Mc Tilly Chizenga
JF-Expert Member
- Feb 7, 2012
- 4,641
- 3,675
Nahisi na tabia za kike katika mapenz naomba nieleweke wanajamii!!
1.Napenda sana kusifiwa kama umependeza au hakuna mwanaume mzuri kama wewe Duniani.
2.Napenda sana kufarijiwa/kujaliwa mfano kupewa pole hata kama kazi niliyo fanya ni ndogo.
3.Napenda sana kubembelezwa kila wakati kwakifupi napenda kudeka sanaaa..
4.Napenda sana kupewa za wadi hata ya pipi nitalizika.
5.Napenda sana Kukumbatiwa kila niwapo na mpenzi wangu.
Ringopet,
1.kwanza hongera sana una jina zuri....Ringopet....nadhani jina lako ni zuri kuliko wanaume wote humu ndani!
2.nikupe pole sana kwa kuandika thread hii,utakuwa umechoka sana,maana umeweka pointi nyiingi kweli..5!poleeee
3.eti ringopet,utanijibu hii posti yangu...nijibu pleaseeeeeee,nijibu basi mbona unaona aibu unatizama chini...nijibu
4.nina kazawadi kako kukupongeza kwa kuwa na hulka za kike...sio kubwa ni pipi ivori
5.hii namba 5 inamuhusu Boflo....ndio maana amekuwa mwanaume pekee kui-like post yako
all the best huko unakoelekea!nasikia mna vyama vyenu kabisa