Zabron Hamis
JF-Expert Member
- Dec 19, 2016
- 6,517
- 10,427
Bora wewe unafananishwa. Mimi nilishakutana na watu zaidi ya wawili ambao tunfanana. Wakati nasoma kuna mmoja alienda shule kuomba kazi ya kufundisha (temporary) siku hiyo sikuwa sikwenda shule, jamaa nusura apokee stick sema nguo alizokuwa amevaa siku hiyo sikuwahi kuwa nazo na pia sauti yake ilikuwa tofauti. Poa alikuwa na alama shingoni ambayo mimi sina ndio ikawa ponapona yake. Kesho yake alikuja shule nakunikuta ilibidi tushangaane na hakuna aliyemsemesha mwenzie maana tuliduwaa wote. Muhimu ni kumuomba Mungu tu usifananishwe na vibaka katikati ya kundi la watu unaweza kufaEti wanasema bhangi zangu! wakati hii ni kweli kama unavyosema kuna mtu anakuja anakuletea stor inabid nawewe ujifanye unamjua tu mamake ukimuuliza imakuwa bado humfaham, nashukuru mkuu kumbe sio peke yangu ni hali ya kawaida tu