Nahitaji Faraja Moyo wangu Unateketea.

Nahitaji Faraja Moyo wangu Unateketea.

Pole sana mkuu, sijui unataka dalili gani nyingine ya kukuonyesha kuwa hapo ulipo sipo!!!
Mapenzi ya dhati ukiwa hauna kitu yamebakia kuwa historia tu, and hope unalielewa hilo.

Hivi mtu alokunyanyasa kiasi hicho bado unafikiria kumvisha pete!! Okey unataka umuoe wakati hauna kitu ili ugundue nini kipya? Utaweza kuyavumilia masimango yake mkiwa tayari ndoani?
Huyo ana shida na "harusi" sio ndoa, mwenye utayari na ndoa hawi hivyo ulivyo mdescribe.

NB: kudate na mwanaume asie na kitu ni kipaji, na wamejaaliwa wachache sio wote.
Dah mamaee mwanamke Umeeleza jinsi gani mlivyo wanawake. By the way huo ndo ukweli and I love that being honest.
 
Ishi kulingana na hali uliyo nayo mkuu. Piga chini hizo dharau utavumilia mpaka lini? Wekeza nguvu na akili yako katika kutafuta mkwanja ndio thamani yako ataiona. Maumivu siku mbili tatu mambo yataenda sawa. Hatua ya kwanza kata mawasiliano nae. Wanawake wapo wengi tu kwa nini ujitafutie matatizo ya kiafya kwa sababu ya mtu ambaye hatambui wala athamini juhudi zako?
 
Nashukuru sana kwa nasaha zako, Ila najua milango itafunguka japo sikupenda ifunguke yeye akiwa nje nilitaka wote tuingie ndani.
mhenga kijana inaelekea hukuelewa maana ya zile methali mfano;
1. asiyesikia la mkuu huvunjika guu
2. asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu
3. sikio la kufa halisikii dawa
4. mtaka nyingi nasaba hufikwa mingi misiba

pia kuna misemo kama;
1. mpende akupendaye asiyekupenda achana naye
2. akufukuzae hakwambii toka

tafadhali jaribu kutafuta maana za methali na misemo hapo juu ukiielewa utapata faraja ya moyo unayoitafuta.
 
Napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wale wote ambao watashiriki kwa namna fulani ama nyingine kunisaidia ili niwe sawa kiakili na kimawazo nahisi huwenda nikiendelea hivi nitaingia kwenye matatizo hasa ya Kiafya.

Miaka ya nyuma kidogo nimekuwa ndani ya mahusiano na binti mmoja ambaye ametumia nafasi hiyo kuniumiza kila leo kwa kuniponda sana moyo wangu, Siwezi kumaliza wiki moja kabla sijaumizwa na makosa ambayo ninaona anafanya makusudi kwangu ili tu niumie na kila siku amekuwa mtu wa kushuhudia natokwa na machozi kwa ajili yake ila anatumia mwanya huo kuniponda kila leo, Nimejaribu kumweka sawa japo bado nipo kwenye utafutaji najua kesho na keshokutwa Mungu atanifungulia milango ya ajira ili niweze kuishi nae kama mke wangu ila pia hali yangu inachangia sana anione kama siwezi kupata ajira daima ila naamini katika Mungu yote yanawezakana.

Nimekuwa najitolea sehemu mbalimbali ila hata pale napopata kidogo najitahidi sana hata nusu apate yeye na nusu nipate mimi, ili tu ajue kwa namna gani ninahangaika kupata kazi ili baadae tuishi wote lakini juhudi zangu anaziona hazina maana kwake, Hivi karibuni nilipanga kwenda kumtembelea nilitamani sana ningepata walau chochote nipeleke kama zawadi lakini hali yangu ilikuwa mbaya sana na kushindwa kupata zawadi yoyote kwake, lakini aliniambia kama ungekuwa na pesa ningependa sana uniletee pete ya uchumba nikamwambia kama Mungu akipenda ajira nikapata basi yote yatawezekana kwa jina lake. Yote haya yanakuja kwa sababu baadhi ya marafiki zake wameolewa na wengine wamevishwa pete hivyo kwa hali yangu huwenda anaona kama ninamchelewesha sana, Ana tabia za kufuata na kutaka awe kama wao ila hali yangu haijakaa sawa mimi kuweza kumudu kile ambacho anakitaka.

Nimeshuhudia Sms kwenye simu yake akiwa anachat na wanaume na kuwaomba pesa kwakweli inaniuma sina la kufanya ila najua penzi langu halipo kwenye taswira nzuri hata kama ni uaminifu nimeanza kumshusha sana kutokana na yale ninayoyaona, najitahidi sana ila anaona juhudi zangu zote ni kupoteza muda. Kuna wakati inafikia hadi namdanganya kuwa mwezi ujao nitaajiriwa anafurahi wana na kuwa karibu namimi ila mwezi ukiisha ukaribu wake na mimi hupotea. Na sikupenda siku moja nipate ajira kisha niachane nae nahisi atanihisi vibaya na kuona kama nimemsaliti baada ya kupata ajira.

