Nahitaji Faraja Moyo wangu Unateketea.

Nahitaji Faraja Moyo wangu Unateketea.

Kiukweli kwanza kabisa wewe ni bwege,tens bwege mtozeni.
Pili wewe hujitambui,
Tatu hujithamini,
Nne hujipendi na mwisho
Tano hujiheshimu.
sijawahi sikia mwanaume aise na akili timamu kama wewe. Endelea kulia kaka utatengeneza bahari yako ya machozi siku moja,kila la kheri.
Hata mimi sijawahi ona mwanume weak kiasi hiki. Labda kipindi cha shule tena o level

Hata kwenye maisha ya kawaida bado napata ukakasi kama atayamudu vilivyo
 
Pole bro.
Hayo ndiyo maisha ya wanawake na wanaume wote waliomo humu duniani.
Kama huna pesa, jiandae kwa masimangano na dharau hata kama ni mkeo na umezaa nae.
Nachokuusia
Achana na matamanio yasiyo ndani ya uwezo wako. Mwambie Mungu akusaidie kukuepusha na changamoto ya huyo mwanamke. Fanya Ibada iwe faraja kwako. Utapata uhuru wa kufikiri kuhusu maisha yako na muda ukifika Mungu atakupa wa aina yako.
Usidanganywe na rangi ya chai, utamu ni wa sukari. Vipo vingi vilivyo vizuri lkn ndani vimeoza bro!!!!! .
 
Napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wale wote ambao watashiriki kwa namna fulani ama nyingine kunisaidia ili niwe sawa kiakili na kimawazo nahisi huwenda nikiendelea hivi nitaingia kwenye matatizo hasa ya Kiafya.

Miaka ya nyuma kidogo nimekuwa ndani ya mahusiano na binti mmoja ambaye ametumia nafasi hiyo kuniumiza kila leo kwa kuniponda sana moyo wangu, Siwezi kumaliza wiki moja kabla sijaumizwa na makosa ambayo ninaona anafanya makusudi kwangu ili tu niumie na kila siku amekuwa mtu wa kushuhudia natokwa na machozi kwa ajili yake ila anatumia mwanya huo kuniponda kila leo, Nimejaribu kumweka sawa japo bado nipo kwenye utafutaji najua kesho na keshokutwa Mungu atanifungulia milango ya ajira ili niweze kuishi nae kama mke wangu ila pia hali yangu inachangia sana anione kama siwezi kupata ajira daima ila naamini katika Mungu yote yanawezakana.

Nimekuwa najitolea sehemu mbalimbali ila hata pale napopata kidogo najitahidi sana hata nusu apate yeye na nusu nipate mimi, ili tu ajue kwa namna gani ninahangaika kupata kazi ili baadae tuishi wote lakini juhudi zangu anaziona hazina maana kwake, Hivi karibuni nilipanga kwenda kumtembelea nilitamani sana ningepata walau chochote nipeleke kama zawadi lakini hali yangu ilikuwa mbaya sana na kushindwa kupata zawadi yoyote kwake, lakini aliniambia kama ungekuwa na pesa ningependa sana uniletee pete ya uchumba nikamwambia kama Mungu akipenda ajira nikapata basi yote yatawezekana kwa jina lake. Yote haya yanakuja kwa sababu baadhi ya marafiki zake wameolewa na wengine wamevishwa pete hivyo kwa hali yangu huwenda anaona kama ninamchelewesha sana, Ana tabia za kufuata na kutaka awe kama wao ila hali yangu haijakaa sawa mimi kuweza kumudu kile ambacho anakitaka.

Nimeshuhudia Sms kwenye simu yake akiwa anachat na wanaume na kuwaomba pesa kwakweli inaniuma sina la kufanya ila najua penzi langu halipo kwenye taswira nzuri hata kama ni uaminifu nimeanza kumshusha sana kutokana na yale ninayoyaona, najitahidi sana ila anaona juhudi zangu zote ni kupoteza muda. Kuna wakati inafikia hadi namdanganya kuwa mwezi ujao nitaajiriwa anafurahi wana na kuwa karibu namimi ila mwezi ukiisha ukaribu wake na mimi hupotea. Na sikupenda siku moja nipate ajira kisha niachane nae nahisi atanihisi vibaya na kuona kama nimemsaliti baada ya kupata ajira.

Usiku mwili wangu iligeuka kuwa tanuru la moto nimechomwa sana rohoni kwa sms nilizoona wakichat na Mtu nilikuwa naona kifo na macho ila najua ombi langu Mungu atalisikia, japo kazoea kila siku namwambia nitapata kazi ila najua muda si mrefu nitapata kazi hata kama ni kuzibua chemba ili tu nisije kudharaulika kwake.

Nahitaji sana faraja kwa kipindi hiki jamani hali yangu japo iko vibaya ila hili linanitia sana simanzi, nadharauliwa sana.

Mungu Simama nami.
Kwanza, kwahiyo sisi wazibue chemba umetudharau,kuwa upate kazi hata ya kuzibua chemba.
Pili; kaza moyo Mkuu wanaume hatuwi weak hivyo,najua kuna kupenda lakini fikiria kwani kabla ya kumjua uliishi vp? Wengi tumepita huko kutoa chozi lakin unapiga moyo konde unaaga,na usigeuke nyuma,mapenzi ni kuheshimiana,afu umependa usipopendwa
Take next step in Jesus name am sure you will win the battle.
 
Pole bro.
Hayo ndiyo maisha ya wanawake na wanaume wote waliomo humu duniani.
Kama huna pesa, jiandae kwa masimangano na dharau hata kama ni mkeo na umezaa nae.
Nachokuusia
Achana na matamanio yasiyo ndani ya uwezo wako. Mwambie Mungu akusaidie kukuepusha na changamoto ya huyo mwanamke. Fanya Ibada iwe faraja kwako. Utapata uhuru wa kufikiri kuhusu maisha yako na muda ukifika Mungu atakupa wa aina yako.
Usidanganywe na rangi ya chai, utamu ni wa sukari. Vipo vingi vilivyo vizuri lkn ndani vimeoza bro!!!!! .
Ni kwel kk umempa ushaur mzur xana
 
Sasa ndugu yangu huoni hilo tanuru la moto wewe ndo unalikumbatia?
 
Huwa naona ni vigumu kufanya maamuzi hayo kwake maana hata kama nikiyafanya hawezi hata kuumia hata robo ya maumivu yangu, ninahisi kama nitajitesa sana kuliko sasa.
Upo weak sana ndugu yangu na kama utaendelea hivi utasumbuliwa sana.
 
Ukiona mwanaume mwaminifu sanaaa ujue hana hela, mapenzi ya siku hizi mwanaume lazima uwe na hela ndiyo kilainishi na kitendea kazi ktk mapenzi,kinafanya mapenzi yateremke tu bila ukakasi,achana na mapenzi kwanza tafuta hela kwanza, kuwa mwanaume sio kazi ya kitoto
Naomba hela eh
 
Material girl hivi vijana wa siku hizi mmerogwa na nani yani kujua tu huyo ana tamaa na mpenda pesa kazi?
 
Sasa hao wanaompa pesa unafikiri wanampa bure? Simama kama mwanaume, jipange na tafuta mtu wa kupanga naye maisha lakini sio huyo ulo naye, kwa akika hamtafika mbali.
 
Pole sana kijana ILA hapo una ajira mbili. Chamsingi chagua moja kwanza. Chagua maisha wanawake wapo wengi na hawatoisha. Jenga maisha yako na kama hapo ulipo ni pagumu hama nenda kajaribu kwingine mkoani. Tafuta MTU ambaye atakuamini akupe mtaji mfanye biashara pamoja na usipende kulia lia kuhusu wanawake. Kuna watu wana mitaji ILA hawana watu wakusaidiana nao. Hakikisha umekua stable kwenye maisha ndo uangalie wanawake poti. Mwache ahangaike na wanaume we hangaika na kazi.

Ni hayo tu
 
Ndugu samahani, usinielewe vibaya, HUYO SI MKE mke anapaswa awe tayari kuishi na wewe kwa hali yoyote, furaha au huzuni mshikamane, sasa huyo anayekuponda kisa huna kazi hujui hakufai? Leo ukiajiriwa atakupenda na utaishi kwa amani ,je siku umepoteza ghafla ajira si naye atakukimbia, chukua hatua HERI KUVUNJA UCHUMBA KULIKO KUVUNJA NDOA. Tafuta mwanamke mwingine wapo ambao wanahitaji mme na si wanaohitaji ajira yako kama huyo.
 
Natamani iwe hivyo ila...
Ama kweli kuoenda ni upofu!!!
Na vipi mambo yakiharibika baadae tena mkiwa ndoani!!!! Maana ashakuonyesha yeye ni wa jinsi gani wakati ambapo hauna kitu.

Au huyu binti hana tatizo ila wewe ndio unajistukia kwakuwa hauna kitu????!!!!!!
 
NB : na hao wachache Mungu hua anawaangalia na kuwabariki
Yesu Kristo alizaliwa kwenye zizi la mbuzi sehem chafu chafu mbaya mbaya sehemu isiyo kua na kiyoyozi wala kitanda lakini pale Mungu alipaona hapa ndipo atazaliwa mwanae mpendwa mfalme wa wafalme duniani
NB: Adamu aliumbiwa kila kitu ndio akaumbiwa Hawa. Hope unaelewa ina maana gani hiyo
 
Ukiwa na mahusiano na mwanadada hlf analazimisha umuoe unatakiwa kuwa makini nae sana
 
Napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wale wote ambao watashiriki kwa namna fulani ama nyingine kunisaidia ili niwe sawa kiakili na kimawazo nahisi huwenda nikiendelea hivi nitaingia kwenye matatizo hasa ya Kiafya.

