kuwa alikuwa mmiliki mwenza) pia alikuwepo kiboko ya wachoraji wakati huo, akiitwa PHILIPO NDUNGURU.
 
Mimi ninalo langu la mwaka 1979 nikupateje mchoraji alikuwa marehemu Philip Ndunguru nikupateje? Na mtunzi wa Sokomoko Ted Marreale.Hebu mtafute Ted Mareale atatusaidia.Enzi hizo kulikuwa na hadithi ya USIKU WA BALAA na USO WA MAUTI namkumbuka mzee OLE
 
Mi nipo Mwanza, ila haya magazeti yapo Nyumbani Chunya. Bwana mdogo nimemuomba anipigie picha na kunitumia. Nakumbuka, hilo gazeti la TABASAMU ninalo kuanzia toleo namba 1 mpaka la mwisho. Bongo kuanzia namba 5. Ambha ninalo namba 1 mpaka la mwisho. Sani sina uhakika kuanzia namba ngapi!
Kuna sehemu nimeyahifadhi. Bado mapyaaa!
Yaani haya magazeti nilyapenda sana plz tunaomba ukiyapata utujulishe hata kwa.malipo tutanunua ili tutoe copy kwa ajiri ya kujisomea wengine digital world imekaa pembeni
 
Nico ndo muanzilishi wa lile gazeti... enzi izo said anafanya kaz benk tanga... alipoielewa ile idea akamshawishi nico waiprint kwa ushirikiano(niko awe anasanifu, said awe anatoa pesa)... jina wakaita sani (SAid na NIco) baadae biashara ilivokua said akamdhulumu nico kwa kuwa jamaa wa watu hana tamaa akamuacha tu.... uaminifu kupita kias na kutojali kulimponza nico.... alilipwa mia4 tu ya kipindi icho tena kama msaada sio malipo ya mgao... so sad
😔
 
Nico ye Mbajo ni Muasisi mwenza wa gazeti la Sani - Yeye na rafikiye Said M. M. Bawji Walianzisha Gazetila Sani lililokuwa maarufu tokea Miaka hiyo ya 1980
. Sani ni muunganiko wa silabi za mwanzo za majina yao - 'SA' kutoka kwenye Said na 'NI' kutoka kwenye Nicco. Ndiye aliyewabuni wahusika wakongwei wa gazeti la Sani: Kipepe, Ndumilakuwili...huyu ni mkongwe asiyevuma lakini mwenye mchango mkubwa sana kwenye fasihi simulizi kupitia utunzi, uandishi na uchoraji. Inasemekana baada ya kutofautiana na Bawji ndiyo alianzisha jarida lake la 'Mcheshi'.

Kumbuka kuwa Miaka ile Ya Nyuma Majarida Vitabu na Michezo ya Redio ilitumika sana kuelimisha Jamii yetu ...Burudani ilikua kubwa sana kupitia Fasihi Andishi



Nico mwenyewe huyo hapo chini.

Chanzo: fesibuku

View attachment 1555689
rekebisho kidogo wahusika kipepe na ndumilakuwili ni wa marehemu Philip Nduguru
 
Back
Top Bottom