Usiku mwili wangu iligeuka kuwa tanuru la moto nimechomwa sana rohoni kwa sms nilizoona wakichat na Mtu nilikuwa naona kifo na macho ila najua ombi langu Mungu atalisikia, japo kazoea kila siku namwambia nitapata kazi ila najua muda si mrefu nitapata kazi hata kama ni kuzibua chemba ili tu nisije kudharaulika kwake.

Nahitaji sana faraja kwa kipindi hiki jamani hali yangu japo iko vibaya ila hili linanitia sana simanzi, nadharauliwa sana.

Mungu Simama nami.
sikia bro,pambana na maisha kutafuta kipato na huyo mwanamje muage kwa furaha na amani kuwa mmeshindana tabia,mtakiane kila la kheri,kila mmoja afate hamsini zake.Wala usiyumbe mkeo bado hujakutana nae
 
Labda kama ni story ulichokiandika..
Lakini kama ni maisha halisi basi niseme tu kuwa umeamua kujichimbia kaburi mapema sana.
Dalili zote hizo unapambana, unachokitafuta utakipata. Yangu ni hayo
 
Mwanaume Kulia lia kwa sababu ya mapenzi ni usenge, tafuta pesa utagonga mpaka wazuri kama majini, mtu hujamuoa unalia je siku akikuacha baada ya kumuoa si ndo utajiua kabisa, jiwekee akilini kitu kimoja Demu ambae hujamuoa si wako ni wa wote upo nae kwa sabb anatafuta wa kuwa nae ila bado hajapata.
We umeamua kumpa makavu..na hata kama ukilizwa na demu lia mara moja tembea mbele.
Anajitafutia magonjwa ya moyo huyu.
 
Ukimuoa ukiwa hela na akaja zizoea hela atatafuta kingine kipya usichokuwa nacho, utajitahid ukipate atatafute kingine ambacho huna tena!

Najua moyo ukipenda huwez ona kibaya....heri ya christmass mkuu
 
Usilie wewe ni mwanaume kaza moyo...

Anafanya hivo kwakua haupo vizuri kiuchumi na seems hauna sauti kiviile kwake kama mwanaume
Usijali pambana
5e1b44846f1c91af72405b7dfa3dfbc0.jpg



Cc Smart911
 
E
We je mshikaji ni mara yako ya kwanza

Jiajiri au usubiri ajira lakini huyo si wako achana inawezekana atakuwa kama goli kipa anaakaa golini anasubiri kona zipigwe na penalit zipigwe ni Nouma

Mkaushie huyo tafuta mwingine tofauti na hapo utaumia kinyama

Kama disco cheza sana , cheki movies ndefu ndefu za kininja na nyinginezo zitakufanya ujihisi km hao wanaigiza na kumuona huyo ni wa kawaidaa saaana

Utakuja baadae unaleta mrejesho Mujarabu
 
Napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wale wote ambao watashiriki kwa namna fulani ama nyingine kunisaidia ili niwe sawa kiakili na kimawazo nahisi huwenda nikiendelea hivi nitaingia kwenye matatizo hasa ya Kiafya.

Miaka ya nyuma kidogo nimekuwa ndani ya mahusiano na binti mmoja ambaye ametumia nafasi hiyo kuniumiza kila leo kwa kuniponda sana moyo wangu, Siwezi kumaliza wiki moja kabla sijaumizwa na makosa ambayo ninaona anafanya makusudi kwangu ili tu niumie na kila siku amekuwa mtu wa kushuhudia natokwa na machozi kwa ajili yake ila anatumia mwanya huo kuniponda kila leo, Nimejaribu kumweka sawa japo bado nipo kwenye utafutaji najua kesho na keshokutwa Mungu atanifungulia milango ya ajira ili niweze kuishi nae kama mke wangu ila pia hali yangu inachangia sana anione kama siwezi kupata ajira daima ila naamini katika Mungu yote yanawezakana.

Nimekuwa najitolea sehemu mbalimbali ila hata pale napopata kidogo najitahidi sana hata nusu apate yeye na nusu nipate mimi, ili tu ajue kwa namna gani ninahangaika kupata kazi ili baadae tuishi wote lakini juhudi zangu anaziona hazina maana kwake, Hivi karibuni nilipanga kwenda kumtembelea nilitamani sana ningepata walau chochote nipeleke kama zawadi lakini hali yangu ilikuwa mbaya sana na kushindwa kupata zawadi yoyote kwake, lakini aliniambia kama ungekuwa na pesa ningependa sana uniletee pete ya uchumba nikamwambia kama Mungu akipenda ajira nikapata basi yote yatawezekana kwa jina lake. Yote haya yanakuja kwa sababu baadhi ya marafiki zake wameolewa na wengine wamevishwa pete hivyo kwa hali yangu huwenda anaona kama ninamchelewesha sana, Ana tabia za kufuata na kutaka awe kama wao ila hali yangu haijakaa sawa mimi kuweza kumudu kile ambacho anakitaka.