Miaka ya nyuma kidogo nimekuwa ndani ya mahusiano na binti mmoja ambaye ametumia nafasi hiyo kuniumiza kila leo kwa kuniponda sana moyo wangu, Siwezi kumaliza wiki moja kabla sijaumizwa na makosa ambayo ninaona anafanya makusudi kwangu ili tu niumie na kila siku amekuwa mtu wa kushuhudia natokwa na machozi kwa ajili yake ila anatumia mwanya huo kuniponda kila leo, Nimejaribu kumweka sawa japo bado nipo kwenye utafutaji najua kesho na keshokutwa Mungu atanifungulia milango ya ajira ili niweze kuishi nae kama mke wangu ila pia hali yangu inachangia sana anione kama siwezi kupata ajira daima ila naamini katika Mungu yote yanawezakana.

Nimekuwa najitolea sehemu mbalimbali ila hata pale napopata kidogo najitahidi sana hata nusu apate yeye na nusu nipate mimi, ili tu ajue kwa namna gani ninahangaika kupata kazi ili baadae tuishi wote lakini juhudi zangu anaziona hazina maana kwake, Hivi karibuni nilipanga kwenda kumtembelea nilitamani sana ningepata walau chochote nipeleke kama zawadi lakini hali yangu ilikuwa mbaya sana na kushindwa kupata zawadi yoyote kwake, lakini aliniambia kama ungekuwa na pesa ningependa sana uniletee pete ya uchumba nikamwambia kama Mungu akipenda ajira nikapata basi yote yatawezekana kwa jina lake. Yote haya yanakuja kwa sababu baadhi ya marafiki zake wameolewa na wengine wamevishwa pete hivyo kwa hali yangu huwenda anaona kama ninamchelewesha sana, Ana tabia za kufuata na kutaka awe kama wao ila hali yangu haijakaa sawa mimi kuweza kumudu kile ambacho anakitaka.

Nimeshuhudia Sms kwenye simu yake akiwa anachat na wanaume na kuwaomba pesa kwakweli inaniuma sina la kufanya ila najua penzi langu halipo kwenye taswira nzuri hata kama ni uaminifu nimeanza kumshusha sana kutokana na yale ninayoyaona, najitahidi sana ila anaona juhudi zangu zote ni kupoteza muda. Kuna wakati inafikia hadi namdanganya kuwa mwezi ujao nitaajiriwa anafurahi wana na kuwa karibu namimi ila mwezi ukiisha ukaribu wake na mimi hupotea. Na sikupenda siku moja nipate ajira kisha niachane nae nahisi atanihisi vibaya na kuona kama nimemsaliti baada ya kupata ajira.

Usiku mwili wangu iligeuka kuwa tanuru la moto nimechomwa sana rohoni kwa sms nilizoona wakichat na Mtu nilikuwa naona kifo na macho ila najua ombi langu Mungu atalisikia, japo kazoea kila siku namwambia nitapata kazi ila najua muda si mrefu nitapata kazi hata kama ni kuzibua chemba ili tu nisije kudharaulika kwake.

Nahitaji sana faraja kwa kipindi hiki jamani hali yangu japo iko vibaya ila hili linanitia sana simanzi, nadharauliwa sana.

Mungu Simama nami.
Kwanza usimuhusishe MUNGU maana huo ni uchumba wa zinaa,
Lkn pole sana sana sana,
Ktk mahusiano makosa ni sehemu ya kuendelea mbele na kujitengeneza,
Lkn makosa ya makusudi ni ishara ya taabu utazopata milele ukiendelea kuwa nae,hyo ni alarm,
Bila kuzunguka zunguka nakusihi achana nae haraka sana hiyo ni sumu unakunywa,mtu siyo mke unahangaika nae wa nini,ukilazimisha itakuumiza sana siku ukimuoa,hebu kaa pembeni kidogo muachie nafasi ya yy kuhanhaikia tamaa zake, wewe hangaikia uchumi na maisha yako ya kiroho,
Usiwe na mahusiano na mwanamke mshari na mwenye makusudi,
 
Mhhh pole but hakuna mahusiano yaliyo fanikiwa bila kupitia ups and downs ni swala la mda tu ajira zipo mda ukifika utaajiriwa kikubwa mvumilie tu mwoneshe upendo wa kweli mjali Mambo yataenda vzuri tu..... Happy nyu year in advance
Makusudi unaiitaje ups an downs,
Visa vya makusudi lengo ni kukuumiza,mke ni msaidizi,Huyo anamsaidia kuumia badala ya kutulia,
 
Pole sana...
Kuna msemo unasema, "To every successful man there is a strong women behind"...

Huyo siyo strong woman, she will never motivate you to success sana sana, ukishapata hiyo kazi atakuburuza, kuku-demand na hata kuku-comand kwa kivuli cha amekuvumilia wakati wa shida zako, kumbe siyo kweli...

Follow your heart but carry your brain with you...


Cc: mahondaw
 
Itakuwa ngumu kwako kupata kazi maana unastress sana and believe me fanya maamuzi magumu usimfuatilie kwa lolote focus kwenye namna ya kujikwamua na hali yako kiuchumi... bila hivyo miaka itakatika utashangaa na roho yako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom