Habari,napenda kujua ni lini zina toka nafasi za jkt kwan anaye fahamu hiii alielekeze ili nijipange kwa hilo.
Sent using
Jamii Forums mobile app
Vuta subira kijana, tunza afya yako.... Endelea kufuatulia. Kuhusu kujiunga na JWTZ, hakuna nafasi za moja kwa moja au labda tu itokee kuwa na uhitajio wa kundi la watu maalumu i.e Madaktari, Wahandisi, na watu wenye fani za Urubani au fani nyingine zitakazokuwa zikihitajika kwa wakati huo.
Utaratibu wa sasa kujiunga na chombo chochote cha ulinzi na usalama ni sharti mtu apitie kwanza JKT kwa lengo la kujifunza Uzalendo na Ukakamavu ( Though hakuna General rule hapa, mambo hubadilika kulingana na uhitaji}
Unapohitaji kujiunga na vyombo hivi basi, one of the thing you need to primarily train yourself kwanza ni kuwa na disciple na uvumilivu. Vitu hizi lazima uvianze mapema sana. Kwa wakati huu ukiwa bado unaendelea kungojea nafasi zitoke basi endelea kuwa mvumilivu na endelea kufuatilia. Mi vema ukatafuta taarifa katika vyanzo halisi na vya uhakika kuliko habari za kuambiwa na watu. Tambua kuwa huwa kuna matapeli na watu wengi wameingizwa mkenge katika mambo haya. Tembelea tovuti rasmi ya Jeshi la Kujenga Taifa{ jkt.go.tz) kwa taarifa kuhusu nafasi na vigezo vya kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa kwa nafasi ya Mujibu wa Sheria au kama kijana wa kujitolea.
Endapo nafasi zitatoka na ukafanikiwa kuwa na sifa na ukaweza kujiunga, soma vizuri na elewa mkataba utakaosaini ili baadae mambo yakienda tofauti na matarajio usije anza regret. Kwa kukusaidia tambua kuwa JKT haiajiri ila tu ni mahali ambapo unaweza fanyiwa usaili (endapo utakuwa na vigezo) kuandikishwa (maana jeshi pia haliajiri ila huandikisha) katika majeshi mbalimbali ie Bakabaka( maana ninyi vijana huita hivi), Polisi, Magereza, Askari wanyamapori, TISS (sometimes),.... etc etc.....
Nakutakia kila lakheri katika safari yako unayotarajia kuianza.
But one more thing: Usiniambie kuwa movies za John Rambo ndio zimekuvutia utafute career ya kuwa askari au umesikia kule wanatoa mishahara mizuri na au pengine unadhani kuwa askari ni high social status kwamba utavutia madem au utakuwa mbabe as *** au pengine umeona kitaa hakieleweki

. Be realistics, avoid illusions, utafanikiwa!
Sent using
Jamii Forums mobile app