Nimeshuhudia Sms kwenye simu yake akiwa anachat na wanaume na kuwaomba pesa kwakweli inaniuma sina la kufanya ila najua penzi langu halipo kwenye taswira nzuri hata kama ni uaminifu nimeanza kumshusha sana kutokana na yale ninayoyaona, najitahidi sana ila anaona juhudi zangu zote ni kupoteza muda. Kuna wakati inafikia hadi namdanganya kuwa mwezi ujao nitaajiriwa anafurahi wana na kuwa karibu namimi ila mwezi ukiisha ukaribu wake na mimi hupotea. Na sikupenda siku moja nipate ajira kisha niachane nae nahisi atanihisi vibaya na kuona kama nimemsaliti baada ya kupata ajira.

Usiku mwili wangu iligeuka kuwa tanuru la moto nimechomwa sana rohoni kwa sms nilizoona wakichat na Mtu nilikuwa naona kifo na macho ila najua ombi langu Mungu atalisikia, japo kazoea kila siku namwambia nitapata kazi ila najua muda si mrefu nitapata kazi hata kama ni kuzibua chemba ili tu nisije kudharaulika kwake.

Nahitaji sana faraja kwa kipindi hiki jamani hali yangu japo iko vibaya ila hili linanitia sana simanzi, nadharauliwa sana.

Mungu Simama nami.
Unamiaka mitano toka uzaliwe?
 
Pole sana mkuu, sijui unataka dalili gani nyingine ya kukuonyesha kuwa hapo ulipo sipo!!!
Mapenzi ya dhati ukiwa hauna kitu yamebakia kuwa historia tu, and hope unalielewa hilo.

Hivi mtu alokunyanyasa kiasi hicho bado unafikiria kumvisha pete!! Okey unataka umuoe wakati hauna kitu ili ugundue nini kipya? Utaweza kuyavumilia masimango yake mkiwa tayari ndoani?
Huyo ana shida na "harusi" sio ndoa, mwenye utayari na ndoa hawi hivyo ulivyo mdescribe.

NB: kudate na mwanaume asie na kitu ni kipaji, na wamejaaliwa wachache sio wote.
NB : na hao wachache Mungu hua anawaangalia na kuwabariki
Yesu Kristo alizaliwa kwenye zizi la mbuzi sehem chafu chafu mbaya mbaya sehemu isiyo kua na kiyoyozi wala kitanda lakini pale Mungu alipaona hapa ndipo atazaliwa mwanae mpendwa mfalme wa wafalme duniani
 
Mkuu usiumize kichwa, HAUPENDWI na HUTOPENDWA NAYE HUYO MWANAMKE
kama kuna uwezekano wa kuondoka uende ukatafute maisha sehem ya mbali nenda kapambane na Mungu atakusaidia. mwambie tu kistaarabu kwamba umefikia mwisho kwaio kila mtu aende njia yake mwache na uwe na amani, tena furahia na ushangilie mana utakua umejiokoa.
Muombe Mungu ukiwa na nia ya dhati atakuletea mwanamke anayekustahili.
 
Pole mkuu...ungemuacha kwanza utafute life, then likitick ndo utajua umrudie au ummwage!
 
Wewe naona unajipa mizigo miwili wa kutafuta kazi na wa kumfikiria mtu mwingine.

Mwache tena mueleze mama sina kazi siwezi kukuhudumia na pia naona nakuchelewesha maisha wenzako wanaolewa naona nakupa wakati mgumu...hapo achague kusuka au kunyoa...

Nimeupenda ushauri wako...
UKWELI utamuweka huru.
 
Pole sana mkuu, sijui unataka dalili gani nyingine ya kukuonyesha kuwa hapo ulipo sipo!!!
Mapenzi ya dhati ukiwa hauna kitu yamebakia kuwa historia tu, and hope unalielewa hilo.

Hivi mtu alokunyanyasa kiasi hicho bado unafikiria kumvisha pete!! Okey unataka umuoe wakati hauna kitu ili ugundue nini kipya? Utaweza kuyavumilia masimango yake mkiwa tayari ndoani?
Huyo ana shida na "harusi" sio ndoa, mwenye utayari na ndoa hawi hivyo ulivyo mdescribe.

NB: kudate na mwanaume asie na kitu ni kipaji, na wamejaaliwa wachache sio wote.
Umemchoma kama pasii, mwenzio ndio kapenda kapitiliza.
 
Kwa maelezo yako hakikisha hupiti karibu na wauza sumu za panya maana huchelewi kununua. Pole sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom