Nahitaji Faraja Moyo wangu Unateketea.

Nahitaji Faraja Moyo wangu Unateketea.

Kuna wanawake ambao ndoa haitawahusu hata vitabu vya dini vimesema ukute na ye ni mmoja wapo
 
Pole sana mkuu, sijui unataka dalili gani nyingine ya kukuonyesha kuwa hapo ulipo sipo!!!
Mapenzi ya dhati ukiwa hauna kitu yamebakia kuwa historia tu, and hope unalielewa hilo.

Hivi mtu alokunyanyasa kiasi hicho bado unafikiria kumvisha pete!! Okey unataka umuoe wakati hauna kitu ili ugundue nini kipya? Utaweza kuyavumilia masimango yake mkiwa tayari ndoani?
Huyo ana shida na "harusi" sio ndoa, mwenye utayari na ndoa hawi hivyo ulivyo mdescribe.

NB: kudate na mwanaume asie na kitu ni kipaji, na wamejaaliwa wachache sio wote.
Duh! Mkuu kama wewe ni mwanamke nimekupenda bure.
 
Kama unakuwa muoga wa kufanya maamuzi aisee wanawake watakusumbua sana. Anyway komaa nae huenda akabadilika, lakini ningelikuwa mimi hata namba yaake nigelikuwa nimeshafuta.[/QUOTE

Mkuu, tatizo ni kuifuta kwenye phoebook alafu ikabaki kichwani.
 
Ajira ziko nyingi na vyepesi mno kupata ila watu wanataka ajira za heshima kubwa


Tafuta vibarua mbona vingi sana tu

Mwanaume anayeogopa kuchekwa hafai wala hastahili ni bora kabisa kabisa akawa aka
 
Maswahibu yanatukuta wengi Kwa namna tofauti.Nilivyoshinda na kuimaliza siku ya Jana Mungu anajua. Pole Mkuu,relax kama mie na usimweke kipaombele huyo binti.Hawa watu ni hatari.
Wenye maumivu ya namna hiyo tupo wengi.
Mimi nimetemana na mchumba wangu ambae tumekaa kwenye mahusiano almost 6years.
 
Sikia kaka jipende nafsi yako kabla ya kumpenda yeye mchukulie ni MTU tu ambae ni MTU tu uliyekutana nae ukubwani.Kitendo cha kukaa muda mwingine unamfikilia yeye kitakurudisha nyuma utashindwa kufanya mambo yako ya maendeleo mambo mengi hapa duniani.

Muache aende akajifunze maisha wewe tafuta pesa.unaumia kwa sababu unamuweka akilini mtoe mawazoni kwako fight wewe ni mwanaume kesho atakuita baba huyo...chukua hii thamani yako ataiona itakavyokuwa nae mbali achana nae tu.
Ofcoz yes. Ukiamua unamsahau japo inachukua muda
 
Kaka pole .kwa maelezo uliyotoa mpenz wako anasukumwa na presha za rafiki zake.
Yaani wameolewa nae anakupush ili hali akijua hali yako si nzuri.

Kaka mpaka unakuta sms ni kwamba ana force,sasa wewe mwache aende, Muombe Mungu sana,utafanikiwa. Just beleive kwamba yatapita.

One day utafanikiwa na huyu dada atakukumbuka sana.
 
Jiulize hili swali...
Hivi bila huyo mwanamkw hupumui, bila kuongea nae nitakufa..na maswali kama hayo.....
Nachokiona kwako sio kwamba unampenda huyo mwanamke issue ni kwamba unahofu na woga kama ukimwacha unaweza pata mwingine kulingana na hali uliyonayo kiuchumi...hii hofu inaweza ikawepo bila hata wewe kujua..wewe ukahisi ni upendo....
Kunamsemo unasema However good you are you will always be replaced....
Hivyo usiogope..achana nae....na amini utapata mwingine bila kutarajia....Hakuna kosa kubwa duniani kama kutojiamini au kujiona mnyonge....Achana nae..na kubali kuface maumivu..usiyakwepe kwa kunywa pombe...yaache yaje.....
 
Watu mna moyo sana hivi inakuwa vipi mtu ambaye mmekutana ukubwani akukoseshe amani ya maisha yako, achana nae.
Hivi unataka umuoe ili ugundue nini cha ziada ww ni mwanaume unapaswa uwe na maamuzi ya kiume
 
Mkuu unavyoitwa mwanaume sio kwasababu tu unamiliki gegedeo, uanaume ni pamoja na kuchukua maamuzi magumu. Piga chini uyo mkuu halafu songa mbele saka life. Usiupe uchi kipaumbele kiasi icho mpaka unakutoa machozi. Asee ita gheto kula mzigo halafu mrushie chupi yake mwambie vaa sepa tusijuane tena uku ukiwa umevaa sura ya ukatili, ukiwajulia hawa hawakulizi mkuu
Hahahaa! Sasa unaingia Tarime Muraa
 
Pole sana mkuu, udhaifu wako wa kukosa sifa za mwanaume anayejiamini ndio shida sio huyo bidada.
 
Tengeneza kwanza mambo ya nyumba yako mkuu, halafu ukishakuwa vizuri ndio uoe. Kwa sasa achana na pressure
 
Hata mimi sijawahi ona mwanume weak kiasi hiki. Labda kipindi cha shule tena o level

Hata kwenye maisha ya kawaida bado napata ukakasi kama atayamudu vilivyo
Yaani sitaki kuamini ni hadithi ya kweli hii.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom